Hiki kiarabu kina maana gani?

Hiki kiarabu kina maana gani?

The ice breaker

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2023
Posts
880
Reaction score
1,985
Nilikuwa Nina shida Fulani, itabidi nikamuone shekhe ndio anaweza kunisaidia, ila baada ya kunisomea Dua , akanipa hili karatasi kama niweke kwenye wallet

Naomba tasfiri yake wakuu, isije ikawa nimepewa jini kijanja, maana napata hela, sijui zinapo ishia
 

Attachments

  • IMG_20241227_231339_460.jpg
    IMG_20241227_231339_460.jpg
    685.6 KB · Views: 5
Ulipeleka njiwa au jogoo? Hiyo damu, jini hilo.
Jogoo ni kujikinga na maadui,watu wabaya,wafitini hamna madhara.
Njiwa,kunguru, bundi ni mauaji na hapo huchomoki.
So we kaa utulie mda si mrefu utapata majibu
 
Hayo maneno ya juu ni suurat nnaswir ni sura ya 110 katika qur an na hayo ya chini ni dua anajiombea mwenyew aliendika kwasabab kaandika Ewe allah wewe ni mwenye kutoa na mimi ni mwenye kuomba, hakuna yeyote atakae muacha muombaj ispokuwa atampa ewe mola wangu ewe mola wangu ewe mola wangu baada ya hapo amemswalia mtume na hayo maneno ya upande wa kushoto kaandika ewe allah ewe allah ewe allah ewe allah na hayo ya kwenye kibox sijui maan yake kwasababu ni herufi tu katika herufi za kiarabu ni sawa wewe unadike (uuuuuuu aaaaa) kwa ufupi hiyo ni dua anajiombea muandishi.
 
Nilikuwa Nina shida Fulani, itabidi nikamuone shekhe ndio anaweza kunisaidia, ila baada ya kunisomea Dua , akanipa hili karatasi kama niweke kwenye wallet

Naomba tasfiri yake wakuu, isije ikawa nimepewa jini kijanja, maana napata hela, sijui zinapo ishia

Juu ya karatasi kaandika surat nasr (idhajaa), kushoto ni kamtaja Allah (the almighty mara tatu) , chini ni dua na katika kibox ni herufi tu za kiarabu , ila kuna shida mahali 👇👇👇

"Nilikuwa Nina shida Fulani, itabidi nikamuone shekhe ndio anaweza kunisaidia........."

1. Tengua hiyo kauli hapo juu hakuna shaikh anaweza kukusaidia ukiwa na shida si shaikh tu hakuna nabii wala mtume (hapa naongelea wakina Nuhu(alayhi salaam), ibrahim(alyhi salaam) , isa(alayhi salaam) na hata mtume muhammad (swalallahu alayhi wasalam) anayeweza kukusaidia ukiwa na shida anayeweza hayo ni ALLAH (the almighty) PEKEEE HAKUNA MWENGINE FULL STOP

2. Watu tunapokosea ni kwamba hatufanyi ibada , wala kujituma kukamilisha ibada za faradhi na nyenginezo kwa wakati na kujikurubisha kwa Muumba wetu halafu tunataraji tukipata shida na matatizo ndo tunamkumbuka 😂 utaenda kwa mashaikh , utaenda kwa waganga utamaliza kila kitu kumbe tatizo ni WEWE.

3. SISAPOTI KWENDA KWA SHAIKH ILI KUTATULIWA SHIDA ZAKO , MAOMBI YAKO KWENYE SIJDA YANA NGUVU KULIKO KITU CHOCHOTE HIVYO KAMA UNA SHIDA JUA WEWE NDO UNA NAFASI KUBWA YA KUSIKILIZWA NA MUUMBA KULIKO MWENGINE IBADA IBADA IBADA FULLSTOP.

4. KWA MSAADA WA HARAKA CHUKIA KIBERITI CHOMA HIYO TAWIZ , yaani unaandikiwa dua kwenye karatasi kwa kutumia zafarani halafu anakwambia ubebe nenda kachome hiyo kitu hakuna mtu anaweza kukusaidi kwa kukuandikia dua chache kwenye karatsi shida ipo kwako , kwa msaada kachukue wudhu swali na kila sijda lalamika kweli kweli mpaka ujibiwe inshaallah.


N.B
kuna watu ni waganga ila wanatumia kivuli cha dini kujitia u shaikh chungeni mtabebeshwa majini
 
Nilikuwa Nina shida Fulani, itabidi nikamuone shekhe ndio anaweza kunisaidia, ila baada ya kunisomea Dua , akanipa hili karatasi kama niweke kwenye wallet

Naomba tasfiri yake wakuu, isije ikawa nimepewa jini kijanja, maana napata hela, sijui zinapo ishia
 

Attachments

  • 5851466-20e16fd0b98c2357e9ca61e2b5957c5d.mp4
    4.8 MB
Sasa mbona hiyo ni tarasimu,hakuna tarasimu isiyohusiana na majini hapo tayari umepewa jini sasa na wewe unapewa vitu hata huulizi?,ngoja uanze kupigwa midudu usiku ukiwa umelala ndio utashangaa
Oya kweli ?
 
Back
Top Bottom