Hela zimesharudi mtaani?

Hela zimesharudi mtaani?

Moja ya malalamiko ya kipumbavu kabisa yaliyokuwepo enzi za utawala wa Rais Magufuli ni kuwa eti hela hazikuwepo mtaani.

Sijui ni lini hasa Tanzania hii ambapo hela zilikuwepo bwerere mtaani! Kwa sababu, Tanzania ni nchi maskini. Ni nchi ya ulimwengu wa tatu...
Hata kama mtu unapesa hauwezi kukubali kuranguliwa.

Ukitaka kujua pesa ipo mtaani au lah basi angalia kasi ya ujenzi , idadi ya watu kwenye shopping malls /super markets /local markets etc
 
Magufuli anatekeleza sera za Chadema .....huyu hafai hela zote anapeleka kwenye miradi, miradi yenyewe hasara tupu! Sasa ndege nani atapanda! Alafu analipa cash, si angekopa tu! Stendi ya mbezi ni ovyo italeta foleni kubwa! Magufuli ni dikteta amekataza siasa! Flyovers zipo Kenya zile za Magufuli hamna kitu!

Haya mzee wa watu kapumzika, shangwe likaibuka, kwisha Mataga, Sukuma gang watakoma! Mama achana na miradi ya Magufuli haina maana! Mama anaupiga mwingi! Mama anafungua uchumi! Sasa nchi inapumua, tuko huru kukosoa na kufanya siasa.

Sasa hivi, tuone mataga na sukuma gang wakisema Mama anaupiga mwingi ni block tu, Mama ni dikteta wa kike! Hata Magufuli hakuwahi kutufungulia mashtaka ya ugaidi! Huyu Mama ndio atakuwa the worst President ever!

Dah! Haya maneno yote yanasemwa na watu wale wale!



Two wrongs don't make a right - Kubutua kwa Maza hakumsafishi JIWE.
 
Kuziona fedha mtaani huwezi kuziona kama unavyoona chupa za maji zilizotumika au karatasi. Bali yafuatayo ndiyo kisababishi;

1. Serikali ikilipa madeni ya ndani (local creditors). Kumbuka Mwendazake alisema anakakiki madeni ya ndani na akawa halipi. Wanaoidai Serikali wakilipwa nao watawalipa wanaowadai.

2. Mabenki kuongeza kasi ya kukopesha fedha kwa wenye miradi. Wakati wa Mwendazake Mabenki yalipunguza Imani kwa wakopaji kwa kuwa Serikali ilikuwa inaweza kuwanyang'anya fedha wakati wowote.

3. Wenye fedha kuzipeleka Benki. Watu wengi waliwekwa nje ya nchi na wengine walichimbia chini fedha kwa kuwa Serikali ya Mwendazake ilikuwa inaweza kuangalia akaunti ya mtu na kumfungulia mashtaka au kuzinyang'anya.

4. Wawekezaji wa nje wanapoanzisha miradi. Wakati wa Mwendazake hakukuwa na miradi mipya ambayo ingetengeneza ajira.

5. Kukuza biashara ya nje. Biashara ya mahindi na mbao kwenda Kenya ilikuwa imesimama. Kwa hatua za kuruhusu biashara mipakani mzunguko utaendelea.

6. Mwananchi mwenyewe kujihusisha na uzalishaji mali/ huduma kwa kuwa hakuna mtu anagawa fedha mtaani.

Katika hayo siyo rahisi kuyaona katika kipindi cha mwezi mmoja bali ni kipindi cha miezi 9 hadi mwaka.
 
Hata kama mtu unapesa hauwezi kukubali kuranguliwa.

Ukitaka kujua pesa ipo mtaani au lah basi angalia kasi ya ujenzi , idadi ya watu kwenye shopping malls /super markets /local markets etc
Watu walipunguza kwenda magengeni wakati wa Magufuli?
 
😂😂😂😂😂
Moja ya malalamiko ya kipumbavu kabisa yaliyokuwepo enzi za utawala wa Rais Magufuli ni kuwa eti hela hazikuwepo mtaani.


Sijui ni lini hasa Tanzania hii ambapo hela zilikuwepo bwerere mtaani! Kwa sababu, Tanzania ni nchi maskini. Ni nchi ya ulimwengu wa tatu.

Vipato vya wananchi wake ni vya chini sana. Si nchi nyingi ambazo nchi yetu imezipita kwa vipato vya wananchi.

Na tumekuwa nchi ambayo wananchi wake ni wa kipato cha chini tokea tuwe taifa na nina uhakika kabla hata ya kuwa taifa.

Lakini katika utawala uliopita tuliaminishwa mzunguko wa hela umebanwa na hivyo kupelekea kutokea upungufu wake mtaani/ mitaani.

Baada ya kumpata huyu Rais wetu mpya, aliye mpole na msikivu, mwenye kuongea Kiingereza kizuri kabisa 😉, tukaambiwa sasa mzunguko wa hela utarudi na hela zitakuwepo mtaani kama ilivyokuwa kabla ya kuja kwa dikteta Magufuli!

Sasa niaje raia? Mama kesharudisha hayo mahela mitaani?

Kama hayo mahela yamesharudi mitaani kwa nini mnalialia kuhusu vijitozo vya shilingi 100 mtumapo hela kwenye Em Pesa?

Kwa mnaojua hayo mahela yalipo, msiwe wachoyo. Tauambieni na sie wengine tuje tuyaokote bana.

Vilivyo vizuri kuleni na sie ndugu zenu.

Tuendelee kuupiga mwingi 😉.
 
Watu walipunguza kwenda magengeni wakati wa Magufuli?

Enzi za jiwe malalamiko fedha hakuna yalikuwa mengi sana ukilinganisha na sasa , mimi ni fundi ujenzi ,nimejaribu kufanya mizunguko sehemu mbali mbali ,watu wameanza kujenga sana maybe inachangiwa na serikali kupeleka huduma za kijamii hivyo mtu anaona bora ajenge aachane na kupanga!
 
Moja ya malalamiko ya kipumbavu kabisa yaliyokuwepo enzi za utawala wa Rais Magufuli ni kuwa eti hela hazikuwepo mtaani.

Sijui ni lini hasa Tanzania hii ambapo hela zilikuwepo bwerere mtaani! Kwa sababu, Tanzania ni nchi maskini. Ni nchi ya ulimwengu wa tatu.

Vipato vya wananchi wake ni vya chini sana. Si nchi nyingi ambazo nchi yetu imezipita kwa vipato vya wananchi.

Na tumekuwa nchi ambayo wananchi wake ni wa kipato cha chini tokea tuwe taifa na nina uhakika kabla hata ya kuwa taifa.

Lakini katika utawala uliopita tuliaminishwa mzunguko wa hela umebanwa na hivyo kupelekea kutokea upungufu wake mtaani/ mitaani.

Baada ya kumpata huyu Rais wetu mpya, aliye mpole na msikivu, mwenye kuongea Kiingereza kizuri kabisa 😉, tukaambiwa sasa mzunguko wa hela utarudi na hela zitakuwepo mtaani kama ilivyokuwa kabla ya kuja kwa dikteta Magufuli!

Sasa niaje raia? Mama kesharudisha hayo mahela mitaani?

Kama hayo mahela yamesharudi mitaani kwa nini mnalialia kuhusu vijitozo vya shilingi 100 mtumapo hela kwenye Em Pesa?

Kwa mnaojua hayo mahela yalipo, msiwe wachoyo. Tauambieni na sie wengine tuje tuyaokote bana.

Vilivyo vizuri kuleni na sie ndugu zenu.

Tuendelee kuupiga mwingi 😉.
Zirudi wapi. Soon wataanza kumkumbuka Magufuli wasimpate. Hakuna taifa lenye fedha mitaani zaidi ya uvivu na ukosefu wa ubunifu.
 
Enzi za jiwe malalamiko fedha hakuna yalikuwa mengi sana ukilinganisha na sasa , mimi ni fundi ujenzi ,nimejaribu kufanya mizunguko sehemu mbali mbali ,watu wameanza kujenga sana maybe inachangiwa na serikali kupeleka huduma za kijamii hivyo mtu anaona bora ajenge aachane na kupanga!
Huu uongo sijui unasaidia nini
 
Sijui maana alishanipiga block kitambo , imagine mtu anatembeza block kwasababu ya hoja kinzani hapo hawezi kuamrisha Polisi! Hilo sikutegemea kabisa kwa mtu wa aina yake! Baada ya hapo nikala [emoji724] ya Jasusi Chahali [emoji38]
Wanaharakati wanapiga block sio mchezo, kupinga hoja yake ni tusi kwake.

Alafu wanataka uhuru wa kujieleza. Wapumbavu sana wale watu.
 
Hela zipo angalau watu sasa wanajenga, nendeni site huko mkaone mijengo ya maana, we kutwa upo mtandaoni kuanzisha vi thred uchwara utabaki kama ulivyo kuwa chawa tu,

Mama anaupiga mwingi
Hili la ujenzi upo sahihi kabisa. Mafundi ujenzi wengi walihamia kwenye kuendesha bodaboda....

Hivi sasa sura zao zinaota nuru...
 
Waliotupumbaza kumpinga JPM na harakati zake kwa mazingira yanavyoonekana wanakutana na hela ila sisi pangu pakavu mazingira yamekuwa magumu zaidi kuliko awali maana jamaa wanataka kufidia hasara ya miaka 6 ndani ya muda mfupi.
JPM angevumiliwa walau miaka 5 tena nchi ingebadilika walau kwa asilimia kadhaa kuliko sasa ambapo tunarudi nyuma kwa kasi.
Tulidanganywa na siasa uchwara za mitandaoni tukamkatisha tamaa jpm.
Kauli ya jpm kuwa matajiri wataishi kama mashetani ilimaanisha matajiri wetu wengi ni wezi hivyo alikuwa anaitaka pesa ya umma kufanyia shughuli za umma.
Hakika tulimuelewa vibaya yule mzee.
 
😂😂😂😂😂
Niliona hicho alichosema Mwigulu!

The guy is an idiot.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Huu uongo sijui unasaidia nini

Uongo gani Mkuu? Watu wengi wanajenga sana mkuu ,sehemu nazopitaga serikali inaweka miundombinu ya maji ,umeme na barabara kwa kasi kubwa sana! Enzi zetu tunakua maji tulikuwa tunafata zaidi ya 6km ila sasa maji yapo sebuleni,yapo washroom etc.

2016-2018 watu walikuwa hawajengi ,mafundi wengi tulipiga mihayo.
 
Enzi za jiwe malalamiko fedha hakuna yalikuwa mengi sana ukilinganisha na sasa , mimi ni fundi ujenzi ,nimejaribu kufanya mizunguko sehemu mbali mbali ,watu wameanza kujenga sana maybe inachangiwa na serikali kupeleka huduma za kijamii hivyo mtu anaona bora ajenge aachane na kupanga!
Malalamiko ya watu si lazima yaakisi uhalisia wa mambo.

Wengine kulalama ni jadi yao tu hata iweje.
 
Kuziona fedha mtaani huwezi kuziona kama unavyoona chupa za maji zilizotumika au karatasi. Bali yafuatayo ndiyo kisababishi;

1. Serikali ikilipa madeni ya ndani (local creditors). Kumbuka Mwendazake alisema anakakiki madeni ya ndani na akawa halipi. Wanaoidai Serikali wakilipwa nao watawalipa wanaowadai.

2. Mabenki kuongeza kasi ya kukopesha fedha kwa wenye miradi. Wakati wa Mwendazake Mabenki yalipunguza Imani kwa wakopaji kwa kuwa Serikali ilikuwa inaweza kuwanyang'anya fedha wakati wowote.

3. Wenye fedha kuzipeleka Benki. Watu wengi waliwekwa nje ya nchi na wengine walichimbia chini fedha kwa kuwa Serikali ya Mwendazake ilikuwa inaweza kuangalia akaunti ya mtu na kumfungulia mashtaka au kuzinyang'anya.

4. Wawekezaji wa nje wanapoanzisha miradi. Wakati wa Mwendazake hakukuwa na miradi mipya ambayo ingetengeneza ajira.

5. Kukuza biashara ya nje. Biashara ya mahindi na mbao kwenda Kenya ilikuwa imesimama. Kwa hatua za kuruhusu biashara mipakani mzunguko utaendelea.

6. Mwananchi mwenyewe kujihusisha na uzalishaji mali/ huduma kwa kuwa hakuna mtu anagawa fedha mtaani.

Katika hayo siyo rahisi kuyaona katika kipindi cha mwezi mmoja bali ni kipindi cha miezi 9 hadi mwaka.
Big up mkuu..na jiwe pia ikumbukwe hakuajiri..so kuongeza hata lower to middle income peoples hakukufanyika kwa kipindi chake..huku nako kunapafanya mtaani kuwe pagumu.
 
Back
Top Bottom