Hii kwa wanaume wote

Hyrax

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2023
Posts
964
Reaction score
2,675
Tabia ya tamaa imewaangusha wanaume wengi sana till date: Tamaa ya fedha, tamaa ya kutaka maisha ya juu kupita uwezo, tamaa ya wanawake, tamaa ya kutaka kuyafikia mambo makubwa kupita uwezo.

Mpaka umri huu nilionao nimeshuhudia marafiki zangu 58 wakipata madhira mbalimbali kwasababu ya tabia ya tamaa zilizozidi kiasi; Kati ya hao kuna waliopo jela mpaka sasa, kuna waliopo mahabusu za muda mrefu, kuna waliotekwa na waliouwawa kwa visasi, waliokufa kwa magonjwa makubwa, wengine wanateseka hospitalini kwa mgonjwa yasiyoeleweka, wachache waliobaki hai kwasababu ya tamaa zao kuzidi kiasi kwasasa wanaishi maisha magumu sana kwasababu ya mitego ya madeni, kushiriki shirki kwa waganga na mmoja huyu yeye aliamua kuacha jinsia yake sasa ni shoga aliyeolewa huko Ujerumani.

We mwanaume na kijana unayepambana kufikia ndoto zako Nachotaka kukwambia ni kwamba fanya yote kwa kiasi kwa maana TAMAA IKIZIDI KIASI LAZIMA UTENDE DHAMBI, DHAMBI IKIZIDI KIASI LAZIMA UINGIE KIFONI.

Asanteni
 
Ukawahesabu marafiki zako yaani 1,2,3... hadi 58????
 
Ni vizur zaidi kwa mwanaume kua na tamaa ya mafanikio kupitia kilimo na ufugaji my friends 🐒
 
Kwaiyo wanaoteseka na magojwa hospitalini walikuwa na tamaa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…