Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Wachezaji wa zamani wanapaswa kuwa na umoja wenye nguvu sio kuishia kujisifia enzi zao walifanya nini.
Mbwana Samatta ni mchezaji aliyefanikiwa kuliko wote katika historia ya Tanzania lakini humsikii akiongea au kufanya jambo pasipo akili ya ziada.
Pale ikulu leo mchana walitakiwa wawepo wachezaji wengi kuliko hawa wauza sura wa kibongo tunawaona kwenye runinga mara kwa mara. Lakini alikuwepo Tenga na TIno.
Pengine wingi wa wachezaji wa zamani ungeweza kumfikirisha rais JPM akaweza kuja na wazo jingine lenye faida kwa wanasoka wote wa zamani.
Kumlaumu au kumsema vibaya Tino hakuna msaada wowote, kakabidhiwa kiwanja na kapewa milioni tano kwa sababu alikuwepo mle ukumbini.
Wachezaji wa zamani wengi wao kwa bahati mbaya elimu ndogo, wanakosa nguvu ya ushawishi, tofauti na wachezaji wa zamani wa Zambia, Nigeria na mataifa mengine yenye kutambua nini maana ya elimu.
Nafasi ile ile aliyopewa Tino kuongea mbele ya watu na rais JPM angepewa Segun Adegbami au Okocha au Kalusha Bwalya angeongea mambo ya msingi ndani ya dakika chache alizopewa.
Mbwana Samatta ni mchezaji aliyefanikiwa kuliko wote katika historia ya Tanzania lakini humsikii akiongea au kufanya jambo pasipo akili ya ziada.
Pale ikulu leo mchana walitakiwa wawepo wachezaji wengi kuliko hawa wauza sura wa kibongo tunawaona kwenye runinga mara kwa mara. Lakini alikuwepo Tenga na TIno.
Pengine wingi wa wachezaji wa zamani ungeweza kumfikirisha rais JPM akaweza kuja na wazo jingine lenye faida kwa wanasoka wote wa zamani.
Kumlaumu au kumsema vibaya Tino hakuna msaada wowote, kakabidhiwa kiwanja na kapewa milioni tano kwa sababu alikuwepo mle ukumbini.
Wachezaji wa zamani wengi wao kwa bahati mbaya elimu ndogo, wanakosa nguvu ya ushawishi, tofauti na wachezaji wa zamani wa Zambia, Nigeria na mataifa mengine yenye kutambua nini maana ya elimu.
Nafasi ile ile aliyopewa Tino kuongea mbele ya watu na rais JPM angepewa Segun Adegbami au Okocha au Kalusha Bwalya angeongea mambo ya msingi ndani ya dakika chache alizopewa.