Hii tabia ya watu kuja na thread "Leo ni siku ya mwisho kutumia JF"

Hii tabia ya watu kuja na thread "Leo ni siku ya mwisho kutumia JF"

Sheria za jf zinasemaje kuhusu maongezi ya pm?!
Yabaki huko huko pm.

Sasa maajabu yake ni kwamba jamaa ndiyo alianza kulalamika na wadada ndiyo wakaja kuonyesha ya upande wao.
 
Shemeji kumbe ushalishuhudia hilo

kuna watu wakitoka humu jf nadhani ata elimu wengine tutakosa.

Kuna nyuzi nyingine ya ajabu lakini unakuta imeonwa mara 30,000 sasa anzisha uzi wa jinsi ya kujua bidhaa feki la haula mpaka kesho unaweza ukakuta una onwa mara 63.

wenyewe tunaogopa kujulikana alafu mtu anatuchezea eti anaondoka pyeeee zake aka RIP
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Habari

Kuna ka mtindo hapa kameanzishwa na memba humu kututishia kwamba wanaacha kutumia jf

Katika uchunguzi wangu niliofanya nikagundua yafuatayo:

1. Unatumia simu, laptop, au mfano wake ila ukiamua kuacha jf unaitangazia dunia nzima vizuri lakini japo ni haki yako

2. Unaamua kutoka jf kama Miss Natafuta ila baada ya siku tatu unakuja tena na unakuwa active zaidi ya Troll JF au @joseverout

3. Unaamua kutoka jf tena unatupa muda ikifika saa kumi jion utakuwa ushatoka ila ikija comment ya saa tatu usiku unajibu na kesho na kesho kutwa unakuwa bado upo

4. Unaamua kujitoa jf lakini uki-tag-iwa unakuja kwa spid ya mwanga wala haipiti sekunde 59

5. Wengine wanaamua kujitoa wanaanzisha uzi ila anapata comment tatu. Kesho anakuja na nyuzi nyingine baada ya kukosa support

6. Wengine wanaamua kutoka jf ili waone nani watamlilia abaki

7. Wengine wanamua kujitoa eti kwa sababu wanafuatwa. unatumia id fake hujui ni ya jike au dume alafu unasema watu wanakufuata mmmhhh

KAMA MNATOKA TOKENI NA KWENDENI KABISA
Naunga hoja mkono
 
Back
Top Bottom