Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Kuna siku hapa nikasema hapa hapa huyu TandaleOne mbona ni Nape?halafu Butimba TTC kuna Advance?...na kumbe Tz Diploma unaweza soma kwa mwaka mmoja?ebu jipange
 
Uongo wa karne...angekwenda boarding kwa qualification zipi?? Kusoma EGM kwa F ya Basic Mathematics?? Kwenda zako huko katafute wajinga wenzio hapa si mahala pake.

Mkuu unajua huyu mleta wasifu alikuwa anacopy kama mnyika alivyoandika kuwa hakupenda kusoma shule za serikali basi na Nape naye akupenda kukaa boarding tatizo Mnyika alitoa Reason ila yeye kapepesa macho
 
Hiyo imekaaje kaka, Butimba TTC ni Chuo Cha Ualimu, huwa wanafundisha na EGM, n.k? i had no idea about that

Nahisi hujasoma,na kama umesoma ni katika ngazi ya chini sana(kama sivyo niwie radhi). Unapoona title au status ya shule/chuo sio lazima specifically iwe kinachofundishwa ni hicho unachoona kwenye title pekee,kwa mfano TTC sio lazima iwe ualimu pekee,kuna shule zinaitwa Technical school kwa mfano Moshi Technical,Tanga,lakini kuna wanafunzi wamesoma PCB katika shule hizi,hujaelewa nini.
 
Nahisi hujasoma,na kama umesoma ni katika ngazi ya chini sana(kama sivyo niwie radhi). Unapoona title au status ya shule/chuo sio lazima specifically iwe kinachofundishwa ni hicho unachoona kwenye title pekee,kwa mfano TTC sio lazima iwe ualimu pekee,kuna shule zinaitwa Technical school kwa mfano Moshi Technical,Tanga,lakini kuna wanafunzi wamesoma PCB katika shule hizi,hujaelewa nini.
Mimi ni mwenyeji sana Mwanza, na ni mdau wa Elimu. Nakifahamu vema chuo cha Butimba TTC, hakina A level.

Tena kuna shule ya sekondari ya Butimba, nayo inaishia Form IV.
 
Alishindwa hata kutaja jina la mkuu wa mkoa yeyote?

noo majimaji ni kwenye history civics ni tanzania ilipata uhuru lini,rais wa kwanza? Muungano, rangi za bebdera ya taifa n.k
 
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC


Wadau naomba na mimi nijaribu kurekebisha hali ya hewa iliyochafuliwa humu na mleta mada - TandaleOne.

Ni kweli kabisa pale chuo cha ualimu Butimba Mwanza miaka hiyo ya 1990 hadi mwanzoni mwa miaka ya 2000 pale Butimba TTC walikuwa wanafundisha masomo ya A-level na hatimaye mwanafunzi anakuja kufanya mtihani wa A- level kama PRIVATE CANDIDATE. Hilo halina ubishi kwa yeyote aliyesoma Butimba TTC analifahamu hilo.

lakini hii ilikuwa ni maalumu tu kwaajili ya walimu waliokuwa wanajiendeleza kielimu kutoka ualimu daraja la IIIA kwenda diploma ambapo walisoma kwa mwaka mmoja kama A-level private students na baadaye wanamalizia mwaka wa pili elimu ya diploma na kutunukiwa na baraza la mitihani cheti cha A-level pamoja na kile cha diploma. Na hapo chuoni watu hawa walikuwa wakijulikana/fahamika kwa jina maarufu la UGAD (up grading advanced level to diploma) na kwa vile nape naye anaisoma thread hii kwa sasa basi atanikosoa kama nimekosea. Mama Kabaka (waziri wa kazi) akiwa kama mkuu wa chuo wakati huo na mama Malingumu kama mwadili noma, wengine ni pamoja na mwl machange, ndibalema, lubasa, kilonzo nk.

Ishu ambayo imenifanya nichangie pamoja na kuweka sawa hali ya hewa iliyochafuliwa na TANDALEONE ni kutokuona nape akitajwa kama mwalimu, maana asingeweza kusoma A-level Butimba TTC kama hakuwahi kuwa mwalimu maana sifa moja kubwa ya kusoma UGAD mtu alipaswa kuwa ni mwalimu (hasa shule za msingi)

Sasa hapo kwenye red bila kumtaja nape kwamba ni mwalimu binafsi inanitia shaka juu ya hii "CV" tuliyoletewa
 
Last edited by a moderator:
Nampenda nape lakini kwa f ya civics sitomsamehe? why lakini?


hapa ndipo huwa namfuatilia hyu Msanii R.o.m.a anapoimba kila neno huwa lina maana na lilishatokea hapa nilikuwa sjaelewa aliposema ''elimu zetu bongo ni za kuunga unga''
nikajua anazungumzia wale wanatafuta C kila mwaka!!!!
 
Kama wakati huo alipata hivyo, ingekuwa mwaka huu sijui. Nape, ananikumbusha jamaa mmoja alikuwa na mdomo mrefu kweli kama kiranja, lakini darasani alikuwa na pressure.
 
Mjinga yeye au wewe unayetudanganya kuwa kasoma EGM huku ana mswaki wa hesabu?? au ndo wale wale form four filure?? I doubt. Uwezo wako wa kudangganya mdogo sana..

Kweli uwezo wake katika kudanganya ni mdogo sana,ukiwa mwongo yapasa uwe na kumbukumbu nzuri,angalia sasa huyu jamaa alivyojikanyaga hapo juu,mara Nape hakupenda boarding wakati alihama day o level na kwenda bweni,ooh mara Butimba TTC High School,mara Private Candidate!Yaani ni full kujikanyaga!
 
mbona umetoa matokeo ya primary....
lakin ya secondar hujatupa?
 
aisee,nchimbi amepata phd pale mzumbe akiwa kiongozi kwenye awamu ya jk,nape naye kapata hiyo anayosema digrii na masters kipindi hikihiki cha JK,hapa kuna utata!!!
halafu mbona nape ni kilaza namna hii?
 
Mkuu jielekeze kwenye Hoja ya msingi...BUTIMBA kuna EGM?Ilikuwaje EGM kwa matokeo ya D na F?

Majibu ya swali lako,labda ungejibu na hili kwa niaba ya Mnyika(maana mwenyewe hawezi kujibu zaidi ya kutunga swali),Mnyika alitaka kupata Bachelor degree kwa matokeo yepi ya Form six? Au kwa kifupi,alijiunga chuo kwa matokeo yepi?Tujuze alipata credits gani kwenye masomo yote ya A-level.
 
Elimu ni elimu hata kama kahitimu kwa msuli(Rejea degree za uongo za akina Nchimbi/Kamala)

Hongera sana Nape kwa kutokata tamaa!CHADEMA tusipinge kila kitu jamani na ni wakati huu sasa tumshauri MB Mnyika amalize degree yake!
 
Mtu wa Shamba,
Una uhakika hiyo Butimba sio center ya mitihani ya A-level pia?

Kwa muda mrefu sasa vyuo vya ualimu pia ni center ya mitihani ya form four na six.

Muhimu hapa ni kuangalia je huo mwaka 2000 kweli nape alifanya mitihani hiyo? Lakini hili la kwamba Butimba sio A-level nafikiri mnapoteza nguvu bure. Vyuo vyote sasa vina centers za mitihani. Ukitaka ingia website ya NECTA na angalia kama kuna center ya mitihani ya Butimba.

Mimi ni mwenyeji sana Mwanza, na ni mdau wa Elimu. Nakifahamu vema chuo cha Butimba TTC, hakina A level.

Tena kuna shule ya sekondari ya Butimba, nayo inaishia Form IV.
 
Hongera Nape kwa kuwaacha mbali KIELIMU viongozi waandamizi wa Chadema ambao ni: Mbowe (Form Six), Arfi (Standard Four), Mnyika (Form Six), Nyerere (Form Four), Mr 2 (Form Four)

Ongeza na Lameck Airo mbunge wa Rorya (La Saba),Lusinde (La Saba),Lukuvi (La Saba)
 
Back
Top Bottom