Hii ndio sababu Magenius hawawezi kuwa matapeli

Hii ndio sababu Magenius hawawezi kuwa matapeli

Katika aya ya kwanza nadhani kuna tofauti mimi niliwahi mno kuongea
Niko very sensitive
Nikikaa nje halafu mtu anataka kuniita namfikia kabla hajanyanyua mdomo
Kwenye kupika nako hivyo hivyo nikiunguza labda nina stress sana.

Kuna vitu vingi mno hata nikiwa kwenye biashara naweza mpoint mtu nikamwangalia mpaka akanunua bidhaa namna nilivyotarajia

Nina sense vitu vingi vya baadae
Naongea kidogo nikiwa najisikia naongea sana

Mwanangu sasa yeye haongei kabisa, ila baba yake akiwa njiani anakwambia naenda kumpokea baba na hapo sijamwambia na pengine sijui
Mara atakwambia mvua hiyo mkikaa dakika kadhaa mvua inanyesha
Na mambo yake mengi mengi
Ameanza kuongea mdogo sana ila anaongea kwa nadra sana
Duh hata hii sentensi inasound kitapeli sana dah
 
Hizo za kwanza kuna mtoto wa baba mdogo wangu yupo std 2 anazo mpaka wanamuogopa wanatamani hata kumpeleka kwa wataalamu maana

Haongei na watu hata wazazi wake
Anajifungia ndani watoto wenzake wakija kwao
Performance yake ipo low sana (Na hapa ndio wazazi wake wanachanganyikiwa)
 
Duniani tumo binadamu wa aina tatu kiakili na wote tunaishi pamoja in harmony na tumegawanyika katika makundi makuu matatu kiutendaji na utekelezaji wa akili zetu.

Kundi la kwanza ni wale Magenius.. Hawa mabwana wana IQ kubwa kuliko binadamu wa kawaida wana score around (160 - 300) wana uwezo mkubwa sana wa kuchakata taarifa vichwani mwao na kufumbua mafumbo magumu kuliko ila bahati mbaya zaidi hawa asilimia 90% yao ni wagonjwa wa ugonjwa wa usonji( Autism). Ugonjwa wa akili huu, ugonjwa huu wa usonji mara nyingi huwapata wakiwa watoto wa mwaka na nusu na kuendelea. Dalili zao huwa wanapenda kukaa peke yao, hawapendi kelele, wanachelewa kuongea, wana hisia Kali sana za kunusa na kusikia na wako very bright kwenye kitu kimoja pekee. Na pia huwa wanaongea kidogo sana..they only do "small talk" they are not good conversationalist. Sio waongeaji wazuri sana.

Nilifuatilia zaidi na kuyajua mengi juu ya Autism baada ya mpwa wangu kugundulika ana ugonjwa huu wa usonji akiwa na miaka 3..huyu dogo ana miaka 10 tu kwa sasa mnaweza kuwa mmekaa nje akawambia mtoto analia na kweli after a second dogo analia ndani...then mmekaa nje anakwambia maharage yanaungua..na kweli mnasikia harufu ya maharahe kuungua jikoni punde baada ya yeye kusema. Wako very sensitive. Ni wakimya na pia very loner..wanapenda kukaa wenyewe tu na huwa wanaconcetrates na kitu kimoja tu mawazoni mwao huyu dogo shuleni ni mtupu but he is very artistic genius and creative, unaweza ukatembea nae mjini then mkirudi home anadrawing kit yake ya kuchorea tu anachora mji mzima mlimopita kwa usahihi bila kurejea popote pale hadi huwa navurugwa ufahamu ukizingatia Mimi hata kuchora kagari tu siwezi. Nikagundua dogo is genius sababu ya ugonjwa wake wa usonji.

Nikarejea historia ya Michelangelo na Vincent Von Gosh hawa wote walikuwa artistic genius..huyu Van Gosh alikuwa anaweza kuuchora hadi upepo unaovuma..hakyamungu! This is insanely genius..ukingalia kwenye picha zake za starry starry night utaona kazi zake but alikuwa mwehu na michoro hii aliichora akiwa kwenye chumba cha vichaa alipojipiga risasi na kufariki akiwa mpweke sana. Michaelangelo huyu ni balaa yeye hata simzungumzii maana anahitaji Uzi wake kabisa ili tumtendee haki. Tukipata muda tutamjadili.

Albert Einstein Mwanamahesabu na mwanafikizia ambae amebadilisha maisha ya binadamu anaaminika kuwa the most influential scientist of the 20th century, amechangia mengi kwenye aerospace engineering, astrophysics, mathematic, spirituality e.t.c alifanya kazi kubwa ya sisi kuishi hivi Leo kwa theory yake of relativity ya E=MC sqaure ndio theory iliofagia njia ya kutengeneza mabomu ya nyuklia Leo hii. Akiwa na miaka 10 usonji ukiwa umemuandama hakuweza kuongea vizuri wala kuwa na marafiki akiwa na IQ kubwa kabisa aliweza kufaulu somo moja tu la hisabati tu shuleni yaliyobaki alifeli vibaya sana. Alipofikisha miaka 16 alikuwa anaitwa chuoni kusolve complex mathematics equations zilizowashinda maproffesor na akiwa na miaka 25 hakukubaliwa na vyuo vingi maana kwenye mtihani wa kujiunga na chuo alifaulu somo moja pekee mathematics kwa asilimia 100. Watu hawa huwa wanakuwa na ugonjwa wa Usonji unaowafanya kufikiri kitu kimoja tu deeply kutokana na nerve circuit zao zilivyoundwa kwenye brain. Magenius maarufu Waliothibitika kuwa na Autism ni Albert Einstein, Charles Darwin, Sir Issac Newton, Michelangelo, Aristotle, Tesla e.t.c Wengi wao wana muandiko mbaya sana maana mikono yao haiwawezi kuendana na kasi ya ubongo unavyofikiri, hivyo wanajikuta wanaandika fasta na rough ili kukimbizana na kasi ya ubongo wao unachokifikiria.

Tunahitimisha kwa kukubaliana na mwanafalsa maarufu wa ugiriki ya kale kwamba any genius is accompanied with some sense of madness.. Magenius wengi ni vichaa na hii inapigiliwa msumari na kauli hii "too much of anything is harmful " akili ikizidi kipimo muhusika anakuwa hayuko normal na hivyo anakuwa psychiatric Case hivyo ni ngumu sana kichaa kukutapeli maana ni mgonjwa wa akili maana ana complex things kichwani ambazo hata yeye hawezi na hana lugha ya kuzielezea kwa watu wakamwelewa kirahisi atawezaje kukushawishi uingie mkenge!? Jibu ni hawezi kukutapeli maana hata hawana good socializing ability kama wengine. lakini hapa sasa ndipo linapoibuka kundi la watu wengine wanaitwa "intelligent people" watu hatari sana hawa.

Hawa intelligent people bongo zao ziko katikakati kiakili wana uwezo wa kupata maneno sahihi ya kuelezea zile complex ides za genius..hawa uandika hata zile manual zinavoelezea namna ya kutumia vitu mbalimbali vilivyoundwa na magenius kwa lugha rahisi na nyepesi maana wanayo maneno sahihi na ya kueleweka kirahisi, hawa wanaandika kimkakati hoja zao na kuweza kushawishi watu kirahisi sana kama alivyosema Fid Q msanii wa hip hop kwamba "neno zuri huwa halina ukweli na neno baya ndio lenye ukweli " hawa intelligents siku zote Daima dumu wana maneno sahihi na matamu ya kukufanya uuone ukweli au usiuone.. Aina ya watu hawa ni Adolph Hitler, Barack Obama, Hemingway, e.t.c na Kwenye hili kundi wanakaa matapeli pia Kariba ya brother wa Forex n.k sijawahi kuona katika maisha yangu tapeli asie jua kupachika maneno sahihi na matamu kwenye maandishi au maneno yake. Sijawahi kumuona! Mtaji wao ni maneno yake matamu.

Then group la mwisho ni "normal people" au tunafahamika zaidi kama watapeliwa Ahahaha. Sisi tunafit Kwenye social world maana tunaenda clockwise na jamii yetu na bongo zetu hazijisumbui kuchakata taarifa zaidi wala kuconcertrates na kitu kimoja we are carefree hatuna tofauti na simu za Motorola za zamani mwanga ukizima zinazima moja kwa moja hadi ndani tofauti na intelligents ambao wao ni simu janja(smartphone) zenyewe screen ikizima na kuwa nyeusi ujue imezima kinafiki internal background inaprocess more informations kifupi hazilali bongo zao tofauti na normal people sisi ambao ni kundi kubwa akili zetu ni za kawaida sana na ndio akili za binadamu wenye afya na wazima kiakili maana hatuoverload brain zetu na sisi sio wagonjwa wa akili kama hao wawili hapo juu wanaosumbukiwa na Autism na Bipolar disorder.

Tujitahidi tujue mechanism za matapeli na tuwaepuke mapema before its too late.

Na je unadhani wewe unafit group gani hapo juu? Kwanini unahisi group ulilochagua linakufaa? Tupe sababu?
Singependa kutofautiana na wewe kwa yote ulioandika au kusema kwa maana upo sahihi kwa kiwango kikubwa sana. Ila naweka nyongeza inawezekana kwa kutumia lugha na mtazamo mwingine ambao ukiangalia kwa kina utakuta tunaongea jambo moja ambalo linaweza kuonakena tofauti kwa wanaowaza kidogo. IQ kirefu ni Intelligence Quotient ni uwezo wa kujifunza na kufikiri kwa kina(critical thiking) na uwezo wa kufikiri kimantiki( logical thinking) ni utafiti uliofanywa zadi ya miaka 100 iliyopita na mtu kama Francis Gatton na kuanza kufanyiwa majaribio baadaye na mtu kama Alfred Binet sio watu pekee walioendelea kufanya utafiti au majaribio ya kujua uwezo wa akili ni wengi sana na bado wanaendelea. Umeongelea IQ kwa mapana yake na kugawa kiwango cha binadamu katika matumizi ya akili zao katika makundi matatu singependa kurudia ulichoongea kwa urefu maana nipo kuunganisha ulichoongea na ungunduzi mpya zaidi ambao bado wengi pia wanaendelea kuufanyia kazi kwa maana ya matumizi. Kuna ungunduzi mpya wa EQ kirefu chake ni Emotion Intelligence ni uwezo wa kujitambua ambao unasemekana ni bora kuliko IQ. Binadamu ni kiumbe ambacho hakitofautiani sana na wanyama wengine kwa maana ya kuzaliwa na akili ila binadamu amekuwa tofauti na wanyama katika kutumia akili kujifanyia maisha bora zaidi kwa kutatua changamoto zinazojitokeza katika maisha wanyama wamekuwa na uwezo mdogo sana wa kupatia majibu changamoto zinazojitokeza ndio maana Wazungu au ngozi nyeupe zinawafananisha waafrika na wanyama sio kwa ajili ya rangi ya ngozi ila katika uwezo mdogo wa kupatia majibu changamoto tukiwa tumezungukwa na mazingira rafiki kwa maana ya hali ya hewa na rasilimali. EQ ni utafiti takiribani miaka 30 tu iliyopita na Wayne Paynes na kama miaka Ishirini iliyopita watu kama Daniel Goleman ndio waliogundua kuwa EQ ni bora kuliko IQ. Dunia haijalala kila siku kuna mabadiliko ya mazingira kwa maana ya maumbile kutokana na mambo mengi ambayo mengine ni asili lakini mengine yanatokana na maendeleo ya binadamu kutaka maisha bora ambayo yanaongeza athari za kimazingira ni jambo pana sana naweza kuandika kitabu kikubwa sana lakini sio lengo, nataka kueleza kwa kifupi jinsi ugunduzi,utafiti na ubunifu ambao unaendelea kila siku unavyoleta mabadiliko na kuzalisha matajiri na wenye kufikri vizuri kwa maana ya kusaidia wengene kufikri. Kwakua maendeleo ya binadamu yanatokana na uwezo wake wa matumizi ya akili yake kama tulivyoona katika tafiti za IQ na EQ kwa maana ya binadamu kugundua akili ndio kila kitu sasa wanafanya utafiti kujua jinsi akili inavyofanya kazi. Kwa sasa dunia inatengeneza matajiri wengi sana kila siku kutokana na ufahamu wa matumizi ya akili kuongezeka baada ya watu wengi kujua kutumia akili zao kwa kuzipa maarifa kwa maana ya taarifa sahihi kila siku na sasa pia kupata taarifa imekuwa rahisi kuliko kipindi chochote cha nyuma kugundulika kwa EQ kutawezesha dunia kuwa na maendeleo ya ajabu sana miaka Ishirini ijayo maana idadi kubwa zaidi ya wanadamu wenye kujitambua itaongezeka. Kwa leo naomba kuishia hapo ila nafahamu nachoelezea inawezekana sijakuwa na mpangalio mzuri inaweza kusababisha kutumia nguvu nyingi kuelewa ninachomanisha lakini tupo tutaendelea kuhabarishana...............
 
Mkuu uwe una tag mim ila u mwaka post zako zimepungua uku ukileta chakula ya ubongo nitafrai kupata habari mapema🕵🏽
 
We utakuwa Ni tapeli pia, Maana hayo maana hili andiko ladhibitisha ya kuwa ww ni intelligent, na intelligents wengi wao ni matapeli kama ulivodadavua.

Mi nishajijua nipo kundi gani
 
mi nimepewa mtoto ana autism. ni kweli usemayo. yuko vizur mno ila anaish dunia yake. naumia sana nikimuona. na ninampenda mpaka naumwa.
 
Aisee Usonji ni mtindio wa ubongo bhana na sio autism. Autism ni kama Aspergers syndrome. Mi najua wenye usonji ni wale mataila wa kutoa udenda. Labda autism ina jina jingine la kiswahili
 
Hizo za kwanza kuna mtoto wa baba mdogo wangu yupo std 2 anazo mpaka wanamuogopa wanatamani hata kumpeleka kwa wataalamu maana

Haongei na watu hata wazazi wake
Anajifungia ndani watoto wenzake wakija kwao
Performance yake ipo low sana (Na hapa ndio wazazi wake wanachanganyikiwa)
Mtu ambae ni highly intelligent(genius) na aliye chini ya normal( mental defect-upungufu wa akili, ulemavu wa akili) Mara nyingi tabia zao zinashabihiana hasa kwenye suala la ukimya na kukwepa watu hivyo wachunguze yupo kundi lipi maana kuna namna ya kuwatofautisha
 
kuna ka-article flani nilikasoma, kuhusu utafiti wazungu walifanya kwenye hiyo kitu ya genius kuwa born or made.
walichukua identical twins, ambao gene content yao inafanana, then wakatenganishwa wakiwa bado wadogo, kwa maana kwamba bado wako kwenye umri ambao hawajawa na personality zao zinazojitegemea. mmoja aliwekwa kwenye mazingira magumu kuliko mwenzake, na matokeo yakaonesha huyo aliyekuwa kwenye mazingira magumu hata IQ yake ilikuwa ndogo kuliko ya mwenzake.
Naweza sema huyo wa mazingira magumu IQ yake ilidrop kutokana kwamba hakujifunza aliyokuwa akiyajua mwenzake. Ila kama akijifunza anauwezo wa kuwa na IQ sawa na mwenzake
 
Back
Top Bottom