Hii hapa biashara ya mtaji wa 5000 itakayokupa 150000 kwa mwezi

Hii hapa biashara ya mtaji wa 5000 itakayokupa 150000 kwa mwezi

aise

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2018
Posts
5,175
Reaction score
16,488
Kwakweli mama anaupiga mwingi sana kuelelekea golini kwake.

Kama hauna kazi, na unashinda kijiweni.
Na hauna mtaji wa maelfu ya pesa.

Chukua sahani kubwa hapo nyumbani (yanaitwa masinia ya kupakulia ubwabwa wa kula watu wengi),
au deli au chochote, chukua na kisu.

Chukua na maji kwenye kidumu cha lita tano.

Nenda sokoni nunua tikiti moja kubwa, au nanasi au chochote.

Rudi mpaka kijiweni, osha tikiti lako, katakata vipande vya mia mbili, weka kwenye sahani lako na uweke hapo kijiweni.
Anza kuzisubiri mia mbili zako.

Tikiti litaisha, na faida haukosi 3,000.

Kazi kwako, ukae kijiweni tu unapiga soga au ukae kijiweni ukichukua mia mbili miambili.
 
Ikiwa kama unaona aibu, mchukue hata mdogo wako, katakata tikiti lako ukiwa nyumbani, si unaona aibu?

Mpe dogo abebe aende mpaka kijiweni na wewe uende umfuate dogo nyuma. Mkifika pale kaa kama wanakijiwe wengine.

Utashuhudia dogo anavyojikusanyia miambili miambili hadi kumuonea wivu.
 
Ikiwa kama unaona aibu, mchukue hata mdogo wako,
katakata tikiti lako ukiwa nyumbani, si unaona aibu?
mpe dogo abebe aende mpaka kijiweni
na wewe uende umfuate dogo nyuma.
Mkifika pale kaa kama wanakijiwe wengine.
Utashuhudia dogo anavyojikusanyia miambili miambili hadi kumuonea wivu.
Mkuu tumekupata Wala usijali
 
sasa unauhakika gani kama hapa nyumbani kwangu kuna sinia kubwa?

Kama hauna sinia chukua hata ndoo, ikoshe vizuri tia matiki humo, juu pale ya mfuniko weka kipande cha tikiti na "kabango kadogo umeandika 200"

Ikiwezekana tia na barafu la mia humo ili yawe ya baridi utawakamata sana watu wakati wa jua.

Kama hata ndoo hauna, basi bora ufe.
 
Kama hauna sinia chukua hata ndoo, ikoshe vizuri tia matiki humo, juu pale ya mfuniko weka kipande cha tikiti na "kabango kadogo umeandika 200"
Ikiwezekana tia na balafu la mia humo ili yawe ya baridi utawakamata sana watu wakati wa jua.

Kama hata ndoo hauna, basi bora ufe.
Kama ndoo hana akachukue hata ya chooni
 
Kwakweli mama anaupiga mwingi sana kuelelekea golini kwake.

Kama hauna kazi, na unashinda kijiweni.
Na hauna mtaji wa maelfu ya pesa.

Chukua sahani kubwa hapo nyumbani (yanaitwa masinia ya kupakulia ubwabwa wa kula watu wengi),
au deli au chochote, chukua na kisu,

chukua na maji kwenye kidumu cha lita tano.

Nenda sokoni nunua tikiti moja kubwa, au nanasi au chochote.

Rudi mpaka kijiweni, osha tikiti lako, katakata vipande vya mia mbili, weka kwenye sahani lako na uweke hapo kijiweni.
Anza kuzisubiri mia mbili zako.

Tikiti litaisha, na faida haukosi 3,000.

Kazi kwako, ukae kijiweni tu unapiga soga au ukae kijiweni ukichukua mia mbili miambili.
Msimu wa nanasi bado ila ukija wengi huwa wanafanya hivyo!
 
Back
Top Bottom