Hii ndo inaenda kuwa ajali ya kisiasa kwa Boni Yai, Yericko Nyerere, Ntobi na wengine wote waliojitoa ufahamu na kufanya kampeni zilizokosa staha

Ngoja nikuulize swali naomba unijibu.

Wewe kwenye maisha yako kuna watu waliwahi kukukosea na ukawasamehe? Natumai jibu hapo ni ndiyo.

Je, uliwaamini tena baada ya hapo hata kama uliwasamehe?
Mkuu, niliwasamehe ndio ila hapo awali sikuwaamini na hata baada ya hapo sina sababu ya kuwaamini tena.
 
Namjua Baba yangu mzazi
Ninamwanini Mungu sana
Umejibu vyema mkuu, unamjua baba yako kwa sababu umemuona au umeadithiwa au pengine uliona hata picha yake ila Mungu unamuamini kwa sababu humjui. Unachokiamini siku zote hukijui ndio maana umeweka imani.

Je, knower ni nani? Ni anayetambua na kufahamu pasipo na shaka yoyote.

Believer ni anayeamini asichokijua Wala kukifahamu kwa undani.
 
Mkuu ipo hivi,,

Watu wadhaifu na wapumbavu hulipiza kisasi.

Watu wenye nguvu husamehe na kusonga mbele.

Watu wenye weledi hupuuzia yote na kuendelea na misheni zao.

TAL ana NGUVU na WELEDI.
 
Hiyo si ndio demokrasia sasa ulitaka Lissu Tundu akose wapinzani huo ni udikteta sasa....sidhani kama kutakuwa na mambo ya huyu hakuwa upande wetu tumtenge.
Nahisi hii mada kwako ni nzito sio size yako kuijadili. Pita tu kama mimi usome comment
 
Kwani chadema walikuwa wanapata nini? chadema siyo CCM ambapo kuna vyeo and for tht matter LAJI. Chadema ni kujitolea na maumivu makali......and therefore they will be relieved of pain and sufferings being a chadema active member
 
CHADEMA HAMNA VISASI, WATARIDHIANA NA KURUDI PAMOJA KUJENGA CHAMA.
Hilo lipo kisiasa zaidi kuliko uhalisia.

Kama usemayo yana ukweli, basi mmoja wao kati ya uliowataja, angetupiwa rapu rapu la cheo ama wadhifa katika chama jana, ili kuonesha kuwa hayo yaliyopita ni mambo ya kawaida!
 
Mmh, hawakufaa na hawafai, sikio ni ulafi au uzumbukuku au
. . .!
 
Hapana, CDM siyo CCM, Sisi tunasema "usizitazame dhambi zao" angalia zaidi "Imani kwa chama, CDM"; hawa walitetea Chama kisife wanaweza kuwa na sababu za msingi, ndiyo demokrasia. Ila yule YUDA, kwa kutaka kuuza Chama kwa vipande 30 (Wenje) lazima achunguzwe, kukiwa na evidence kua alishirikiana na Abdul kugawa rushwa na kutaka kukisaliti chama lazima aadhibiwe. Yaani Wenje.
 
Hiyo si ndio demokrasia sasa ulitaka Lissu Tundu akose wapinzani huo ni udikteta sasa....sidhani kama kutakuwa na mambo ya huyu hakuwa upande wetu tumtenge.
Mkuu upo sahihi.watu kutofautiana kwa hoja au mtazamo sio dhambi.
Uongozi wa demokrasia ya kweli ni kushindanisha hoja na sio hoja za kuwaburuza wengine wasiokubaliana na wewe.
Kifaa au mfumo wa kusukuma hoja kidemokrasia ni sanduku la kura yaani wengi wape.
Uchaguzi umekwisha walioshinda wameshinda wanastahili pongenzi.
LAKINI haiwapi madaraka ya kuwabeza wanachama ambao hawakuwaunga mkono.Kule ndio kukigawa chama katika vipande viwili vinavyokaribia kulingana!
Matokeo yake yako wazi labda hata kuliko NCCR Mageuzi ya leo ukilinganisha na NCCR Mageuzi 1995 ya Mrema.
Mtoto akitaka wembe mpe.
 
Kwa Ntobi na Yericko ni sawa ila Boni Yai hakuwa na maneno makali sana.

Namwelewa Sasa Kwanini Malisa gj aliamua kutulia tu ... Faida yake ndo hii Sasa! Amejilinda.

Tunaweza kusameheana ila kuaminiana ni kipengele kizito sana.
" Tunaweza kusameheana ila kuaminiana ni kipengele kizito sana " - makutupora
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…