Hidden cancer cures

Hidden cancer cures

Hapo kwenye kamba umenigusa mkuu..maana nahusika..tulikua tukitumia sana enzi hizo..tuko pamoja mkuu..nimekupata.
 
Hapo kwenye kamba umenigusa mkuu..maana nahusika..tulikua tukitumia sana enzi hizo..tuko pamoja mkuu..nimekupata.

Unajua mkuu hapa duniani kama isingekuwa ubinafsi wa watu wachache,kusingekuwa na shida kama hizi zinazotuzunguka kwa sasa ambazo zinatatulika kwa urahisi tu.Hebu chukulia mfano huu wa bangi kwa mfano;

1.Kwa uwezo wa bangi kutoa diesel,tungeweza kulisha nchi yetu umeme wa uhakika kwa watu wote na kwa matumizi ya viwandani pia,na pia tungeweza kuondokana na kupoteza fedha za kununulia mafuta nje ya nchi.

2.Kwa kutumia masalia ya bangi tungeweza kujenga viwanda vingi sana nchini kujenga uchumi wetu na kuongeza ajira kwa watu wetu kama vile;
-Viwanda vya sabuni
-Viwanda vya Vipodozi vya asili
-Viwanda vya dawa za asili
-Viwanda vya kuzalisha gesi ya kupikia majumbani
-Viwanda vya karatasi zenye ubora
-Viwanda vya kamba ngumu
-Viwanda vya vifaa vya kujengea nyumba
-Viwanda vya kutengeneza vyakula vya mifugo
nk

Hebu fikiria tu mwenyewe baadhi ya hizo faida utaona kwamba zimegusa maeneo muhimu ya kiuchumi ambayo hasa ndio yanafanya maisha yetu yawe magumu.
 
Mkuu Deception nakubaliana na wewe sana kuhusu zao hilo la bangi, maana nilishawahi kusoma jarida la drum la south africa katika miaka ya tisini lilionyesha bidhaa zitokanazo na bangi, nilishangaa kuona wameteneza viatu vizuri vinakavyo na ngozi iliyozalisha kutokana na bangi na bidhaa nyingine nyingi. ila kipindi kile sikuhoji sana kwanini inakatazwa wakati inatoa bidhaa zinazotumia kila siku.
 
Last edited by a moderator:
Sidhani kama tatizo la umeme tanzania ni diesel itakayotokana na bangi. Kama ingekuwa tatizo ni hilo mbona tumegundua gas huko lindi karibu miaka kumi sasa je tatizo la umeme limekwisha. Acha ku promote vitu visivyo na maana . Bangi ikiruhusiwa kulima utaweza kuidhibiti isitumiwe vibaya. Nenda mkoa wa tabora ukaone bangi ilivyoharibu vijana. Wa tz msipende sana kusikia vitu rahisi rahisi
 
Sidhani kama tatizo la umeme tanzania ni diesel itakayotokana na bangi. Kama ingekuwa tatizo ni hilo mbona tumegundua gas huko lindi karibu miaka kumi sasa je tatizo la umeme limekwisha. Acha ku promote vitu visivyo na maana . Bangi ikiruhusiwa kulima utaweza kuidhibiti isitumiwe vibaya. Nenda mkoa wa tabora ukaone bangi ilivyoharibu vijana. Wa tz msipende sana kusikia vitu rahisi rahisi
Hakuna anayesupport uvtaji wa bange kwa vile hayo ni matumizi mabaya kiafya kama ilivyo uvutaji wa sigara ingawa sigara inaonekana halali na huku wakiwatangazia watu inaua na kusababisha cancer lakini cha ajabu Tumbaku inaachiwa ilimwe na support kubwa inafanyia ingawa haina faida kiafya hata kidogo. Iweje bange zao ambalo lina manufaa kiafya lisiachiwe lilimwe na kudhibitiwa matumizi yake kwa kuweka sheria kali kama itatumika vibaya.
 
Mkuu Deception nakubaliana na wewe sana kuhusu zao hilo la bangi, maana nilishawahi kusoma jarida la drum la south africa katika miaka ya tisini lilionyesha bidhaa zitokanazo na bangi, nilishangaa kuona wameteneza viatu vizuri vinakavyo na ngozi iliyozalisha kutokana na bangi na bidhaa nyingine nyingi. ila kipindi kile sikuhoji sana kwanini inakatazwa wakati inatoa bidhaa zinazotumia kila siku.

Ndio mkuu,hapo ndipo utakapoona kwamba haya mambo ni tofauti kabisa na jinsi tuyajuavyo.Niliwahi kusema kwamba huhitaji muda mrefu kugundua kwamba sheria inayosema bangi ni haramu yenyewe ni haramu.Hutahitaji evidence kutoka kwa mtu mwingine kujua ukweli huu,ukijiuliza maswali madogo tu kama haya utajua ukweli,bangi pia huweza kutumika kutengeneza nguo(textile),fikiria soko la pamba hapa litakuwaje?

Marekani wenyewe walioanzisha sheria hiyo wameitoa bangi kutoka schedule I drug kwenda schedule II na kuanza kuiruhusu katika baadhi ya majimbo lakini wanafanya hivyo kwa ujanja ujanja huku wakiweka restrictions.Haya mambo mkuu ukijiuliza kidogo tu utajua ukweli.Wenyewe wanajua kwamba sigara/tumbaku inaua lakini bado inaruhusiwa kutumika na binadamu,pombe pia inaua na ina hasara kwa mtumiaji lakini nayo imeruhusiwa kutumika,bangi haiui lakini ndio imewekewa sheria ya kuharamishwa eti kwasababu ni psychoactive.Lakini kumbuka kwamba ili bangi iwe na madhara hayo lazima mtumiaji awe anaitumia kwa kuvuta kama sigara.Sasa jiulize,kuna dawa moja inayotumika kwa kuchua mwili ili kuondoa maumivu,dawa hii inaitwa Salimia,dawa hii imeandikwa 'for external use only' kama warning,sasa endapo atatokea mtu atakunywa Salimia anaweza kufa.Je,mtu mmoja akifa kutokana na kunywa dawa hii,je sababu hii inatosha kuifanya Salimia iwe haramu kwa watu wote na hivyo kuzuiwa kuzalishwa na kuuzwa madukani?Jibu ni kwamba, HAPANA.Sasa kwa nini kila mtu anayekamatwa na bangi anapata wakati mgumu bila kujali anaitumiaje hiyo bangi?

Mimi nataka kuwapa taarifa tu ili kuwaongezea wigo wa kujua jinsi mambo yanavyoendeshwa katika dunia yetu.
 
Samahani ndugu Deception natoka nje kidogo ya mada kwa vile nimehamasika sana na maelezo yako nikaamua nigoogle kuangalia ugonjwa wa kisukari nikakukutana na hiki kitu click here
 
Last edited by a moderator:
Samahani ndugu Deception natoka nje kidogo ya mada kwa vile nimehamasika sana na maelezo yako nikaamua nigoogle kuangalia ugonjwa wa kisukari nikakukutana na hiki kitu click here

Kama unakumbuka niliwahi kusema kwamba mtu yeyote akiamua kujua ukweli wa mambo haya atajua tu kama ataamua kufuatilia.Sasa hiyo website uliyotoa inaendelea kuthibitisha mambo ninayosema na hata wewe mwenyewe unaona jinsi walivyoelezea ugonjwa wa diabetes kwa mantiki kubwa.Magonjwa haya sugu yanaingiza pesa nyingi sana kwenye viwanda vya madawa hivyo wasingependa watu wajue chanzo halisi na tiba za magonjwa hayo kwa maana kutibu chanzo cha haya magonjwa watakuwa wamepunguza kwa kiwango kikubwa sana cha faida wanayoipata kwa kutibu dalili pekee.Sasa tuchambue kidogo hiyo website;

Quote 1:"That is the problem when they are treating diabetes (especially Type 2) as a disease. It is like building a never ending vicious cycle that ensure steady stream of income for the Big Pharma"

Tatizo la mainstream doctors wanatibu kisukari kama ugonjwa na ndio maana tunaambiwa kisukari hakiponi au hakina tiba.Kile wanachokitibu kwa watu wenye kisukari si ugonjwa bali ni dalili tu.Hakuna mtu yeyote aliyepona kisukari kwa tiba za mainstream/conventional medicine,mgonjwa ataendelea kula dawa mpaka kifo chake.

Na ndio utaratibu huuhuu wanaofanya wakati wanahudumia watu wenye cancer,huwa wanatibu cancer wakidhani ndio ugonjwa wenyewe kumbe zile ni dalili tu,na ndio maana pia tunaambiwa hakuna tiba ya cancer na hasa pale unapochelewa,wanasahau pia kwamba hata malaria au TB ukichelewa kuitibu pia unakufa.Angalia quote yangu mwenyewe nilivyosema jinsi mainstream doctors wanavyoichukulia cancer hapo chini;

..Why the mainstream cancer treatments rarely cure cancer?
To answer this question,we must know that,the definition of cancer for mainstream/ allopathic doctors is very different from that of naturopathic doctors.Therefore,these two treatments are based on their definition of cancer. For allopathic/mainstream doctors,cancer is a tumor/lump of malignant abnormal cells.So what they do is to concentrate on the ways of removing away the tumors/malignant cancer cells from the body.

There are mainly 3 ways of doing that which are:
i/. To poison the cancer cells by using chemotherapy,
ii/. To burn the cancer cells by using radiations/mionzi,
iii/. To cut away the tumors if possible by surgery.

......That is why up to now we are told there is no known cure for cancer.Its is because they don’t deal with cancer but rather they deal with the symptoms of cancer.Tumor/lump/malignant cells are just symptoms of cancer.

Quote 2:"If you start to look at the problem of diabetes or hyperglysemia as symptom instead of disease, you will realize the problem is not as complicated as it seems to be. Diabetes is actually one of the symptoms or warning signs that tells you the internal body environment has changed. You should focus on reversing the internal body environment instead of wasting your time, money and life trying all sorts of drugs which could be not much better than a placebo. Deal with the root, not the symptoms!"

Kisukari ni ishara tu inayokukumbusha au kukufahamisha kwamba mwili wako umeanza kuwa na kasoro tofauti na kawaida ya ufanyaji kazi wake ulivyo.Cha msingi ni kubaini kilichosababisha hizo kasoro na kukiondoa na utakuwa umepona kabisa na utarudia afya yako kama zamani.Hata wale miungu waliotudanganya usifikiri kwamba hawajui hili,wanalijua hili vizuri sana lakini wanatupumbaza kwa faida zao binafsi.Hawatengenezi madawa ili kuonesha upendo kwa watu, bali wako kibiashara zaidi.


Quote 3:"Hyperglysemia or high blood sugar level is just one of the ways your body call for help or alert, it is one of the earliest signs that warn you that your body is heading towards acidosis.

It is like a house that is full of dirty rubbishes, mice and cockroaches will keep coming no matter how hard you try to eliminate them, it is a never ending process. Stop wasting time and money trying to kill those nasty pest! Focus on cleaning the house and throw away all those rubbishes instead."

Wakati nazungumzia ARVs niliwahi kusema blood ACIDOSIS ndio mzizi wa magonjwa yote sugu yakiwemo Cancer,Kisukari na AIDS(not HIV/AIDS).Hapa kwenye hii website wameonesha hili kwa upande wa kisukari.Sasa unapoendelea kula dawa za hospitali kutibu dalili tu unajiongezea matatizo zaidi kwa kuongeza kiwango cha acid kwenye damu na kuzalisha matatizo mengine.Angalia quote nyingine hapo chini;

Quote 4:"Synthetic chemical drugs or medicines not only cannot cure modern illnesses, they will gradually make your body internal environment becomes more polluted which eventually leads to other secondary organ failures. The very first victim of drug dependency is the kidney followed by the liver."

Nilipokuwa naongelea side effects za ARVs ambazo ndio ukimwi wenyewe nilisema kwamba mojawapo ya madhara yake ni BLOOD ACIDOSIS na LIVER FAILURE.Nadhani unaweza kujionea hata hapo kwenye hiyo website mambo haya yanavyoendana.Madhara ya dawa za Kisukari,Chemotherapy/mionzi na ARVs yanarandana kabisa,na ndio maana niliwahi kusema kwamba mojawapo ya magonjwa yanayowaua watu wanaotumia ARVs kwa muda mrefu ni Kisukari,Cancer,Ini na Figo.

Quote 5:"By now you should have an idea why most diabetes patients are still suffering from Type 2 Diabetes no matter how much medicine and injections they have taken"

Kinachosemwa hapo juu kwenye quote ya 5 ni sahihi pia kukisema kuhusu wagonjwa wa cancer na HIV/AIDS(feki).

Ukiamua kuutafuta ukweli,ukweli utajidhihirisha kwako kirahisi sana,hapa unajionea mwenyewe jinsi haya mambo yanavyorandana.
 
Dah haki ya Mungu....babu Na kikombe chake alipoanza nilipinga sana Ila kwa sababu watu wanapenda sana kusikiliza Mazingaombwe badala ya sayansi matokeo yake tuliyaona hasa wadau wa afya walioko mahospitalini.... Steve Jobs alidanganyika mpaka ikawa too late....kuna ukweli fulani unaongea ila suala la kutibu kansa kwa chakula aisee hapo utaumiza watu....mainstream medicine ni corrupt kweli Tena sana Ila si kihivyo ndugu yangu....ipo siku utatambua hilo maana Na wewe upo kwenye giza..
 
Dah haki ya Mungu....babu Na kikombe chake alipoanza nilipinga sana Ila kwa sababu watu wanapenda sana kusikiliza Mazingaombwe badala ya sayansi matokeo yake tuliyaona hasa wadau wa afya walioko mahospitalini.... Steve Jobs alidanganyika mpaka ikawa too late....kuna ukweli fulani unaongea ila suala la kutibu kansa kwa chakula aisee hapo utaumiza watu....mainstream medicine ni corrupt kweli Tena sana Ila si kihivyo ndugu yangu....ipo siku utatambua hilo maana Na wewe upo kwenye giza..

Tupe ukweli sasa.... mkuu Nini kakosea. Ni wapi kaenda chaka.. kuliko kuacha na kusema tu yupo gizani
 
Dah haki ya Mungu....babu Na kikombe chake alipoanza nilipinga sana Ila kwa sababu watu wanapenda sana kusikiliza Mazingaombwe badala ya sayansi matokeo yake tuliyaona hasa wadau wa afya walioko mahospitalini....

Usikurupuke na kupinga kabla hujasoma,sisi ngozi nyeusi ndivyo tulivyo,tunakimbilia kukurupuka kupinga kabla ya kudadisi.Haya mambo ni tofauti kabisa na kikombe cha babu,hii ni sayansi iliyothibitishwa maabara hivyo soma nilichowasilisha chote kwa undani ndio utaona ukweli kama kweli unataka kujua lakini,sikulazimishi.Epuka tabia ya kukurupuka na kupinga tu bila kutoa hoja za msingi.

.... Steve Jobs alidanganyika mpaka ikawa too late......

Nikikuuliza utuambie kuhusu historia ya cancer ya Steve Jobs je,unaweza kutuandikia hapa kwa mkono wako mwenyewe ili tuone kama kweli unaijua?Vinginevyo na hapa pia utakuwa umekurupuka.

...kuna ukweli fulani unaongea..

Ukweli upi huo?

... ila suala la kutibu kansa kwa chakula aisee hapo utaumiza watu......

Unajua cancer inasababishwa na nini?Ngozi nyeusi tuna matatizo sana,na ndio maana tunaendelea kutawaliwa na wakoloni hadi leo hii.

......mainstream medicine ni corrupt kweli Tena sana Ila si kihivyo ndugu yangu....ipo siku utatambua hilo maana Na wewe upo kwenye giza..

Nitatambua nini?Mimi nimemponya mtu aliyekuwa na cancer mbaya ya ini,labda sijakuelewa nitatambua nini,au unataka kunitafuta unidhuru kwa kuhatarisha biashara ya wakubwa?

Watu kama ninyi mnaokurupuka kupinga huwa mara nyingi ninyi au ndugu zenu hamjawahi kupata matatizo kama haya,na kama ndugu zenu walipata matatizo haya basi mtakuwa hamna uchungu na roho za ndugu zenu.Nina uhakika watu kama ninyi mkikumbwa na matatizo haya mtarudi humuhumu kutafuta kuokoa roho zenu baada ya kupoteza matumaini ya tiba za hospitali,na hiyo itakuwa ni siri yenu.

Kama una hoja za msingi lete hapa watu waone kama mimi kweli nadanganya,kama huna kaa kimya.Mimi sipati faida yoyote humu zaidi ya kuonesha upendo wangu kwa wengine,ningekuwa nafanya biashara ungeanza kupata mashaka,lakini sifanyi biashara humu,je wewe huwezi kujiuliza?Sijawahi kutoa mawasialiano yangu ya aina yoyote kwa mtu yeyote labda pale ninapolazimishwa na shida ya mtu tena hatuonani na huwa ninatoa ushauri tu bila gharama yoyote.Bado ninapata tatizo kujua kwa nini watu kama ninyi mnaokurupuka kupinga huwa mnakuwa hamna hoja za msingi lakini bado mna ujasiri wa kupinga,kwa nini hampendi kusoma?Kwa nini usisome ninachowasilisha hapa halafu ukakifanyie uchunguzi?Nina mashaka na uwezo wenu wa kufikiri.
 
Acha jazba na ubaguzi wa rangi....hii haiusiani Na rangi hata kidogo...
Kuhusu cancer nimetumia miaka saba kusoma hayo makitu kaka Na hata navyoandika ujumbe huu namalizia zamu yangu wodi ya watoto wenye kansa...so hamna jipya la Zaidi utakalonieleza kuhusu hilo

Natumia simu ila nikipata muda tutajadili tu kwa faida ya wote hata Na mimi pia...elimu ni pana sana na kubali hufahamu kila kitu ndio utajifunza...

Nini kutibu Kansa kaka...babu wa kikombe alitibu mpaka na ukimwi...😃

Hivi unajua kuna some sort of cancer huwa zinapotea tu bila tiba ? Nitarudi tupeane shule.....hizo hizo alternative medicine zina hadi degree marekani tena doctorate kabisa kama MD ila hujiulizi mbona hospitalini watu hawapungui ? Nitarudi kaka
 
Wazungu wako wajanja Na wenye akili mpaka leo wanajenga mahospitali na wanatumia chimo mpaka leo hii pamoja Na kwamba yote unayoongea yanatoka kwao...tatizo umeamua kuwa negative sana...wala sishangai maana hayo ma_conspiracy theories yalinitawala sana wakati naanza chuo...ni utoto tu !
 
Wazungu wako wajanja Na wenye akili mpaka leo wanajenga mahospitali na wanatumia chimo mpaka leo hii pamoja Na kwamba yote unayoongea yanatoka kwao...tatizo umeamua kuwa negative sana...wala sishangai maana hayo ma_conspiracy theories yalinitawala sana wakati naanza chuo...ni utoto tu !

Kaka umemaliza kila kitu . Na najitoa rasmi kusoma huu upuuzi wa jamaa. .....uko sahihi 100%. Jamaa hana akili na ujuaji wa kutoto. Sio issue ya ubaguzi maana kansa inaua zaidi wazungu kuliko africa. Na hizo theories anazotupa either negative or positive zote anatoa kwa hao hao wazungu. Harafu anaponda waafrica. Harafu nakushauri achana naye maana jamaa ukimpinga anakuwa mkali sana maana anajua utamuharibia ulaji..........eti anatishiwa maisha. Kweli utoto. Nani akutishie maisha kwa kunakili theories za watu.......leta ya kwako mwenyewe na u prove. Wahed
 
So dawa ya kisukari ni???

Kwanza kabisa,unaweza kujiuliza hivi:

1.Kisukari sio infectious,yaani hakisababishwi na vijidudu.Hivyo basi lazima kitakuwa kimesababishwa na mabadiliko kwenye mwili wa mtu.

2.Hapo mwanzo mtu hakuwa na kisukari,lakini baadaye mtu anapata kisukari.Kwa kuwa kisukari sio infectious,hivyo lazima huyo mtu mwili wake utakuwa na mapungufu fulani.Sasa ili kujua dawa yake,lazima uyajue hayo mapungufu kwanza.

3.Unapogundua kwamba mtu ana kisukari inabidi ujue kwamba hakupata tatizo hilo siku chache zilizopita,bali mabadiliko ya mwili wake yalifanyika kwa muda mrefu sana yaweza kufikia hata miaka 10 iliyopita.

4.Kutokana na muda ambao kisukari kinajijenga mwilini,vivyohivyo tiba yake itachukua muda mrefu kwa kuwa kinachofanywa na tiba hii ni kurudisha mwili ukae kwenye hali yake ya kawaida ambayo imeharibiwa kwa muda mrefu sana.Hivyo tiba hizi huweza kuchukua kuanzia miezi 2 au 3 na kuendelea kutegemea na aina ya kisukari na muda ambao kimejijenga mwilini.

Ili upone kisukari ni lazima ufanye total body cleanse and rejuvenation.Utaratibu huu unafanikiwa kwa kubadili style ya maisha hasa katika masuala ya vyakula(vilaji na vinywaji).Ukijua sayansi ya kisukari ndio utajua tiba yake,hivyo kutokana na sayansi yake kisukari huweza kutibika kwa vyakula tu,yaweza kuwa vyakula vya kawaida au supplements.Vyakula hivi vina kazi ya kuondoa sumu mwilini,kupunguza lehemu mbaya,kusafisha mfumo wa chakula,kurudisha madini yaliyopotea mwilini na kuweka damu katika pH sawia ya alkaline ambayo ni 7.365.Utaratibu huu ni sayansi iliyothibitishwa kabisa na si tiba za kikombe cha babu kama wengi wanavyodhani.Nilipanga kuanzisha uzi maalum wa kisukari kuelezea haya,lakini si mbaya pia nikaeleza sasa kwa kuwa umeniuliza.

Kuna kisukari type I na type II.Type I ni IDDM(insulin dependent diabetes mellitus) na type II ni NIDDM(non insulin dependent diabetes mellitus).

IDDM huwa inasababishwa na autoimmune condition ndani ya mwili ambapo kinga ya mwili inaua insulin producing beta cells kwenye islet ya pancreas/kongosho.Wakati type II mara nyingi inasababishwa na mwili kushindwa kuitikia insulin kutokana na uchafu uliopo mwilini kama vile lehemu nk.

Huwezi kupata autoimmune disease kama pH ya damu yako iko sawa yaani 7.365.Hivyo kama huwezi kupata autoimmune pia huwezi kupata IDDM.Huwezi kupata NIDDM kama mwili wako ni msafi(nazungumzia usafi wa ndani ya mwili) yaani hauna sumu,hauna lehemu mbaya,una madini yote muhimu na mfumo wa chakula ni msafi.Asilimia zaidi ya 95 ya magonjwa yote sugu huanzia kwenye utumbo,kisukari,cancer,AIDS(not HIV/AIDS) nk yana sayansi zinazorandana.

Nikipata muda wa kutosha nitawapa mtiririko mzuri wa kujitibu kisukari kutokana na sayansi tajwa hapo juu.Njia hii si uchawi bali ni sayansi iliyothibitishwa ambayo hutaambiwa na mainstream doctors.Najua kuna watu watakimbilia kupinga.Nitaweka tiba hii kwa kuwa najua kuna watu wanaihitaji ambao wameshagaragazwa sana na kisukari,mtu akipinga aendelee kupinga siwezi kumzuia.Nitatoa mwongozo huu bure kwa wale wahitaji ili wajitibu wenyewe na ndugu zao,lakini inabidi wajue kwamba huwezi kupona kwa siku 1 au 2,hii ni total body cleanse na rejuvenation,hivyo inahitaji muda kidogo kama nilivyosema hapo juu.Najua kwa watu ambao sio waelewa wanaweza kutumia labda wiki 1 na wakiona hamna mabadiliko wanaacha,ninatoa tahadhari mapema ili watu wajue kwamba ugonjwa wenyewe hujijenga hata kwa miaka 10 hivyo kuuondoa inahitajika nidhamu ya hali ya juu kwa kipindi kisichopungua miezi 2 au 3.Na hizi ndizo sababu zinazowafanya watu waone kwamba kisukari hakina tiba,watu wanategemea kupona ghafla,kisukari hakiko hivyo.Ukiwa na nidhamu kwenye utaratibu huu,ninakuhakikishia kwamba baada ya miezi 2 au 3 utaanza kuona tofauti kubwa,hamna kubahatisha hapa.
 
Acha jazba na ubaguzi wa rangi....hii haiusiani Na rangi hata kidogo...
Kuhusu cancer nimetumia miaka saba kusoma hayo makitu kaka Na hata navyoandika ujumbe huu namalizia zamu yangu wodi ya watoto wenye kansa...so hamna jipya la Zaidi utakalonieleza kuhusu hilo

Natumia simu ila nikipata muda tutajadili tu kwa faida ya wote hata Na mimi pia...elimu ni pana sana na kubali hufahamu kila kitu ndio utajifunza...

Nini kutibu Kansa kaka...babu wa kikombe alitibu mpaka na ukimwi...😃

Hivi unajua kuna some sort of cancer huwa zinapotea tu bila tiba ? Nitarudi tupeane shule.....hizo hizo alternative medicine zina hadi degree marekani tena doctorate kabisa kama MD ila hujiulizi mbona hospitalini watu hawapungui ? Nitarudi kaka

Wazungu wako wajanja Na wenye akili mpaka leo wanajenga mahospitali na wanatumia chimo mpaka leo hii pamoja Na kwamba yote unayoongea yanatoka kwao...tatizo umeamua kuwa negative sana...wala sishangai maana hayo ma_conspiracy theories yalinitawala sana wakati naanza chuo...ni utoto tu !

Tunakusubiri
 
..Hivi unajua kuna some sort of cancer huwa zinapotea tu bila tiba ? Nitarudi tupeane shule.....hizo hizo alternative medicine zina hadi degree marekani tena doctorate kabisa kama MD ila hujiulizi mbona hospitalini watu hawapungui ? Nitarudi kaka

Ungesoma yote niliyoandika usingekuja na upuuzi huu,hicho ulichoandika ni kitu kidogo sana na usingeandika kama ungenifuatilia vizuri toka mwanzo,nilishayazungumzia yote hayo,lakini kwa kuwa umekurupuka ndio maana unaona kwamba ulichoandika ni kigeni sana.Nikikuuliza hizo spontaneous cancer zinaponaje zenyewe unaweza kunijibu?

Ninakusubiri tuwape watu faida na watu waone ukweli uko wapi kati ya yale unayoyasema wewe na yale niyasemayo mimi.
 
mkuu Deception umesema asilimia 95 ya magonjwa yote sugu uanzia kwenye utumbo unaweza ukaelezea zaidi kwa hapo?! ni kivipi?!

kwa mfano mtu anaweza akawa na food intolerance kutibu hiyo inakuwaje au allergies?! ikiwa msosi ndio tiba?!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom