Hii imekaaje kwa wanandoa?

Anna pita

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2012
Posts
227
Reaction score
426
Hii imekuaje japo mapenzi hayana ratiba maalum. Je hii ni Sawa?

Inakuaje inapofika usiku mmesambaa kwenda kulala mwanaume anabaki seblen aidha kuchati na simu au kuangalia zake tv.

Mwanamke kutokana na pilika za kazi + za nyumbani, watoto unaingia kulala dakika 10 tu usingizi ushakupitia tena mzito

Jamaa anakuja kulala saa 7 au 8 anataka mfanye mapenzi saa hiyo umelala kama umekufa yaani hii ni Sawa jamani?

Kwanini tusije wote kulala tuandaane vizuri tufurahie tendo?

Kwanini uje kulala saa 7 au 8
 
Wanajifanya kutaka muda wowote watakao.MAPENZ SI UTUMWA!!!
 
Mama J jana usiku kulikuwa na mechi ya mpira wa miguu kali sanaa..😉
 
Umejaribu kuongea nae kuhusu hiyo issue? na majibu yake yalikuaje?
 
Zungumza naye....

Kuna matatizo mawili hapa....kubaki kuchat wakati Familia imelala na kukudandia usiku wa manane.

Tatizo la kwanza umeliendekeza wewe....mmeo anabakije sebuleni anachat na haufanyi chochote...wewe ndiye quality assurance wa nyumba.

Lalamika hata kutumia kigezo cha kazi kumwambia hatakiwi abakie usiku wa manane...asubuhi atakusumbua kumwamsha.... ikitokea amelala late siku moja moja saana.
 
Kwa nini usibaki sebuleni na mmeo ukaanzisha uchokozi mkaenda chumbani, tatizo wanawake wengi mlio kwenye ndoa mnaona wanaume ndo tuna shida sana ya kufanya mapenzi so mnashindwa kujua majukumu yenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…