Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Naomba taarifa hii nzima kama unayo. Taarifa hii inaweza kutoa direction ya fursa ya uwekezaji.

Ukiacha mkoa wa DSM na majiji ambao vyanzo vyao vinatokana na uchumi wenye mjumuiko wa vitu vingi mikoa mingine ina kitu ambacho data hizo hazijakiweka wazi.

Nimeona Iringa na Njombe, halmashauri zao zinafanya vizuri sana. Na line ya Wilaya zote kutoka Iringa hadi Tunduma zinafanya vizuri sana. Nini kipo nyuma ya mapato hayo?

Nimeangalia baadhi ya sehemu Halmashauri za Wilaya zimefanya vizuri kuliko Manispaa husika. Natamani kujua chanzo cha mapato hayo, mfano Muleba DC imefanya vizuri kuliko Bukoba MC, Kilwa DC kuliko Lindi MC, etc.

Zipo baadhi ya sehemu kama Kahama, Geita TC, Tarime DC sababu ni madini. Halmashauri za Pwani kuna viwanda, hao wengine nini kimewabeba?

Kama ni kilimo tujue ni kilimo kipi kusaidia wananchi wajue walime nini. Pili kama ni kwa sababu ya structure ya kodi/tozo/ushuru kwenye mazao fulani ni vema liwe wazi pia.
Taarifa ndio hiyo kwenye pdf kama ilovyowekwa na Serikali

Kuna Halmashauri zingine zina Eneo kubwa na vimiji au vijiji vilivyochangamka kibiashara kwa hiyo vinakuwa na fursa nyingi kimapato kigen their population.

Pili kuna Halmashauri zina Mazao ya kilimo ya biashara na chakula ambayo yanauzwa sehemu nyingi za nchi na Dunia kwa mfano Mbozi(kahawa),Njombe(Miti,chai,parachichi), Mjinga (kahawa)Tunduru (Korosho),Kilwa (Mazao ya samaki nk)Muleba (Kahawa)

Halmashauri za ukanda wa Iringa hadi Tunduma ni mambo ya kilimo cha Mazao ya biashara,kilimo,viwanda vidogo na biashara maana ziko kwenye ukanda wa njia kuu ya kwenda nchi za Kusini mwa Afrika.

Mikoa ya Nyanda za Juu shughuli kubwa ni kilimo biashara cha Mazao ya chakula na biashara,miti,viwanda vidogo na biashara.

Ni mpaka uingie Tamisemi uchambue Halmashauri moja baada ya nyingine ndio utapata picha kamili shughuli za kiuchumi zilizoko Eneo husika
 
Ndugu zangu wa Singida wanazembea somewhere. Wangetumia fursa ya uadimu wa mafua kulima alizeti, wangetoka. Wizara ya kilimo ikapige kambi Singida ku boost kilimo cha alizeti.
Kweli mkuu maana inashangaza hadi Singida Manispaa ni hamna kitu
 
Dodoma Imeingiaje?
Waulize Tamisemi but hiyo Dodoma usiichukulie simpo kuna uwekezaji mkubwa unaendelea kule,juzi tuu nimeona kampuni kubwa ya Burundi wanawekeza kiwanda cha kutengeneza mbolea zaidi ya dola mil.400 hapo unazungumzia trioni moja,usisahau kiwanda cha kusafisha dhahabu na miradi mingi inayoendelea pale

Tena hayo mapato ya Dom yameshuka walipouza viwanja walifikosha bil.73
 
Iringa ipo vizuri mno,ukijumlisha Hizo sehemu zake ukiachana njombe nadhani ilitakiwa kuwa ya 3 katika hiyo orodha ,hongereni sana wana wa iringa,kazi iendeleeeeee
Mkuu ya tatu kivipi mimi nimetoa vigezo vya Mji/Halmashauri sio kimkoa,hata hivyo pdf hapo chini imetoa summary ya kimkoa
 
Sasa mkuu umeweka halmashauri yangu akati nikijicheki mfukoni kuna masalia ya maganda ya karanga tu?[emoji16] halmashauri nyingi znabebwa na uwepo wa natajiri wakubwa tu, unaweza kukuta hiyo kodi ni ya watu wachache sana.
Hiyo ni personal issue iko nje ya uwezo wangu,hizo pesa wamelipa watu ko na wewe fanya wanachofanya utapata pesa
 
Muleba imeizid bukoba mjini yenye bandari na viwanda na viwanja vya ndege naomba nielimishwe kidogo.

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Unaweza kuta mengi ya mapato ya Bukoba ni yale ambayo TRA wanakusanya ,tafuta regional statistics za TRA unaweza kuta Kagera iko vizuri

Lakini kwa mapato ya mtu mmja mmja na vyanzo ambavyo Tamisemi inasimamia basi huo ndio ukweli kwamba mna pesa kiduchu hapo Manispaa uchwara ya Bukoba,TRA hiyo hapo check kama mpo
 

Attachments

Unaweza kuta mengi ya mapato ya Bukoba ni yale ambayo TRA wanakusanya ,tafuta regional statistics za TRA unaweza kuta Kagera iko vizuri

Lakini kwa mapato ya mtu mmja mmja na vyanzo ambavyo Tamisemi inasimamia basi huo ndio ukweli kwamba mna pesa kiduchu hapo Manispaa uchwara ya Bukoba
Nimekupata mkuu

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Lakini Makambako tunakosaje hapo?
Njombe wameigawa hovyo hovyo kieneo Halmashauri za Wilaya ya Njombe Vijijini,wangin'gombe na Makambako zina eneo dogo sana Kama Makambako wangekuwa na Njombe Vijijjini wangeingia.

Hata hao Njombe TC wameingia kwa kuwa wana eneo kubwa sana la kiutawala ambalo ni zaidi ya KM 100 kutoka mjini.

By the way Mkoa wenu wa Njombe bado unaongoza kwa kipato cha MTU Moja moja kwa Tanzania ukitoa Mkoa wa Dar es Salaam na Kilimanjaro.
 
Ifuatayo ni orodha ya Miji na Halmashauri 36 ambazo watu wake Wana kipato cha Uhakika na kuwa na purchasing power inayotoa fursa ya uhakika wa biashara kwa Tanzania.
Orodha imehusisha Halmashauri zenye mapato yanayoanzia shilingi za Tanzania bilioni 3.5 kwenda juu.

Orodha hii imetokana na makusanyo ya ndani ya kila Halmashauri kiutoka kwenye vyanzo vya mapato vya Halmashauri ambavyo ni shughuli za kawaida za wananchi kutoka Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
Mapato hayo ni nje ya vyanzo vinavyokusanywa na TRA na wakala zingine za.serikali.

Kama wewe ni mfanyabiashara hii itakuwa picha halisi ya uchaguzi wa sehemu ya kuwekeza.

1.Dar (Na Halmashauri zake zote)=173.3bln

2.Dodoma CC=53.2bln

3.Mwanza City incl. Ilemela MC=22.4bln

4.Arusha City=19.2bln

5.Mbeya City=13.0bln

6.Tanga City=12.8bln

7.Geita TC=9.2bln.

8.Morogoro MC=7.5bln

9.Kahama MC=7.12bln

10.Chalinze DC=7.1bln

11.Mkuranga DC=6.6bln

12.Mufindi DC=6.1bln

13.Moshi MC=5.7bln

14.Iringa MC=5.62bln

15.Njombe TC=5.6bln

16.Tunduma TC=5.4bln

17.Tarime DC=5.2bln

18.Kilolo DC=5.0bln

19.Mtwara MC=4.8bln

20.Mafinga TC=4.7bln

21.Tunduru DC=4.7bln

22.Muleba DC=4.61bln

23.Kilwa DC=4.6bln

24.Geita DC=4.5bln

25.Arusha DC=4.01bln.

26.Mlimba DC=4.0bln

27.Rungwe DC=3.89bln

28.Mbozi DC=3.97bln

29.Tandahimba DC=3.92bln

30.Mbarali DC=3.9bln

31.Kilosa DC=3.8bln

32.Mbeya DC=3.8bln

33.Mbinga DC=3.65bln

34.Chato DC=3.64bln

35.Kibaha TC.3.62bln

36.Chunya DC=3.5bln

My take kuna Mikoa/Miji ni ya kuonea huruma mfano Tabora,Singida,Rukwa,Katavi,Kigoma,Simiyu na Manyara.Hii mikoa haina hata Halmashauri moja yenye mapato kwa kiwango cha kuanzia bilioni 3.5 au zaidi

Kiufupi inatoa picha ya hali mbaya ya umaskini wa kipato kwa wananchi wake.Hali kadharika Mikoa ya Dar, Mbeya,Geita na Iringa ina hali nzuri ya kimapato kwa watu wake.

Pdf ya Tamisemi hii hapa [emoji116][emoji116] unaweza kujionea mwenyewe
View attachment 1763405
Uzi wa maana sana kwa wenye kujua ya maana. Kudos mkuu.

Wenye kutu ya SIASA vichwani mwao huu uzi hautakuwa na msaada kwao...sana sana wataishia kuuharibu tu.
 
Back
Top Bottom