Hersi ametisha Sana supu ni tamu Sana ukinywa baada ya kupiga khamsa Makolokwinyo ila kwangu Mimi bado Hersi hajamaliza kazi.
Bado tunamtaka Eng Hersi amsajili Kibu Denis awe mwananchi ili kuizika rasmi Simba! Goli la kichwa alilotufunga mbele ya ukuta wa Berlin wa Yanga derby ya juzikati ni goli classic ila kosa lake ni kutuchokoza kwa kutoa ishara ya kutufunga mdomo Simba wakala khamsa 5G! Hivi Sasa jezi wanapigia deki!! Ukisema khamsa unakula makonde jamaa wamejaa sumu!! Hersi Mtu mbad sana eti ye alitaka Makolokwinyo wapigwe goli tano tu japo wachezaji walimwambia wana uwezo wa kuigeuza Simba ile kuwa Simba Queens na kuitungua goli za netiboli kuanzia tisa hadi dazeni 12!! Eti waliwaonea huruma tu kwa zile khamsa!!
Imagine na Yanga hii ya moto Kibu awe pale mbele na Max Nzegeli na Ki Aziz, Simba wangekula wiki (7-0)!