Hekaheka Uzeeni

Hekaheka Uzeeni

UTANGULIZI

Maisha baada ya kustaafu huwa yana ‘stress’ nyingi. Kujaribu kupunguza stress hizo nilifungua ‘account’ hii JF ili kujiburudisha na kuburudishwa. Account zangu nyingine JF zina ‘personality’ tofauti kabisa.

Michengesho (decoys) zipo kama kawaida ili kulinda nukta kuunganishwa.

HEKAHEKA UZEENI

Sehemu ya kwanza – KUSTAAFU UTUMISHI WA UMMA SI JAMBO LA GHAFLA.


Katika kazi za utumishi wa umma, wapo wanao staafu wakiwa na miaka arobaini na mitano na kuendelea, mimi nilibahatika kufanya kazi hadi miaka sitini na kustaafu kwa mujibu wa sheria. Kujifunza ‘hakwishi’, kuna karaha zake baada ya kustaafu hususani wakati wa kufuatilia stahiki zako. Angalau siku hizi utaratibu ni mzuri sana usumbufu umepunguwa kwa kiasi kikubwa.

Kwakuwa kustaafu ‘hakukuji’ ghafla, yampasa mtumishi yeyote aliyeajiriwa kuajiandaa na maisha baada ya kustaafu. Tumeshuhudia wengi baada ya kustaafu kuendelea Kwenda eneo la kazi na kukaa kupiga soga nk, hii hutokana na ama kufuatilia mambo yake ama kukosa sehemu muafaka ya Kwenda kwakuwa labda hakujiandaa na mahali ya Kwenda baada ya kustaafu.

Miaka 45 ni mtu mwenye nguvu bado, hivyo anaweza kufanya Maisha yaendelee kwa mtindo mwingine bila kuathirika na kazi alizozioea kazini, vivyo hivyo kwa miaka 50 ama 55 ama 60 na hata 65 bado mtu anaweza kujishughulisha na mambo ambayo yatamfanya asiwe ‘bored’

Mara nyingi kwa watumishi wengi maisha yao baada ya kustaafu huwa ni ya upweke, ‘kupigwa mizinga’ kutoka kwa ndugu na jamaa na usipokuwa makini utajikuta unapata magonjwa ya kisukari na moyo pasipo kutarajia kutokana na mtindo wa maisha utakao kuwa nao.

“…hela ya mafao ya kustaau siyo ya kujengea kaka…!” aliwahi kuniambia mzee mwenzangu mmoja aliyetangulia kustaafu.

“…hiyo hela ni ya kukutunza wewe, ni ya kufurahia maisha yako ya uzeeni hadi siku Mwenyezi Mungu atakapo kuchukuwa…”

“…ndugu na jamaa wengi watakuletea shida zao, sisemi usiwasaidie, lakini saidia kwa kiasi tu ili usiharibu fungu lako wala uhusiano wako na ndugu na jamaa, ikiwezekana tangaza hali mbaya ya uchumi kabisa ili wasiweke dhana kwamba una hela, singizia chochote kuepusha usumbufu, mwenzako yamenikuta sana…” Ni maneno yamzee mwenzangu mwingine ambaye yeye alitangulia kustaafu pia.

Sentesi ya ‘hela ya kustaafu ni ya kufurahia maisha..’ ndiyo iliyonifanya nianze kuandika simulizi hii.

Kama nilivyoserma awali, kwakuwa kustaafu ‘hakukuji’ ghafla yapaswa kujiandaa kwa kuwa na miradi midogo midogo wakati ukiwa bado katika utumishi. Hii ni kwa wote, watumishi wa umma na wa sekta binafsi. Anzisha mradi wowote wenye kukuingizia kipato hata kama ni kidogo ili mradi kiweze kukidhi mshahara wa anayesimamia, kutunza mtaji, kukuza mtaji na kujipatia faida kidogo. Hapa nazungumzia wale ambao kima chao cha mshahara ni cha chini. Kwa wale wenye vima vya juu nawashauri wafikirie kufanya miradi mikubwa yenye kuleta ajira kwa vijana na kutopeleka hela nje ya nchi, wekezeni humu humu nchini hiyo miradi yenu mikubwa kwa maana mzunguko wa fedha hizo zitabaki ndani. Sisemi msiwekeze nje ya nchi lakini nasema msisahau kuwekeza ndani kuwasaidia hawa vijana wetu wanaomaliza masomo yao kila mwaka.

Hebu niache haya mambo ya ushauri-nasihi usio rasmi maana kila mtu anajipangia mambo yake mwenyewe, lakini usisahau pia kuishi na mkeo / mmeo vizuri maana ukitangulia kustaafu kabla ya mwenza wako na haukuwa unaishi naye katika mahaba tarajia ‘stress’ za vijimambo vidogovidogo tu ambapo sasa vitakusanyika na kuwa kero.

nijikite sasa kwenye hii sentesi …”..hela baada ya kustaafu ni za kufurahia Maisha…”

Wakati na mbwela-mbwela kusubiria ‘fuba’ la mkupuo si nikapata mkataba fulani hivi kusaidia mambo fulani nchini DRC!. Ulikuwa ni mchongo wa miezi mitatu. Namshukuru sana yule jamaa aliyeniunganisha maana alikuwa anajuwa uwezo wangu katika fani ile kuhusiana na mchongo huo.

‘Paapu’, nikaambiwa niripoti Goma – Kivu ya kaskazini DRC tarehe fulani. Nikajiangalia mfukoni nikaona kuchukuwa flight hakunifai.

“…bora nipande basi kwa kuwahi wiki moja kabla ya tarehe husika…” nilijisemea moyoni.

Wakati huo Stendi ya Mbezi, “Magufuli Bus Terminal” ilikuwa bado haijaanza kutumika, hivyo nikatinga Ubungo bus terminal kuangalia usafiri maridhawa. Nilikuta kuna basi mbili za kampuni moja ambayo niliambiwa ni wazuri kwenye huduma ambazo zote zilikuwa zinaenda Kigali. Nikakata tiketi ya basi kubwa kama walivyokuwa wakiita wenyewe.

Kwakuwa huwa napenda kuona mbele ya basi kwenye lami, nilichaguwa siti ya nyuma ya dereva siyo upande wa dirishani lakini ingawaje palikuwa bado hapajachukuliwa. Sababu nyingine iliyonifanya kuchukuwa nafasi hiyo nili ile nafasi kati ya dereva na siti nyuma yake ni kubwa pa kuweza kunyoosha miguu na pia kuna kama meza fulani hivi mbele (fridge) hivyo kufanya paonekane ni sehemu muafaka kwangu kwa safari ndefu kama ile.

Siku ya safari nikafika mapema sana Ubungo bus terminal, moja kwa moja kwenye eneo ambalo basi husika lilikuwa linapakilia abiria, nilikuta baadhi ya abiria wakiwa tayari ndani ya basi ingawaje nilifika takribani nusu saa hivi kabla ya safari. Sikuwa na mizigo bali backpack Fulani hivi kubwa kiasi ambayo iliweza kubeba laptop yangu pamoja na nguo zangu chache ambazo nilidhani kwa kazi ya siku 90 ningeweza ‘kupiganisha’ bila kuhisi sina nguo za kubadilisha.

Kampuni ya basi ilikuwa inaitwa ‘utatu mtakatifu’, kwa kweli basi nililopanda walijitahidi sana kufanya liwe na hadhi yake mle ndani, viti vyenye vitambaa vya ngozi (synthentic leather), nafasi kubwa kati ya siti na siti, ila kwenye lugha za kuhudumia wateja walikuwa wanafeli sana, sijui ni kwa sababu ya kutojuwa Kiswahili vizuri ama nini. Hakika kwenye hili walikuwa wanafeli, siku hiyo kulikuwa na madereva wawili, mmoja Mtanzania na wa pili ni Mnyarwanda, na mhudumu tuliye safiri naye mmoja mwanume na mwingine ambaye alishukia njiani alikuwa ni wakala wao, akisindikiza gari.

Nilitulia kwenye kiti vizuri huku basi likiwa limekaribia kujaa kabisa abiria lakini kwenye kiti changu bado hapakuwa na abiria aliyekuja. Shingo nikiwa nimeinua juu kidogo kuangalia kwaya walizoweka kwenye runinga ya basi pale mbele mara nikasikia sauti ikiniambia…

“Excuse me, let me pass that is my seat..” alikuwa ni binti mrembo na kwa sura ile moja kwa moja nikajuwa huyu ni Mnyarwanda.

Nikampisha bila kusema neno, na alipokuwa ameketi sasa ikanibidi siti nibonyeze sehemu ili kuongeza nafasi ili tuenee vizuri maana si kwa ma ‘hips’ yale.

“Hujambo?” nilimsalimia na akaitikia kwa kichwa huku akiendelea na mambo yake mara kashika hiki mara kashika kile ili mradi alikuwa hatulii kama ana wasiwasi fulani hivi kama vile kuna jambo halijakamilika.

Macho nikarudisha kwenye runinga kuendelea kuburudika na kwaya za kisabato, ‘what a beautiful melody!’

Punde si punde mlango wa basi ukafungwa na tukawa kwenye foleni ya kutoka nje ya bus terminal. Ajabu ni kwamba vurugu za mabasi kugombania kutoka nje ya geti zilikuwepo licha ya utaratibu mzuri ambao uliwekwa na uongozi wa kituo na kusimamiwa na askari.

Baada ya chekecha chekecha ya hapa na pale hatimaye tukawa kwenye mstari ulionyooka sasa wa kutoka nje. Nikageuza shingo kuangalia nyuma, hakika basi lilikuwa limejaa na hakukuwa na mtu aliyesimama zaidi ya mhudumu mmoja na Yule msindikizaji ambao wote walisimama pale mlangoni, wakati huo tayari yule wakala msindikizaji alikuwa amesha maliza mambo ya ushuru wa getini nk.

===

Safari iliendelea hadi maeneo ya Mbezi Luis ambapo yule msindikizaji alikuwa ameshakamiliza zoezi lake la kukabidhi kila abiria tiketi ya mashine ingawaje tulikuwa na zile tiketi za karatasi. Tiketi hizi za mashine (POS) hazikuwa hizi zilizounganishwa na mifumo ya LATRA na TRA bali zilikuwa kwa ajili ya udhibiti wa kiofisi yao tu.

Niliangalia begi langu kwa mara nyingine, nikajiridhisha lipo salama haliwezi kumuangukia abiria wa jirani maana nililiweka kwenye kibebeo (carrier) cha upande wa kushoto wakati mimi nipo siti za upande wa kulia ili niweze kuliona muda wowote ninapotaka ingawaje watu wengine hupenda kuweka upande huo huo alipo kaa yeye tena juu sehemu aliyokaa.

Safari iliendelea, wakati huo video ilikuwa imezimwa na kufunguliwa radio (RFA) tukiendelea kupata habari. Kwenye hili la kelele za miziki, video za ndani ya basi walikuwa wamefanikiwa, maana hawakuwa wakifungulia kwa sauti za juu, ilikuwa sauti ya kadri tu ambapo hata ukiongea na simu kwa sauti ya chini bado mtasikilizana.

Basi lilitembea mwendo wa Serikali, ‘tatu bila, tano bila nane bila’ hadi tulivyofika Chalinze na misafara ya mabasi kuongozana na kukimbizana ikapungua na mabasi kuanza kumwaga moto. Kutoka Mbezi hadi Chalinze nadhani siku hiyo kulikuwa na fatiki kabambe ya ‘traffic police’ kwa maagizo ya kamanda wa wakati huo, maana kabla ya safari kulisikika tangazo pale Ubungo bus terminal kuwa madereva wote wakusanyike sehemu husika kwa ajili ya kuongea na Kamanda (alitajwa). Nadhani semina fupi ile iliwaingia hadi Chalinze tu, sijui madereva wa mabasi wana matatizo gani, kha!

Basi lilikuwa ni YUTONG, sijui namba ngapi ngapi lakini wenyewe wanasema ndio kubwa katika mfululizo wa wakati huo. Huko mbele ya safari ndio nikajuwa maana niliona ilivyokuwa inafunguka. Licha ya kuchezewa vts lakini pia nahisi ‘limiter’ ya spidi pia ilichezewa, si kwa mwendo ule baada ya kuvuka Rusumo border.

Chalinze hadi Moro basi lilitembea lakini ile kibongo bongo, minara ilikuwa inafanya kazi maana yule mhudumu muda wote alikuwa na simu sikioni na mkono mmoja ameweka juu ya dashboard, mara anapiga dashboard mara anainua kama vile anaita yani alikuwa anapata taarifa nje ya basi na yeye alifikisha ujumbe kwa dereva kwa kupiga dashboard, kuinua kiganja na kuita kwa kiganja.

Mwendo haukuwa hatarishi kiasi cha kuripoti kwa askari waliokuwa akiuliza sehemu za ukaguzi na dereva wala hakuwa mchafuzi wa overtake za ‘kubeti’ ila kwenye mwendokasi sehemu za hamsini hadi tulivyofika mbele kidogo ya Singida. Huko ilikuwa muda mwingi ni over 90kph.

Kabla ya kufika Morogoro, jirani yangu ambaye katika simulizi hii nitampa jina la Janeth, alikuwa ametulia, maana muda wote tangia Dar alikuwa kwenye simu akiongea mara akiandika jumbe za simu. Nikaanza kumsemesha sasa kwa Kiswahili ili kujuwa uwezo wake katika lugha hii adhimu, alikuwa anajibu kwa tabu sana ingawaje alifinyanga finyanga tukawa tunaelewana.

Kwa haraka haraka kutokana na maongezi ndani ya basi, nikajuwa mle ndani kuna Wabongo, Wanyarwanda, Warundi, Wakongo, wa Uganda na Wakenya. Pia kulikuwa kuna watu weupe wawili mmoja akiwa mwanamme, sijui ni Wazungu au Wamarekani lakini hawakuwa Waasia.

Janeth hakuwa mweupe wa rangi, bali maji ya kunde na aling’aa vyema kama ngozi yake ilivyokuwa ikionesha, alivaa ‘tracksuit’ na raba kama vile alikuwa ametoka kufanya mazoezi, nywele alisokota rasta bila kuunganisha nywele za bandia. Hakunizidi urefu, mana pale Chalinze tulipokuwa tunakunywa chai tuliteremka pamoja na kutembea pamoja kabla hatujaachana njia mimi nikielekea maliwatoni upande wa wanaume.

Kwakuwa mimi ni mpenda chai ya maziwa yenye kahawa, basi nilienda upade ule kwenye huduma hiyo na yeye Janeth wa sikumuona tena alipoelekea.

Kwenye jambo hili la kuwapa muda wa kutosha abiria wakati wa chakula, hawa jamaa nao walifaulu vizuri, maana mhudumu alipotangaza alisema tutatumia nusu saa kuchimba dawa pamoja na kupata chochote, tuzingatie namba ya basi maana yalikuwa mawili, baadaye sana ndio nikajuwa kuwa moja litaelekea Uganda na lile tulilopanda ndio litaelekea Kigali.

Kwakuwa siti yangu ilikuwa jirani na sikuwa nakaa dirishani, niliingia wa mwisho mwisho kwenye basi na kumkuta Janeth akiendelea kula nyama za kuchoma alizofungiwa kwenye bahasha fulani hivi ya khaki.

“Welcome nyama choma…” alinikaribisha huku akimaanisha nichukuwe msongo mmoja niendelee nao…

“Aaah, ahsante sana, unaitwa nani?” nilijibu huku moyoni nikikataa kuchukuwa nyama kwa ishara ya kuonesha nimetosheka (nimeshiba)

“Yaleyale ya kupewa chakula na usiyemjuwa wala kuona chakula kilipotoka mwisho wa siku unajikuta umeshaibiwa…” niliwaza.

Nikatoa ‘chewing gum’ za ‘mint’ na kuanza kutafuna ili kuweka kinywa changu katika hali ya kuanzisha maongezi ya kisafari safari.

“Karibu bublish…” nilinyoosha mkono na kumpatia kadhaa na akapokea kimya kimya na kuzihifadhi kwenye kimfuko kidogo kilichopo kwenye lile friji mbele ya siti zetu huku akiendelea kutafuna minofu ya mishikaki ya ng’ombe.

Safari ikaanza tena tukiitafuta mizani ya Mikese, mwendo mzuri, nane bila na uchafuzi wa speed kiasi maana dashboard nilikuwa naiona lakini ilikuwa haizidi 89kph. Pila nilikuwa na Garmin Drive 52 iliyoipata katika harakati za kutafuta ugali ambapo katika safari hii nilitarajia itanisaidia kule niendako ambako sikuwa na uhakika wa coverage ya internet.

Kelele za king’amuzi (vts) kilikuwa almost muda wote alipokuwa zaidi ya 85kph kinasikika kwa mbali sana, sijui waliweka kitu gani wale jamaa, maana kama sio mjuzi wala huwezi kuelewa ni kitu gani kinaendelea, dereva huyu Mtanzania alikuwa na nidhamu ya michoro ya makatazo ya kuovateki ila alikuwa ana ‘maintain maximum’ ya Latra muda mwingi, hii ilifanya tusiwe nje ya muda wa ratiba ya gari.

Janeth mkononi alikuwa amevaa kitu mama shanga hivi maarufu kama “culture” lakini ilikuwa na bendera ya Kenya.

“Wewe ni mkenya?” nilimuuliza huku nikiutolea macho mkono wake wa kushoto ambao ndio alikuwa amevaa hiyo shanga.

“No, Mnyrwanda” alijibu huku akitabasamu.

Nikachukuwa smartphone yangu, nikafungua playstore ili nidownload dictionary ya English – Kinyarwanda lakini haikunisaidia sana maana wakati huo bado haikuwa na maneno mengi.

“Do you speak English” nilimuuliza tena ili kama vipi tuhamier kwenye Kiingereza maana Kiswahili chake kilikuwa hakieleweki.

“Kidogo…” alijibu kisha akaendelea … “French and Kinyarwanda okay...”

Katika harakati za maisha sikubahatika kujifunza Kifaransa, bali niliyajuwa maneno machache sana maana rafiki yangu wa zamani sana, mototo wa Kihindi aitwaye Raani alinipatia kamusi ya Kifaransa kwa kiingereza lakini wala sikuwa na mzuka. Raani binti yule wa Kihindi urafiki wetu haukudumu kwa sababu ya Sue mototo wa Kispaniola ambaye naye pia wala hatukufika mbali, maana baada ya chuo tu miezi ishirini hivi baadaye mawasiliano yalikatika.

Alivyojibu kuwa kwenye Kifaransa na Kinyarwanda ndio yuko vizuri, basi sikuwa na chaguo lingine zaidi ya kuvumilia Kiswahili chake na kiingereza chake ingawaje kwenye kiingereza alikuwa yuko vizuri zaidi kuliko Kiswahili.

Hili ni jambo lingine la kushangaza, yani ukitoka Bongo kwenda Rwanda, hapo Rwanda wenyeji wanazungumza kilugha chao tu na Kifaransa, siyo wengi wazungumzao kiigereza. Ila ukivuka Rwanda kwenda Congo DR huko utakutana na Kiswahili cha aina yake, lakini angalau watu wanaelewana.

Kigali haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, lakini huko Goma ndiyo ilikuwa ‘fisrt time’. Niliuchangamkia huo mchongo ingawaje Hamida alinikataza nisiende kwa kuhofia hatari iliyopo ya vita baina ya majeshi ya Serikali na watu wanaojiita waasi.

“The first time when I saw you, I knew for sure you are Mnyarwanda…” nilisema.

“Why?” aliniuliza.

Hapo ndipo nikafunguka kuhusu jinsi sisi Wabongo tunavyowaona Wanyarwada. Nilimwambia kuhusu maumbile yao ya urefu, sura nyembamba, urembo wa asili, nyama za kutosha sehemu ambazo huwafanya wanaume wageuke nyuma kuangalia ili kuburudisha macho, nikaeleza weee mwishoe naye akaniambia kuwa hiyo dhani si asilimia mia sahihi, siyo Wanyarwanda wote warembo kama nilivyowapamba…

Eeee ni kweli nilimpamba sana ‘mixer’ ukweli na chumvi ili kuwasifia kama ilivyo kawaida ya wanaume.

Kwakuwa Rwanda haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, nilikuwa najuwa hawa warembo tunaowaona kwenye mitandao ni wachache tu, wanawake wa Kinyarwanda wapo kwa maumbile mbalimbali na sura tofauti wengi ni wa kawaida sana na tofauti kabisa na tunao waona hawa wa kwenye mitandao. Hata hivyo haiondoi ukweli kwamba wapo wanawake warembo wa sura na maumbile huko Rwanda. Tabia zao tu ndio zina ukakasi kiasi fulani juu ya kujiona wapo matawi ya juu sana, kuwa na ukatili uliojificha labda kutokana na historia yao nk.
“…Lakini sasa mbona umevaa bendera ya Kenya?” nilidadisi.

Hapa akafunguka kuwa yeye ni mfanyabiashara, ana duka la nguo za wanawake kwao Kigali na kabla hajajuwa machimbo ya Tanzania alikuwa akifungia mizigo yake Uganda na Kenya, na hiyo ‘bracelet’ aliyovaa aliipatia Kenya…

Mazungumzo ya kawaida yaliendelea kama ilivyo kawaida kwa abiria na abiria. Safari nayo ilisonga salama kabisa hadi tukafika Dodoma pale jirani na panapoitwa ‘four ways’, tukawa na ‘short break’ ya dakika kumi ya ajili ya kuchimba dawa kisha safari iliendelea hadi Singida baada ya mizani mbelembele kidogo gari ikaingia sehemu fulani kuna hoteli ambapo napo tulipata dakika ishirini za kuchimba dawa na kupata chochote kisha safari ikaendelea. Tulipokaribika Igunga giza fulani hivi lilianza kuingia, hadi tunapita mzunguko wa Nzega pale tayari dereva yuleyule tuliyetokanaye Dar akiwa anaendesha hadi muda huo aliwasha taa hafifu zilizowaka kwenye sakafu ya basi pembeni pembeni na kufanya mandhari kuwa nzuri sana ndani ya basi.

Awali nilidhani basi litanyoosha moja kwa moja hadi border ya Rusumo lakini kumbe hayapitilizi bali wanalala Kahama kisha asubuhi na mapema safari huendelea hadi boda.

“Have you made your reservation to pass your night at Kahama…” Janeth aliniuliza wakati gari ikiwa inakunja Tinde kuelekea Isaka.

Nilimjibu kuwa sijafanya chochote, si nitalala ndani ya basi!

“Please don’t sleep in the bus, you will get tired, and you won’t enjoy your looong journet from there to Kigali, its tiresome…” alisema Janeth na alikuwa anamaanisha. Nilijua hivyo siku ya pili baada ya kufika Rusumo.

“I don’t have enough cash with me…” nilitaka kujitetea akanikatisha…

“Don’t worry, I will pay for you and you will refund me when we reach border or Kigali…”

Sikumwambia kuwa mie pale mpita njia tu naelekea DRC. Nadhani alidhani namie ni mmoja wa wanaoelekea kwenye “sabasaba yao” (trade fair) maana tarehe hizo kulikuwa na maonesho ya kibiashara hapo Kigali iliyoanza kama siku mbili zilizopita na inayotarajiwa kuwepo kwa siku kadhaa zijazo.

“Why spend a lot of money! We can share the room…” nilichombeza huku nikiwa simaanishi.

“…Really!?” alihoji

“Why not!” nikajikuta tu neno limenitoka.

Mazungumzo yaliendelea na akaniambia yeye hufikia Gaprena Hotel. Nikatafuta review ya hotel hiyo harakaharaka kwenye simu nikaona ni zile wanazoita hotel kumbe ni lodge tu iliyochangamka. Anyway, ni Hotel. Sifa kuu aliniambia kuwa pako salama na ni karibu na stendi kuu pia gharama ni ndogo kulinganisha na hadhi ya hoteli yenyewe. Mimi wakati huo nimeshasoma review kadhaa na kupata picha halisi ya sehemu anayotarajia kufikia.

Tukaingia mizani Kahama na baada ya kutoka hapo mhudumu alitutangazia ratiba ya gari na kutupatia elimu maelekezo na tahadhari. Moja ya maelekezo aliyotoa ni kwamba basi halitoendelea na safri hadi kesho saa kumi na mbili asubuhi, hivyo anashauri abiria watafute lodge za kupumzika kwa watakaopenda kufanya hizo, na wale watakao amua kulala ndani ya basi wawe makini na mizigo yao ya ndani ya basi maana ulinzi wa mali iliyo ndani ya basi ni wa abiria husika.

“Muwe makini na mutu mugeni yanakuja ndani ya basi, hakuna abiria naingia usiku huu…” alimalizia yule mhudumu na Kiswahili chake kibovu.

Gari ikakunja kulia moja kwa moja hadi stendi kuu. Stendi ilikuwa imechangamka sana na ilikuwa ni majira ya saa tatu hivi usiku. Watu wengi, wauza vyakula mama lishe wengi huku wakikaribisha wateja, wapiga debe wa lodge pia wengi wakijitahidi kutafuta wateja, hakika Kahama palikuwa pamechangamka sana.

Wahudumu wa basi tulikuwa nao safarini wote waliondoka akaja wakala mkazi wa hapo ambaye alikuwa akisimamia ‘shoo’ bila shaka na walinzi wao pia walikuwepo ingawaje sikuwaona mara moja.

Abiria walikuwa wanajivuta sana kushuka mimi na Janeth tukiwemo. Nusu saa baadaye tuliamua kutembea kuelekea hoteli ambayo abiria mwenzangu alikuwa ameweka nafasi. Bajaj, tax na bodaboda zilikuwepo, lakini tuliamua kunyoosha miguu baada ya safari ndefu.

Tulivyofika pale mapokezi tulikaribishwa kwa bashasha lakini ‘walinikata maini’ nilipoulizia kama kuna chumba…

“Ishi, kwani hampo pamoja!...” aling’aka yule mhudumu

“Vyumba vyote vimejaa, basi ngoja nikupeleke hoteli ya jirani na hapa, pale unaweza kupata ila bei ipo juu kidogo…” aliongea yule mhudumu kwa lafudhi ya kisukuma.

Janeth akaingilia kati…

“Lets share as you said, no problem… are you going to swallow me!?”

Yani hapa angalau kwenye uandishi inabidi nikinyooshe kidogo hivi vilugha vya watu maana jinsi alivyokuwa akiongea Janeth unaweza ukawa unacheka tu kila mara.

“Well, its okay, lets share the room and I promise will not swallow you…” tukawa tunacheka huku tukielekea chumba husika maana mwenzangu pale inaonekana ni mwenyeji.

======

INAENDELEA…

View attachment 2540333View attachment 2540338View attachment 2540341


Are you going to swallow me?????🤔🤔🤔🤔🤔!!

Ngoja niendelee na episode 2 nione if someone was swallowed that night!🙇
 
INAENDELEA…

“Well, its okay, lets share the room and I promise will not swallow you…” tukawa tunacheka huku tukielekea chumba husika maana mwenzangu pale inaonekana ni mwenyeji.


2. Sehemu ya pili – KISOMO CHA WATU WAZIMA

Tahadhari zote nilikuwa nazo, za kiusalama wangu na mali zangu pamoja na kifaragha maana matukio ya kusikitisha hutokeaga kama hivi. Hoteli ilikuwa ni ghorofa, sisi tulipata’ first floor’ na chumba kilikuwa kikubwa kiasi cha kusema kwa hela ile ni halali tu.

Nilikagua kila chumba kama kuna kamera-fiche, nikaona pako salama, nikawa nimekaa kwenye kochi na mwenyeji wangu wakati huo alikuwa kwenye kitanda. Mara simu ya mezani pale chumbani ikaita, Janeth akaipokea , kumbe aliweka oda tayari ya chakula kwa ajili ya watu wawili. Mlango ukabishwa na akaingia mhudumu kuleta chips kuku mbili na kuondoka.

“Tule kwanza kisha ndio tuangalie utaratibu wa kulala…” nilipendekeza na ikapita bila kupingwa.

Nilipendekeza pia tuanze sahani moja kwanza wote kwa pamoja na kama hatujashiba basi tuhamie sahani nyingine. Hii ilikuwa mbinu ya kujihami na madhara ya kwenye vyakula, kama yapo basi yatupate sote na wakati wa kula nilihakikisha nasoma lugha ya uso wake ili kujiridhisha.

Maskini binti wa watu wala hakuwa na makuu bali ni ukarimu tu wa kawaida na kama alikuwa na agenda ya siri basi sikuiona haraka ukiachilia mbali na suala la kushiriki tendo la ndoa.

Mfukoni kweli sikuwa na hela za kutosha kwa mambo ya ziada, zaidi ya yale niliyo jipangia hadi kufika Congo, hivyo sikuwa na mzuka maana boom la kustaafu lilikuwa bado kutoka na tayari nilishasota mtaani miezi kadhaa hivyo vihela vyangu vilikuwa vya kuunga unga. Nikatuma ‘txt msg’ kwa Jason Jr ili aniazime dola mia tano atume kwenye account yangu ya benki just incase. Kabla sijalala muamala ulisoma kwenye akaunti yangu.

Janeth alikuwa huru tu, akaingia bafuni na kibegi kidogo na alipotoka alikuja amevaa kaptura na juu alikuwa amevaa fulana nyepesi (haikuwa night dress hizi tunazozijua)

“I am in my period so don’t try anything nasty…!” aliniambia huku akiingia kwenye blanket tayari kuutafuta usingizi.

Moyoni nikajisemea afadhali maana umenirahisishia mambo mengi ambayo tayari nilikuwa nawaza kichwani. Sikuwa na soksi wa vipimo vya kupimia tanesco kama ipo. Nikaingia bafuni na kuanza kuoga, wala sikutumia muda mrefu nikatoka kuja kuungana na Janeth ndani ya blanket na kuanza kuzungumza mengi katika kutaka kufahamiana zaidi.

Saa sita kasoro hivi usiku, Janeth alipitiwa na usingizi akiwa bado amelalia mgongo, nilijuwa baada ya kumuuliza swali fulani ili niendeleze stori niliyokuwa namsimulia lakini hakujibu, kugeuka ndio nikaona amelala hana habari. Nikamfunika blanket vizuri nami nikavuta upande wangu nikawa kama nimelala lakini nipo hadhiri masikio waruuu!

Saa tisa na nusu hivi usiku aliamka kwenda maliwatoni , nilikuwa macho bado maana sikutaka usingizi unipitie hata chembe ingawaje nilifunga macho.

Huwa nina kawaida ya kuamka asubuhi saa kumi na robo kwa ajili ya maandalizi ya siku pamoja na ibada za asubuhi lakini siku hiyo sikusikia alarm hadi saa kumi na moja haja ndogo iliponibana nikaamka na kuangaliaa saa! Nilishangaa sana. Janeth bado alikuwa amelala. Nikaenda maliwatoni na kujimwagia maji safi ya moto tayari kwa maandalizi ya kuendelea na safari. Nilivyotoka bafuni nilimkuta Janeth naye ameamka amekaa kitandani.

“Goodmonring Jane! Leo nimechelewa kuamka na wala sikusikia alarm ya simu…” Nilimsalimia na akajibu…

“Goodmornind Dad, pole kwa uchovu…”

Nje pilika za bodaboda zilikuwa zinazidi kuongezeka, bajaji na magari madogo maana tulikuwa kando kando tu ya barabara ielekeayo stendi.

“Kumekucha, kajiandae tusije tukachelewa…” nilimwambia.

“Bado kuondoka, saa kumi na mbili ndio basi litaondoka, muda bado hata hivyo ngoja nijiandae haraka haraka…” alisema.

Kama nilivyoeleza awali kuwa katika kuandika najaribu kunyoosha maneno yake angalau wewe unayesoma uelewe, lakini ilikuwa ni lugha gongana kwenda mbele ingawaje tulielewana kwa kuchanganya lugha zote mbili Kiswahili na Kiingereza.

Awali nilimuona Janeth kama ni aina ya wale wanawake wafanya biashara ambao wapo tayari ku ‘risk’ chochote ili mradi aingize hela hivyo nami nika ‘adopt’ uelewa ule ndio maana nikaomba nitumiwe hela ambayo hata haikuwa kwenye bajeti ya safari yangu. Uchumi wangu ulikuwa ni wa kawaida tu wa kujikimu ndio maana fursa hii ya kufanya kazi siku 90 DRC niliichangamkia.

“Uko mubaba muzuri, hujanisumbua…” alisema Janeth wakati akimalizia kujipamba.

“My period ended the day before yesterday but I’m not that clean for the game ndio maana nilikuambia nipo kwenye siku zangu…” Aliendelea kujisemesha.

“it’s okay Janeth, mimi wala sikuwa na mpango wowote na nilidhani ningelala kwenye basi, ahsante kwa ushauri wa kupumzika lodge…” nami nilijiongelesha.

Tulitoka pale huku akikataa mimi kuchangia gharama za lodge na chakula, lakini nikawahi kulipia bodaboda mbili ambazo zilitufikisha stendi saa kumi na mbili kasoro dakika kumi.
===

Kifungua kinywa tulipata Ushirombo ambapo pia walitumia nafasi hiyo kujaza mafuta kwenye basi, baada ya hapo moja kwa moja hadi Nyakanazi tulipoacha lami na kuanza njia ya vumbi na mashimo kuelekea Rusumo. Ni kilomita chache tu lakini tulitumia muda mwingi sana kufika border ya Rwanda na Tanzania.

Baada ya kukamilisha taratibu za border na kuvuka, nikaenda kwenye ‘restaurant’ upande wa Rwanda sasa ili nipate chakula, wakati huo Janeth yeye na wafanyabiashara wengine walikuwa wakikaguliwa mizigo yao hapo border ya ajili ya mambo ya ushuru nk. Alinirusuhu nikale maana huenda yeye angechukuwa muda mrefu kukamilisha zoezi. Ni kwamba hapo mpakani kwenye basi hushuka abiria wote na mizigo yote hushushwa ya kwenye buti na ndani ya basi na kila mmoja kupitia ukaguzi kulingana na mzigo wake kisha kwenda uhamiaji kama taratibu za kuvuka boda zilivyo.

“Nipatie mashilingi hayo nikupe faranga, ‘rate’ nzuri kabisa nakupatia…” alisikia ‘husler’ mmoja hapo nje ya restaurant.

Nilibadili dola mia kwake na nikamwomba anipatie kijana anayesajili line ya mtandao wa MTN ili nipate simcard ya Rwanda.

Zoezi la kuvuka hadi basi kuwa tayari kuondoka lilichukuwa zaidi ya saa tatu na kufanya tuwe nyuma ya ratiba ya kawaida ya basi. Abiria wengi walikuwa na mizigo ambayo ilikuwa na utata katika kuvusha lakini hatimaye wote tulifanikiwa kuvuka.

Baada ya kuvuka, dereva tuliyetoka naye Dar alipumzika kwenye siti namba moja na yule dereva wa pili, Mnyarwanda alichukuwa nafasi.

Sasa sijui kwa kuwa tulikuwa nyuma ya ratiba ama ndio uendeshaji wake, ee bwana ee, mwendo ulikuwa si wa kitoto, kuna wakati kwenye gps yangu speed ilisoma hadi 160kph ikabidi niinuke niangalie dashboard ya basi. Njia ilikuwa ya lami lakini nyembamba halafu basi lilikuwa linatembea upande wa kulia, kila mara nikajikuta nabana breki mimi ilhali siye ninaye endesha maana si kwa kuhisi hatari zile! Tena mpambe nilimsikia akisema amsha amsha!

Kabla ya kufika Rusumo, njiani kuna baadhi ya abiria washuka, mmoja tulimwacha pale kizuiani maana watu wa uhamiaji walimtuhumu ame ‘overstay’, wengine walishukia Lusahunga, Benaco na Mizani. Hivyo basi ilipata nafasi kiasi cha kupakia abiria wengine pale boda baada ya kuvuka. Mmoja wa hao abiria nadhani alikuwa wakala wapo ndiye alikuwa akihamasisha sana kuwa gari imechelewa.

Nilikuwa nadhani Rwanda mabasi hayakimbii kama nilivyosikia awali lakini ilikuwa kinyume chake hadi tuliposogea mbele mbele sana na giza likaanza kuingia ndip mwendo ukawa wa kawaida. Ni wastani wa kilomita 160 hivi kutoka Rusumo border hadi Kigali, lakini huwezi kuamini, tulifika saa tatu hivi usiku iwakuwa wakati tunakaribia mjini Kigali tukakuta foleni ndefu sana iliyotulazimu kutembea ‘jino moja moja’.

Safari ilichosa sana kipande cha Nyakanazi hadi Rusumo, tulitembea taratibu mno kwakuwa njia ilikuwa na mashimo na rasta baadhi ya sehemu, haikuwa njia rafiki kwa kweli licha ya umuhimu wake njia kuu hiyo. Nadhani sikuhizi pako vizuri, sijapita tena kwa barabara.

Janeth alinipa ofa ya kwenda kufikia kwao, ingawaje niliikataa na kumweleza kuwa mimi ni mpita njia tu naelekea Rubavu (nilimdanganya). Rubavu ni moja ya majimbo ya Rwanda jirani na Congo huko. Akaniambia basi kesho yake nisiondoke ili anitembeze Kigali kwenye ‘sabasaba’ yao. Focus yangu haikuwa kwenye kutalii bali kibarua kinachonisubiri huko Goma. Lakini nikaangalia kalenda nikaona bado nipo mbele ya muda na nina siku 4 mbele kabla ya kuripoti nikamkubalia ombi la kunitembeza Kigali.

Haikuwa mara yangu ya kwanza kuwepo Kigali lakini nilitaka nipate ‘experience’ nyingine kupitia huyu Janeth ambaye naona kama anataka kunizibia kufurahi na watoto wengine wa Kinyarwanda. Alikuwa anakaba sana kana kwamba tumekubaliana chochote.

Wajihi wangu ni bonge la mtu, mrefu futi sita hivi, maji ya kunde, heavy weight 105Kgs, ndevu zote mvi kichwani nimenyoa unga kuficha wingi wa mvi, nilivalia kawaida tu suruali ‘cadet’ na shati ‘cadet’ la mikono mirefu nililovaa Kahama maana kutoka Dar nilivaa ‘tshirt simple’. Sura yangu haijazeeka ingawaje ukiniangalia kwa makini ndio utaona kilomita zimeenda, hivyo nadhani nilikuwa naonekana bonge la Bwana. Yeye Janeth alibadili nguo zote pale Kahama, mimi suruali sikubadilisha. Alivaa gauni refu na mapambio yake.

Tulibadilishana namba za whatsapp na nikampa namba yangu ya MTN. wote tulishuka Nyabugogo bus terminal. Yeye Janeth alichukuliwa na pickup townhiace ambayo pia ilipakia na mizigo yake, mimi nikachukuwa TOYO (bodaboda) na kunipeleaka Kaizen Hotel ambayo haikuwa mbali na stendi.

Pamoja na mambo mengine, chumbani nilipokelewa na kitanda chenye godoro lenye ‘finishing’ ya material yasiyopitisha maji. Mawazo yakarudi kwa Janeth.

“Hawa si ndio mabingwa wa kurusha maji katika harakati za kilimo ya umwagiliaji!, kwanini nisitumie fursa hii kupata elimu ya watu wazima…” niliwaza. Nikaanza kuona saa haziendi. Kabla ya saa tano usiku kwa saa za Bongo nilikuwa nimeshaegesha, na usingizi haukuchukua muda kunipata kwa kuwa nilikuwa na uchovu uliotokana na usingizi wa mang’amng’am wa Kahama na uchovu wa safari. Nikakumbuka maneno ya Janeth kuwa nisilale kwenye basi nitachoka sana, nikaona kumbe alinishauri vyema ingawaje uchovu mwingi ulitokana na mimi kutolala vema kule Kahama.

Saa kumi na robo simu iliniamsha, nikachungulia nje bado giza sana, ikabidi nirekebishe saa yangu iendane na majira ya kule, hivyo nikarudisha dakika sitini nyuma. Nikaendelea kuegesha huku nikitafakari baadhi ya mambo. Usingizi ukanichukuwa tena hadi nilipostuka saa moja asubuhi kwa saa za Rwanda. Nikaamka na kujiandaa kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.

Restaurant wageni wenzangu walikuwepo wengi wakijihudumia kupata breakfast, nami nikaungana nao, wengi wao walikuwa wakiongea kinfaransa na baadhi Kinyarwanda. Wahudumu wa kike wa hoteli walikuwa kama wale tunaowaona kwenye mitandao lakini huko mitaani wanawake wengi sana ni wa kawaida tu tena wengine wala si warefu ama warembo kivile ama wenye maumbile hamasishi. Nikakumbuka ule usemi, ukitaka kuifaidi Kigali, fikia hotel zenye hadhi ya juu ama tembelea kwenye ma-‘shopping mall’ na sehemu kama hizo huko ndiko kuna vile vitu wabongo wengi tunababaikaGa navyo.

Wakati nikiendelea kupata staftahi nilipokea simu ya kwanza kwenye line ya MTN kutoka kwa Janeth, nilijuwa tu ni yeye maana namba bado sikuwa nimeigawa kwa watu wengine.

“…I will be at Nyabugogo terminal at ten thirty, lets meet at Trinity Bus office…” aliniambia.

Ilipofika saa nne kasoro kidogo nami nikakabidhi mzigo wangu mapokezi na kushuka chini kuchukuwa toyo ili inifikishe jirani hapo stendi. Saa nne na dakika chache nikaona nafwatwa kwa ishara ya kukumbatiwa, alikuwa na tabasamu na mwenye uso uliokunjuka.

Baada ya kumbatio motomoto pale na kupeana pole za uchovu akaniambia kuwa yeye hakai mbali sana na hapo, anaishi maeneo ya Kacyiru. Akaniahidi kunipelea kwao. Nikakubali. Lakini akaniambia tuelekee kwenye maonesho kwanza ili tuzunguke humo wee kisha ndio tuende kwao kisha kuzurura jijini Kigali.

Akaniambia tuchukuwe taxi.

“Nyamuneka utujyane i Magerwa…” alisema Janeth akimwambia yule dereva wa teksi atupeleke sehemu iitwayo Magerwa.

Dakika chache tu baadaye tukafika hapo Magerwa, ni kama vile bandari kavu fulani hivi, hatukuingia ndani badala yake akaniambia tutembee kuelekea upande uliouoneshea kidole.

“We are heading to Gikondo area, sio mbali ni paleeee…” alisema.

Kumbe hapo Gikondo ndio kuna sabasaba yao, tukalipa kiingilio na kuingia ndani. Pamoja na mambo mengine ya ki-‘trade fair’, nilikutana na visu hasa, yani Jane wangu nilimuona wa kawaida sana, ingawaje yupo vizuri kisu haswa lakini asikwambie mtu, macho ya wanaume hayachoki kuona vitu vizuri. Tulijifunza mengi humo na baada ya kuchoka tuka kaa sehemu kama mghahawa hivi mumohumo kwenye maonesho na kuanza kuongea mawili matatu huku tukipata viazi mbatata, maharage na samaki kama sato.

Baada ya hapo tulifanya mzungukowa pili ambao sasa huu ulilenga sehemu maalumu tulizoziona kwa ajili ya kununua baadhi ya bidhaa alizotaka nami nikaambulia kununuliwa mkanda wa ngozi pamoja na wallet kutoka kwa wafanyabiashara waliotoka Misri.

“Zawadi yako uwe unanikumbuka…” alisema Janeth.

Baada ya muda kidogo tulitoka tukiwa na mizigo yetu na kuchukuwa Taxi.

“…Kacyiru…” Janeth alimuambia yule dereva na tukaanza kuondoka.

Nilifurahia nidhamu ya barabarani ya madereva wa kule, yani madereva wote wa vyombo vya moto. Sheria za usalama barabarani zilikuwa zinafuatwa vyema.

Baada ya kona mbili tatu nikaona dereva akiuliza maelekezo ya ziada, alipopatiwa nikaona amekuja tena kona kadhaa kisha tukafika eneo tulivu lenye nyumba nzuri yenye ‘umatemate’ fulani hivi.

Nilikaribishwa vizuri na tulikuja kupokelewa na watu wengine mle ndani. Baada ya utambulisho mle ndani mwao kwa waliokuwepo tukaletewa chakula. Kulikuwa na ndizi nyama na vikorobwezo vingine, tukala huku tukiendelea na mazungumzo ya kawaidia.

Baada ya kama saa moja hivi akaniambia twende sasa nikutembeze Kigali. Tukatoka mle ndani, akawasha gari yake vw golf (baby walker) na tukaelekea katikati ya jiji moja kwa moja kwanza kwenye duka lake. Awali nilidhani ni duka dogo tu la wajasiri-amali, lakini kumbe dooo! Ni bonge la duka lililosheheni nguo za wanawake tu.

Alinitembeza kwa gari pale mjini, kisha kwa miguu hadi ilipofika saa moja jioni kwa saa za Rwanda tukarudi dukani kwake ili achukue gari turudi nyumbani kwao. Kwa kweli nilifurahia kubaki Kigali siku hiyo. Tulifika kwao saa mbili kasoro hivi kwa saa za kule na kukaribishwa. Safari hii nilikuta familia imeongezeka, yaani baba yake alikuwepo, mama yake, dada zake na kaka zake. Ilikuwa ni familia yenye furaha. Ilikuwa ni familia ya aina yake ambayo baba ni Mhutu na mama ni Mtutsi, ni familia ambayo imejaribu kuvuja jambo la ukabila katika nchi hiyo na Baba ni afisa wa Polisi katika Serikali ya Rwanda.

Niliwaza hapa nikijichanganya tu napata ndoa ya uzeeni, maana si kwa ukarimu ule sijui hata Janeth aliwaambia nini. Janeth alikuwa mtoto wa tatu kuzaliwa akitanguliwa na dada zake wawili kisha kufuatiwa na kaka zake wawili. Dada zake wote walikuwa wameshaolewa, lakini yeye na kaka zake walikuwa bado hawajapata ndoa. Baada ya chakula cha jioni, niliaga ili niwahi kupumzika maana asubuhi nilitaka nianze safari kwenda Gisenyi -Rubavu Province kama nilivyomuambia Janeth. Sikutaka ajuwe kama nitavuka mpaka na kuingia Congo kwa wakati huo.

Tulitumia gari ya Janeth hadi aliponifikisha Hotelini kwangu na nikamkaribisha hadi chumbani.

Dhambi iliyofuata nilishaitubu na ugomvi wake na Hamida ulishaisha maana hata yeye alifurahia elimu ya watu wazima niliyoipata huko Kigali niliporudi. Nilikuwa najuwa ‘katerero’ lakini hapa nilipata elimu ya ‘kuyanza’, sijui hata kama nimepatia inavyoandikwa. Ni hatari sana.

Katika kuitumia elimu hii ni muhimu wote muwe na afya njema vinginevyo mtaambukizana maradhi yatokanayo na kujamiiana (ngono). Ni kama vile katerero lakini hii tuseme ni katerero promax. Mtanisamehe, siwezi kuielezea hii hapa kwa sababu ya kuepuka matumizi mabaya ya hii kitu kwa wasiokuwa na ndoa.

“Usiondoke na basi za asubuhi, ondoka saa nne ili upate kupumzika vizuri…” yalikuwa maneno ya Janeth baada ya kumuomba anifundishe kilimo cha umwagiliaji kama kifanywavyo na wanyarwanda.

Nilipata elimu murua, na hakika wana haki ya kuweka sheria ya kila nyumba ya kulala wageni kuwekwe zile foronya zisizopitisha maji. Ewe kijana unayefikiria kuoa Mhaya ama Mnyarwanda, hakikisha unajifunza kilimo cha umwagiliaji maana kwao ni muhimu na haki ya msingi vinginevyo tarajia kutembelewa na kutambulishwa ndugu zake wa kiume usiowajuwa ama kuombwa safari ya kurudi kusalimia mara kwa mara alipotoka ili mradi tu kilimo cha umwagiliaji kifanyike.

Nilikubaliana na wazo lake la mimi kuondoka saa nne asubuhi, hivyo sehemu kubwa ya usiku nilikuwa darasani hadi maji yalipoamua kukatika kabisa, tukalala.

Saa nne na nusu tayari nilikuwa stendi kuu, pale kulikuwa na basi ziendazo Gisenyi, kila baada ya dakika kadhaa basi moja hutoka. Nilipanda RITCO, kampuni yenye huduma bora kabisa Rwanda ambayo baadaye nikaja kujuwa ni mpango mzuri wa viongozi wa Jeshi lao kubuni mradi huo. Safari ilikuwa nzuri na mwendo mzuri kwa sheria za kwao lakini nilikerwa na waendesha baiskeli ambao hushikilia malori kwa nyuma na kupata lifti hatarishi isiyo rasmi.

Kuna sehemu nimeshapasahu, tulipumzika kupata chakula kisha tukaendelea na safari. Yes panaitwa Nyirangarama, nimeona kwenye picha niliyopiga. Njia ni ya milima na mabonde, dereva huko inabidi awe timamu kuweza kuendesha bila kusababisha ajali. Takribani kilomita 150 kutoka Kigali nikaanza kuona ziwa upande wa kushoto, nilipouliza nikaambiwa ni ziwa Kivu, basi lilikuwa linashuka mlima taratibu maana kona ni kali mlima una mwinamo mkali lakini hatimaye tukafika Stendi kuu ya Gisenyi mpakani kabisa na mji wa Goma – Congo, Kivu Kaskazini.

Kwakuwa ilikuwa jioni, sikupenda kuvuka mpaka siku hiyo, bado nilikuwa nina siku mbili za ziada kabla muda wa kuripoti kibaruani. Hivyo niliamua kutafuta sehemu nzuri ya kupumzika. Baada ya kuuliza wenyeji sehemu ya bei nafuu lakini patulivu na usalama mkubwa ndio nikaaelekezwa sehemu Fulani wanapaitwa kwa Mapadri. Nikachukuwa bodaboda hadi huko. Ile sehemu ni kama Msimbazi centre ya Dar es Salaam. Wana rest house nzuri na tulivu sana. Hapo ndipo akili ya kazi ikaanza kurudi upya maana nilitulia na kuanza kutafakari kibarua ninachokiendea.

Ilikuwa siku ya Ijumaa jioni nikiwa hapo kwa Mapadri, nikapata wasaa wa kutembea kwa miguu hadi ufukweni mwa ziwa Kivu sehemu ambapo watu hupenda kutembelea jioni kama vile Coco beach ya Dar. Hapo uzalendo ukanishinda ikabidi niingie kuogelea na kuchanganyika na wenyeji lakini sehemu ya upande wa watu wazima maana kama vile watu walijigawa, hapo nikakutana na visu vingine hatari. Pia kulikuwa na boti kadhaa za wajasiri-amali ambao walikuwa wanapiga debe ili wapate wateja wa kuwatembeza ziwani kwa ujira wa fulani (dola 10).

Siku yangu iliisha vizuri na giza lilipoingia nilitembea kurudi kiotani kwangu hapo kwa Mapadri. Baada ya chakula cha jioni ambacho nilikipata jirani na hapo kwa Mampadri nilirudi chumbani na kuendelea kuandika simulizi ya Hamida nikisogeza ‘episode’ kuwapunguzia arosto wafuatiliaji wa kila siku mwaka huo. Baadaye nikaanza kupitia yanayohusu kinachonipeleka Goma kwa kuhakikisha nimehabarika ipasavyo kufikia tarehe ya siku hiyo.


INAENDELEA…
ERoni sasa nimeelewa kilimo cha umwagiliaji ulichomaanisha!!
Ile kitu nyieeeee nyieee🙌🙌🙌!!
 
Na huko kanda yenu ndio nasikia ipo mito na chemchemi za kutosha sana kwa kilimo cha umwagiliaji🤣🤣
Hii kanda ya wenye nayo Eroni afu sijui huwa kuna siri gani huku!! Sijui ni vyakula labda!!
Nilianza hekaheka nikiwa form 6 ila miaka yote hio umwagiliaji nilikuja kuukuta huku baada ya kuajiriwa yule Mwamba siwezi msahau😎!!
 
Hii kanda ya wenye nayo Eroni afu sijui huwa kuna siri gani huku!! Sijui ni vyakula labda!!
Nilianza hekaheka nikiwa form 6 ila miaka yote hio umwagiliaji nilikuja kuukuta huku baada ya kuajiriwa yule Mwamba siwezi msahau[emoji41]!!
Kwa hiyo chemichemi bado ipo au baada ya kumalizana na mwamba nayo ikajiondokea zake
 
Kwa hiyo chemichemi bado ipo au baada ya kumalizana na mwamba nayo ikajiondokea zake
😊🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️
 
(iii). Cute Eyes – Macho mazuri ‘analia’ juu ya mapenzi.


Bosio ni mtoto wa pekee katika uzao wa tumbo la mama yake, hana kaka wala dada na baba yake alishafariki wakati akiwa mdogo. Baba yake alikuwa ni kabila la wabembee na mama yake ni kabila la myombe. Ilikuwa familia yenye maisha ya chini, baba yake alifariki migodini huko katika harakati za kutafuta ugali wa mke na mtoto wao wa pekee.

Ingawaje Bosio alikuwa katika maisha ya dhiki lakini uzuri wake haukujificha ukichagizwa na macho yake mzuri hata wazazi wake waliliona hilo tangia utoto na kumpatia jina la Beaux yeux, aka Bosio. Mama yake alimlea kwa shida binti yake ili apate masomo vizuri na kwa kudra za mwenyezi Mungu Bosio alimaliza masomo ya sekondari.

Katika kupitapita akakutana na kijana ambaye alikuja kumuoa na kuzaa naye watoto wawili mmoja wa kiume na mwingine wa kike. Mume wake huyo alikuwa ni askari ya jeshi la nchi yao na katika harakati za kuilinda nchi alifariki kishujaa akiwa kazini. Faraja kwa Bosio ikawa na wale watoto na mama yake. Kwakuwa mume wa Bosio alikuwa katika ‘mission’ ya kimataifa, alipata kifuta machozi kiasi fulani cha fedha ambacho sehemu ya hiyo hela ndio alianzisha biashara ya kunua na kuuza vitenge jijini Kishasa. Biashara zake ziliendelea vizuri kwakuwa Bosio alikuwa na nidhamu ya hela na historia ya hali ngumu kulikomfanya azidi kuwa makini katika kila jambo ili awatunze watoto na kumlea mama yake kipenzi.

Katika harakati za biashra ndipo alikutana na mpenzi huyu sasa aliye muumiza kiasi cha kutotamani tena kusikia neno mapenzi.

“…tulikalaga naye tunatumikisha biashara mzuri lakini kumbe mwenzangu ako na mambo ya mingi… “ ilikuwa na sehemu ya maelezo ya Bosio.

Kwanza jamaa huyo alikuwa Mario, yaani alikuwa hapendi kujishughulisha kutafuta bali alikuwa akimtegemea Bosio kwa kila kitu, alikaa kama kupe. Pili alikuwa anatembea na wanawake wengi…

“…aliikala kwangu, akawa mupinki muzuri lakini akaanza kutomboka tomboka juu ya madamee wengine…”

“…Kuna siku moya nimetoka Bukavu nikamuta ako na madamee mwingine mu nyumba yangu bako banabukana…”

“…iiii nililia siku hiyo na kumfukuza atoke ku nyumba yangu aendage…”

“…aendage tu iko na mambo ya mingi sana…” kilio kikaanza…

Hapa ilikuwa ni pale sleep in hotel Kariakoo Dar akinihadithia, ndipo akaweka kichwa chake kwenye bega langu na kuangua kilio tena chenye kwikwi.

Baada ya kubembelezana, peleka moto kidogo na kurudi kawaida akaendelea kusimulia…

“..Ndo vile nikaamua basi tena, nitakaa peke, juu nimeishi maisha magumu tangia niko mudogo, kila siku kunidanjere danjere nimechoka!...”

“…Alitoka na baadhi ya faranga zangu, sikujali, nilitaka atoke tu aende, yani aende!...”

“…Ndiyo nikaanza kupiganisha biashara ya vikwembe (vitenge), nikaanza kuchukuwa vikwembe vyenyewe vya byee ndio niko nakuza mutaji na sasa naweza kamata kontena moja peke ndio napiganisha biashara iende muzuri…”

Tangia apate pigo hilo aliamua kupambana, na hakika amefanikiwa katika kupambana kwakuwa hakuwa na mambo mengi tena, yeye na mama yake na watoto wake akisomesha katika shule nzuri huko Kinshasa.

Nikampachika swali la kizushi.

“Sasa Bosio, unakula unashiba, viungo vingine havisikii njaa?!”

Baada ya kulielewa swali alicheka kisha akajibu ya kuwa anajisaidiaga mwenyewe, hapati magonjwa wala ‘stress’.

Ukimya ulitawala na hatimaye tukajaribu kumwagilia bustani kwa maji hafifu ‘though’.

Nikawa kama nimechokoza vilivyo lala ingawaje sikuwa na mpango wa kuchonga mzinga bahati nzuri muda wa yeye kusafiri ndio ulikuwa umefika na tulimsindikiza na Hamida airport kama nilivyoeleza huku nyuma.
===



ITAENDELEA…



(fupi fupi tamu eee)
Eendiwo mkuu fupi fupi tamu sana!!

Namuona Bosie mutoto ya Kinshasa!

"Kutomboka tomboka" Kweli language is arbitrary!!
 
Nakadori dear njoo umalizie kuisoma hapa mwishoni ni fupi fupi ila mzee amezipiga bana!!😊

NB: Janet na Bosio wako Wako vizureee mkuu simulizi muzuri na tamu !.
Big up✌️✌️✌️
Leo usiku kama sitabanwaa ntaitafutia usingizi hii
Asante unaniita kwenye utamu utamuu😋😋😋😋😋😋😋
 
Back
Top Bottom