Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Ndugu zangu wa Singida wanazembea somewhere. Wangetumia fursa ya uadimu wa mafuta kulima alizeti, wangetoka. Wizara ya kilimo ikapige kambi Singida ku boost kilimo cha alizeti.
Alizeti inalimwa lakini hakuna support kutoka serikalini
 
Umeandika mlimba hiyo mlimba ya morogoro? Mbona kilombero umeiyacha, ina maana makusanyo ya tanesco na kilombero suger hawaingizi kipato cha kutosha?
sina uhakika km Tanesco wanapozalisha umeme wa Kidatu wanalipa kwa Halmashauri au Sugar wanapouza sukari Nchi nzima naona malipo yanaenda Serikali kuu
 
Ifuatayo ni orodha ya Miji na Halmashauri 36 ambazo watu wake Wana kipato cha Uhakika na kuwa na purchasing power inayotoa fursa ya uhakika wa biashara kwa Tanzania.
Orodha imehusisha Halmashauri zenye mapato yanayoanzia shilingi za Tanzania bilioni 3.5 kwenda juu.

Orodha hii imetokana na makusanyo ya ndani ya kila Halmashauri kiutoka kwenye vyanzo vya mapato vya Halmashauri ambavyo ni shughuli za kawaida za wananchi kutoka Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
Mapato hayo ni nje ya vyanzo vinavyokusanywa na TRA na wakala zingine za.serikali.

Kama wewe ni mfanyabiashara hii itakuwa picha halisi ya uchaguzi wa sehemu ya kuwekeza.

1.Dar (Na Halmashauri zake zote)=173.3bln

2.Dodoma CC=53.2bln

3.Mwanza City incl. Ilemela MC=22.4bln

4.Arusha City=19.2bln

5.Mbeya City=13.0bln

6.Tanga City=12.8bln

7.Geita TC=9.2bln.

8.Morogoro MC=7.5bln

9.Kahama MC=7.12bln

10.Chalinze DC=7.1bln

11.Mkuranga DC=6.6bln

12.Mufindi DC=6.1bln

13.Moshi MC=5.7bln

14.Iringa MC=5.62bln

15.Njombe TC=5.6bln

16.Tunduma TC=5.4bln

17.Tarime DC=5.2bln

18.Kilolo DC=5.0bln

19.Mtwara MC=4.8bln

20.Mafinga TC=4.7bln

21.Tunduru DC=4.7bln

22.Muleba DC=4.61bln

23.Kilwa DC=4.6bln

24.Geita DC=4.5bln

25.Arusha DC=4.01bln.

26.Mlimba DC=4.0bln

27.Rungwe DC=3.89bln

28.Mbozi DC=3.97bln

29.Tandahimba DC=3.92bln

30.Mbarali DC=3.9bln

31.Kilosa DC=3.8bln

32.Mbeya DC=3.8bln

33.Mbinga DC=3.65bln

34.Chato DC=3.64bln

35.Kibaha TC.3.62bln

36.Chunya DC=3.5bln

My take kuna Mikoa/Miji ni ya kuonea huruma mfano Tabora,Singida,Rukwa,Katavi,Kigoma,Simiyu na Manyara.Hii mikoa haina hata Halmashauri moja yenye mapato kwa kiwango cha kuanzia bilioni 3.5 au zaidi

Kiufupi inatoa picha ya hali mbaya ya umaskini wa kipato kwa wananchi wake.Hali kadharika Mikoa ya Dar, Mbeya,Geita na Iringa ina hali nzuri ya kimapato kwa watu wake.

Pdf ya Tamisemi hii hapa [emoji116][emoji116] unaweza kujionea mwenyewe
View attachment 1763405

Mmeambiwa watumishi muache kuvujisha nyaraka za Serikali, hiii kauri huwa siielewi kabisa mie
 
Mmeambiwa watumishi muache kuvujisha nyaraka za Serikali, hiii kauri huwa siielewi kabisa mie
Hii sio nyaraka ya kuwa siri ipo kwenye tovuti ya Tamisemi,nimeambatanisha mada hii na pdf kutoka kwenye hotuba ya Waziri wa Tamisemi
 
Naomba taarifa hii nzima kama unayo. Taarifa hii inaweza kutoa direction ya fursa ya uwekezaji.

Ukiacha mkoa wa DSM na majiji ambao vyanzo vyao vinatokana na uchumi wenye mjumuiko wa vitu vingi mikoa mingine ina kitu ambacho data hizo hazijakiweka wazi.

Nimeona Iringa na Njombe, halmashauri zao zinafanya vizuri sana. Na line ya Wilaya zote kutoka Iringa hadi Tunduma zinafanya vizuri sana. Nini kipo nyuma ya mapato hayo?

Nimeangalia baadhi ya sehemu Halmashauri za Wilaya zimefanya vizuri kuliko Manispaa husika. Natamani kujua chanzo cha mapato hayo, mfano Muleba DC imefanya vizuri kuliko Bukoba MC, Kilwa DC kuliko Lindi MC, etc.

Zipo baadhi ya sehemu kama Kahama, Geita TC, Tarime DC sababu ni madini. Halmashauri za Pwani kuna viwanda, hao wengine nini kimewabeba?

Kama ni kilimo tujue ni kilimo kipi kusaidia wananchi wajue walime nini. Pili kama ni kwa sababu ya structure ya kodi/tozo/ushuru kwenye mazao fulani ni vema liwe wazi pia.
Pdf hii ya wizara ya TamisemiView attachment HOTUBA YA WN OR TAMISEMI 2021.22.pdf
 
Kweli kabisa sasa hivi mufindi Kuna viwanda vingi vya mchina kwa vijana wanaotafuta maisha bila kujali ugumu wa kazi njoo mufindi hakika hautojuta
Shida ya huko baridi Kali balaa na vumbi LA kutosha
 
Ni kweli ukizigawa moja moja Dom inazipita vizuri tuu,nakumbuka ule mwaka juzi Dom waliuza Sana viwanja wakapiga bil.73 ndio iliongoza kwa Halmashauri moja moja watu wakapagawa.

Dom unakuja Kazi Sana na viwanda vinajengwa Sana
Kuna watu walishasema wanauza viwanja wakaambiwa kwani nyinyi hamna viwanja. Kuna sababu Dodoma wanauza na kuhamia serikali na wafanyakazi wote hiyo ni boost kubwa sababu nchi hii bado katika kukopesha wafanyakazi wa serikali wanapata urahisi na biashara inawafuata.
 
Moshi inatia huruma na zile safari za kuhesabisa hamna kitu ,kimji cha kizamani kimechoka kama taulo la guest
Japo 'umewaua' kwa kuwa ni ngome ya watani zako kisiasa ila kiukweli Moshi ni moja ya miji isiyo na fursa kabisa.

Hakuna ardhi, ukabila unaathiri sana uwekezaji wa watu kutoka maeneo mengine kwa kuwa biashara zinafanyika 'kindugu'. Moshi nadhani jamii kutoka maeneo mengine kwa zaidi ya 90% ni watumishi.

Ndiyo maana watu wa Moshi/Kilimanjaro wamesambaa maeneo mengine ya nchi kusaka fursa kwa kuwa kwao ni 'mtihani'.

Moshi unaweza itafuta buku hata wiki nzima, kitu labda cha maana kwa mtu wa kuja ni lile soko la mitumba (King George Memorial) na hapo uwe unaenda kuuza nje ya mkoa wa Kilimanjaro.

Pia watu wa Kilimanjaro wana namna fulani ya 'ubahili' kwenye purchasing ya bidhaa na huduma. Kitu pekee wananunua bila kuwaza ni bidhaa za pombe na nyama ambazo nazo wanaangalia ni bar ya nani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Then unaskia sera za majimbo unabaki kujiuliza hayo majimbo yangefanya maendeleo kwa mapato gani?
Taarifa km hizi ni muhimu sana watu kua nazo kabla hawajaropoka kuhadaa uma.
Tena Majimbo ndio yangesaidia Sana mikoa dizaini ya Singida ku maximize their full potential kuliko saizi ambapo wanajua hata tukikusanya mia watapata ruzuku ya serikali kuu sasa hii sio fair
 
Japo 'umewaua' kwa kuwa ni ngome ya watani zako kisiasa ila kiukweli Moshi ni moja ya miji isiyo na fursa kabisa.

Hakuna ardhi, ukabila unaathiri sana uwekezaji wa watu kutoka maeneo mengine kwa kuwa biashara zinafanyika 'kindugu'. Moshi nadhani jamii kutoka maeneo mengine kwa zaidi ya 90% ni watumishi.

Ndiyo maana watu wa Moshi/Kilimanjaro wamesambaa maeneo mengine ya nchi kusaka fursa kwa kuwa kwao ni 'mtihani'.

Moshi unaweza itafuta buku hata wiki nzima, kitu labda cha maana kwa mtu wa kuja ni lile soko la mitumba (King George Memorial) na hapo uwe unaenda kuuza nje ya mkoa wa Kilimanjaro.

Pia watu wa Kilimanjaro wana namna fulani ya 'ubahili' kwenye purchasing ya bidhaa na huduma. Kitu pekee wananunua bila kuwaza ni bidhaa za pombe na nyama ambazo nazo wanaangalia ni bar ya nani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kelele nyingi moshi hakuna jipya
 
Back
Top Bottom