Hii ndiyo pembetatu ya Bermuda (Bermuda triangle)

Hii ndiyo pembetatu ya Bermuda (Bermuda triangle)

Pembe tatu ya Bemuda ni eneo lililoko bahari ya Atlantiki ikiwa inapakana na Miami ,Bemuda na Puertorico sehemu ambapo meli na ndege nyingi zimepata kupotea katika mazingira tatanishi sana kiasi kwamba watu wameshindwa kuelezea na kujikuta akisema pana maajabu yasiyoelezeka.

katika mazingira hayo yasiyoelezeka na ya kutatanisha kuna moja ya U.S Navy bomber alipoteza uelekeo wa ndege na wakati anaruka kwenye neneo hilo na ndege haijawahi kupatiakana. baadhi ya boti na ndege na meli zimekua zikipotea kwenye eneo hili kwenye mazingira mazuri tu ya hali ya hewa hata bila kuripoti kwamba kuna tatizo la hali ya hewa hutokea tu ghafla. Pamoja na kuwa na nadharia kwamba eneo hilo ni la kuogopwa kutokana na kupotea huko kwa kutatanisha kwa baadhi ya vyomba vaya anga na majini bila kupatikana bado hakuna udhibitisho kwamba ni eneo hatari sana maana kila uchwao bado kuna vyomba vinakatiza eneo hilo salama salimini wa salamat bila kupatwa na maswahibu hayo ya kupotea.

WADAU WA BEMUDA WANASEMAJE

Sehemu hii inayoitwa pembe tatu ya bemuda au pembe tatu ya shetani (Devil’s Triangle) ina ukubwa wa laki tano squire miles ya eneo la bahari upande wa kusini mashariki wa jimbo la Florida marekani. kwa wanahistorial wanamklumbuka mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Christopher Columbus yeye anasema kwamba wakati amefika maeneo haya kwa mara ya kwanza ambapo inasemekana yeye ndio aliyegundua eneo la marekani aliripoti kwamba aliona moto mkubwa ukidondoka eneo hilo na inasadikika kwamba ni kimondo. Anaendelea kwamba baada ya wiki kadhaa palitokea mwanga flani ambao yeye hakuelewa ni wa kitu gani ila wajuzi wa jiografia wanadai ni kimondo hicho. Pamoja na hayo amezungumzia masuala ya kusoma kompasi , ila wadau pia wakasema ni kwa kuwa eneo hilo ndipo kwa kipindi hicho ndipo sehemu chache Duniani ambapo True North na Magnetic North zinapita kwa pamoaja. Hapa kwa wanajiografia wanaelewa zaidi.

Kuna mdau mmoja anaitwa Joshua Slocum yeye alijipatia sifa ya kusafiri baharini mwenyewe ingawaje alipotea mwaka 1909 na inasadikiwa alipotelea kwenye pembe tatu ya bemuda wakti akiwa anaelekea marekani ya kusini kutokea Martha Vineyard.Ingawaje bado kulikua na utata kwamba alipotelea sehemu gani hasa lakini inasadikiwa alipotelea maeneo ya pembe hii yenye maajabu mengi kwenye ulimwengui huu.

William Shakespeare mwanamashairi na plays nguli na mahiri kwenye ulimwengu huu aliwahi kuongelea kwenye play yake “The Tempest,” ambapo wanazuoni wa masuala ya play wanasema alikua akizunguimzia eneo hilo la bemuda na kupotea kwa meli katika eneo hilo. Ingawaje haya yote hayakuteka jamii ya watu mpaka kwenye karne ya 20 ndipo jamii ilianza kuwa na wasiwasi na eneo hili. Hii inapata uzito zaidi pale ndege meli ya marekani ya Navy ilipopotea ikiwa na USS Cyclop ikiwa na ukubwa wa 542 mita urefu na ilikua ya mizigo ikiwa na wanajeshi wa maji 300 na tani elfu kumi za manganese ilipozama maeneo ya karibu na Barbados and the Chesapeake Bay. Meli hiyo haikutuma mawasiliano yoyote pamaja pamoja na kuwa na uwezo wa kufanya hivyo hamna mtu a najuaye ni nini kilichotokea kwenye meli na meli hiyo mpaka leo ni Mungu na bahari tu ndio wanaelewa kilichotokea. Baadae aliyekuwa Rais wa Marekani Woodrow Wilson wakati huo alikuja kudhibitisha kwamba meli mbili ndogo zilizoambatana na meli hiyo kubwa na zenyewe zilikuja kupotea maeneo hayo hayo mwaka 1941.

mfululizo wa kupotea baadhi ya vyombo na vingine kukutwa vimetelekezwa ndio hasa unaowatisha watu kuhusu eneo hilo . Mwaka 1945 five ne navy bombers zilizokua zimebeba watu 14 zikitokea Fort Lauderdale. Hizi zilikuwa zimepelekwa huko kwa ajili ya mazoezi na wanajeshi ila cha kushangaza zilikutwa zimetelekezwa. Inasadikiwa kwamba Compas ya kiongozi wa msafara huo ilishindwa kufanya kazi na wenyewe kujikuta wamepotea baada ya kuzunguka na kuishiwa mafuta na hata hivyo ndege iliyotumwa kwa ajili ya uokozi na yenyewe ilipotea ikiwa na watu 13 ndani. waliwatafuta bila mafaniio na mwishoni wakahitimisha kwamba ilipotea kana kwamba immeelekea sayari ya Mars.

Hapo kwenye mita 542 urefu, hukusema kweli. Meli ndefu zaidi duniani kutengenezwa haijazidi mita za urefu 458.46 nayo ni super tanker yenye jina Seawise Giant.

Hiyo "USS Cyclop" uliyoitaja ilikuwa na mita 165 tu. Pia Inasemekana kuna uwezekano ilizamishwa na wajerumani wakati wa vita kuu ya kwanza kwani ilibeba shehena ya malighafi ya kutengenezea silaha.

Kafanye homework yako tena uje na vitu vya uhakika.
 
Picha iko wapi......ujue vitu vingine bila picha havishawishi aaaagggggrrrrr[emoji21] [emoji21] [emoji21] [emoji21] [emoji21]

Sent using Jamii Forums mobile app
329564.jpg
 
kwann wasitume drone camera's tujee kuna nn vipi hawataki watu wa kujitolea kwenda kufanya utafiti maana mie kila nikickiaga kuhusu ili eneo napata shauku kufika

G.O.M.D
Drones na zenyewe zinapotea Mkuu.
 
Hapo kwenye mita 542 urefu, hukusema kweli. Meli ndefu zaidi duniani kutengenezwa haijazidi mita za urefu 458.46 nayo ni super tanker yenye jina Seawise Giant.

Hiyo "USS Cyclop" uliyoitaja ilikuwa na mita 165 tu. Pia Inasemekana kuna uwezekano ilizamishwa na wajerumani wakati wa vita kuu ya kwanza kwani ilibeba shehena ya malighafi ya kutengenezea silaha.

Kafanye homework yako tena uje na vitu vya uhakika.
You're smart tho sometimes you're arrogant.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kwenye mita 542 urefu, hukusema kweli. Meli ndefu zaidi duniani kutengenezwa haijazidi mita za urefu 458.46 nayo ni super tanker yenye jina Seawise Giant.

Hiyo "USS Cyclop" uliyoitaja ilikuwa na mita 165 tu. Pia Inasemekana kuna uwezekano ilizamishwa na wajerumani wakati wa vita kuu ya kwanza kwani ilibeba shehena ya malighafi ya kutengenezea silaha.

Kafanye homework yako tena uje na vitu vya uhakika.
You are right 542 ft

"Never stop learning because life never stop teaching"
 
Kwa wale wanaopenda kujua matukio mbalimbali, basi watakuwa wanaifahamu vyema historia ya bermuda triangle.


Tangu mwaka 1945, zaidi ya meli 100 zimeshazama na vifo vya watu zaidi ya 1,000 vimeshatokea katika eneo hili ambalo ni maarufu sana kwa vyombo vya safari kupita. Pia ni eneo ambalo linasifika sana kwa kubadilika kwa hali ya hewa kwa haraka na bila kutarajiwa.


Matukio mengi yalitokea katika kipindi cha miaka ya 1940 - 1960, nayo yalihusu upoteaji wa kiajabu wa vyombo vya usafiri hasa ndege na meli.


Mwaka 1944, Dick Stern alikuwa anaruka na ndege ya kivita eneo hili, ghafla ilipoteza uelekea kwa muda na ikawa inaelekea kuanguka Bahari ya Atlantiki, lakin baadaye iliweza kutulia yeneyewe na kuendelea na safari vizuri. Na katika miaka ya 60 alipita tena eneo hilo akiwa na mkewe katika ndege ya kawaida wakapata msukosuko mkubwa.


Kwenye miaka ya 1945, 1958, 1964 na 1967 kuna ndege zilipotea tena katika eneo hilo ambapo mabaki yake hayakuweza kupatikana kabisa. Kuna baadhi ya marubani ambao waliwahi kuripoti kabla ya kupotea au kuokoka kwamba rada zao zilikupoteza uelekeo na kiasi kwamba wakashindwa kujua wako wapi, kuna mmoja aliripoti kuongezeka kwa kasi ya kwenda kwa ndege na kila kitu kikapoteza control, na baadaye vikarudi sawasawa.



Pia kuna rubani mmoja wa ndege ndogo alitaka kutua eneo hilo, lakini alipofika sehemu aliyotaka kutua, hakuiona ilhali watu waliokuwa chini walikuwa wanamuona na kumshangaa akizunguka tu hewani na kisha kuondoka. Baadaye alikiri kuzunguka juu baada ya kutokuona sehemu aliyotaka kutua wakati compass yake ilimuonyesha ameshafika.



Meli amabazo zimekumbwa na misuko sehemu hiyo zimekuwa zikiripotiwa kukutana na mvutano wa ajabu wa kwenda chini na mwishowe kuzama, au kukutana na machafuko ya bahari ya ghafla.


Kuna baadhi ya wafanyakazi wa meli walio okolewa waligeuka na kuwa vichaa!


Kituko cha funga dimba ni kile kilichoripotiwa mwaka 1967 kutoka kwa watu waliokuwa kwenye meli ya Elizabeth I pale waliposhuhudia ndege ndogo ikiwa mita chache kutoka walipo ikipotea ghafla ikiwa inaruka!!!!


Maajabu makubwa ambayo tutayaongelea, KWANZA ni kupotea kwa ndege nyingi ambazo zimepita katika anga la eneo hilo PILI ni kupotea kwa meli nyingi zinazopita katika eneo hilo. na kubwa zaidi ni kutopatikana kwa taarifa yoyote kuhusu mahali ambapo meli na ndege hizo huelekea baada ya kupotea. Swali kubwa linalozuka ni Je ninini chanzo kikubwa cha kupotea kwa vyombo hivyo? kwa miaka mingi iliyopita chanzo chake hakikujulikana, lakini katika uchunguzi uliofanywa hivi karibuni na kituo kikubwa ulimwenguni cha uchunguzi wa anga NASA, inahisiwa kuwa eneo hilo limezungukwa na nguvu za usumaku zinazofanya kutokea kwa nguvu kubwa ya uvutano inayovuta kitu chochote kinachopatikana eneo hilo au katika anga la eneo hilo

Pia inahisiwa kuwa katika eneo hilo kuna kemikali ya METHANE iliyoyeyuka na kuchangamana na maji hayo jambo linalofanya maji ya eneo hilo kutokuwa na uwezo wa kuhimili uzito wa meli katika eneo hilo, swali ni je kuna uhusiano gani kati ya upotevu wa ndege na uwepo wa kemikali katika maji..

Jamani hili eneo hadi wameliita pembe tatu ya shetani au mlango wa kuzimu kuna nini hapa panapopelekea hadi meli na ndege kubwa kuzama na zaidi zikizama hazijulikani zinaenda wapi,? Mara hii sehemu tunaambiwa ALIENS wanakaa eneo hili kwaio sababu wao wana teknolojia isiyoweza kushindanishwa na za huku duniani wanasema inawezekana pia kitu chochote kinachopita eneo.hilo kinashindwa kuhimili hio nguvu ya teknolojia yao kwaio inapelekea wao kuzichukua kwa sababu zao au kuzitokomeza.

downloadfile.jpg
 
Back
Top Bottom