Ozone star
Member
- Aug 1, 2018
- 7
- 3
Kuna documents kutoka halmashauri ya wilaya fulani hivi. Inaelezea tathmini ya jinsi ya kutatua migogoro ya mifugo itakapoharibu kila aina ya mazao na malipo yake.
Mfano:
Ng'ombe wakiingia shamba la mahindi muda wowote wa ukuaji wa mazao hata kama mahindi yana wiki toka kupandwa, inapigwa hesabu yote toka kuandaa shamba kupanda, kupalia hadi mavuno. Mfano, Tsh 600,000/. Ni uendeshaji shamba.
Halafu inajumlishwa na mauzo ya mazao yote baada ya mavuno. Mfano, Mauzo ni Tsh 1,200,000/-. Hivyo 600,000+1,200,000= 1,800,000. Hivyo mwenye mifugo atatakiwa kumlipa mkulima 1,800,000/-Tshs.
Maswali:
Je, hapo haki imetendeka? Hii ni sheria ya nchi inayotumika hata mahakamani? Je, hizi kanuni zinazoletwa vijijini zilizotungwa na watu wachache huko halmashauri pia zipo mahakani? Inawezekana vipi gharama za uendeshaji zijumlishwe na mauzo ndo alipwe mkulima tena kwa umri wowote wa mazao?
Maoni/mawazo binafsi:
Ingetakiwa mfugaji auziwe mazao kwa tathmini tu kwamba kama angavuna?, Ingetoa gunia kadhaa zenye thamani ya Tsh 1,200,000/. Maana yake mkulima angepata faida ya Tsh 600,000/-
NB: Hii ni tathmini aliyoifanya bwana shamba leo na kumpa mkulima hesabu ya mfano huu alipwe au aende mahakamani.
Naomba wataalam wa sheria mnisaidie.
Mfano:
Ng'ombe wakiingia shamba la mahindi muda wowote wa ukuaji wa mazao hata kama mahindi yana wiki toka kupandwa, inapigwa hesabu yote toka kuandaa shamba kupanda, kupalia hadi mavuno. Mfano, Tsh 600,000/. Ni uendeshaji shamba.
Halafu inajumlishwa na mauzo ya mazao yote baada ya mavuno. Mfano, Mauzo ni Tsh 1,200,000/-. Hivyo 600,000+1,200,000= 1,800,000. Hivyo mwenye mifugo atatakiwa kumlipa mkulima 1,800,000/-Tshs.
Maswali:
Je, hapo haki imetendeka? Hii ni sheria ya nchi inayotumika hata mahakamani? Je, hizi kanuni zinazoletwa vijijini zilizotungwa na watu wachache huko halmashauri pia zipo mahakani? Inawezekana vipi gharama za uendeshaji zijumlishwe na mauzo ndo alipwe mkulima tena kwa umri wowote wa mazao?
Maoni/mawazo binafsi:
Ingetakiwa mfugaji auziwe mazao kwa tathmini tu kwamba kama angavuna?, Ingetoa gunia kadhaa zenye thamani ya Tsh 1,200,000/. Maana yake mkulima angepata faida ya Tsh 600,000/-
NB: Hii ni tathmini aliyoifanya bwana shamba leo na kumpa mkulima hesabu ya mfano huu alipwe au aende mahakamani.
Naomba wataalam wa sheria mnisaidie.