Hii ndio picha bora ya wiki nchini Tanzania, imepigwa Kigoma

Hii ndio picha bora ya wiki nchini Tanzania, imepigwa Kigoma

CHADEMA - KIINGEREZA NA TEKNOLOJIA NI LAZIMA KWA SHULE ZOTE ZA SERIKALI ILI VIJANA WAPATE UFUNGUO WA MAISHA



CHADEMA leo tarehe 21 May 2023 wamehitimisha ziara yao ndefu ya kila jimbo ndani ya mkoa wa Kigoma katika Operesheni 255 iliyo ingia mpaka ngazi ya vijiji pia tarafa kupitia mikutano ya hadhara kutoa elimu ya uraia kuhusu Haki, Uhuru, Demokrasia na Maendeleo ya Watu.

Ziara hii ya mafanikio makubwa sasa itahamia mkoa mwingine Tanzania bara.
 
Njombe, Tanzania

KAZI YA KIONGOZI NI KUSHUGHULIKA NA MATATZO YA WATU - Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Nyasa Mh. Peter Msigwa



Katika hotuba yake Mchg. Peter Msigwa alaumu serikali kupuuza maendeleo ya watu katika maeneo nyeti huku vigogo wa serikali wakitumbua kodi za wananchi kwa matumizi ya anasa mfano magari ya kifahari ya gharama za kufa mtu kama VX8 huku kinamama wajawazito wanalazimika kulipia Tshs. 300,000 wanapokwenda kujifungua pia hakuna huduma za maji katika maeneo ya makaazi ....
Safi sana

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
CHADEMA KIJIJINI MNANILA BUHIGWE KIGOMA OPERESHENI 255

Wananchi mamia wa kijiji cha Mnanila washika vifua vyao na kusema Mbowe we love You, we missed You kwa kipindi cha miaka 6 ....


Operesheni hiyo kali ya kisiasa ya siku 4 mkoani Kigoma leo imepita Kasulu Mjini
, Muyama kwenda hadi Munzese na kuishia Mungonya ambapo CHADEMA inaongea na wananchi wa majimbo ya mkoa wa Kigoma kutoa elimu ya uraia na kuimarisha chama.

Mwenyekiti Freeman Mbowe awaelezea wananchi wa Kasulu na Kigoma kuwa chama cha siasa kikiwa hakijengi mazingira ya kuwepo Maendeleo ya Watu katika biashara, ukulima, ufugaji n.k wakiache na kuchagua CHADEMA ili wawe huru kukihoji inapokengeuka kwani chama dola kongwe CCM hakiamini katika uhuru huo...

Asnte san Bagamoyo
 
CHADEMA - KIINGEREZA NA TEKNOLOJIA NI LAZIMA KWA SHULE ZOTE ZA SERIKALI ILI VIJANA WAPATE UFUNGUO WA MAISHA



CHADEMA leo tarehe 21 May 2023 wamehitimisha ziara yao ndefu ya kila jimbo ndani ya mkoa wa Kigoma katika Operesheni 255 iliyo ingia mpaka ngazi ya vijiji pia tarafa kupitia mikutano ya hadhara kutoa elimu ya uraia kuhusu Haki, Uhuru, Demokrasia na Maendeleo ya Watu.

Ziara hii ya mafanikio makubwa sasa itahamia mkoa mwingine Tanzania bara.

HIi 255 imezaa matunda sana
 
Hapana, hii ndio picha ya mwezi!
IMG_2807.jpg
 
Kasulu, Kigoma
Tanzania

MKUTANO WA CHADEMA WA OPERASHENI 255, KTK KATA YA KITANGA KASULU VIJIJINI



Mamia ya wananchi wa kata ya Kitanga wajitokeza kwa wingi kumsikiliza Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Mh. Freeman Mbowe

Kitanga ni kata ya Wilaya ya Kasulu Vijijini katika Mkoa wa Kigoma nchini Tanzania. Wenyeji wa kata hiyo shughuli yao kubwa za kiuchumi zimejikita katika sekta ya Kilimo na Ufugaji .

Changamoto nyingine mbali ya ktk kilimo na ufugaji , ni miundo mbinu ya barabara kutoka vijiji vya Makere, Kitanga, Asante Nyerere, Kigabye, Kalela, Kwaga, Rusesa, Muzye, Bugaga na Kagerankanda n.k kwenda Kibondo ni barabara ambayo inasimamiwa na TANROADS, Mkoa wa Kigoma. Kuna changamoto katika Daraja hili la Mto Malagarasi, eneo hili ndiyo wananchi wa Kitanga wanapata shida kuvuka kwenda Kibondo.

Kabla mwenyekiti wa CHADEMA hajahutubia, wananchi walipewa fursa ya wazi kutoa dukuduku lao kuhusu mambo mbalimbali mbele ya umma uliofurika katika Ziara ya kikazi ya Operesheni 255 ya CHADEMA nchini kote .

Muhila kabisa apo
 
Back
Top Bottom