Uchaguzi 2020 Hili la kuondoa vitambulisho vya machinga umebugi stepu

Marekani inaongoza kwa kukopa duniani.

Kujijenga kiuchumi haimaanishi tuache kukopa...

Jibu na swala la vitambulisho lililosababisha kuchafua mji vibanda mpaka kwenye service roads za wapita kwa miguu kisa wanalipa elfu20?
Tuliambiwa nchi ina uwezo wa kujiendesha yenyewe kwa kodi zetu mbona bado unaendelea kuongelea swala la mikopo ya bei nafuu? Kumbe mnajua nchi haijitoshelezi nilazima ikope?

kumbe mtukufu anavyosema tunajiendesha kwa fedha zetu kumbe ni uongo? Tunakopa?na nyie mnaolipwa vijisent ili mje kupiga kelele humu mnalijua hilo? yaan kuondoa wafanyakazi hewa, kutopandisha mishahara, kuto kutoa ajira na kukusanya kodi nyingi kuliko viongozi wote walopita lakini kumbe bado tunakopa!![emoji12]
 
Lakini unasema wewe, Lisu amesema atafuta vitambulisho bila ya kusema nini kinatafuata Kwa wamachinga ili waweze kwendelea kufanya biashara bila bughudha iliyokuwa ikiwatesa kipindi hicho

Jaribu kuwa mwelewa, kinachotakiwa kumlinda mmachinga sio kitambulisho, bali kuwepo na kanuni zinazotambua haki za machinga kisheria.
[/QUOTE
 
Kama hataji nini atawaboreshea zaidi ya hapo, anajiundia bomu la nyukilia nakwambia
 
Uliza mbadala wa vitambulisho itakuwa nini kabla hujapingapinga
 
Asilimia kubwa thread zako wewe, ni kumponda Lissu tu!
 
Kwani kitambulisho sio sera?
Mbona wafanya biashara wakubwa pia wana leseni kulingana na biashara yake kwa hiyo hiyo sio sera?
Au umekurupuka
Wajasiriamali duniani kote hulindwa na sera bora sio kitambulisho!
 
Kwani kitambulisho sio sera?
Mbona wafanya biashara wakubwa pia wana leseni kulingana na biashara yake kwa hiyo hiyo sio sera?
Au umekurupuka
Kitambulisho ni sera! Nmekurupuka mjuzi.
 
Yaan tunasema Kipande system kwa
Njia mpya
 

hili la korona kabisa ndo mwiba wa cdm, yaani walibugi sana kwa kifupi mchakato wa kumfuta tu ukamilike na wale jamaa waliomkosa na risasi wamalize walipoishia
 
Hataondoa vitambulisho bali atawapa bure siyo kuwalipisha pesa acha upotoshaji wewe
 
Hataondoa vitambulisho bali atawapa bure siyo kuwalipisha pesa acha upotoshaji wewe
jamani chadema waongo, amesema kabisa ataondoa vitambulisho vya machinga, huyu ni adui wetu namba moja, anataka kufukarisha watanzania
 
Kumbuka ukiweka kanuni pia watalazimika kukaa maeneo maalum tofauti na sasa ambapo utawakuta hadi masaki.

Kwa hiyo bado watarudi kule kule walikotoka na wengi wao hawaamini kukaa sehemu moja.

Ninyi watu ni wa ajabu na wasahaulifu sana....

Kwanza dhana yenyewe tu ya "kitambulisho cha Machinga/mjasriamali mdogo" haieleweki...

Haieleweki pesa zinakusanywa na nani japo tunaambiwa ni TRA, lakini ukweli siyo huo...

Haieleweki pesa hizo zinakwenda wapi na kufanya mini...

Ambacho tunaamini ni kuwa, huo ni mpango wa M/kiti wa CCM (taifa) ambaye pia ni Rais na kwa kutumia vibaya mamlaka yake ya "URAIS" anakitafutia chama chake fedha kwa ajili ya kuendesha shughuli za chama ikiwemo kampeni za uchaguzi, kununua wanasiasa wa vyama pinzani nk...

Hili ni rahisi mno kulieleza kwa wananchi na kueleweka kuwa kumbe wanaibiwa tu, wanafisidiwa tu, hamna lolote....

Kwa hiyo, hii kitu inapaswa kukomeshwa mara moja kwa sababu kwa vipimo vyote huu ni WIZI mtupu....
 
Nyie kweli zumbukuku..kwani kodi na makusanyo mrngine zote unajua zinaenda kwa nani?

Punguzeni kujitia aibu.

Halafu ukisema dhana yenyewe kwani wamachinga hawafanyi biashara?? Kuna malalamiko yoyote toka waingie mkataba na serikali kupitia hicho kitambulisho kwamba wanasumbuliwa?

Ya wamachinga muwaachie wamachinga. Hayo ndio madhara ya kutokuwa na hoja..matokeo yake badala ya kutafuta kura unapoteza hata zile chache za huruma.
 
Sheiza m, the Sukuma gang, mmefikwa na mabaya , poleni Sana machinga

Makusanyo yote ya pesa yanajulikana yanaenda wapi, zingine zinaenda halamashauri ya wilaya au mji, zingine ni za TRA vitambukisho vya machinga, magufuli pesa aliweka wapi?
Halafu mtu anauza vitumbua vimejaa ndoo vyenye thamani ya elfu 5.halafu unataka kabla hajafanya hivyo biashara akate kitambulisho elfu 20.Hapo si umemla mtaji?
Hata hivyo machinga wanatofautiana levo, wapo wanaouza hata elfu50 Kwa siku wengine hata elfu 2 kupata shida. Imagine mtu anauza vichori au mchicha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…