Hii ndo inaenda kuwa ajali ya kisiasa kwa Boni Yai, Yericko Nyerere, Ntobi na wengine wote waliojitoa ufahamu na kufanya kampeni zilizokosa staha

Hii ndo inaenda kuwa ajali ya kisiasa kwa Boni Yai, Yericko Nyerere, Ntobi na wengine wote waliojitoa ufahamu na kufanya kampeni zilizokosa staha

Mikopo Consultant

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2024
Posts
529
Reaction score
1,150
Ajali ya kisiasa ni tukio ambalo linamtokea mtu kwa yeye mwenyewe kulitengeneza au kutengenezewa, na ambalo linamuondoa moja kwa moja kwenye ulingo na ramani ya kisiasa.

Zitto Kabwe ni mfano hai wa mwanasiasa Tanzania aliyepigwa na ajali ya kisiasa ambayo imempoteza kabisa kwenye ramani ya kisiasa angali bado yupo kwenye prime age ya kufanya siasa za ushindani kwa kiwango cha juu kabisa.

Baada ya kutamatika uchaguzi Chadema, kuna watu ajali za kisiasa zitakuwa zimewafikia. Kwangu ni Boni Yai, Yericko na Ntobi na wapuuzi wengine

Hawa watu walijiona ni miungu watu kwenye kipindi cha kampeni na hata wengine kufikia kujiita 'Machinery ya Chama' na maneno makali sana na dhihaka.

Natumai Lissu sio mtu wa visasi, ila kwa uchaguzi huu, atakuwa ameweza kusoma vyema uwezo wa kufikiri na kujenga hoja kwa aina ya wanachama dizaini ya Yericko na Ntobi, wamejipotezea heshima na kuaminika mbele ya wanachama wa kawaida na viongozi wengine wa chama.

Ajali ya kisiasa imewapiga rasmi kwa kushindwa kuwa na akiba ya maneno
 
CHADEMA HAMNA VISASI, WATARIDHIANA NA KURUDI PAMOJA KUJENGA CHAMA.
Sina wasiwasi kwenye hilo ila kibali chao kimepotea rasmi. Ni ngumu sana kuliona hilo.

Hata wewe binafsi kuna watu wamewahi kukukosea na ukawasamehe, ila ndo imekuwa mwisho wa wewe kuwaamini tena ama kuhusiana nao tena maana unakuwa umeshajua akili zao zipoje.
 
Kwa Ntobi na Yericko ni sawa ila Boni Yai hakuwa na maneno makali sana.

Namwelewa Sasa Kwanini Malisa gj aliamua kutulia tu ... Faida yake ndo hii Sasa! Amejilinda.

Tunaweza kusameheana ila kuaminiana ni kipengele kizito sana.
 
Mbona kama kitumbo alikua anataka kulia ukumbini

1737534270115.jpg
 
Kwa Ntobi na Yericko ni sawa ila Boni Yai hakuwa na maneno makali sana.

Namwelewa Sasa Kwanini Malisa gj aliamua kutulia tu ... Faida yake ndo hii Sasa! Amejilinda.

Tunaweza kusameheana ila kuaminiana ni kipengele kizito sana.
The fact kwamba Boni alishiriki kwenye kejeli mwanzoni maana yake inamuweka kwenye kundi la kina Ntobi, hakuweza kusoma alama za nyakati vyema.

Of coz, najua Lissu hatalipa kisasi, ila utakubaliana na mimi kwamba, amekipoteza kibali chake. Atasamehewa ila hata aminika tena, amejifunua tuione akili yake ni ya namna gani
 
Kibali au vibali ni nadharia dhanifu kwa wanaoiamini. For your information Yeriko na Boni sio believers wa hayo makitu bali wao ni knowers. Kwa hiyo hakuna kitakachowapata sababu sio waumini ila ni watambuzi.
 
Ajali kivipi? Bon atagombea ubunge na Yericko atagombea ubunge Kigamboni. Pia Lissu kutomuamini Bon kunamuathiri vipi Bon?
We utaona tu... ilikuwa rahisi sana kuaminika hapo kabla ila sio kwa sasa, watakumbwa na upinzani mkali kwa wanachama wenzao wa chini.

Chadema ya Lissu itakuwa ya kidemokrasia na hawa watu wakileta pua zao kwa wajumbe watakiona cha moto.

Wamepoteza vibali vyao
 
Kibali au vibali ni nadharia dhanifu kwa wanaoiamini. For your information Yeriko na Boni sio believers wa hayo makitu bali wao ni knowers. Kwa hiyo hakuna kitakachowapata sababu sio waumini ila ni watambuzi.
Ngoja nikuulize swali naomba unijibu.

Wewe kwenye maisha yako kuna watu waliwahi kukukosea na ukawasamehe? Natumai jibu hapo ni ndiyo.

Je, uliwaamini tena baada ya hapo hata kama uliwasamehe?
 
Hiyo si ndio demokrasia sasa ulitaka Lissu Tundu akose wapinzani huo ni udikteta sasa....sidhani kama kutakuwa na mambo ya huyu hakuwa upande wetu tumtenge.
Vizuri kabisa ni demokrasia hiyo ndio lakini kunaweza kuwa na tofauti kubwa sana ya walichokifanya hawa watu.

Walishindwa kutawala hisia zao na kufanya demokrasia yenye staha na kushindanisha hoja.

Maana yake ni kwamba imewafunulia watu wawajue zaidi uwezo wao wa kufikiri upo vipi.
 
Back
Top Bottom