Hii ndiyo njia sahihi (ya kisayansi) ya kuwaumiza 'haters' wako

Hii ndiyo njia sahihi (ya kisayansi) ya kuwaumiza 'haters' wako

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
18,037
Reaction score
33,681
Hakunaga binadamu asiyetaka kuwaprove wrong haters wake. Kuwaprove wrong watu waliokuwa wanasema hatoweza ku accomplish jambo fulani. Hakunaga.Hata Mungu alimruhusu Shetani amjaribu Ayubu kwa sababu alitaka kuprove kitu kwa hater wake.

Kama kuna watu walikuwaga wanasema hutoweza kutimiza jambo fulani nature ya binadamu huwaga ni "Nikifanikiwa lazima wajue".

Ex lover alikuwa anakuzingua kwa sababu ya wewe kutokuwa na vitu fulani fulani eidha hela, mali, kazi, madaraka, kutokuwa na uwezo wa kuzaa etc then ukamove on, siku ukifanikiwa kupata hivyo vitu utataka tu ajue.

Mtaani kwenu kuna haters wanakusimanga wanaponda kazi au biashara unayo fanya etc, wazo la mwanadamu SIKU zote huwa ni "Nikipata maendeleo kupitia hii kazi ninayo ifanya lazima wajue".

Sasa basi kosa kubwa linal fanywa na watu wengi waliofanikiwa kupata vitu ambavyo haters walikuwa wanasema hawatoweza kuvipata ni kutumia nguvu nyingi sana kuwaonesha haters wao kwamba 'I have made it'.

Mfano kupiga picha kwenye mitandao ya kijamii kuonyesha ukiwa una safiri sehemu mbali mbali nje ya nchi, kuonyesha magari, nyumba, mpenzi, happy family etc.

Hilo ni kosa kubwa sana la kiufundi, kwanini? Kwa sababu haters ni wanasaikolojia wazuri sana, wamekuwa wanasaikolojia wazuri kupitia experience ya kuhate watu wengi so wanajua abc za human Psychology.

Ukianza kuwaonyesha haters wako mafanikio yako unakuwa una peleka ujumbe kwao kwamba wao ni watu muhimu kwako ndio maana una waonyeshea mafanikio yako ili kuwaumiza.

So, kwa sababu hiyo hawatoumia beleive me, haters huumia zaidi pale wanapogundua wewe wanaekuhate you don't care about what they think about you. Na kwamba wao sio watu muhimu kwako.

Ufanye nini sasa?

Fanya kama mimi, usitumie nguvu yoyote kuwaonyesha haters wako mafanikio yako.

Mimi nilipo anza kumiliki vitu ambavyo haters walisema sintoweza kuvimiliki nilifanya kinyume. Nilitumia mbinu ya kimedani ya Sun Tzu kwenye Kitabu cha "Art of war" aliposema, "Pretend to be weak when ur strong and strong when ur weak".

Nilitumia nguvu nyingi sana kuuza false image to my haters. Mfano;

1. Nilistop kwenda bar za mtaani, kwanini? Kwa sababu sikutaka watu wajue kwamba nina miliki gari kali; kwenda bar za mtaani kungefanya watu waone kama vile nawaonyeshea sasa nipo na gari kali.

2. Gari langu nili weka vioo tinted, kwanini? Watu wasinione nikiwa naendesha.

3. Si post kuhusu safari zangu za nje ya nchi. Sipost picha ya gari wala nyumba. Sipost kuhusu mpenzi wangu mpya (sikutaka ex wangu avimbe kichwa kuona kama nna muonyeshea nipo na mali mpya).

Nikipost kwenye Facebook napost ujinga ujinga wa Simba na Yanga.

Nikawa busy na mambo yangu sijichanganyi kabisa na watu wa mitaani labda kwenye misiba tu na nikienda kwenye msiba siendi na gari napaki gari nyumbani navaa kawaida na story napiga za ujinga ujinga wa Simba na Yanga.

Ikitokea bahati mbaya nimekutana na mtu wa mtaani katika mazingira yanayo suggest kwamba nina mafanikio basi eidha nita pretend sio mimi au baadae watu wakija kuniuliza (ataenda kutangaza) nakanusha.

Kwa mfano kuna siku nilikuwa mitaa ya Mlimani City ile nafungua mlango kuingia kwenye gari langu ex wangu akaniona akaniita kwa nguvu "Likuuuud", nikamwangalia kama simjui vile nikapanda kwenye gari nikatekenya nikasepa.

Siku tatu baadae nakutana naye mtaani ananiambia ninaringa siku hizi ninaringa kwa sababu nimenunua gari,nilicho mfanyia Mlimani City hatokisahau. nikamwambia sio mimi bana labda umenifananisha, mimi napata wapi pesa ya kununua gari wakati hela ya kula yenyewe tia maji tia maji (alitoa bonge la tabasamu/alifurahi kujua kwamba sikuwa mimi kwenye ile gari)?

Kuna siku nilikutana na jamaa wa mtaani kwetu Dizonga kwenye high classic function (jamaa ni mwanasheria alienda kwenye workshop Dizonga, ni mbea mbea sana); nikamwambia mtu yoyote asijue kama umekutana na mimi huku (nilijua lazima ataongea mtaani na hivyo ndivyo ilivyo kuwa but watu walikuwa wakiniuliza nikawa nakataa).

Mwisho wa siku haters walikuwa ku conclude kwamba "Likud" ni mbinafsi na anadharau. Sasa hivi ameshika vihela hela anazuga hana hela kwa sababu anajua watu wata muomba etc.

Sikuonekana tena kama mtu ambae ninataka kuwaonyeshea watu kwamba nina hela, ningefanya hivyo watu wangeni dharau.

Sasa hivi ninaishi maisha yangu kawaida kwa sababu watu tayari wamesha zoea kwamba nina hela. So, mimi kuwa na gari kali, kusafiri nje siyo kitu cha kushangaza tena kwao.
 
Siku zote huwaga siendeshwi na mitizamo na Maoni ya Watu hasa wasio na mchango wowote kwangu.
Siwezi kujificha Kwa sababu ya Watu wanaonifuatilia. Ninafanya kinachonifurahisha na kinachonipa Faida.

Yaani nisifanye kitu ninachokipenda kisa kuna Zuzu mmoja ATI ananifuatilia?

Kikawaida MTU unatakiwa uishi Maisha yako bila kuangalia Watu wengine. Ilimradi haumuumizi mtu
 
Spiritual%20cleansing_%205%20homemade%20tricks%20%E2%8A%9B%20_%20Ritual_%20(1).jpg
 
Siku zote huwaga siendeshwi na mitizamo na Maoni ya Watu hasa wasio na mchango wowote kwangu...

Point yangu ni usifanye kitu kwa ajili ya kuprove KITU KWA hater wako..

Kama una weka UJUMBE kwenye social network ukisema " Robert Heriel is travelling to London" blv me ur posting that not for you but for other people. Maana yake ni kwamba u care more about other people

Hata hivyo hekima ya mababu zetu onatutaka kutokuonyesha mafanikio yetu KWA watu ambao hawajafanikiwa.

Ni hekima zaidi
 
Mkuu kula maisha acha kujibanabana na kujifichaficha kama pesa za kafara
SASA hivi wamesha zoea . Shida kubwa ya hater ni kwamba ubongo wake una uwezo wa mdogo sana kupokea taarifa ya mafanikio makubwa ya mtu anae mfahamu hasa taarifa hiyo inapokuwa mbichi but after sometimes haters huwa Wana izoea hiyo taarifa na ku move on.

Kwao taarifa ya mtu kufanikiwa huwa wanaipokea kama taarifa ya msiba. Msiba huwa mchungu mwanzoni but after sometime huwa wafiwa wanazoea
 
Point yangu ni usifanye kitu kwa ajili ya kuprove KITU KWA hater wako....

Kiufupi kwenye Maisha haupo kwaajili ya ku-prove Kwa yeyote iwe Followers or haters.

Ishi Maisha yako. Wanakupenda wakupende, wanaokuchukia wakuchukie.

Hiyo haikuhusu.

Ni hekima kutokuonyesha Mafanikio yako Kwa Watu ambao hawajafanikiwa Ila ni utumwa pia kufanya hivyo ikiwa furaha yako ni kujiachia.

Kama furaha yako ni kujiachia, jiachie.

Kama furaha yako ni kujionyeshe,jionyeshe.

Hata siku ukianguka au kurudi Chini usijali kwani ndio Maisha. Hayo.

Mambo ya kuwa- entertain mazuzu huo muda haupo
 
Back
Top Bottom