Hii hapa biashara ya mtaji wa 5000 itakayokupa 150000 kwa mwezi

Hii hapa biashara ya mtaji wa 5000 itakayokupa 150000 kwa mwezi

Kwakweli mama anaupiga mwingi sana kuelelekea golini kwake.

Kama hauna kazi, na unashinda kijiweni.
Na hauna mtaji wa maelfu ya pesa.

Chukua sahani kubwa hapo nyumbani (yanaitwa masinia ya kupakulia ubwabwa wa kula watu wengi),
au deli au chochote, chukua na kisu,

chukua na maji kwenye kidumu cha lita tano.

Nenda sokoni nunua tikiti moja kubwa, au nanasi au chochote.

Rudi mpaka kijiweni, osha tikiti lako, katakata vipande vya mia mbili, weka kwenye sahani lako na uweke hapo kijiweni.
Anza kuzisubiri mia mbili zako.

Tikiti litaisha, na faida haukosi 3,000.

Kazi kwako, ukae kijiweni tu unapiga soga au ukae kijiweni ukichukua mia mbili miambili.
Sawa Mkurugenzi, tutafanyia kazi.
 
Kama hauna sinia chukua hata ndoo, ikoshe vizuri tia matiki humo, juu pale ya mfuniko weka kipande cha tikiti na "kabango kadogo umeandika 200"
Ikiwezekana tia na balafu la mia humo ili yawe ya baridi utawakamata sana watu wakati wa jua.

Kama hata ndoo hauna, basi bora ufe.
Kweli Bora afe Tu!
 
Ikiwa kama unaona aibu, mchukue hata mdogo wako,
katakata tikiti lako ukiwa nyumbani, si unaona aibu?
mpe dogo abebe aende mpaka kijiweni
na wewe uende umfuate dogo nyuma.
Mkifika pale kaa kama wanakijiwe wengine.
Utashuhudia dogo anavyojikusanyia miambili miambili hadi kumuonea wivu.
Haha mkuu, umenikumbusha mbali sana nikiwa darasa la tatu mama yangu alikuwa akienda kuuza ndizi magodown zinadoda kila siku zinabaki
Sijui akili ilitoka wapi jioni baada ya kurudi shule nikawa nachukua ndizi na matunda yaliyododa naenda kwa mamantilie mmoja anaepika chakula cha usiku pale mtaani kwakweli mpaka mama alininunulia kiti na meza vya kusomea maana biashara ilikua vizuri inaonyesha maana mzigo unaouzwa usiku ukawa mkubwa kuliko mchana
 
Mwehh watu wanataka ela ya maendeleo uko iyo 150k si uende kuajiriwa viwandani uko, jiajiiri tengeneza pes nyingi
 
Mwehh watu wanataka ela ya maendeleo uko iyo 150k si uende kuajiriwa viwandani uko, jiajiiri tengeneza pes nyingi
Kuna watu hawana mitaji ya kutenpenezea hizo pesa ndefu.
Mimi hapa nimetoa mwanga kidogo kwa washkaji wa vijiweni.
 
Kuna watu hawana mitaji ya kutenpenezea hizo pesa ndefu.
Mimi hapa nimetoa mwanga kidogo kwa washkaji wa vijiweni.
Mkuu wengine sio walengwa wa wazo , mkuu hawajui kutengeneza laki kwenye shilingi mia mia sio jambo dogo kabisa
 
Kwa 5000 unapata matatu, bado hoja ya mtoa mada ni Ile Ile kata kata weka kwenye sinia peleka kijiweni kwako ujiokotee mia mbili mia mbili, Kama tikiti moja litakuletea 150000 kwa mwezi je kwa hayo matatu??? Nenda kajiokotee mia mbili mia mbili

Kupanga ni kuchagua.
Atakaye panga na akachagua hii aidia atapata mafanikio chanya.
 
Back
Top Bottom