Hiki ni nini? Naombeni ushauri nachanganyikiwa. Nimekopa Milioni 14 natakiwa kurudisha Milioni 39

Hiki ni nini? Naombeni ushauri nachanganyikiwa. Nimekopa Milioni 14 natakiwa kurudisha Milioni 39

Usikope utakuwa desparate ,usikope ni dhuluma ya mifumo ya bank .

Usikope achana na riba utafilisika hapa duniani.

Usikope ni mtego jaribu kubangaiza kuishi ndani ya bajeti kuwa na watoto hata wawili wanatosha.

Mikopo unapewa ukiwa na ndoto ambazo hautotimiza kabisa.
 
Nimevumilia ila nimechoka acha niwaambie, ndugu walimu nimekopa AbC bank shilingi milioni 14 nikatwe kwa miaka nane sawa na miezi 96, nakatwa shilingi laki nne na elfu 14 kwa mwezi.

Nimeshangaa kukuta kwenye salary slip deni ni milioni 39😥😥😥, nimelia sana yaani nakopa 14M narudisha 39?
Mimi kwakua nilikua nina dharula ya haraka sana nilienda ABC maana niliabiwa kule hauzunguki sana na nilipofika niliongea nao tu mda ule ule nikajaza fomu nikaondokq mkopo ukaingia kesho yake, najuta sikupata mda wa wenda kusoma makubaliano na wala hawakunipa nakala yoyote!

Hii sio haki serikali iko wapi jamani?

Nifanyeje naombeni ushauri wenu
View attachment 2744997
Hapo ndio wengi wanapolizwa,unapewa vigezo na masharti karibu ukurasa mzima,unaona uvivu kusoma unaamua kusaini,kumbe kila kitu kiko hapo,subiri sasa kwenye makato...
 
Kwanini usingeenda NMB au CRDB?
Bayport walinifata ofisini ili wanikopeshe nilipowauliza riba ni asilimia wakaanza chenga chenga braah braah kibao,nikambananisha mmoja wao akaniambia riba ni 47% nikawafukuza ofisini.
Seriously?? 😭😭😭😭😭😭😭😭😭👆🏾
 
Wewe ungemkopesha mtu mil 14 kwa miaka nane ungemdai kiasi gani?
Lipa hela ya watu boss hao wanafanya biashara.
Mikataba husomi halafu unalialia.
 
Tusimtishe hapo wamekosea, haiwezekani umdai 39 wakati ulimpa 14. Inatakiwa adaiwe 14 na riba ya wakati huo, ili akiamua kulipa kwa mkupuo analipa deni na kitu inaitwa early settlement fee.

Mleta mada dai mkataba wako angalia riba ni kiasi gani uza mkopo kwa mabenki kama CRDB then enjoy maisha. Usiwe mnyonge na mtumwa. Kukopa sio dhambi.
Unafikiri akiuza hilo deni crdb wtaandikaje kwenye salary slip?
 
Kila siku tunatoa ushauri humu acheni kukopa kwenye taasisi uchwara za kifedha hamsikiii..hawa ABC,Platinum sijui..Bayport ni kausha damu haswa..
Hata angekopa CRDB au NMB mambo ni yale yale huwezi kukopa million 14 kwa miaka 8 utegemee ulipe million 20 au chini ya hapo.
MKopo unapozidi kukaa nao riba inakuwa kubwa zaidi...
 
Deni lolote benki kama si kwa matumizi ya kibiashara ni hasara tupu!! Ili mtu afanikiwe kutokukopa benki inabidi awe na mkakati huo tangu mwezi wa kwanza wa ajira yake. Iko hivi: Amua kuishi kwa kadri ya kipato unachopata. Amua kuweka 250,000/= benki kama akiba ambazo uhesabu kuwa hazipaswi kuingia kwenye matumizi yako. Panga chumba cha bei rahisi kimkakati, kula kimkakati na vaa kimkakati. Ukifanikiwa zoezi hili kwa miaka 5 utakuwa una akiba ya sh 15,000,000/=.

Hapo unaweza kuanza kukopa toka kwenye akiba yako mwenyewe, na zoezi la kutunza 250,000/= kwa mwezi liwe endelevu muda wote uwapo kazini. Mkakati huu unawezekana tu kama ukiuanza mwanzoni kabisa mwa ajira yako. Usikubali kuiga maisha ya watu, unajua wenzio watakopa benki na kuanza kuendesha magari, kununua vitu vya kifahari nk, hao watakutisha kwa miaka 5 tu basi!! baada ya miaka 5 utakuwa na akiba ya kukutosha kufanya vitu vya kimaendeleo. Lakini usipokuwa na mikakati hiyo utajikuta unalazimika kukopa ili kupeleka watoto shule, kununua kiwanja na kuanza ujenzi wa nyumba!! Ukikwepa mikopo utaokoa mamilioni ya riba ambazo wakopaji hulazimika kulipa. Utafanikiwa kupata vitu walivyopata wenzio bila gharama ya riba.

Lakini ukijiingiza kwenye mikopo, utajikuta unakuwa mkopaji muda wote uwapo kazini. Unakopa marejesho kwa miaka 8 kabla hujamaliza unapata shida nyingine unafanya top up, na mchezo huo huendelea hadi mtu anastaafu. Hutakwepa kukopa kama hutafanya mkakati wa ku-save pesa from day one!!
 
Unafikiri akiuza hilo deni crdb wtaandikaje kwenye salary slip?
Asiuze deni!! AAmue tu kulifanyia mkakati wa kulilipa hata kutoka vyanzo vingine ili liishe mapema!! Halafu aachane na mikopo labda kama ni ya mradi, na mradi uwe na uwezo wa kurejesha hilo deni!!
 
Deni lolote benki kama si kwa matumizi ya kibiashara ni hasara tupu!! Ili mtu afanikiwe kutokukopa benki inabidi awe na mkakati huo tangu mwezi wa kwanza wa ajira yake. Iko hivi: Amua kuishi kwa kadri ya kipato unachopata. Amua kuweka 250,000/= benki kama akiba ambazo uhesabu kuwa hazipaswi kuingia kwenye matumizi yako. Panga chumba cha bei rahisi kimkakati, kula kimkakati na vaa kimkakati. Ukifanikiwa zoezi hili kwa miaka 5 utakuwa una akiba ya sh 15,000,000/=.

Hapo unaweza kuanza kukopa toka kwenye akiba yako mwenyewe, na zoezi la kutunza 250,000/= kwa mwezi liwe endelevu muda wote uwapo kazini. Mkakati huu unawezekana tu kama ukiuanza mwanzoni kabisa mwa ajira yako. Usikubali kuiga maisha ya watu, unajua wenzio watakopa benki na kuanza kuendesha magari, kununua vitu vya kifahari nk, hao watakutisha kwa miaka 5 tu basi!! baada ya miaka 5 utakuwa na akiba ya kukutosha kufanya vitu vya kimaendeleo. Lakini usipokuwa na mikakati hiyo utajikuta unalazimika kukopa ili kupeleka watoto shule, kununua kiwanja na kuanza ujenzi wa nyumba!! Ukikwepa mikopo utaokoa mamilioni ya riba ambazo wakopaji hulazimika kulipa. Utafanikiwa kupata vitu walivyopata wenzio bila gharama ya riba.

Lakini ukijiingiza kwenye mikopo, utajikuta unakuwa mkopaji muda wote uwapo kazini. Unakopa marejesho kwa miaka 8 kabla hujamaliza unapata shida nyingine unafanya top up, na mchezo huo huendelea hadi mtu anastaafu. Hutakwepa kukopa kama hutafanya mkakati wa ku-save pesa from day one!!
Unaongea kirahisi rahisi tu nyie ndio watu hamjawahi kushika hela mnaongea kiubwete ubwete tu hapa
 
Deni lolote benki kama si kwa matumizi ya kibiashara ni hasara tupu!! Ili mtu afanikiwe kutokukopa benki inabidi awe na mkakati huo tangu mwezi wa kwanza wa ajira yake. Iko hivi: Amua kuishi kwa kadri ya kipato unachopata. Amua kuweka 250,000/= benki kama akiba ambazo uhesabu kuwa hazipaswi kuingia kwenye matumizi yako. Panga chumba cha bei rahisi kimkakati, kula kimkakati na vaa kimkakati. Ukifanikiwa zoezi hili kwa miaka 5 utakuwa una akiba ya sh 15,000,000/=.

Hapo unaweza kuanza kukopa toka kwenye akiba yako mwenyewe, na zoezi la kutunza 250,000/= kwa mwezi liwe endelevu muda wote uwapo kazini. Mkakati huu unawezekana tu kama ukiuanza mwanzoni kabisa mwa ajira yako. Usikubali kuiga maisha ya watu, unajua wenzio watakopa benki na kuanza kuendesha magari, kununua vitu vya kifahari nk, hao watakutisha kwa miaka 5 tu basi!! baada ya miaka 5 utakuwa na akiba ya kukutosha kufanya vitu vya kimaendeleo. Lakini usipokuwa na mikakati hiyo utajikuta unalazimika kukopa ili kupeleka watoto shule, kununua kiwanja na kuanza ujenzi wa nyumba!! Ukikwepa mikopo utaokoa mamilioni ya riba ambazo wakopaji hulazimika kulipa. Utafanikiwa kupata vitu walivyopata wenzio bila gharama ya riba.

Lakini ukijiingiza kwenye mikopo, utajikuta unakuwa mkopaji muda wote uwapo kazini. Unakopa marejesho kwa miaka 8 kabla hujamaliza unapata shida nyingine unafanya top up, na mchezo huo huendelea hadi mtu anastaafu. Hutakwepa kukopa kama hutafanya mkakati wa ku-save pesa from day one!!
Mkuu uko njema sana kiakili nakupa maua yako. Na nawapa wazazi wako maua yao wamekuza mtu timamu na makini sana
 
Nimevumilia ila nimechoka acha niwaambie, ndugu walimu nimekopa AbC bank shilingi milioni 14 nikatwe kwa miaka nane sawa na miezi 96, nakatwa shilingi laki nne na elfu 14 kwa mwezi.

Nimeshangaa kukuta kwenye salary slip deni ni milioni 39😥😥😥, nimelia sana yaani nakopa 14M narudisha 39?
Mimi kwakua nilikua nina dharula ya haraka sana nilienda ABC maana niliabiwa kule hauzunguki sana na nilipofika niliongea nao tu mda ule ule nikajaza fomu nikaondokq mkopo ukaingia kesho yake, najuta sikupata mda wa wenda kusoma makubaliano na wala hawakunipa nakala yoyote!

Hii sio haki serikali iko wapi jamani?

Nifanyeje naombeni ushauri wenu
View attachment 2744997
Watu inatakiwa wa fahamu kwamba

Riba ya Benki = riba ya mwaka x miaka ya kulipa

Mfano kwa Benki hiyo riba ni 22.3%


Riba ya jumla ni 22.3% x miaka 7 = 156.1%


Hivyo faida ya Benki itakuwa 156.1% ya 14M

= 1.56
Nimevumilia ila nimechoka acha niwaambie, ndugu walimu nimekopa AbC bank shilingi milioni 14 nikatwe kwa miaka nane sawa na miezi 96, nakatwa shilingi laki nne na elfu 14 kwa mwezi.

Nimeshangaa kukuta kwenye salary slip deni ni milioni 39😥😥😥, nimelia sana yaani nakopa 14M narudisha 39?
Mimi kwakua nilikua nina dharula ya haraka sana nilienda ABC maana niliabiwa kule hauzunguki sana na nilipofika niliongea nao tu mda ule ule nikajaza fomu nikaondokq mkopo ukaingia kesho yake, najuta sikupata mda wa wenda kusoma makubaliano na wala hawakunipa nakala yoyote!

Hii sio haki serikali iko wapi jamani?

Nifanyeje naombeni ushauri wenu
View attachment 2744997
 
Back
Top Bottom