Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Sheria ungekuwa unatunga wewe ?
Bunge letu halitungi sheria, bali muswaada wa sheria huletwa na serikali halafu bunge linaujadili, kuupitisha( tena kwa bunge hili LA 11) huo muswaada hubaki ukipigiwa makofi na kupongezwa badala ya kuboreshwa.

Sent from my TECNO F3 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna kada inayolipa kama siasa nchi hii. Mtu anaacha kazi yake anaingia siasani, 5yrs on ana kibunda cha 230milioni. Acheni masihara na siasa.
 
Miazi sita Wazee wanadao huu mwaka wa 2
 
Hakuna haki Mkuu, wanasiasa Ni kundi linaloongoza kufilisi nchi yetu
 
Wabunge walifanywa vichaa baada ya Spika kuliharibu kimaslahi. Safari hii ndio litakuwa baya zaidi likiongozwa na ngongoti.
 
Unahitaji kwanza kufanya mambo haya matatu, halafu endelea na mengine:
1. Usiwaamini wanasiasa;
2. Usiwaamini wanasiasa; na
3. Usiwaamini wanasiasa.
 
Mleta mada yeye kaona katika hili wa kulaumiwa ni Magufuli na ccm tu,ila mie naona hawa wanasiasa wa upinzani ndio wanatakiwa kulaumiwa kwa unafki wa kutopigia kelele masuala yenye kugusa masilahi yao.
Wapo radhi kuandaa kiki zao za kipumbavu ndo ujue jinsi gani walivyoukuwa wabinafsi na Rejea kisa cha mbwa wa nasari alivyouwawa kwa risasi uongozi wa chama CDM walikusanyika kwenda kumzika mbwa full makamera na hata hao wanasiasa wa chama tawala halikadhalika...hii inchi ina mfumo mbovu sana juu ya kutetea mtu wa tabaka la chini...ukitaka kuona rangi yao halisi wakate posho za vikao vya bunge ndo utawaona front wakitafuta huruma ya wananchi. Yaani wapinzania walinisikitisha sana haswa Chadema walishindwa hata kwenda front baada ya tukio la lissu badala yake wapo tweeter wanatweet ugoro tu.

Watu tunateseka huku tuna vimilioni vyetu kwenye akaunti za mifuko ya hifadhi ya jamiii hizo kalenda sasa kama unafukuzia demu wa kihindi....Wanasiasa angalieni na watu watabaka la chini sio wanaumia huku...nyie mkija majimbo mbwembwe nyingi maneno mengine anayatumia kuwaomba wawasaidie kupita,mkishapita mnawa dump this is not fear
 
Usawa hautakuwepo kamwe
Hata kama huo usawa usipokuwepo lakini haki itendeke kwa kila mtu apate chake kwa wakati sio mtu ana amana yake lakini haipati kwa wakati tena kwa kuisujudia ....Je ingetokea hao wabunge waliohudumu hizo nafasi na kuja kulipwa mafao yao baada ya 70 tena kwa kuwasujudia watu ungewaona humo bungeni?..Kikubwa serikali itengeneze utaratibu wa kuwasaidi hawa wastaafu kupata chao mapema bila ya kughuza hii itasaidia watu kutokufa kwa kihoro maana kazini anawajibika kwa kutoa jasho ikifika wakati wa mafao nao atoe jasho.
 
Ila mbunge mpinzani mwenzio anakula mema ya nchi.
 
Hao jamaa wajanja wametugawa tusiwe wamoja hatuwezi kuwa na sauti moja,leo humu ukisema uhoji yale waliyoyafanya wabunge wetu majimboni utaona watu wanaanza kuwatetea wabunge wao.
 
Kama wabunge wa ccm awamu hii ni hasara kabisa wamekula bure Kodi zetu, wametumia mda kumsifia mungu wao kuliko kuzuia matumizi mabaya ya Kodi zetu.
Bunge limekuwa kibogoyo Kama Umoja wa Africa kushindwa kumlinda Gaddafi asiuwawe na mabeberu.
 
Hawa jamaa hawana utofauti wowote ndio walewale tu wamefanikiwa kutugawa kuna watu hawagundua unafki wa hawa wapinzani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…