Hii imekaaje kudharau watumiaji wa simu za Tecno na Itel ilihali wote mnakuwa na access ya vitu vinavyofanana

Hii imekaaje kudharau watumiaji wa simu za Tecno na Itel ilihali wote mnakuwa na access ya vitu vinavyofanana

Tecno, itel na infinix ni simu ila za kiwango cha chini.

Lazima tukubaliane kwamba kwenye maisha kuna viwango ama levels, hizi zinatokana na vitu vingi mojawapo ni ubora.

Mfano, unaweza kupanda toyo la miguu 3 kutoka Dar kwenda Dodoma, utafika tu sawa na Shabiby ingawa mtatofautiana muda wa kufika. Barabara mnapita moja ile ile lakini tofauti ya yoto ama guta na Shabiby iko wazi.

Wewe unaweza kua na paso mwingine ana range rover sports mnaenda Arusha kutokea Dar, yote ni magari na mtafika wote Arusha kwa nyakati tofauti lakini kuna vitu kama speed, comfortability, security, safety nk ndio vitatofautisha paso na range.

Kwenye simu iko hivyo hivyo. Tecno ni simu ila za viwango vya chini, choka mbaya. Vifaa vinavyotumika kutengeneza tecno ni vya ubora hafifu ama wa chini.

Tecno tunatumia tu kwa sababu ya umasikini ila tukiwa na hela tungetamani kutumia simu za maana kama Samsung, Iphone, Huawei, Vivo, Xiaomi, LG, Lenovo ama makampuni mengine ya maana.
 
Mkuu jifunze kwa wazungu..
Wale jamaa awapendi vitu under quality
Simu tajwa hapo juu zina vingi vya kujifunza kutoka kwa Simu za mzungu..
Na kwa kuanzia tu hizo simu tajwa hazitumiki huko zinakotengezwa.

Just imagine mtu anapika vitumbua af yeye mwenyew hatak watoto wake wale ila anawauzia wengine..
Tecno n mdhamin wa Man City , kama hazitumik huko kwann wakadhamin club ya huko?
 
Kiukweli kwa mtu ambaye anajua simu nini. Tecno, Itel na ndugu zake huwezi tumia. Hizi ni simu ni kwa watu wanaoingia JF, Facebook, WhatsApp, Twitter n.k
Ukiinstall application km Canva, Adobe n.k
Utachokutana nacho, utajuta. Unfortunately, Google play store has stopped
Natumia Infinix , nafanya graphics mwenyewe kila siku kwenye simu yangu (kwaajili ya biashara) hiyo canva , adobe etc zipo

Mna ujinga mwingi
 
Tecno, itel na infinix ni simu ila za kiwango cha chini.

Lazima tukubaliane kwamba kwenye maisha kuna viwango ama levels, hizi zinatokana na vitu vingi mojawapo ni ubora.

Mfano, unaweza kupanda toyo la miguu 3 kutoka Dar kwenda Dodoma, utafika tu sawa na Shabiby ingawa mtatofautiana muda wa kufika. Barabara mnapita moja ile ile lakini tofauti ya yoto ama guta na Shabiby iko wazi.

Wewe unaweza kua na paso mwingine ana range rover sports mnaenda Arusha kutokea Dar, yote ni magari na mtafika wote Arusha kwa nyakati tofauti lakini kuna vitu kama speed, comfortability, security, safety nk ndio vitatofautisha paso na range.

Kwenye simu iko hivyo hivyo. Tecno ni simu ila za viwango vya chini, choka mbaya. Vifaa vinavyotumika kutengeneza tecno ni vya ubora hafifu ama wa chini.

Tecno tunatumia tu kwa sababu ya umasikini ila tukiwa na hela tungetamani kutumia simu za maana kama Samsung, Iphone, Huawei, Vivo, Xiaomi, LG, Lenovo ama makampuni mengine ya maana.
Ubora au uwezo wa simu unapimwa kwa specifications sio mtazamo wako

Porojo nyingi
 
Hebu support hii na Data

Hakuna simu inayozima kwa kuwekewa mzigo mzito, unless ina miaka zaid ya minne au mitano ua matumiz
Siyo, Kweli!
Nimezitumia ITEL na TECNO sana.

Nilikuwa na ITEL mpya kabisa imetoka shop na hata miezi 5 bado ukiipiga mzigo mzito inazima.

Na TECNO hivyo hivyo niliinunua shop mpya kabisa nikichat sana hapa JF inazima.

Nikidownload files kubwa inazima au inakata network na haijamaliza miaka miwili.

Jamaa zangu wawili nao walipiga mchongo, Halafu wakaingia shop wote wakachukua ITEL mpya.

Lakini cha ajabu ITEL zao zinakata NETWORK kila wakipiga simu au wakishusha files na tuko mjini kati Rock City.

Tukairudisha dukani ITEL inayokata NETWORK mara kwa mara, Tukapewa nyingine mpya nayo ina 4G na tukaweka HALOTEL 4G lakini inasumbua sana kwenye kudownload, ni nzito, inapakua slow slow sana tofauti na Infinix, Samsung, Iphone, Smartphones zingine.

ITEL na TECNO zina SAR kubwa pia. Kwanini MCHINA hatumii TECNO kwao?
 
Hakuna anayemdharau mtumiaji wa TECNO au AITEL isipokua tunawatania Kama tunavyowatania wasukuma kwa ushamba walionao, au wangoni kwa kupenda pombe na wanawake, au wakinga kwa uchawi, au waha kwa uchafu na ubishi, au wapare kwa ubahili au waluguru kwa kuongea upupu au wakurya kwa tabia zao mbaya.
 
Ukishusha mzigo mzito zina jam, Zinazima.

Hazipakui High Quality Pure HD.

Zina viwango vikubwa vya SAR tofauti na zile za Ulaya na America.
Mzigo mzito wa tani ngapi? Na high quality pure HD ndo ipoje? Yawezekana mi mgeni kwenye ulimwengu wa teknolojia viwango vya SAR ndoa vinakuwaje?
 
Unakuna pale unapoweza.

Kumekuwapo na imani kuwa watumiaji wa simu wa makampuni ya Tecno na Itel ni watu washamba na wasio na uwezo kifedha. Kiukweli katika mtizamo wa kutokuwa na uwezo kifedha naweza kuunga mkono lakini katika kuwa washamba ni jambo lisilo na ukweli.

Hivi inakuwaje mtu una akili zako timamu kabisa unaanza kumdiss mtu anayetumia Tecno au Itel wakati wote.
Najua unaipenda tecno yako ila nakwambia tu hiyo ni upuuzi sio simu
 
Kiukweli kwa mtu ambaye anajua simu nini. Tecno, Itel na ndugu zake huwezi tumia. Hizi ni simu ni kwa watu wanaoingia JF, Facebook, WhatsApp, Twitter n.k
Ukiinstall application km Canva, Adobe n.k
Utachokutana nacho, utajuta. Unfortunately, Google play store has stopped
Hivyo vitu mna uhakika navyo au mnaandika vitu vya kusadikika watu wameinstall apps za ukubwa tofauti na still simu inapiga mzigo kama kawaida
 
1. Nina 4 ya 28.

2. Diploma ya Uhasibu ( Sikuwahi kufeli hata somo moja, nilimaliza na GPA 4.5)

3. Bachelor Degree in Logistic and Transport Management. ( Sikuwahi kufeli hata somo moja, nilimaliza na GPA 4.1)
4. Mtuache na 4 zetu.

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Wanaume wa Dar unapata 4 ya 28 unajisifu?
Umeunga unga elimu mpaka kinyaa
Sikia ndugu, soma std 7 faulu, soma f 1 hadi 4 faulu soma f 5 na 6 faulu nenda University. Kuunga unga ina maana shule wewe umelazimisha tu umetumia ujanja ujanja[emoji23][emoji23]
 
Haya mambo ni hulka. Kuna watu, wengi tu wana uwezo wa kumiliki simu kali lakini wanatumia simu za kawaida sana. Na mwingine yuko radhi amiliki simu yenye thamani ya mishahara yake mitatu.

Binafsi hapa namiliki Infinix! Miaka miwili sasa. Naweza kufanya kazi za ofisi, kupiga na kupokea simu, kutuma sms na ina whatsapp. Na kwa vile maisha yangu napeleka nnavyotaka mwenyewe na serikali yangu. Hainisumbui kuitoa popote pale.

Nikienda kwa wakala au benki hawaniulizi unatumia simu gani? Ilimradi salio liwepo.
Mkuu umeumaliza kila kitu. Ishi unavyotaka wewe sio wanavyotaka walimwengu utakuwa mtumwa.
 
unachekesha sana.
nipe sababu ya kulinganisha majina na vitu.
bmw inamiaka mingapi na passo ina miaka mingapi
Kwa tafsiri hiyo ukiwa unamiliki bmw unakuwa na kibali cha kumdharau anayemiliki Passo kuna wakati tujifunze kuappreciate vitu vya watu.

Kuna mataasisi yenye wataalamu yanasimamia standard ya hivi vitu ukiona bidhaa imeingia sokoni ni wazi kuwa imekidhi viwango vilivyowekwa.

Sasa wewe unayejifanya mjuaji na akili zako za darasa la saba b unakomaa kuwa Tecno sio simu ilihali hata basics za kutengeneza calculator huzijui.
 
Mkuu nunua iphone au Samsung Ili uwafurahishe watu,

Dunia haina usawa
Kuanzia mavazi,malazi, chakula,ndinga nzuri majumba mazuri

Vyote hivi hufanyika kulingana na walimwengu wanataka Nini .ukibisha utapata taabu Sana.

Bodi wangu alinunua Toyota Prado bila kupenda kisa tu walimwengu hawakuipenda Toyota Corolla yake[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ni mtu anayejiamini na mwenye akili hawezi kufanya kitu sababu ya kufurahisha watu au sababu ya kuogopa watu watakachosema wasiojitambua ndo anaweza kuwa na akili mbovu kiasi hicho
 
Back
Top Bottom