Hifadhi ya Taifa Kigosi yafutwa rasmi na kuwa msitu wa hifadhi ya Kigosi

Mungu wangu! Imefanyika makusudi Ili mwarabu aje kuchota dhahabu. Hii hapana aisee?
 
Hizi ni nyuzi za kusambaza chuki dhidhi ya utawala wa Raisi, leteni ushahidi kama mnao kuliko kumponda mtu bila evidance yoyote mtu anatunga anacho taka na sie tunaanza kujadili.
Soma post number 26.
 
Aibu kwa Taifa

Carbon emissions projects eti mwarabu ndo asimamie. NA achukuwe mauzo ya Carbon na gawio kidogo atume Aibu kwa Taifa!!!!....hiii miradi haitaji hata senti moja kuwekeza

Unawekeza watalaam tu wa kupima viuno vya miti kushirikiana na GIS experts then chakata ripoti yako contact Verification experts huko Ulaya baada ya hapo peleka tani zako za carbon SOKONI
 
Nimeisoma ila sababu ni tofauti na unao sema pale ni mgogoro wa aridhi.
Mwanzo ulisema uongo,sasa unasema sababu ?.

Kwa taarifa yako Kigosi mwanzo ilikuwa chini ya TAWA kwaajili ya uwindaji.

Sasa jiulize kwanini imepelekwa TFS na mwarabu kaingia mikataba ya misitu yetu.

Kwa taarifa yako Kigosi ina deposit kubwa ya dhahabu kuliko mgodi wa Geita ni suala la muda utagundua viongozi wetu wapo kwaajili yao na familia zao.

Magufuli pamoja na matatizo yake ya kuminya Demokrasia asingefanya haya yinayoyaona sasa.
 
Viwanda vya UONGO
You are an idiot!
Kabla Hifadhi haijafutwa lazima GN itangaze
Je huu nao ni uongo?

BUNGE limepitisha na kuridhia Azimio la serikali la kufuta Hifadhi ya Taifa Kigosi ili kuruhusu kuanzishwa kwa Hifadhi ya Msitu Kigosi, itakayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Akiwasilisha Azimio hilo bungeni Dodoma jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohammed Mchengerwa alisema baada ya kuanzishwa kwa Hifadhi ya Kigosi eneo hilo lilisimamiwa na Sheria ya Hifadhi za Taifa Sura 282 inayozuia kufanyika kwa shughuli za kibinadamu ukiwemo ufugaji nyuki, uvuvi wa samaki na shughuli za kimila.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…