Hii ni Taifa Stars iliyoifunga Zambia kuingia African Cup (Tumemkumbuka Peter Tino, tumemsahau Thuwein Ally)

Hii ni Taifa Stars iliyoifunga Zambia kuingia African Cup (Tumemkumbuka Peter Tino, tumemsahau Thuwein Ally)

..Mechi ya Dsm Taifa Stars ilishinda bao moja bila.

..Goli lilifungwa na Mohamed Adolf Rishard kutokana na kona iliyopigwa na Mohamed Kajole "Machela."

..Tulipokwenda Ndola Tz ilihutaji draw au ishindwe kwa mabao 2 kwa 1.

..Goli la Peter Tino lilitupeleka Lagos kwasababu lilikuwa goli la kusawazisha.
NNi historia nzuri sana!
Mohamed Rishard Adolf... Jamaa yupo simple sana na hana makelele...! Mara ya mwisho nlimuona Kisutu akiwa na Tenga Ktk Mazishi ya Mzee Mbwezeleni!
 
Kwenye hiyo picha ya Taifa Stars, Kutoka kushoto ni:

Godian Mapango (Pan), Salim Amir (Balimi-Bukoba), Idi Pazi (African Sports), George Kulagwa (Simba), Thuwein Ally (Simba), Ibrahim Kiswabi (Pan), Peter Tino (African Sports), Omar Hussein (Yanga), Juma Mkambi (Yanga), Hussein Ngulungu (Pan), Juma Matokeo (Pan), Mohamed Salim (Coastal), Adolf Rishard (Pan).

Uwanja wa Ndege ni Dar Esalaam International Airport, Terminal 1
... inaoenekana enzi hizo Pan ilikuwa na vifaa sio mchezo!
 
..Tulicheza mechi ya kwanza Dsm na aliyefunga goli alikuwa Mohamed Rishard "Adolf."

..Jiulize kwanini tulifuzu kwenda Lagos kwa matokeo ya bao moja kwa moja.

..Mohamed Rishard naye anastahili sifa sawasawa na Peter Tino.
Kifupi goli la Peter Tino lilichagizwa na goli la Dsm la Mohammed RRichard
 
Mbona hili ni la kutumia akili ndogo tu kuelewa? Swali aliyetupeleka African Cup alikuwa ni Nani?

Inawezekana Huyo Thuwein Ally alifunga hayo magoli....lakini bahati mbaya hayakuwa na msaada kwa team maana mwishoni tulitolewa. Nampongeza pia kwa juhudi zake. Ila asingepata nafasi ya kufunga huko mama PETER TINO ASINGEFUNGA LILE MOJA KULE ZAMBIA

PETER TINO HOYEEEE !

Samahani lakini, naomba kukuuliza.
Kwani huyu PETER TINO aliukokota mpira kutoka golini mpaka kufunga bila msaada wa wenzake? Samahani lakini.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
1: HATUA ZA MAKUNDI:

Kwanza turekebishe jina, kuna watu wanasema tunaingia AFCON mara ya pili, wakati ule mwaka 1980 ilikuwa ni African Cup, jina AFCON limekuja miaka ya karibuni.

Thread zilizopita zimeongelea sana kuhusu Peter Tino, mchezaji aliyeifungia Taifa Stars bao lililotupeleka Nigeria. Hebu tujikumbushe mambo yalivyotokea na JF ionekane ni mahala pa kukimbilia data.

Kwanza kabisa, ingawa watu wanasema ni mwaka 1980 ukweli ni kwamba mechi tunayoisema ilifanyika mwishoni mwa mwaka1979, tena tukiwa na uchumi mbovu kutokana na kumalizika kwa vita ya Tanzania na Uganda.

Mechi ile tulikuwa tunahitaji draw ili tuingie finali na Zambia walikuwa wanahitaji ushindi na mechi ilifanyikia Ndola, Zambia.

Katika dakika ya 20, Zambia wakapata bao la kuongoza Hadi half-time Zambia (1) na Tanzania (0).

Kipindi cha pili timu zote ziliongeza kasi lakini Zambia ikiutawala mpira zaidi na ikishangiliwa uwanja mzima. Kuna waandishi husema mshambulia hatari wa Zambia, Godfrey Chitalu, hakufua dafu. Huu si ukweli.

Zambia ilitawala mchezo na golikipa wa Tanzania, Juma Pondamali alipohojiwa na waandishia alisema alimwogopa sana Godfrey Chitalu kwani alikuwa anapiga mikwaju hatari na yeye anaipangua.

Hadi watu wanaanza kuondoak uwanjani na wengine kuacha kusikiliza redio walijua Taifa Stars imetolewa. Ndipo zikiwa zimebaki dakika 2 kumalizika mchezo, Peter Tion akaifungia Taifa Stars bao lililotupeleka Nigeria.

Formation ya wakati huo ilikuwa ni 4-2-4. List ya mchezo huo kama nitaikumbuka vizuri ninaiandika humu, kama ina makosa madogo wanaokumbuka wanisahihishe.

01: Juma Pondamali, (Pan)
02: Leopard Tasso, (Balimi-Bukoba)
03: Mohammed Kajole, (Simba)
04: Salim Amir, (Costal Union)
05: Jella Mtagwa, (Pan)
06: Leodegar Tenga, (Pan)
07: Hussein Ngulungu, (Pan)
08: Omari Hussein, (Yanga)
09: Peter Tino, (African Sports)
10: Mohamed Salim, (Costal Union)
11: Thuweni Ally, (Simba)

2: FINALI (NIGERIA):
Baada ya kufuzu hiyo mechi ya mwaka 1979, ndipo fainal zenyewe za AFRICAN CUP zikafanyika March 1980. Mambo yalikuwa hivi huko Nigeria. Tanzania ilipangwa na wenyeji Nigeria, Egypt na Ivory Coast, siku hizi inaitwa Cote d'Ivoire (tamka kwodivaa).

Mechi ya ufunguzi, March 08, 1980, Tanzania tukacheza na Nigeria kwenye uwanja uitwa Surulele, Tanzania tukachapwa 3-1. Nigeria ilikuwa a washambuliaji hatari kama Ousegun, kwa kifupi Segun, Tunde Obamidele. Bao la pekee la Tanzania likafungwa na Thuwein Ally, mzanzibari pekee katika timu ya Taifa.

Mechi ya pili March 08, 1980, Tanzania tukacheza na Ivory Coast, tukachapwa 2-1. Hapo pia bao la pekee la Tanzania likafungwa na yuleyule Thuwein Ally. Kimsingi tukawa tumeshatolewa mashindanoni tukabaki kukamilisha ratiba.

Mechi ya tatu nimekosa kumbukumbu ilichezwa lini lakini cha uhakika ni kwamba Tanzania itulicheza na Egypt, tukatoka sare 1-1. Hapa tena bao la pekee la Tanzania likafungwa na yuleyule Thuwein Ally.

3: JUMA PONDAMALI, PETER TINO, THUWEIN ALLY, ABDALAH KIBADENI:

NImesoma mahala kwamba Peter Tino ameenziwa, sijui ni kweli au la maana sijaipitia vizuri taarifa hiyo. Lakini tukifanya tathmini vizuri, pale Zambia aliyengara alikuwa ni golikipa Juma Pondamali maana Taifa Stars ilizidiwa kasi kwa muda mwingi wa mchezo na Pondamali ndiye aliyeokoa michomo mingi ya wazambia.

Mwishoni wlalipobadili mbinu ndipo Peter Tino akasawazisha. Kama ni man of the Match alikuwa ni Juma Pondamali na si Peter Tino maana alikokoa magoli mengi ya wazi tena wakati mwingine defense imeshapitwa yote.

Kule Nigeria tumeona kwamba Tanzania ilikuwa inapata goli moja kila mechi, mfungaji akiwa ni Thuwein Ally. Huyu alikuwa ni mchezaji wa Simba akitokea KMKM ya Zanzibar.

Yale magoli matatu yalimfanya Thuwein Ally asifike maana hakuwa anajulikana sana na ndiyo yalifanya aonekane Simba imepata mchezji mzuri.

Sifa ya Thuwein Ally ilikuwa ni mashuti makali ya mguu wake wa kushoto. Kuna shuti alipigia free kick pale CCM Kirumba wapo wanaoamini lilikuwa ni moja ya mashuti makali kupigwa hapa nchini.

Hivyo, kule Nigeria, Thuwein Ally alituletea sifa Tanzania na hata jina lake likabadilika kuwa mfungaji wa magoli matatu kule Nigeria. Hivyo, kwa washabiki wa kipndi kile Thuwein Ally alivuma kuliko Peter Tino.

Peter Tino hakuvuma sana wakati ule kwa sababu hata timu aliyokuwa yaani African Sports ya Tanga, ukiachilia uhasama na Coastal Union, haikuwa tishio.

Kimsingi, Peter Tino hakuvuma sana zaidi ya hilo goli la pale Zambia. Mtu aliyekuja kuvuma alikuwa ni beki (centre half) Jelah Mtagwa ambaye hadi aliwekwa kwenye Stamp ya Posta, yaani ukituma barua lazima uone picha ya Jellah Mtagwa.

Leodgar Tenga hakuendelea sana a mpira liukweli ni kama vile alistaafu mpira kipindi hicho aana nadhani alijikita zaidi na tmasomo pale Chuo Kikuu.

4: ZAMOYONI MOGELA:
Mwaka 1980 wote uliisha baridi namna hiyo ndipo mwaka uliofuata (1981) akaibuka mshambuliaji Zamoyoni Mogela, kwenye mashindano ya CECAFA, ambako kama Thuwein Ally, zile mechi tatu alikuwa lazima afunge goli hadi kikamfanya aitwe Golden Boy.

Kimsingi Peter Tino na Thuwein Ally walikuja kipindi ambapo Abdalah Kibadeni umarufu wake ulikuwa unaondoka na hasa alipoanza ukocha kwa Majimaji ya Songea mwaka 1978.

Hivyo, mwaka 1978 hadi 1980 hakukuwa na mshambulia anayemiliki jina ndiyo maana mtu akiibuka kwenye mechi moja anatawala kidogo kama Peter Tino na Thuwein Ally.

Lakini Thuwein Ally alimzidi umaarufu Peter Tino kama ilivyoelezwa huko juu, kutokana na magoli matutu kule Nigeria. Lakini hawa wote wawili walizidiwa na Zamoyoni Mogela kuanzia Novemba 1980 hadi Mogela alivyoacha mpira.

Kama mnakumbuka mwaka 2011, Zamoyoni Mogella alipewa nishani ya kitaifa kuwa mchezaji bora kwa miaka 50 ya uhuru. Hawakukosea waliofanya hivyo.

Kuna wanaosimulia goli ambalo Zamoyoni Mogela alimfuga golikipa Juma Mhina wa Pamba pale CC ingekuwa sasa hivi lilikuwa linafungwa Ulaya, alimfunga baada ya kuipiga chenga difensi nzima ya Pamba na kumdanganya kipa kwenye upenyo mdogo akaingizia hapohapo goli.

Peter Tino alikuja kuhamia Pan mwaka 1981 na hata hivyo hakufua dafu kwa Mogela ambaye kila timu ilikuwa inamuwekea beki maarufu. Yanga ilikuwa inamuwekea beke aliyeitwa Athuma Chama akisaidiwa na Yusuf Bana.

Peter Tino alizidiwa hata na Madaraka Selemani wa CDA ya wakati huo aliyeweza kupiga chenga defense nzima. Peter Tino alisaidiwa sana na urefu wake. Hivyo, suala la Peter Tino unaweza kuliangalia namna hii.

WANASIASA KUVURUGA UZALENDO:
Kingine ni kwamba wakti ule kulikuwa na chama kimoja tu CCM na hata kama kama timu ilisaidiwa au kuhamasishwa waljitokeza kwa nadra sana akijitahidi ni Waziri anayehusika na michezo. Ungeonekana ni kichaa kutojua Taifa stars inacheza, achilia mbali kutoishangilia.

Leo soka imeanza kuingiliwa na wanasiasa, tena wengine hata hawana historia ya mpira na historia hii inayoelezwa humu huenda ni ngeni kwao. Walikuwa wapi wakati huo, jibu mnalo.

Licha ya hayo UCHADEMA na UCCM unaonekana. Akitokea sana mwanasiasa wa chama tofauti akajikita inaonekana anavutia chama chake na ni kweli mwakani atafanya kampeni kwamba kawezesha yeye na chama chake.

Matokeo yako kama timu imewezeshwa na mwanasiasa wa CHADEMA basi yule wa CCM yuko radhi timu ifungwe ilie CHADEMA isije ikachukua sifa hiyo!

Kimsingi, wanasiasa wa vyama vyote wanavurugua utamu wa mpira na walitakiwa wabaki hukohuko kwenye majukwaa ya siasa.

NAWASILISHA.
Masahihisho ;Tanzania ilitoka sare na Code d ivoire sio Misri
 
1: HATUA ZA MAKUNDI:

Kwanza turekebishe jina, kuna watu wanasema tunaingia AFCON mara ya pili, wakati ule mwaka 1980 ilikuwa ni African Cup, jina AFCON limekuja miaka ya karibuni.

Thread zilizopita zimeongelea sana kuhusu Peter Tino, mchezaji aliyeifungia Taifa Stars bao lililotupeleka Nigeria. Hebu tujikumbushe mambo yalivyotokea na JF ionekane ni mahala pa kukimbilia data.

Kwanza kabisa, ingawa watu wanasema ni mwaka 1980 ukweli ni kwamba mechi tunayoisema ilifanyika mwishoni mwa mwaka1979, tena tukiwa na uchumi mbovu kutokana na kumalizika kwa vita ya Tanzania na Uganda.

Mechi ile tulikuwa tunahitaji draw ili tuingie finali na Zambia walikuwa wanahitaji ushindi na mechi ilifanyikia Ndola, Zambia.

Katika dakika ya 20, Zambia wakapata bao la kuongoza Hadi half-time Zambia (1) na Tanzania (0).

Kipindi cha pili timu zote ziliongeza kasi lakini Zambia ikiutawala mpira zaidi na ikishangiliwa uwanja mzima. Kuna waandishi husema mshambulia hatari wa Zambia, Godfrey Chitalu, hakufua dafu. Huu si ukweli.

Zambia ilitawala mchezo na golikipa wa Tanzania, Juma Pondamali alipohojiwa na waandishia alisema alimwogopa sana Godfrey Chitalu kwani alikuwa anapiga mikwaju hatari na yeye anaipangua.

Hadi watu wanaanza kuondoak uwanjani na wengine kuacha kusikiliza redio walijua Taifa Stars imetolewa. Ndipo zikiwa zimebaki dakika 2 kumalizika mchezo, Peter Tion akaifungia Taifa Stars bao lililotupeleka Nigeria.

Formation ya wakati huo ilikuwa ni 4-2-4. List ya mchezo huo kama nitaikumbuka vizuri ninaiandika humu, kama ina makosa madogo wanaokumbuka wanisahihishe.

01: Juma Pondamali, (Pan)
02: Leopard Tasso, (Balimi-Bukoba)
03: Mohammed Kajole, (Simba)
04: Salim Amir, (Costal Union)
05: Jella Mtagwa, (Pan)
06: Leodegar Tenga, (Pan)
07: Hussein Ngulungu, (Pan)
08: Omari Hussein, (Yanga)
09: Peter Tino, (African Sports)
10: Mohamed Salim, (Costal Union)
11: Thuweni Ally, (Simba)

2: FINALI (NIGERIA):
Baada ya kufuzu hiyo mechi ya mwaka 1979, ndipo fainal zenyewe za AFRICAN CUP zikafanyika March 1980. Mambo yalikuwa hivi huko Nigeria. Tanzania ilipangwa na wenyeji Nigeria, Egypt na Ivory Coast, siku hizi inaitwa Cote d'Ivoire (tamka kwodivaa).

Mechi ya ufunguzi, March 08, 1980, Tanzania tukacheza na Nigeria kwenye uwanja uitwa Surulele, Tanzania tukachapwa 3-1. Nigeria ilikuwa a washambuliaji hatari kama Ousegun, kwa kifupi Segun, Tunde Obamidele. Bao la pekee la Tanzania likafungwa na Thuwein Ally, mzanzibari pekee katika timu ya Taifa.

Mechi ya pili March 08, 1980, Tanzania tukacheza na Ivory Coast, tukachapwa 2-1. Hapo pia bao la pekee la Tanzania likafungwa na yuleyule Thuwein Ally. Kimsingi tukawa tumeshatolewa mashindanoni tukabaki kukamilisha ratiba.

Mechi ya tatu nimekosa kumbukumbu ilichezwa lini lakini cha uhakika ni kwamba Tanzania itulicheza na Egypt, tukatoka sare 1-1. Hapa tena bao la pekee la Tanzania likafungwa na yuleyule Thuwein Ally.

3: JUMA PONDAMALI, PETER TINO, THUWEIN ALLY, ABDALAH KIBADENI:

NImesoma mahala kwamba Peter Tino ameenziwa, sijui ni kweli au la maana sijaipitia vizuri taarifa hiyo. Lakini tukifanya tathmini vizuri, pale Zambia aliyengara alikuwa ni golikipa Juma Pondamali maana Taifa Stars ilizidiwa kasi kwa muda mwingi wa mchezo na Pondamali ndiye aliyeokoa michomo mingi ya wazambia.

Mwishoni wlalipobadili mbinu ndipo Peter Tino akasawazisha. Kama ni man of the Match alikuwa ni Juma Pondamali na si Peter Tino maana alikokoa magoli mengi ya wazi tena wakati mwingine defense imeshapitwa yote.

Kule Nigeria tumeona kwamba Tanzania ilikuwa inapata goli moja kila mechi, mfungaji akiwa ni Thuwein Ally. Huyu alikuwa ni mchezaji wa Simba akitokea KMKM ya Zanzibar.

Yale magoli matatu yalimfanya Thuwein Ally asifike maana hakuwa anajulikana sana na ndiyo yalifanya aonekane Simba imepata mchezji mzuri.

Sifa ya Thuwein Ally ilikuwa ni mashuti makali ya mguu wake wa kushoto. Kuna shuti alipigia free kick pale CCM Kirumba wapo wanaoamini lilikuwa ni moja ya mashuti makali kupigwa hapa nchini.

Hivyo, kule Nigeria, Thuwein Ally alituletea sifa Tanzania na hata jina lake likabadilika kuwa mfungaji wa magoli matatu kule Nigeria. Hivyo, kwa washabiki wa kipndi kile Thuwein Ally alivuma kuliko Peter Tino.

Peter Tino hakuvuma sana wakati ule kwa sababu hata timu aliyokuwa yaani African Sports ya Tanga, ukiachilia uhasama na Coastal Union, haikuwa tishio.

Kimsingi, Peter Tino hakuvuma sana zaidi ya hilo goli la pale Zambia. Mtu aliyekuja kuvuma alikuwa ni beki (centre half) Jelah Mtagwa ambaye hadi aliwekwa kwenye Stamp ya Posta, yaani ukituma barua lazima uone picha ya Jellah Mtagwa.

Leodgar Tenga hakuendelea sana a mpira liukweli ni kama vile alistaafu mpira kipindi hicho aana nadhani alijikita zaidi na tmasomo pale Chuo Kikuu.

4: ZAMOYONI MOGELA:
Mwaka 1980 wote uliisha baridi namna hiyo ndipo mwaka uliofuata (1981) akaibuka mshambuliaji Zamoyoni Mogela, kwenye mashindano ya CECAFA, ambako kama Thuwein Ally, zile mechi tatu alikuwa lazima afunge goli hadi kikamfanya aitwe Golden Boy.

Kimsingi Peter Tino na Thuwein Ally walikuja kipindi ambapo Abdalah Kibadeni umarufu wake ulikuwa unaondoka na hasa alipoanza ukocha kwa Majimaji ya Songea mwaka 1978.

Hivyo, mwaka 1978 hadi 1980 hakukuwa na mshambulia anayemiliki jina ndiyo maana mtu akiibuka kwenye mechi moja anatawala kidogo kama Peter Tino na Thuwein Ally.

Lakini Thuwein Ally alimzidi umaarufu Peter Tino kama ilivyoelezwa huko juu, kutokana na magoli matutu kule Nigeria. Lakini hawa wote wawili walizidiwa na Zamoyoni Mogela kuanzia Novemba 1980 hadi Mogela alivyoacha mpira.

Kama mnakumbuka mwaka 2011, Zamoyoni Mogella alipewa nishani ya kitaifa kuwa mchezaji bora kwa miaka 50 ya uhuru. Hawakukosea waliofanya hivyo.

Kuna wanaosimulia goli ambalo Zamoyoni Mogela alimfuga golikipa Juma Mhina wa Pamba pale CC ingekuwa sasa hivi lilikuwa linafungwa Ulaya, alimfunga baada ya kuipiga chenga difensi nzima ya Pamba na kumdanganya kipa kwenye upenyo mdogo akaingizia hapohapo goli.

Peter Tino alikuja kuhamia Pan mwaka 1981 na hata hivyo hakufua dafu kwa Mogela ambaye kila timu ilikuwa inamuwekea beki maarufu. Yanga ilikuwa inamuwekea beke aliyeitwa Athuma Chama akisaidiwa na Yusuf Bana.

Peter Tino alizidiwa hata na Madaraka Selemani wa CDA ya wakati huo aliyeweza kupiga chenga defense nzima. Peter Tino alisaidiwa sana na urefu wake. Hivyo, suala la Peter Tino unaweza kuliangalia namna hii.

WANASIASA KUVURUGA UZALENDO:
Kingine ni kwamba wakti ule kulikuwa na chama kimoja tu CCM na hata kama kama timu ilisaidiwa au kuhamasishwa waljitokeza kwa nadra sana akijitahidi ni Waziri anayehusika na michezo. Ungeonekana ni kichaa kutojua Taifa stars inacheza, achilia mbali kutoishangilia.

Leo soka imeanza kuingiliwa na wanasiasa, tena wengine hata hawana historia ya mpira na historia hii inayoelezwa humu huenda ni ngeni kwao. Walikuwa wapi wakati huo, jibu mnalo.

Licha ya hayo UCHADEMA na UCCM unaonekana. Akitokea sana mwanasiasa wa chama tofauti akajikita inaonekana anavutia chama chake na ni kweli mwakani atafanya kampeni kwamba kawezesha yeye na chama chake.

Matokeo yako kama timu imewezeshwa na mwanasiasa wa CHADEMA basi yule wa CCM yuko radhi timu ifungwe ilie CHADEMA isije ikachukua sifa hiyo!

Kimsingi, wanasiasa wa vyama vyote wanavurugua utamu wa mpira na walitakiwa wabaki hukohuko kwenye majukwaa ya siasa.

NAWASILISHA.
Maelezo mazuri,je bila ya Peter Tino kusawazisha huo mwaka 1979 tungeenda kwenye hayo mashindano?,


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo Pita Tino alikuwa anacheza,anazuia anashambulia, na kudaka mpira mwenyewe.! Hakuna goli linalofungwa na mtu Mmoja. Wachezaji Wote waliocheza 1979/80 ambao mpaka sasa wako hai mpaka sasa wapewe kiwanja.
Tusitoe zawadi za kitaifa Kisiasa !?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa, Wachezaji unaweza kutaja wengi tu, lakini goli la Tino lilikuwa la muhimu sana wakati ule tena kwenye dakika za mwisho!. Pamoja na kushindwa mechi zote za Africa Cup of Nations, Kivutio alikuwa Juma Pondamali aliyejizolea sifa za golikipa mchekeshaji na mcheza sarakasi..... Hawa hapa wachezaji wa enzi hizo na Peter Tino anaonekana hapo katikati kabisa....wengine nimesahau majina yao.
Wachezaji wa zamani walikuwa physique
 
Huyo Pita Tino alikuwa anacheza,anazuia anashambulia, na kudaka mpira mwenyewe.! Hakuna goli linalofungwa na mtu Mmoja. Wachezaji Wote waliocheza Taifa stars Afrcom 1979/80 ambao mpaka sasa wako hai mpaka sasa wapewe kiwanja.
Tusitoe zawadi za kitaifa Kisiasa !?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante kwa historia nzuri lakini naona umejikita kumu undergrade Peter Tino. Wachezaji wote walioshiriki kutuvusha mwaka 1979 wanastahili pongezi kubwa sana lakini kibinadamu yule aliyefunga goli lililotuvusha anakuwa na historia ya pekee bila kujali mengine yote uliyosema.

Nafikiri kwasasa hatupo kwenye mjadala wa mchezaji gani alikuwa mkali enzi hizo ila kupitia kufuzu Afcon safari hii imetufanya leo tuone thamani ya goli lile la Peter Tino.

Hii ni kawaida kibinadamu ndio maana hata Iniesta pamoja na kuwa fundi wa hatari lakini lile goli lake la world cup final itabakia kuwa alama yake kwa wahispania daima.

Nafikiri kwa namna ya kujenga tungeshauri wale wachezaji waliotuvusha mwaka 1979 au familia zao wafanyiwe kitu cha kumbukumbu. Yes, tunashukuru kwa zawadi ya Tino leo ikulu lakini hili litazamwe kwa mapana.

Peter Tino alikuwa mchezaji bora ndio maana akaitwa timu ya Taifa na kuwakilisha nchi, zuri zaidi ndiye aliyefunga lile goli la dhahabu na kutuvusha. Hilo linatosha wala hutufanyi zoezi la comparison la mkali nani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtizamo big up kwa kuweka sawa,huyu jamaa kanichanganya kuonyesha Peter Tino hakua super,kajikita kwa Pondamali na Thuwen Ally,kiukweli bila lile goal hii ndio ingekua mara ya kwanza kufuzu,mwisho tuenzi wachezaji wote wa zamani na familia zao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1: HATUA ZA MAKUNDI:

Kwanza turekebishe jina, kuna watu wanasema tunaingia AFCON mara ya pili, wakati ule mwaka 1980 ilikuwa ni African Cup, jina AFCON limekuja miaka ya karibuni.

Thread zilizopita zimeongelea sana kuhusu Peter Tino, mchezaji aliyeifungia Taifa Stars bao lililotupeleka Nigeria. Hebu tujikumbushe mambo yalivyotokea na JF ionekane ni mahala pa kukimbilia data.

Kwanza kabisa, ingawa watu wanasema ni mwaka 1980 ukweli ni kwamba mechi tunayoisema ilifanyika mwishoni mwa mwaka1979, tena tukiwa na uchumi mbovu kutokana na kumalizika kwa vita ya Tanzania na Uganda.

Mechi ile tulikuwa tunahitaji draw ili tuingie finali na Zambia walikuwa wanahitaji ushindi na mechi ilifanyikia Ndola, Zambia.

Katika dakika ya 20, Zambia wakapata bao la kuongoza Hadi half-time Zambia (1) na Tanzania (0).

Kipindi cha pili timu zote ziliongeza kasi lakini Zambia ikiutawala mpira zaidi na ikishangiliwa uwanja mzima. Kuna waandishi husema mshambulia hatari wa Zambia, Godfrey Chitalu, hakufua dafu. Huu si ukweli.

Zambia ilitawala mchezo na golikipa wa Tanzania, Juma Pondamali alipohojiwa na waandishia alisema alimwogopa sana Godfrey Chitalu kwani alikuwa anapiga mikwaju hatari na yeye anaipangua.

Hadi watu wanaanza kuondoak uwanjani na wengine kuacha kusikiliza redio walijua Taifa Stars imetolewa. Ndipo zikiwa zimebaki dakika 2 kumalizika mchezo, Peter Tion akaifungia Taifa Stars bao lililotupeleka Nigeria.

Formation ya wakati huo ilikuwa ni 4-2-4. List ya mchezo huo kama nitaikumbuka vizuri ninaiandika humu, kama ina makosa madogo wanaokumbuka wanisahihishe.

01: Juma Pondamali, (Pan)
02: Leopard Tasso, (Balimi-Bukoba)
03: Mohammed Kajole, (Simba)
04: Salim Amir, (Costal Union)
05: Jella Mtagwa, (Pan)
06: Leodegar Tenga, (Pan)
07: Hussein Ngulungu, (Pan)
08: Omari Hussein, (Yanga)
09: Peter Tino, (African Sports)
10: Mohamed Salim, (Costal Union)
11: Thuweni Ally, (Simba)

2: FINALI (NIGERIA):
Baada ya kufuzu hiyo mechi ya mwaka 1979, ndipo fainal zenyewe za AFRICAN CUP zikafanyika March 1980. Mambo yalikuwa hivi huko Nigeria. Tanzania ilipangwa na wenyeji Nigeria, Egypt na Ivory Coast, siku hizi inaitwa Cote d'Ivoire (tamka kwodivaa).

Mechi ya ufunguzi, March 08, 1980, Tanzania tukacheza na Nigeria kwenye uwanja uitwa Surulele, Tanzania tukachapwa 3-1. Nigeria ilikuwa a washambuliaji hatari kama Ousegun, kwa kifupi Segun, Tunde Obamidele. Bao la pekee la Tanzania likafungwa na Thuwein Ally, mzanzibari pekee katika timu ya Taifa.

Mechi ya pili March 08, 1980, Tanzania tukacheza na Ivory Coast, tukachapwa 2-1. Hapo pia bao la pekee la Tanzania likafungwa na yuleyule Thuwein Ally. Kimsingi tukawa tumeshatolewa mashindanoni tukabaki kukamilisha ratiba.

Mechi ya tatu nimekosa kumbukumbu ilichezwa lini lakini cha uhakika ni kwamba Tanzania itulicheza na Egypt, tukatoka sare 1-1. Hapa tena bao la pekee la Tanzania likafungwa na yuleyule Thuwein Ally.

3: JUMA PONDAMALI, PETER TINO, THUWEIN ALLY, ABDALAH KIBADENI:

NImesoma mahala kwamba Peter Tino ameenziwa, sijui ni kweli au la maana sijaipitia vizuri taarifa hiyo. Lakini tukifanya tathmini vizuri, pale Zambia aliyengara alikuwa ni golikipa Juma Pondamali maana Taifa Stars ilizidiwa kasi kwa muda mwingi wa mchezo na Pondamali ndiye aliyeokoa michomo mingi ya wazambia.

Mwishoni wlalipobadili mbinu ndipo Peter Tino akasawazisha. Kama ni man of the Match alikuwa ni Juma Pondamali na si Peter Tino maana alikokoa magoli mengi ya wazi tena wakati mwingine defense imeshapitwa yote.

Kule Nigeria tumeona kwamba Tanzania ilikuwa inapata goli moja kila mechi, mfungaji akiwa ni Thuwein Ally. Huyu alikuwa ni mchezaji wa Simba akitokea KMKM ya Zanzibar.

Yale magoli matatu yalimfanya Thuwein Ally asifike maana hakuwa anajulikana sana na ndiyo yalifanya aonekane Simba imepata mchezji mzuri.

Sifa ya Thuwein Ally ilikuwa ni mashuti makali ya mguu wake wa kushoto. Kuna shuti alipigia free kick pale CCM Kirumba wapo wanaoamini lilikuwa ni moja ya mashuti makali kupigwa hapa nchini.

Hivyo, kule Nigeria, Thuwein Ally alituletea sifa Tanzania na hata jina lake likabadilika kuwa mfungaji wa magoli matatu kule Nigeria. Hivyo, kwa washabiki wa kipndi kile Thuwein Ally alivuma kuliko Peter Tino.

Peter Tino hakuvuma sana wakati ule kwa sababu hata timu aliyokuwa yaani African Sports ya Tanga, ukiachilia uhasama na Coastal Union, haikuwa tishio.

Kimsingi, Peter Tino hakuvuma sana zaidi ya hilo goli la pale Zambia. Mtu aliyekuja kuvuma alikuwa ni beki (centre half) Jelah Mtagwa ambaye hadi aliwekwa kwenye Stamp ya Posta, yaani ukituma barua lazima uone picha ya Jellah Mtagwa.

Leodgar Tenga hakuendelea sana a mpira liukweli ni kama vile alistaafu mpira kipindi hicho aana nadhani alijikita zaidi na tmasomo pale Chuo Kikuu.

4: ZAMOYONI MOGELA:
Mwaka 1980 wote uliisha baridi namna hiyo ndipo mwaka uliofuata (1981) akaibuka mshambuliaji Zamoyoni Mogela, kwenye mashindano ya CECAFA, ambako kama Thuwein Ally, zile mechi tatu alikuwa lazima afunge goli hadi kikamfanya aitwe Golden Boy.

Kimsingi Peter Tino na Thuwein Ally walikuja kipindi ambapo Abdalah Kibadeni umarufu wake ulikuwa unaondoka na hasa alipoanza ukocha kwa Majimaji ya Songea mwaka 1978.

Hivyo, mwaka 1978 hadi 1980 hakukuwa na mshambulia anayemiliki jina ndiyo maana mtu akiibuka kwenye mechi moja anatawala kidogo kama Peter Tino na Thuwein Ally.

Lakini Thuwein Ally alimzidi umaarufu Peter Tino kama ilivyoelezwa huko juu, kutokana na magoli matutu kule Nigeria. Lakini hawa wote wawili walizidiwa na Zamoyoni Mogela kuanzia Novemba 1980 hadi Mogela alivyoacha mpira.

Kama mnakumbuka mwaka 2011, Zamoyoni Mogella alipewa nishani ya kitaifa kuwa mchezaji bora kwa miaka 50 ya uhuru. Hawakukosea waliofanya hivyo.

Kuna wanaosimulia goli ambalo Zamoyoni Mogela alimfuga golikipa Juma Mhina wa Pamba pale CC ingekuwa sasa hivi lilikuwa linafungwa Ulaya, alimfunga baada ya kuipiga chenga difensi nzima ya Pamba na kumdanganya kipa kwenye upenyo mdogo akaingizia hapohapo goli.

Peter Tino alikuja kuhamia Pan mwaka 1981 na hata hivyo hakufua dafu kwa Mogela ambaye kila timu ilikuwa inamuwekea beki maarufu. Yanga ilikuwa inamuwekea beke aliyeitwa Athuma Chama akisaidiwa na Yusuf Bana.

Peter Tino alizidiwa hata na Madaraka Selemani wa CDA ya wakati huo aliyeweza kupiga chenga defense nzima. Peter Tino alisaidiwa sana na urefu wake. Hivyo, suala la Peter Tino unaweza kuliangalia namna hii.

WANASIASA KUVURUGA UZALENDO:
Kingine ni kwamba wakti ule kulikuwa na chama kimoja tu CCM na hata kama kama timu ilisaidiwa au kuhamasishwa waljitokeza kwa nadra sana akijitahidi ni Waziri anayehusika na michezo. Ungeonekana ni kichaa kutojua Taifa stars inacheza, achilia mbali kutoishangilia.

Leo soka imeanza kuingiliwa na wanasiasa, tena wengine hata hawana historia ya mpira na historia hii inayoelezwa humu huenda ni ngeni kwao. Walikuwa wapi wakati huo, jibu mnalo.

Licha ya hayo UCHADEMA na UCCM unaonekana. Akitokea sana mwanasiasa wa chama tofauti akajikita inaonekana anavutia chama chake na ni kweli mwakani atafanya kampeni kwamba kawezesha yeye na chama chake.

Matokeo yako kama timu imewezeshwa na mwanasiasa wa CHADEMA basi yule wa CCM yuko radhi timu ifungwe ilie CHADEMA isije ikachukua sifa hiyo!

Kimsingi, wanasiasa wa vyama vyote wanavurugua utamu wa mpira na walitakiwa wabaki hukohuko kwenye majukwaa ya siasa.

NAWASILISHA.
Asante kwa kumbukumbu nzuri ila wewe ni simba damu
 
Aliyefunga bao la kutupeleka Lagos Kule Zambia alikuwa Ni PETER TINO. ila si mbaya nawe uka muenzi mohamed rishard adolf....hujakatazwa... Siku ya simba na AS Vita goli la Thamani zaidi lilikuwa la Chama. Hii ipo hivyo kila sehemu...mi sijaelewa kwa nini watu wametokwa na povu sana. Jamaa kashapata shukrani yake.

..Tulicheza mechi ya kwanza Dsm na aliyefunga goli alikuwa Mohamed Rishard "Adolf."

..Jiulize kwanini tulifuzu kwenda Lagos kwa matokeo ya bao moja kwa moja.

..Mohamed Rishard naye anastahili sifa sawasawa na Peter Tino.
 
Umeongea kitu cha kweli sana! watu walioelimika wanatafuta nafasi kama aliyopata TINO jana kueleza vitu vya maana hata ile 5ml aliyoomba nikama amekurupuka mchezi unaejielewa unamuomba Rais 5m!! utafanyia biashara gani 5m nadhani madogo hawa akina Samata wataonesha mfano wa namna gani Mchezi anatakiwa kuwa!
Wachezaji wa zamani wanapaswa kuwa na umoja wenye nguvu sio kuishia kujisifia enzi zao walifanya nini.
Mbwana Samatta ni mchezaji aliyefanikiwa kuliko wote katika historia ya Tanzania lakini humsikii akiongea au kufanya jambo pasipo akili ya ziada.

Pale ikulu leo mchana walitakiwa wawepo wachezaji wengi kuliko hawa wauza sura wa kibongo tunawaona kwenye runinga mara kwa mara. Lakini alikuwepo Tenga na TIno.

Pengine wingi wa wachezaji wa zamani ungeweza kumfikirisha rais JPM akaweza kuja na wazo jingine lenye faida kwa wanasoka wote wa zamani.

Kumlaumu au kumsema vibaya Tino hakuna msaada wowote, kakabidhiwa kiwanja na kapewa milioni tano kwa sababu alikuwepo mle ukumbini.

Wachezaji wa zamani wengi wao kwa bahati mbaya elimu ndogo, wanakosa nguvu ya ushawishi, tofauti na wachezaji wa zamani wa Zambia, Nigeria na mataifa mengine yenye kutambua nini maana ya elimu.

Nafasi ile ile aliyopewa Tino kuongea mbele ya watu na rais JPM angepewa Segun Adegbami au Okocha au Kalusha Bwalya angeongea mambo ya msingi ndani ya dakika chache alizopewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali la kitoto... Ndo maana katika mechi kuna man of the match. Maana yake huyu alicheza peke yake? Leo hii anavyochukua uchezaji bora ronaldo au messi huwa anacheza peke yake? Ile zawadi ya mfungaji bora wa ligi au kombe anayepewa huwa anakokota mpira peke yake toka golini? Sasa mbona hawapewi team nzima?

Kajipange kijana... Kuuliza si ujinga lakini haimaanishi tuulize maswali ya kijinga

Samahani lakini, naomba kukuuliza.
Kwani huyu PETER TINO aliukokota mpira kutoka golini mpaka kufunga bila msaada wa wenzake? Samahani lakini.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom