Hii tabia ya wapinzani hasa CHADEMA kusifia wastaafu wa CCM inatukanisha upinzani

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Kumekuwa na kautamaduni ka viongozi na mashabiki wa upinzani kuwasifia viongozi wa CCM pindi wanpokuwa wamestaafu toka kwenye majukumu yao ya kiserikali/chama.

Utamaduni huu unawachanganya wananchi hasa wale wenye uwezo mzuri wa kutunza kumbukumbu, kwani mara nyingi unakuta huyu mstaafu wanae msifu kwamba alikuwa mtu mzuri sio kama wa sasa, walimshambulia na kumtupia kila taka.

Kwa hiyo wananchi wanavyoona mnasifia wastaafu wa CCM, wanajua kwamba kumbe hata hawa mnaowatukana leo wakistaafu mtakuja na ngonjera nzuri mlizowatungia za kuwasifu.

Na hii pia nimegundua kwamba husababishwa na kufanya siasa kwa mihemko yaani unakosoa kutukana au kushabikia bila upeo mkubwa wa kupima mambo.

Tufanye siasa kwa utulivu na upeo mkubwa.
 
Ukifanya vzr utaungwa mkono,ukizingua utazinguliwa tu hakuna namna
 
Kila siku ni siasa nashangaa hii kauli siasa za mihemko zinatoka wapi.

Ukiangalia inshu ya mikopo ccm waliruka na maamlaka. Ukiangalia siku mkuu wa mkoa amesema boda hawatakiwi mjini ccm iliamka na maamlaka.

Ata upinzani nao ni vile vile kwa iyo kila siku ya jamhuri ni siku ya siasa.
 
Kwani kusifia ni kosa ama upinzani ni chuki
 
Ukifanya vzr utaungwa mkono,ukizingua utazinguliwa tu hakuna namna
Nachosisitiza ni msimamo sio kikwete yuko madarakani anadhihakiwa kwa mba ni dhaifu kastaafu tu tunaanza kummisi Magufuli akiwa madarakani mnasema dictator ametoka mnasema huyu aliepo ni bora Magufuli hii inaleta tafsiri kwamba wapinzani hawajui wanachokitaka
 

Wapinzani Sio Maadui;
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…