Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Ila kuna watu wana roho ngumu sana kuhusiana na hawa ndugu wanaokuja pasi na kutoa taarifa. Jamaa anawauliza " Je, mlisikia mimi naumwa?" "Hapana tumekukumbuka sana ndo maana tumekuja kukusalimia". "Ok, kwa vile sasa mmekuja na mmeniona nipo mzima, basi kesho asubuhi na mapema mjiandae kurudi mlikotoka".
Ha ha ha.... wewe nimekukubali sana huna kuremba kabisa.
 
Ni upumbavu kudhani unachowaza wewe na wengine wanawaza.. simu ni yangu mtu akinisumbua its either na mblock au nazima nipumzike. Acheni kuja kujipendekeza kwa mashemeji zenu. Mnatusumbua sana nyie wa bush.
Nani wa bush mzee? Mbona una makasiriko, sisi tunaangalia namna mambo yanavyoenda katika jamii, katika kesi nyingi Hali inakua hivo. Na kiuhalisia ukiona una mind vitu Kama ndugu zako wa bush kukupigia simu kuomba msaada, wewe mwenyewe uchumi wako mdogo. Una mansion au villa umejenga na nyumba ndogo ya nje hauwezi kuhangaika na vitu vidogo Kama mtu kula sijui kulala, wewe bado haujajipata ndomaana una makasiriko.
 
acha roho mbaya mjinga we,siku ukipata shida hata huyo mke wako aliyekuoa atakukimbia,ngoja uumwe tu au upate uchizi uone kama huyo mke wako haja wapigia ndugu zako njooni mmchukue ndugu yenu amechizi,raha umekula na mke wako ukipata shida wanatafutwa ndugu zako,pumbafu we limbukeni mkubwa
Matusi ya nini? Kwani hutaeleweka bila matusi? Mwinjaka nini?
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingia simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.




Mimi walienda kusema nafuja sana pesa badala ya kuwasomesha watoto wao. Mtu kazaa watoto 13 anataka nimsomeshee... Mimi nina 3 tu. Bado wanaenda kusema nakuaje na watoto wachache ... Mwanaume gani. Mke amenikalia kichwani anarudi jioni kama mwanamke. Wanataka wife awafulie nguo zao. Na wanakuwa wakali akirudi awapatie chakula n.k sina hamu na ndugu kabisa.

Mmoja tumekaa naye mwaka mmoja amekuja nimsomeshe diploma. Akirudi toka chuo anaangalia TV mpaka saa 4 akipewa kazi basi za home siku yupo asaidie... Anasema anateswa sana hawezi soma. Nikasubiri likizo. Akaenda kwao kusalimia. Nikamwambia atafute chuo aendelee kusoma huko, nitamlipia ada.

Alilia sana anataka arudi Dar. Nilimwambia huku wifi yako atakutesa hutapata muda wa kusoma. Akabembeleza sana nilimkatalia coz alishanipakaza sana kijijini na kumchafua sana wife. Na mtu mwenyewe ni ndugu wa mbali kabisa..
Ubinadam kazi. Nimalizie kwa maneno hayo.
 
Umeona mzee bush wabeba gharama zetu za familia nzima tukiwa kule wanatupa huduma nzuri sometimes wanakopa, ndo mtu mmoja kutoka huko umzimie simu, [emoji23][emoji23] ni umaskini tuu

Maisha ni magumu ndio vyakula vimepanda bei
Kuna watu ni matajiri wana nafasi na hawataki wageni [emoji23][emoji23][emoji23] kila mtu akae kwao[emoji23][emoji23]
 
Wacheni roho mbaya, hao wanakuja na kheri zao.

Wapokeeni bila masimango wala chuki, kwa bashasha na furaha. Siku tatu za mwanzo ni wageni, baada ya hapo waishi kama wenyeji.

Uislam mi mwema sana, haujaacha kitu. Uislam una miongozo mema kabisa ya maisha ya kila siku. Ukiifata huharibikiwi.
Na Mara nyingi sana watu waliotelekezwa wamesaidiwa msikitini, hili nimeliona Mara nyingi.
 
Maisha ni magumu ndio vyakula vimepanda bei
Kuna watu ni matajiri wana nafasi na hawataki wageni [emoji23][emoji23][emoji23] kila mtu akae kwao[emoji23][emoji23]
Wageni ni baraka, changamoto zipo lakini upendo na kuelekezana kiungwana ni jambo zuri zaidi, haijarishi we ni tajiri au maskini kuwa mkarimu na mtoaji ni moyo tu wa mtu. Ukiwa mkarimu unapata thawabu kwa mwenyezi mungu
 
Siku watakapoamua kukusafirisha hao ndio wachimba kaburi wagawa chakula kwenye msiba wako be humble brother..
Watu tunajisahaulisha haraka mno au pengine hatufikiri sawasawa, maisha ya Afrika Ni undugu,likikupata ndugu zako ndio wataokubeba
Huku Hakuna funeral companies kwamba ukifa itaenda lipia gharama uzikwe ,Ni Hao ndugu zetu tunaowanyanyapaa ndio wachimba kaburi
Ikitokea umeumwa Ni Hao Hao ndugu ndio watakua wauguzi
Indeed we need to be humble, mengine Ni umaskini kama walivyosema wachangiaji wengi
 
Back
Top Bottom