Wajameni tusiishi kwa kukariri, miaka 5 ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali umezalisha na kuvutia fursa nyingi za biashara, ujenzi, huduma na viwanda
Nani hajui kwamba Dom ni hot spot ya ujenzi kwa sasa nyuma ya Dar,both kwa private sector na public sector? Unapojenga manake kwamba sekta ya ujenzi inakua kwa hiyo mapato kutoka huko ni makubwa ambayo ni leseni za biashara,kuuza viwanja,vibali vya ujenzi na kodi mbali mbali
Lakini pia Dodoma kuwa makao makuu manake kwamba ina wakazi wengi ambao Wana purchasing power kubwa kuliko miji mingi ukiondoa Dar,tafsiri yake ni kwamba biashara nyingi zimehamia huko kufuata hao wanunuzi.
Kana kwamba haitoshi uwekezaji wa viwanda na biashara nyingine kubwa kubwa unashika kasi,mfano mdogo retail sector kwenye sekta ya mafuta ya magari imekua Sana kiasi kwamba vituo vya mafuta ni vingi Sana Dom nyuma ya Dar tuu.
Hata viwanda vinajenga Sana tuu,juzi Kati hapa karibu wazindue kiwanda cha kuchakata dhahabu kama kile cha Mwanza,pia kampuni ya Burundi inajenga kiwanda kikubwa cha mbolea,dola za marekani milioni 400 zinawekwa.
On top of that population ya Dom saiz ni kubwa nyuma ya Dar,Mwanza juu ya hapo ni population yenye pesa tofauti na ya Miji mingine.
Stay tuned,utashangaa zaidi