Hii kesi mdogo wangu ana haki au hana?

Hii kesi mdogo wangu ana haki au hana?

sikatai kosa ila nauliza shule inatoa wapi mamlaka ya kuitaifisha nakuiharibu
Kabla ya kukomalia simu kurudi jiulize maswali yafuatayo kiongozi.
1. Sheria za shule zinasemaje kuhusu simu ? Mwanafunzi akikamatwa na simu afanyweje ?
Kama sheria inaipa mamlaka shule kutaifisha hiyo simu, jiulize ilikuaje ukamruhusu mdogo wako kuvunja sheria za shule ?
2. Kuna shule mwanafunzi akikamatwa na simu anafukuzwa anasimamishwa masomo au kufukuzwa kabisa shule. Je sheria za shule hiyo zinasemaje ? Usikute adhabu ya kutaifisha simu ndio adhabu ndogo huenda dogo alipaswa asimamishwe shule au kufukuzwa kabisa. Rejea kusoma sheria za shule zinasemaje.
3. Kama sheria za shule zipo kimya kuhusu simu basi una haki zote za kukomalia simu ya dogo irudi. Zama kwenye sheria za shule, huwa zinatolewa walati mwanafunzi anapewa joining instructions. Isome ili kutenda haki pande zote.
 
........ikikamatwa inataifishwa lakini je sheria za nchi zinasemaje,shule inatumia sheria gani kutaifisha mali ya mtu?
Wakati una sign joining instructions kwann hukuhoji hili swali? Yaani umeshasaini alafu unakamatwa ndio unauliza??
 
Sijaona nchi yenye malimbukeni kama yetu. Ni unafiki kwa kwenda mbele. Hivi mwanafunzi wa sekondari tena form 6 kuwa na simu kuna shida gani? Ndiyo maana mijitu ikianza kazi inakuwa na roho ngumu kama mawe, kila saa ni ofisini ni kisirani na huduma hakuna.
Tatizo sio kuwa na simu, tatizo n kuwa na simu sehemu isiyotakiwa
 
Huyu ni dogo mwenyewe mwenye simu iliyochukuliwa asijifiche nyuma ya mgongo

Dogo simu subiri chuo

Huko ni shule , shule kama shule simu ni mwiko
 
nna mdogo wangu alikua shule moja mkoa wa Dodoma, akakamatwa na simu shuleni na mkuu wa shule akiwa form 6 siku chache kabla ya mtihani.mkuu akakaa na simu hiyo na mdogo wangu alipomaliza shule akadai simu yake lakini mkuu wa shule amegoma kumrudishia na anadai simu imeharibiwa.Ni kweli sheria ya shule hiyo simu ikikamatwa inataifishwa lakini je sheria za nchi zinasemaje,shule inatumia sheria gani kutaifisha mali ya mtu?

Hiu hoja sio ya sheria za nchi, ni kujua taratibu (by-laws) za shule zinasemaje. Ila binafsi sioni sababu ya kufatili hili swala kwanza ni utovu wa nidhamu kumiliki simu shuleni.​

Huyu ni dogo mwenyewe mwenye simu iliyochukuliwa asijifiche nyuma ya mgongo

Dogo simu subiri chuo

Huko ni shule , shule kama shule simu ni mw


Zamani tulikua tunaandika barua wenyewe Kila Jumamosi tunapewa barua zetu Toka kwa ndugu na jamaa .

Hata ukiwa na shida unaandika barua .

Je, kwa sasa wanafunzi matatizo yao wanayafikishaje kwa jamaa zao ?

Nadhani simu za vitochi zingeruhusiwa kwa ajili ya kiwasiliana na jamaa zap hasa wazazi .
Lakini pia kwa ajili ya kupokea pesa kwa sababu zamani walitumiwa kwenye EMS au Money Telegram .

Kuna aina Fulani ka ukiritimba na kula pesa za wanafunzi kwa kusema zitumwe kwa namba ya mwalimu hasa kwa wanafunzi wa sekondari. Dunia na mifumo yake inauonevu mkubwa sana na kujengea watu hofu na stress TU bila sababu.
 
Zamani tulikua tunaandika barua wenyewe Kila Jumamosi tunapewa barua zetu Toka kwa ndugu na jamaa .

Hata ukiwa na shida unaandika barua .

Je, kwa sasa wanafunzi matatizo yao wanayafikishaje kwa jamaa zao ?

Nadhani simu za vitochi zingeruhusiwa kwa ajili ya kiwasiliana na jamaa zap hasa wazazi .
Lakini pia kwa ajili ya kupokea pesa kwa sababu zamani walitumiwa kwenye EMS au Money Telegram .

Kuna aina Fulani ka ukiritimba na kula pesa za wanafunzi kwa kusema zitumwe kwa namba ya mwalimu hasa kwa wanafunzi wa sekondari. Dunia na mifumo yake inauonevu mkubwa sana na kujengea watu hofu na stress TU bila sababu.
Kila weekend yaani jumamosi jumapili wanafunzi wote wananafasi ya kupiga simu kwa wazazi ndugu na jamaa kupitia simu za waalimu wote wanapewa namna hiyo ya mawasiliano bado wanapaswa wawe chini ya uangalizi wa waalimu
 
Simu ni muhimu kwa mwanafunzi Kama ataitumia vizuri, hapo alitakiwa mzazi aitwe mtoto aadhibiwe na simu kupewa mzazi.
Rudi ukadai simu
 
Zamani tulikua tunaandika barua wenyewe Kila Jumamosi tunapewa barua zetu Toka kwa ndugu na jamaa .

Hata ukiwa na shida unaandika barua .

Je, kwa sasa wanafunzi matatizo yao wanayafikishaje kwa jamaa zao ?

Nadhani simu za vitochi zingeruhusiwa kwa ajili ya kiwasiliana na jamaa zap hasa wazazi .
Lakini pia kwa ajili ya kupokea pesa kwa sababu zamani walitumiwa kwenye EMS au Money Telegram .

Kuna aina Fulani ka ukiritimba na kula pesa za wanafunzi kwa kusema zitumwe kwa namba ya mwalimu hasa kwa wanafunzi wa sekondari. Dunia na mifumo yake inauonevu mkubwa sana na kujengea watu hofu na stress TU bila sababu.
Sijui sana kuhusu hiyo shule ila shule niliyosoma Mimi advanced level tulikuwa haturuhusiwi kuja na simu shuleni ila line tulikuwa tunaruhusiwa kuwa nazo.

Halafu shuleni kulikuwa na simu ndogo za kutosha ukihitaji kuwasiliana na yoyote sio tu mzazi , unakwenda unaacha Kitambulisho chako unapewa simu tumia ukimaliza rudisha

Na ni shule ya serikal.
 
Je, kwa sasa wanafunzi matatizo yao wanayafikishaje kwa jamaa zao ?
Ndomaana kuna ma patron (wasimamizi wa bweni wakiume) na ma matron (wasimamizi wa kike).
Nadhani simu za vitochi zingeruhusiwa kwa ajili ya kiwasiliana na jamaa zap hasa wazazi .
Ukiwaruhusu unadhani watatafuta jamaa zao ama wazazi kama unavyosema? Wanafunzi wanamambo yako kichwani​
Kuna aina Fulani ka ukiritimba na kula pesa za wanafunzi kwa kusema zitumwe kwa namba ya mwalimu hasa kwa wanafunzi wa sekondari. Dunia na mifumo yake inauonevu mkubwa sana na kujengea watu hofu na stress TU bila sababu
Hili la hofu ni kweli, na nimelizungumzia sana katika Thread 'TANZANIA MPYA: Taifa Lenye Raia Wanaojiamini Wenye Kuleta Maendeleo' unaweza kulisoma na kupigia kura kama linatija.​
 
Sijaona nchi yenye malimbukeni kama yetu. Ni unafiki kwa kwenda mbele. Hivi mwanafunzi wa sekondari tena form 6 kuwa na simu kuna shida gani? Ndiyo maana mijitu ikianza kazi inakuwa na roho ngumu kama mawe, kila saa ni ofisini ni kisirani na huduma hakuna.
Basi pambana na mwalimu mkuu kamnase makofi kwanini alimpokonya simu mwanafunzi. Sasa shule umeifata mwenyewe na ina taratibu zake unakuja kutulalamikia hapa! Walezi wengine kax kweli. Mtoto akiharibikiwa unaanza kutafuta mchawi tena. unamlaumu nani?

We shule ulizosoma ulikua unaruhusiwa kuwa na simu? Huo utandawazi umeutoa wapi kwasababu baada ya kupiga simu huyo mwanao ataanza kuwaonesha wenzake video za porn then nini kitafuata?

Ndo nnachopiga kelele, watu kuwa over exposed! Hata kama yeye hayajui hayo mambo ya porn lakini kuna mwenzake atamuona ataomba aangalie kwenye mitandao.

Subiri kikao kijacho cha shule nyoosha kidole elezea huu ushubwada. Watakupigia makofi mengi
 
Naona huko juu unapambana kuuliza kama mahakamani atashinda. Usipoteze muda. Utaulizwa hivi; sheria za shule zinasemaje? Ulisoma joining instructions? Kipengele cha kifaa cha kielectroniki kinaruhusiwa?

Usije ukajiponza ukafukuzwa au kufutiwa hata hayo matokeo.

Kwanza wewe mwenyewe ndo huyo mwanafunzi, huna akili unatusumbua tu hapa. Hakuna mzazi au mlezi anaeweza kuja hapa kuandika huu ujinga.

Wenzako wanakujaza ujinga uende kudai sasa jichanganye nenda. Kila la kheri
 
Ndio maanz kizaz cha sasa kuw na ninadhamu n ngumu maan ata wew mlez wake upo upande wa mdogo wako mnasak ligi

Achen upuuz
 
nna mdogo wangu alikua shule moja mkoa wa Dodoma, akakamatwa na simu shuleni na mkuu wa shule akiwa form 6 siku chache kabla ya mtihani.mkuu akakaa na simu hiyo na mdogo wangu alipomaliza shule akadai simu yake lakini mkuu wa shule amegoma kumrudishia na anadai simu imeharibiwa.Ni kweli sheria ya shule hiyo simu ikikamatwa inataifishwa lakini je sheria za nchi zinasemaje,shule inatumia sheria gani kutaifisha mali ya mtu?
Dogo soma
 
akienda mahakamani kuidai je uwezekano wa kulipwa upo?

Mlisaini joining instructions ya shule?? Ilikuwa na hiko kipengele?? Kama ulisaini na kipo, imekula kwenu!!

Mnanikumbusha watoto dhehebu fulani wa Ifunda Technical waliandamani ili waruhusiwe kuvaa kofia na kanzu shuleni!! Walifukuzwa wote ilihali wamesaini joinining instructions ya shule ambayo inatoa mwongozo wa mavazi!!

Joining instructions ni mkataba wa huduma mnaoingia kwa hiari baina ya mteja na mtoa huduma!! Unakubalika kisheria kama mikataba mingine yeyote isitake kuleta habari za kusema sijui by laws zinatoka kwa sheria mama!!

Jifunze kuhusu sheria za mikataba
 
Kila weekend yaani jumamosi jumapili wanafunzi wote wananafasi ya kupiga simu kwa wazazi ndugu na jamaa kupitia simu za waalimu wote wanapewa namna hiyo ya mawasiliano bado wanapaswa wawe chini ya uangalizi wa waalimu
Yani mwanafunzi wa form six kwa nini atumie simu ya mwalimu kuwasiliana na wazazi wake.
Form six anauelewa wa kutosha.

Hili liangaliwe vizuri. Wapewe ruhusa ya kuwa na vitochi sio smartphone.

Haya mambo yanatatiza mana Kuna kilio kikubwa cha watoto kulawitiwa au kubakwa na walimu .
Hii ni kutokana na vitisho na kificho .
Mtoto anapewa simu ya mwalimu anapiga simu amesimamiwa na mwalimu hivyo anashindwa kueleza kwa wazi unyanyasaji anaoupitia.

Matokeo yake inakuja kubainika too late.

Dunia imebadilika ,tuliosoma boarding school zamani tulikua na uhuru wa kuandika barua Moja kwa Moja kwenda kwa wazazi ,ndugu,marafiki mpaka nje ya nchi. Zilikua zinapitia posta na zinaletwa kila siku . Ukiwa na shida unawasiliana na jamaa Yako Moja kwa moja.

Barua za urafiki ,mapenzi ya ujana zilikua nyingi sana kama njia ya kurefresh akili tu.

Leo wanafunzi wananyimwa njia ya kuwasiliana na wazazi wao kwa uhuru lakini vitoto vidogo vinapelekwa beach kukaa uchi vikitazama vibabu na vibibi vya kizungu vikiwa uchi ufukweni. Wakirudi wanakua na picha za hovyo kichwani kwa muda mrefu.
Wanatunzi wanajengewa woga mkubwa sana mashuleni na baadhi ya walimu kutumia mwanya huo kuwafanyia vitendo vya kikatili ikiwemo kulawitiwa .

Hili liangaliwe kwa undani zaidi.
Miaka ya nyuma ilikua vigumu sana kusikia mwalimu amemlawiti mwanafunzi.
Kwanza angepokea kichaoo kikubwa sana na mgomo mkubwa ungefuata.

Tunajenga kiizazi laini lkama kuku wa kisasa.
Ndio maana siku hizi wakifika vyuo vikuu wanasumbuka sana na masuala ya mahusiano na hata kujiua . Wanakua kama wametoka gerezani.

Vijana wa kidato Cha sita wanapaswa kujitambua zaidi kuliko kujengewa hofu.

Wanatakiwa wapewe ruhusa ya kuwa na visimu vidogo vya mawasiliano tu . Na muda wa mawasiliano utengwe.
Wanaoridheshwa majina ya wale wenye simu . Zinakusanywa kila Jumatatu asubuhi kupewa Kila Jumamosi asubuhi ili wawasiliane Kwa uhuru na jamaa zao.
 
Yani mwanafunzi wa form six kwa nini atumie simu ya mwalimu kuwasiliana na wazazi wake.
Form six anauelewa wa kutosha.

Hili liangaliwe vizuri. Wapewe ruhusa ya kuwa na vitochi sio smartphone.

Haya mambo yanatatiza mana Kuna kilio kikubwa cha watoto kulawitiwa au kubakwa na walimu .
Hii ni kutokana na vitisho na kificho .
Mtoto anapewa simu ya mwalimu anapiga simu amesimamiwa na mwalimu hivyo anashindwa kueleza kwa wazi unyanyasaji anaoupitia.

Matokeo yake inakuja kubainika too late.

Dunia imebadilika ,tuliosoma boarding school zamani tulikua na uhuru wa kuandika barua Moja kwa Moja kwenda kwa wazazi ,ndugu,marafiki mpaka nje ya nchi. Zilikua zinapitia posta na zinaletwa kila siku . Ukiwa na shida unawasiliana na jamaa Yako Moja kwa moja.

Barua za urafiki ,mapenzi ya ujana zilikua nyingi sana kama njia ya kurefresh akili tu.

Leo wanafunzi wananyimwa njia ya kuwasiliana na wazazi wao kwa uhuru lakini vitoto vidogo vinapelekwa beach kukaa uchi vikitazama vibabu na vibibi vya kizungu vikiwa uchi ufukweni. Wakirudi wanakua na picha za hovyo kichwani kwa muda mrefu.
Wanatunzi wanajengewa woga mkubwa sana mashuleni na baadhi ya walimu kutumia mwanya huo kuwafanyia vitendo vya kikatili ikiwemo kulawitiwa .

Hili liangaliwe kwa undani zaidi.
Miaka ya nyuma ilikua vigumu sana kusikia mwalimu amemlawiti mwanafunzi.
Kwanza angepokea kichaoo kikubwa sana na mgomo mkubwa ungefuata.

Tunajenga kiizazi laini lkama kuku wa kisasa.
Ndio maana siku hizi wakifika vyuo vikuu wanasumbuka sana na masuala ya mahusiano na hata kujiua . Wanakua kama wametoka gerezani.

Vijana wa kidato Cha sita wanapaswa kujitambua zaidi kuliko kujengewa hofu.

Wanatakiwa wapewe ruhusa ya kuwa na visimu vidogo vya mawasiliano tu . Na muda wa mawasiliano utengwe.
Wanaoridheshwa majina ya wale wenye simu . Zinakusanywa kila Jumatatu asubuhi kupewa Kila Jumamosi asubuhi ili wawasiliane Kwa uhuru na jamaa zao.
Huyo bado ni mwanafunzi
Kama unataka hivyo jenga shule yako ufanye hivyo utakavyo
 
Mimi ni mwalimu kiuhalisia hakuna sheria za wizara au za nchi zinazozuia mwanafunzi kumiliki simu,ni utashi na sheria uchwara za walimu na shule

Mimi nimemiliki smu kwa kificho nilipokuwa kidato cha tano na sita na asilimia 99.9 ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita walikuwa na simu japo sheria za shule zilikuwa zinakataza.

Ni wajibu waserikali kutoa tamko/mwongozo wa kuwaongoza walimu na wanafunzi juu ya matumizi sahihi ya simu kwa dunia ya leo ,huku ni kubinya uhuru wa wanafunzi hasa huyu wa kidato cha tano na sita ambaye ni mtu mzima,wengi wao ni miaka 18/19/20 sasa huyu unazuiaje? Wakati huo mwenzake aliyeenda vyuo vya kati mfano diploma au certifivate level akiruhusiwa kumiliki simu
 
Back
Top Bottom