Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Mufindi kuna viwanda vya Mbao,Pareto, Chai......mchina amejaa tele kwenye mbao saizi pale
Kweli kabisa sasa hivi mufindi Kuna viwanda vingi vya mchina kwa vijana wanaotafuta maisha bila kujali ugumu wa kazi njoo mufindi hakika hautojuta
 
Ifuatayo ni orodha ya Miji na Halmashauri 36 ambazo watu wake Wana kipato cha Uhakika na kuwa na purchasing power inayotoa fursa ya uhakika wa biashara kwa Tanzania.
Orodha imehusisha Halmashauri zenye mapato yanayoanzia shilingi za Tanzania bilioni 3.5 kwenda juu.

Orodha hii imetokana na makusanyo ya ndani ya kila Halmashauri kiutoka kwenye vyanzo vya mapato vya Halmashauri ambavyo ni shughuli za kawaida za wananchi kutoka Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
Mapato hayo ni nje ya vyanzo vinavyokusanywa na TRA na wakala zingine za.serikali.

Kama wewe ni mfanyabiashara hii itakuwa picha halisi ya uchaguzi wa sehemu ya kuwekeza.

1.Dar (Na Halmashauri zake zote)=173.3bln

2.Dodoma CC=53.2bln

3.Mwanza City incl. Ilemela MC=22.4bln

4.Arusha City=19.2bln

5.Mbeya City=13.0bln

6.Tanga City=12.8bln

7.Geita TC=9.2bln.

8.Morogoro MC=7.5bln

9.Kahama MC=7.12bln

10.Chalinze DC=7.1bln

11.Mkuranga DC=6.6bln

12.Mufindi DC=6.1bln

13.Moshi MC=5.7bln

14.Iringa MC=5.62bln

15.Njombe TC=5.6bln

16.Tunduma TC=5.4bln

17.Tarime DC=5.2bln

18.Kilolo DC=5.0bln

19.Mtwara MC=4.8bln

20.Mafinga TC=4.7bln

21.Tunduru DC=4.7bln

22.Muleba DC=4.61bln

23.Kilwa DC=4.6bln

24.Geita DC=4.5bln

25.Arusha DC=4.01bln.

26.Mlimba DC=4.0bln

27.Rungwe DC=3.89bln

28.Mbozi DC=3.97bln

29.Tandahimba DC=3.92bln

30.Mbarali DC=3.9bln

31.Kilosa DC=3.8bln

32.Mbeya DC=3.8bln

33.Mbinga DC=3.65bln

34.Chato DC=3.64bln

35.Kibaha TC.3.62bln

36.Chunya DC=3.5bln

My take kuna Mikoa/Miji ni ya kuonea huruma mfano Tabora,Singida,Rukwa,Katavi,Kigoma,Simiyu na Manyara.Hii mikoa haina hata Halmashauri moja yenye mapato kwa kiwango cha kuanzia bilioni 3.5 au zaidi

Kiufupi inatoa picha ya hali mbaya ya umaskini wa kipato kwa wananchi wake.Hali kadharika Mikoa ya Dar, Mbeya,Geita na Iringa ina hali nzuri ya kimapato kwa watu wake.

Pdf ya Tamisemi hii hapa [emoji116][emoji116] unaweza kujionea mwenyewe
View attachment 1763405
tunduru inaizidi Arusha, hebu acheni uchawi basi, mlogage kwengine
 
Naomba taarifa hii nzima kama unayo. Taarifa hii inaweza kutoa direction ya fursa ya uwekezaji.

Ukiacha mkoa wa DSM na majiji ambao vyanzo vyao vinatokana na uchumi wenye mjumuiko wa vitu vingi mikoa mingine ina kitu ambacho data hizo hazijakiweka wazi.

Nimeona Iringa na Njombe, halmashauri zao zinafanya vizuri sana. Na line ya Wilaya zote kutoka Iringa hadi Tunduma zinafanya vizuri sana. Nini kipo nyuma ya mapato hayo?

Nimeangalia baadhi ya sehemu Halmashauri za Wilaya zimefanya vizuri kuliko Manispaa husika. Natamani kujua chanzo cha mapato hayo, mfano Muleba DC imefanya vizuri kuliko Bukoba MC, Kilwa DC kuliko Lindi MC, etc.

Zipo baadhi ya sehemu kama Kahama, Geita TC, Tarime DC sababu ni madini. Halmashauri za Pwani kuna viwanda, hao wengine nini kimewabeba?

Kama ni kilimo tujue ni kilimo kipi kusaidia wananchi wajue walime nini. Pili kama ni kwa sababu ya structure ya kodi/tozo/ushuru kwenye mazao fulani ni vema liwe wazi pia.
Wewe unajua kuchambua data na wawekezaji wote wana sifa hii. Sio wengine wanafyatuka na mitaji kwenda kujilipua
 
Njombe wameigawa hovyo hovyo kieneo Halmashauri za Wilaya ya Njombe Vijijini,wangin'gombe na Makambako zina eneo dogo sana Kama Makambako wangekuwa na Njombe Vijijjini wangeingia.

Hata hao Njombe TC wameingia kwa kuwa wana eneo kubwa sana la kiutawala ambalo ni zaidi ya KM 100 kutoka mjini.

By the way Mkoa wenu wa Njombe bado unaongoza kwa kipato cha MTU Moja moja kwa Tanzania ukitoa Mkoa wa Dar es Salaam na Kilimanjaro.
Kutoka mjini kwenda wapi wewe mbususu..Njombe to Makambako ni km 80 hizo km 100 ni kuelekea wapi wakati unajua Mji unazungukwa na Halmashauri za Vijijini

Visingizio kibao wakati unajua fika kwamba Makambako ni kijiji kikubwa ndio kwanza kinaanza kutambaa
 
Uzi wa maana sana kwa wenye kujua ya maana. Kudos mkuu.

Wenye kutu ya SIASA vichwani mwao huu uzi hutakuwa na msaada kwao...sana sana wataishia kuuharibu tu.
Inasaidia hata serikali yenyewe kujua wapi iongeze nguvu kuibua na kusaidia maeneo maskini huku iliyapromote haya yenye unafuu
 
Mimi mwenyew nashangaa.
Hadi wilaya ya misenyi yenye viwanda kama kagera sugar,kilimo cha vanilla,mpaka wa mutukula na Ranchi kibao inazidiwa na wilaya ya muleba iliyojaa migomba na kahawa
Hiyo migomba na Kahawa ndio vinagusa raia mmja mmja directly kuliko manamba na vibarua wa viwandani mnaowalipa 130,000 per month
 
Kweli kabisa sasa hivi mufindi Kuna viwanda vingi vya mchina kwa vijana wanaotafuta maisha bila kujali ugumu wa kazi njoo mufindi hakika hautojuta
Yeah niliona hapo nilikuwepo kama week hivi
 
TUNAPOPIKA DATA TUWE TUNATUMIA UBONGO SIO MAKALIO.
HIVI DODOMA INAWEZA KUIZIDI MWANZA AU ARUSHA KWA MAPATO???
Pole mkuu ,upike kusaidia nini labda au umesoma mada na attachment yake?

Kubali tuu mkuu kutangulia sio kufika huo ndio ukweli wenyewe na bado mtalia sana
 
Kigoma Ujiji Mc na Kyela dc wanakwama wapi wote wana maziwa makubwa ya uvuvi, wote wanalima mawese na mazao mengine ya kibiashara, wote pia wana advantage kubwa ya kuwa mpakani kabisa na nchi jirani, shida inakuwa wapi
Sijui shida iko wapi hasa Kigoma japo kwa Kigoma inaonekana kuna urasimu Sana unawekwa na Serikali kufanya biashara na DRC huwa naona wafanyabiashara wanalalamika Sana.

Mji na mkoa kama Kigoma ilifaa wawe wanachangia Sana mapato nchi hii
 
Hakuna kupika data ni ukweli hata JPM aliwahi kusema Dodoma wanakusanya zaidi ikawa imepita Dar ukigawa Dar zile halmashauri ila kwa ujumla ukichukuwa Dar kama moja siku zote Dar iko juu 173 Billion Halmashauri zote za Dar ila ukianza kugawa ziko Halmashauri kama Temeke, Kindondoni wako nyuma kwa hiyo Dodoma wanakusanya na huu mwaka wa 3. Halafu upike data ili iweje na ukiangalia kweli huko Kigoma sijui Tabora ina reflect makusanyo yao.
Ni kweli ukizigawa moja moja Dom inazipita vizuri tuu,nakumbuka ule mwaka juzi Dom waliuza Sana viwanja wakapiga bil.73 ndio iliongoza kwa Halmashauri moja moja watu wakapagawa.

Dom unakuja Kazi Sana na viwanda vinajengwa Sana
 
Back
Top Bottom