Acha jazba na ubaguzi wa rangi....hii haiusiani Na rangi hata kidogo...
Kuhusu cancer nimetumia miaka saba kusoma hayo makitu kaka Na hata navyoandika ujumbe huu namalizia zamu yangu wodi ya watoto wenye kansa...so hamna jipya la Zaidi utakalonieleza kuhusu hilo
Natumia simu ila nikipata muda tutajadili tu kwa faida ya wote hata Na mimi pia...elimu ni pana sana na kubali hufahamu kila kitu ndio utajifunza...
Nini kutibu Kansa kaka...babu wa kikombe alitibu mpaka na ukimwi...��
Hivi unajua kuna some sort of cancer huwa zinapotea tu bila tiba ? Nitarudi tupeane shule.....hizo hizo alternative medicine zina hadi degree marekani tena doctorate kabisa kama MD ila hujiulizi mbona hospitalini watu hawapungui ? Nitarudi kaka
Mtu aliyeaminishwa kuwa usiku ni mchana na mchana ni usiku akiambiwa tofauti atakuwa mkali ajabu, tatizo ninaloliona hususan kwa wataalamu wetu wa afya tena wengi wa kiasi cha kutosha ni kukariri na hawafikiri nje ya box.
Nakumbuka wakati fulani niliwahi kuweka malalamiko yangu hapa kuhusu watalaamu wetu wa tiba pale Muhimbili kutokana na kukosa maadili baada ya kumtumia mgonjwa wangu kufundishia bila ridhaa yangu wala ya mgonjwa mwenyewe, lakini badala ya kukiri makosa waliitana hapa na kujaribu kujitetea kijinga kabisa mpaka nikashangaa na kjiulza weledi wao uko wapi!
Si kwamba ni makampuni ya madawa pekee yanayonufaika na afya zetu, hata hawa wataalamu wetu wa afya wenye tamaa ya fedha wanatumia ujinga wa watanzania wachache wasioweza kuhoji weledi wao pale wanapoandikiwa dawa ambapo wamegeuza afya zetu kuwa chumo ili kujinufaisha kiuchumi.
Sasa akijitokeza mtu mwenye weledi wa kile walichokisoma akatoka nje ya box na kuwaelimisha wengine ndiyo utawaona wanakuja na kutokwa na povu, kisa anahatarisha maslahi yao.
Kupitia kansa kisukari, Ukimwi na sasa hivi figo wanapata safari za nje na Per Diem a kutosha kwa kuhudhuria makongamano ya tiba na warsha mbalimbali achilia mbali mishahara minono na marupurupu.
Anachokieleza mkuu
Deception si kigeni sema tu Watanzania ni wavivu wa kusoma na kufanya utafiti lakini kama ukiingia mtandaoni unakuta kila kitu, na awali kabisa hawa wataalamu walioamua kusema ukweli hususan nchini Marekani wengine walifungwa jela.
Wachina wana msemo mmoja kwamba ukitaka kusema ukweli jiandae kukimbia..... Kwa hiyo sishangazwi na mashambulizi anayoapata mtoa mada kwa sababu anagusa maslahi ya watu.
Mkuu endelea kuwafumbua Watanzania macho na hao wanaotaka MODS wafunge huu uzi hilo halitotokea kwa sababu MODS wa JF hawafanyi kazi kwa maslahi ya kundi fulani.....
Kwa kujielimisha fungueni hiyo link hapa chini.....
100 Years of Suppressed Cancer Cures Finally Revealed...