Hidden cancer cures


Hapa utapiga kelele hadi utachoka. Watu waliokata tamaa hasa watanzania wanapenda kusikia uongo kuliko ukweli.........hii ni thread yake ya pili . Ya kwanza amesema ukimwi hauambukuzwi na sex . Pia ana uwezo wa kuutibu. Now same thing anaongelea kansa kwamba dawa wazungu wameficha. Sasa jiulize wanaokufa na kansa wengi ni wazungu . So wamejifichia dawa.
 

Basi wewe chagua moja tu, kumsikiliza mzungu ama kumsikiliza Mtanzania mwenzio, chagua moja na hiyo haki unayo wewe mwenyewe ya kuchagua...!
 
Huyu sio kwamba sijamsikiliza, nimesoma kila kitu alichoandika na hakuna evidence yoyote ile,....

Wewe utakuwa na matatizo sana,Je,ulihitaji evidence halafu hukupewa?


Wewe utakuwa na uelewa mdogo sana wa mambo yanayoendelea duniani na hasa kwenye suala hili la cancer.Unachukulia mambo juujuu sana,kibaya zaidi huna hata haja ya kuhitaji kuhoji anachosema mwenzako,unang'ang'ania kile unachokijua tu.Usichukulie mambo kirahisi hivyo,kuna elimu nzito ambayo unai under-estimate bila kujijua,fungua milango ya akili yako kwanza ndipo nitakapokuwa tayari kujadiliana na wewe,vinginevyo unaweza kubaki na kile unachokijua,sitakulazimisha.

Nikikuuliza je,unaijua Sloan Kettering vizuri?Najua lazima swali hili litakutupa nje ya fence.Nikikuuliza pia je,unaijua historia ya modern/western medicine imeanzia wapi?nje ya fence.Nikikuuliza, unajua nini kilipelekea kutungwa kwa sheria iliyofanya bangi iitwe haramu?nje ya fence.Nikuuliza, unajua ni magonjwa gani ambayo mwanzoni watu waliyachukulia kama infectious disease kwa miaka mingi lakini baadaye yakagundulika kuwa ni deficiency diseases?nje ya fence.Nikikuuliza,unajua kama amygdalin/laetrile,bangi,sodium bicarbonate,.... zimeshafanyiwa utafiti muda mrefu kwamba na zina uwezo wa kutibu cancer?nje ya fence.Nikikuuliza,unajua kwamba hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kutangaza tiba ya HIV/AIDS(pamoja na ufeki wake) na cancer hadharani, na akigundulika na taasisi za magonjwa hayo anachukuliwa hatua kali?nje ya fence.

Usichukulie mambo kirahisi hivyo,soma ujiokoe na utaumwa huo ulionao.Mimi ndio nimeleta mada,kwa nini hutaki kuendelea kujibizana na mimi na badala yake unakimbilia kujibizana na wachangia mada?Kama kweli unajiamini kwamba unajua mambo kwa nini mjadala usiwe kati ya mimi na wewe?

....Soma anything science related utaona jinsi gani science haina utani, ni years of research, fixing errors, finding solutions, hakuna speculations huku ni real facts.

Haya maneno mimi ndio nastahili kuyasema,sio wewe.Na usifikiri kwamba western medicine wanatumia real science kwenye magonjwa yote uliyoyasikia,magonjwa sugu yanayowaingizia pesa nyingi huwa hawatumii real science ya magonjwa hayo,kwa kuwa wakitumia real science hautapita muda mrefu tiba zitakuwa zimeshagundulika(of-course nje ya mainstream tayari tiba zipo) na kuwafanya wapate hasara kubwa.Science ya AIDS na CANCER imeshajulikana miaka mingi iliyopita na wanasayansi walio nje ya mainstream,wewe hujui kwa sababu huwezi kuambiwa darasani na mwalimu wako hajui,pia kwenye vitabu vyenu haijaandikwa.

Ondoa attitude uliyonayo ya kupinga kila kitu kipya kinachokuja mbele yako,je,angesema Obama ungepinga?Usifikiri kwamba mambo haya yako kirahisi kama ujuavyo.Vipi kuhusu ushoga,Obama yuko sahihi eenh?Vipi kuhusu uzazi wa mpango kwa kutumia vidonge je,uko poa eenh?Watoto wachanga kumeza ARVs je,iko poa eenh?Je,uliwahi kusikia kuhusu dawa za kupona ushoga(homofin)?ziko poa eeenh?Nadhani mimi ndio nitakuwa sina akili eenh?Wewe unaonaje?Unaonaje kama huna hoja za msingi basi uwaachie wengine waendelee kupata elimu hii ambayo hawawezi kuipata kutoka mainstream?
 

wewe utakua na benefit na industry medicine,hivyo lazima utetee,na kwa taarifa yako hao wazungu watengeneza dawa hawabagui wa kuumua as long kama umeingia kwenye teritory yao u r going, wewe utakua someone madabida u r in a circle,mnaua watu kengeblue
 
Mkuu Deception kumbe ukichokozwa unatema madini zaidi duhh,maana ni balaaa.

Sijui na mimi nihamie timu yao kina viroboto na magauni!!!!

God bless you

Hahaahahha Dawa Za Kutibu Mashogaaa Daaaah halafu Hapo hapo wanakampeni za Kuhamasisha Mashoga Wajitokezee
 
Nimefuatilia nyuzi mbili za Mr.Deception nimejifunza kitu.
Ninaona itakua vyema kwa wanaompinga kukaa chini na kubaini ukweli.
Mr hayupo hapa kufanya biashara na haiwezekani kupoteza muda wake kuandika nyuzi kwa ajili ya kuwapotosha watanzania wafe na hayo majanga,Kwani anapata faida gani?
Ebu ikiwezekana kaeni chini mfanye utafit kuhusu hayo anayoyaeleza.Ikiwezekana mfanye nae mazungumzo na ndipo mtagundua kuwa ayasemayo ni ya Uongo au lah.
Ahsante Mr.D
 
Last edited by a moderator:

Una uhakika gani hayuko kibiashara . Hivi kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kupoteza muda wake na bundle lake kucheza. Hivi unajua hata babu wa loliondo alisema hafanyi biashara. Coz hapa hatujui kuna waathirika kibao anaongea nao inbox. Ndugu fungua akili. Usiamini kila ukisikiacho au kukiona
 
Last edited by a moderator:
unachosema huna uhakika nacho kupe maana unahisi tuu. na una uhakika gani kama yupo bongo anatumia bundle zetu za tigo au airtel..?
 
Last edited by a moderator:

Kwani hivyo alivyovitaja kwamba ni dawa si vitu vya kawaida vinavyoweza patikana katika mazingira yetu?Mbona ameeleza mazingira ya upatikanaji wake.Kama wewe ni Daktari waweza fanya kitu juu ya hili kwa uhakika zaidi na kuja kutupa uhalisia wa mamb😵K tuishie hapo Ndugu.Lakini nadhani sijashauri ujinga.
Ahsante
 
unachosema hakika uhakika kupe maana unahisi tuu. na unq uhakika gani kama yupo bongo anatumia bundle zetu za tigo au airtel..?

Sijazungumzia bundle,nimezungumzia muda..na kama yupo kwenye biashara tungeshajua..Nina uhakika anapata PMs nying zaid ya replies katika post zake.
Watu wangemueka wazi,kuna watu ambao wanamtumia PMs just kupima anachosema kama ni kweli au lah.Yeye mwenyew anaweza akawa shuhuda wa hili.
Binafsi,nilishapata wasiwasi kuhusu madawa haya ya kizungu.Kwa hiyo ni kitu ambacho sio kipya sana kuingia katika kichwa changu.(Jua kuna michezo mingi tunachezewa bila kujua)
 
Last edited by a moderator:
Samahani ndugu yangu comment yangu ilikuwa nimemlenga kupe anayedai ya kuwa mleta mada yupo kibiashara. kuhusu mjadala unavyoendelea mimi sina shaka na ukweli unaotolewa na Deception.
 
Last edited by a moderator:
Samahani ndugu yangu comment yangu ilikuwa nimemlenga kupe anayedai ya kuwa mleta mada yupo kibiashara. kuhusu mjadala unavyoendelea mimi sina shaka na ukweli unaotolewa na Deception.

Ndio Ndugu,nimejaribu toa ufafanuzi zaidi.Usijal tupo pamoja.
 
Last edited by a moderator:

Kuhusu bangi,nitatoka kidogo nje ya mada kwa kuwa nataka kuzungumzia jambo muhimu sana ambalo ni vyema mkalijua pia.

Mojawapo ya mambo muhimu sana duniani ni NISHATI/ENERGY.Hakuna mtu yeyote ambaye anapingana na hili.Sasa hivi tunasikia vita kubwa maeneo mbalimbali ya dunia yetu,sababu mojawapo kubwa inayosababisha vita hivyo ni vyanzo vya nishati kama vile petroleum/crude oil/gas.Petroleum ni mojawapo ya malighafi inayotumika kuzalisha DIESEL na PETROL.Kwa hapa nitazungumzia DIESEL.

DIESEL ni mojawapo ya chanzo cha nishati kitumikacho maeneo mbalimbali ikiwamo vyombo vya usafiri na mitambo ya kuzalisha umeme.DIESEL huweza kupatikana baada ya kufanya utaratibu wa kikemikali kutoka kwenye PETROLEUM,SYNTHESIS GAS na ANIMAL/PLANTS/VEGETABLE OIL.Hivyo kutokana na utaratibu wa upatikanaji wa DIESEL,tunaweza kuita DIESEL majina ya aina tatu lakini yakimaanisha DIESEL hiyohiyo ila utaratibu wa upatikanaji ni tofauti,majina hayo ni PETROLEUM DIESEL,SYNTHETIC DIESEL na BIODIESEL.

Hapa nitazungumzia BIODIESEL.BIODIESEL ni diesel ambayo hupatikana baada ya kufanya utaratibu wa kikemikali kwenye vegetable oil/mafuta ya mimea au fats za wanyama/animal fats(biolipids).Hapa nitazungumzia zaidi vegetable oil.Kuna vegatable oils nyingi sana ambazo huweza kufanyiwa utaratibu wa kikemikali ili kupata BIODIESEL,mfano,canola oil,soy oil,corn oil,sunflower oil,hemp seeds oil nk.Hapa nitazungumzia HEMP/MARIJUANA SEEDS OIL.

HEMP/MARIJUANA/BANGI ndio mmea wenye uwezo wa kuzalisha BIODIESEL kwa kiwango kikubwa zaidi kuliko mimea yote duniani kutokana na tafiti zilizokwishafanywa.HEMP/BANGI ina uwezo wa kuzalisha hadi mapipa/barrels 30 ya BIODIESEL kwa ekari moja ya HEMP/BANGI.PIPA/barrel moja lina ujazo wa lita takribani 119,hivyo basi kwenye ekari moja tunaweza kupata takribani lita 3,500 za BIODIESEL.Nadhani mnaweza kufikiria wenyewe lita hizo ambazo ni ekari moja tu zinaweza kuzalisha umeme kiasi gani kwa siku au zinaweza kuendesha magari mangapi kwa siku maeneo ya mijini.

BIODIESEL hupatikana kwa utaratibu wa kikemikali uitwao TRANSESTERIFICATION ambapo vegetable(hemp) oil(around 54 degree celcius) inapambanishwa na alcohol(eg methanol+catalyst) na kupata BIODIESEL pamoja na mabaki ya GLYCERIN,glycerin pia huweza kutumika kuzalishia sabuni,shampoo nk.Hii sio miujiza ndugu zangu,ni ukosefu wa uelewa tu ndio unaowafanya wengi washangae,elimu hii hatuwezi kuipata darasani,na hata ikifundishwa lazima mwishoni waweke disclaimer kwamba eti "biodiesel itakayozalishwa na bangi ni kidogo sana kiasi cha kutokuwa na maana yoyote kuhangaika nayo kuizalisha",huu ni uongo mtupu,wanasema hivi ili kuwarubuni watu wasijishughulishe nayo lakini ukweli ni kwamba bangi ni mmea wa ajabu sana na wenye manufaa makubwa sana watake wasitake.Na ndio maana wanapiga vita uzalishaji wa bangi kwa kisingizio cha kwamba bangi ni madawa ya kulevya.Ukweli ni kwamba bangi ni hatari sana kwenye biashara zao za mafuta na gas pamoja na tiba ya cancer ambayo tumeshaizungumzia.

Biodiesel process:




Utaratibu wa kikemikali unaohusisha mlinganyo wa kikemikali mnaweza kuupata kwenye mitandao,sina haja ya kuuweka hapa,lakini unahusisha organic chemical reactions,kwa wale ambao wamepitia vizuri organic chemistry wanaweza kuelewa kiurahisi.

Hapa sasa nadhani mnaweza kupata picha ya sababu halisi kwa nini bangi imeharamishwa.Wengi mtajiuliza,kwa sasa hawatumii bangi kuzalisha diesel kama kweli ina faida kama hii?Jibu lake ni kwamba kutakuwa hakuna tena monopoly ya biashara ya mafuta na hasa diesel,kila mtu anaweza kuzalisha diesel kama atapenda na hivyo kufanya diesel isiwe suala kubwa ki hivyo kama linavyochukuliwa sasa na hivyo bei yake kushuka.Mambo haya ndio hawa jamaa hawayataki,wako tayari kuvamia hata kijeshi nchi yoyote itakayozalisha bangi katika large scale kwa matumizi hayo,kama watagundua hilo.

Hebu angalia hapa uone jamaa anavyozalisha BIODIESEL ili uone kwamba hili suala sio big issue.Pia fahamu kwamba biodiesel ina faida nyingi zaidi kuliko petroleum diesel.Lakini hapa chini hawatumii bangi.

https://www.youtube.com/watch?v=aOzWgyB1FSk

https://www.youtube.com/watch?v=TC9h78b2RM4 (angalia part 1 na part 2)
 

Labda niulize tu mkuu, hayo maelekezo aliyotoa, ukitumia hivyo vitu kama vya kupunguza tindikiali, n.k. ni kweli au si kweli?

Kaka.
 
Niliwahi kusikia kua huko marekani kuna baadhi ya majimbo wameruhusu matumizi ya bangi..huoni kama watakua wanajichanganya wenyewe?kulingana na maelezo yako?Deception...?au ni kwa matumizi gani labda?
 
unachosema huna uhakika nacho kupe maana unahisi tuu. na una uhakika gani kama yupo bongo anatumia bundle zetu za tigo au airtel..?

Kumbe wewe hufuatilii . Na ndii maana hujui kama yuko tz au nje. Mimi nimemfuatilia tokea thread yake ya kwamba ukimwi hauambukizwi na sex . Na anaweza kuutibu. Forget abt bundle. Ngoja nikuulize kwani ukiwa nje unadhani internet ni bure? Na muda je? Wa tz tunapenda story mirracle kama kulala masikini kuamka tajiri....freemason......dawa za mapenzi......dawa za utajiri. Sasa wewe pata kansa au ukimwi harafu ukale hizo mbegu za mapiches huko njombe kama hatutakuokota fasta
 
Last edited by a moderator:
Niliwahi kusikia kua huko marekani kuna baadhi ya majimbo wameruhusu matumizi ya bangi..huoni kama watakua wanajichanganya wenyewe?kulingana na maelezo yako?Deception...?au ni kwa matumizi gani labda?

Jaribu kusoma thread hii toka mwanzo...Ameeleza hilo jambo.
 
Niliwahi kusikia kua huko marekani kuna baadhi ya majimbo wameruhusu matumizi ya bangi..huoni kama watakua wanajichanganya wenyewe?kulingana na maelezo yako?Deception...?au ni kwa matumizi gani labda?

Kwanza kabisa,kuruhusu bangi katika baadhi ya majimbo peke yake ni contradiction.Halafu pia ukijaribu kujitolea muda kufuatilia utagundua kwamba hayo majimbo yenyewe yanaruhusiwa kutumia bangi kwa restrictions,watu wanaotaka kutumia bangi wote wanaripoti sehemu husika,hutumii kiholela tu,je,unaona contradiction hapo?Kwa nini pamoja na tumbaku kuua lakini huhitaji kuripoti kwenye vyombo husika wakati unataka kutumia?Bangi haiui lakini bado wameiwekea restrictions,why?Na kwa nini wasiruhusu majimbo yote kama kweli wamekubaliana nayo?Wanaruhusu bangi katika matumizi ya kawaida sana ambayo hayagusi business interests zao.

Na pia mkuu ninataka nikuhakikishie kwamba,kama wangekua na uhakika kwamba watu wote duniani wanatumia bangi kwa kuvuta peke yake na si matumizi mengine,lazima wangeruhusu bangi itumike duniani kote,hii ni kwa sababu lengo lao si kwamba wanapenda sana afya za watu kiasi cha kuwalinda wasichanganyikiwe,la hasha,bali wanaogopa kama bangi itakuwa free bila restriction yoyote kuna watu wajanja wanaweza kulima maelfu ya ekari ili kuzalisha diesel,gas,methanol,paper,ropes,building materials na dawa za cancer.Sasa kama watu wataitumia bangi kwa namna hizi,inakuwa ni hatari kwao hasa kwenye biashara za mafuta na viwanda vya madawa hasa haya ya cancer.

Hivyo mkuu,ni kweli wanajichanganya,na hata wenyewe wajua kwamba wanajichanganya.Miaka mingi iliyopita bangi ilitumika kutengeneza kamba ngumu,bodi za gari kama zile gari za kwanza kabisa za kina Henry Ford,ilitumika kutengeza karatasi zenye ubora mkubwa sana,watu waliitumia kama dawa nzuri sana kwa magonjwa mengi na ilitumika kuzalisha diesel kuendeshea magari.Henry Ford na Rudolf Diesel walitengeneza engine za kwanza kabisa huku lengo lao likiwa kutumia diesel kutoka kwenye bangi ili kuendesha engine hizo,kipindi kile engine zao hizo ziliendeshwa kwa kutumia diesel kutoka kwenye bangi,lakini sasa hivi kutokana na ubinafsi wa watu wachache ambao wengine humu wanawaona kama miungu,sasa hivi watu wamerubuniwa akili na wanajua kwamba bangi ni haramu.

Note:
Siku moja marehemu Bob Marley wakati wa uhai wake aliulizwa na mwandishi wa habari;"huoni kwamba matumizi ya bangi ni mabaya?"
Bob Marley akamjibu;"Mabaya kwa nani?"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…