Hii imekaaje? Kila nikikaribia kupata pesa mambo yanaharibika

Hii imekaaje? Kila nikikaribia kupata pesa mambo yanaharibika

aziz habib

Member
Joined
Mar 13, 2015
Posts
76
Reaction score
88
Nimekuwa kwenye hali nisiyoielewa kwa muda mrefu sasa. Yaani kila jambo nilifanyalo likikaribia kufanikiwa linaharibika.

Yaani naweza nikapata ramani ya pesa ila ikifikia hatua ya mwisho kuipata dili linaharibika katika hali isiyoeleweka na hata nilipofikia hatua ya kutumia msemo wa kimfaacho mtu chake kwa kutaka kuuza baadhi ya vitu ninavyomiliki hali inakuwa hivyo mteja akipatikana dakika ya mwisho anaingia mitini.

Kukopa nako unapata uhakika wa mkopo ikifikia hatua ya mwisho mambo yanabadilika. Waungwana naomba msaada wenu wa mawazo nijue wapi nakosea maana imefikia hata kodi ya pango najikuta napitisha na nikipata pesa ni kupunguza deni sio kumaliza.
 
Nimekuwa kwenye hali nisiyoielewa kwa muda mrefu sasa. Yaani kila jambo nilifanyalo likikaribia kufanikiwa linaharibika. Yaani naweza nikapata ramani ya pesa ila ikifikia hatua...
Mkuu Jaribu kuamka usiku saa nane ufanye Tahajudi hiyo ndo dawa pia jitenge na ngono na uchafu

Binafsi Mimi napotafta Jambo nikalikosa natumia Nguvu za kiroho hasa kuamka saa nane Usiku na kupiga meditation hapo nikimaliza mara nyingi nafanikiwa pia ngono zinaua bahati na future
 
Dili linakua la kupambania,sasa hakikisha wewe ndo uwe Dili lenyewe tuone kama kuna Dili litaharibika.
 
Mzazi yupo mmoja (mama) huwa mara nyingi ananiambia ni ishu ya muda itapita tu lakini naona imekuwa kwa muda mrefu sasa. Kifupi yeye anaiona kama changamoto ya kawaida sana tofauti na uhalisia ninaoupitia mie
Kaulize kwenu...labda kuna viapo na ushirikina....
 
Mkuu samahani mimi.napenda utani sana hii picha dp ni yako? Mbona.sasa umepaka.mafuta mdomoni? 🤣🤣🤣🤣

Pole.sana ila shukuru kama huna madeni sisi wengine tuna madeni mpka hatupokei cm
Nia yako nicheke tu msibani nionekane mshirikina🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mkuu samahani mimi.napenda utani sana hii picha dp ni yako? Mbona.sasa umepaka.mafuta mdomoni? [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Pole.sana ila shukuru kama huna madeni sisi wengine tuna madeni mpka hatupokei cm
Hahahaha mkuu hiyo picha sikupaka mafuta mdomoni ni picha ya miaka 7 iliyopita nikiwa na umri mdogo kiasi
 
Back
Top Bottom