Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Hii ndio orodha ya Miji na Wilaya za Tanzania zenye watu wenye kipato cha Uhakika

Mapato ya halmashauri hayadecide purchasing power ya eneo husika..

Mapato ya TRA ndiyo yanadecide..
Huo ndio uongo sasa,Mengi ya mapato ya Halmashauri ni shughuli za uchumi za moja kwa moja za wananchi unlike kwenye TRA ambako asilimia kubwa ni kodi ya biashara kubwa na corporate

Sasa kwa mantiki hiyo ni wazi nature ya mapato ya Halmashauri yanatoa picha halisi ya uchumi wa mtu mmja mmja na purchasing power ya watu.

Hata hivyo ukija pia kwenye makusanyo ya TRA still hizo Halmashauri zita feature kwenye list kama kawaida
 
Mufindi kuko vizuri sana mkuu, sema tu marehemu alivuruga mambo mengi sana. Miti saa hizi imeshuka bei hivyo wajanja hawavuni wanasubiri bei ipande juu tena.
Sio tuu Mufindi bali Iringa na Njombe kwa ujumla wake hususani wilaya za Mufindi,Kilolo na Njombe.

Hao wanalima miti na Mazao ya miti,chai,pareto,matunda anuai na Mazao ya chakula kama viazi mviringo.

Njombe na Kilolo ni game changer unlike Mufindi imekuwa hivyo miaka mingi.Mathalani kwenye Takwimu za mapato mwaka 2020/21 hadi february Njombe TC ilishaweka kibindoni 5 bln ikiwa na miezi 4 bado so by 30 June watafikisha mark ya zaidi ya bil.6 au saba,come next year nitakuja na data husika.

Ni swala la Muda tuu Njombe na Kilolo kuizidi Mufindi maana tatizo lilikuwa miundombinu hasa Kilolo ni moja ya wilaya fertile Sana na sehemu kubwa ya Eneo ni virgin

Serikali ingekuwa sikivu ingefungua barabara kwa lami kutoka Iringa Kilolo hadi Ifakara,ile barabara ni muhimu sana kiuchumi
 
Muleba imeizid bukoba mjini yenye bandari na viwanda na viwanja vya ndege naomba nielimishwe kidogo.

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Nafikiri Muleba ina eneo kubwa Kama wilaya na hivyo kuwa na vyanzo vingi. Asilimia kubwa ya visiwa vya ziwa Victoria vilivyopo mkoa kagera viko ndani ya Muleba hivyo pesa kutokana na uvuvi ni kubwa, kilimo hasa kahawa, ndizi, vanilla, n.k
 
Ifuatayo ni orodha ya Miji na Halmashauri 41 pekee kati ya Halmashauri 165 Tanzania ambazo watu wake Wana kipato cha Uhakika na kuwa na purchasing power inayotoa fursa ya uhakika wa biashara kwa Tanzania.
Orodha imehusisha Halmashauri zenye mapato yanayoanzia shilingi za Tanzania bilioni 3.5 kwenda juu.

Orodha hii imetokana na makusanyo ya ndani ya kila Halmashauri kiutoka kwenye vyanzo vya mapato vya Halmashauri ambavyo ni shughuli za kawaida za wananchi kutoka Tamisemi kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
Mapato hayo ni nje ya vyanzo vinavyokusanywa na TRA na wakala zingine za.serikali.

Kama wewe ni mfanyabiashara hii itakuwa picha halisi ya uchaguzi wa sehemu ya kuwekeza.

1.Ilala MC=58.6bln

2.Dodoma CC=53.2bln

3.Kinondoni MC=44.5bln

4.Temeke MC=34.4bln

5.Arusha City=19.2bln

6.Ubungo MC=17.9bln

7.Mbeya City=13.0bln

8.Tanga City=12.8bln

9.Mwanza CC=12.2bln

10.DSM CC=11.4bln

11.Ilemela MC=10.2bln

12.Geita TC=9.2bln.

13.Morogoro MC=7.5bln

14.Kahama MC=7.12bln

15.Chalinze DC=7.1bln

16.Mkuranga DC=6.6bln

17.Kigamboni MC=6.4bln

18.Mufindi DC=6.1bln

19.Moshi MC=5.7bln

20.Iringa MC=5.62bln

21.Njombe TC=5.6bln

22.Tunduma TC=5.4bln

23.Tarime DC=5.2bln

24.Kilolo DC=5.0bln

25.Mtwara MC=4.8bln

26.Mafinga TC=4.7bln

27.Tunduru DC=4.7bln

28.Muleba DC=4.61bln

29.Kilwa DC=4.6bln

30.Geita DC=4.5bln

31.Arusha DC=4.01bln.

32.Mlimba DC=4.0bln

33.Mbozi DC=3.97bln

34.Tandahimba DC=3.92bln

35.Mbarali DC=3.9bln

36.Rungwe DC=3.89bln

37.Kilosa DC=3.8bln

37.Mbeya DC=3.8bln

38.Mbinga DC=3.65bln

39.Chato DC=3.64bln

40.Kibaha TC.3.62bln

41.Chunya DC=3.5bln

My take kuna Mikoa/Miji ni ya kuonea huruma mfano Tabora,Singida,Rukwa,Katavi,Kigoma,Simiyu na Manyara.Hii mikoa haina hata Halmashauri moja yenye mapato kwa kiwango cha kuanzia bilioni 3.5 au zaidi

Kiufupi inatoa picha ya hali mbaya ya umaskini wa kipato kwa wananchi wake.Hali kadharika Mikoa ya Dar, Mbeya,Geita na Iringa ina hali nzuri ya kimapato kwa watu wake.

Pdf ya Tamisemi hii hapa [emoji116][emoji116] unaweza kujionea mwenyewe

View attachment 1764113
Sasa nimeelewa why Magufuli alivunja iliyokuwa halmashauri ya jiji.Maana nimeona Ilala MC,Temeke MC,Kinondoni MC halafu tena DSM CC.Sasa sijui Hilo eneo la Dar lipo wapi
 
Huo ndio uongo sasa,Mengi ya mapato ya Halmashauri ni shughuli za uchumi za moja kwa moja za wananchi unlike kwenye TRA ambako asilimia kubwa ni kodi ya biashara kubwa na corporate

Sasa kwa mantiki hiyo ni wazi nature ya mapato ya Halmashauri yanatoa picha halisi ya uchumi wa mtu mmja mmja na purchasing power ya watu.

Hata hivyo ukija pia kwenye makusanyo ya TRA still hizo Halmashauri zita feature kwenye list kama kawaida
Kwahiyo watu wa Tanga City wana maisha mazuri kuliko wa Moshi MC au Iringa MC??

Unataka kusema Tandahimba wanaishi au wana maisha mazuri kuliko Hai, Masasi, Songea, Njombe??
 
Iweke hapa tuone mkuu
Magufuli alipiga marufuku kutoa takwimu za mikoa baada ya kuona watu tunarefer tunachokichangia kwenye pato la taifa then haturudishiwi chochote..

Kwa kifupi tu ukiangalia data za TRA wakati wanaweka collections za mikoa, ya Kwanza ni Dar, Arusha inafata Kilimanjaro ndio Mwanza. Yaani Mwanza ilikuwa inazidiwa mpaka na Kilimanjaro. Last time walikuwa wakiweka hivyo ni 2018 au 2017 sina kumbukumbu nzuri..

Ngoja nikatafute then nirudi hapa kama bado zitakuwapo..
 
Sio lazima Korosho mkuu pia huko kuna madini na hardwood timbers na Mazao mengine
Unaongea na mtu ambaye huko kote nacheza.. Tena huwa siishii mjini tu, napita mpaka vijijini kwahiyo hali halisi naijua..

Huwezi kuiweka Tunduru mbele ya Masasi au Nachingwea kwa hali yeyote ile..
 
Income inequality ni kubwa sana hapa Tz hicho sio kigezo cha kujua economic status ya mtu wa kawaida, kwa mfano mwz na dar kuna matajiri ni 1% wanao changia hiyo kodi 99% ni maxhinga mama tilie ambao ni mzingo kwa almashauri kuwahudumia hao watu......Dar na Mwz zinaongoza kwa watu wanao shindwa kupata milo mitatu kwa siku ila kimapato ndo wanaongoza.
Kula milo mitatu kwa siku ni Food Abuse
 
Sio lazima Korosho mkuu pia huko kuna madini na hardwood timbers na Mazao mengine
Pitia hizi data za TRA mwaka 2019..

Kilimanjaro iko nyuma ya Arusha na Dar peke yake kwenye almost kila collection
 

Attachments

Sasa nimeelewa why Magufuli alivunja iliyokuwa halmashauri ya jiji.Maana nimeona Ilala MC,Temeke MC,Kinondoni MC halafu tena DSM CC.Sasa sijui Hilo eneo la Dar lipo wapi
Alivunja mwaka huu kwa hiyo mwakani hutaiona hiyo dsm cc
 
Pitia hizi data za TRA mwaka 2019..

Kilimanjaro iko nyuma ya Arusha na Dar peke yake kwenye almost kila collection
Hao nao wawe Wana update data yaani tuko 2020/21 bado wanaleta Takwimu za 2018/19 tena zinaishia kota ya tatu
 
Back
Top Bottom