Hili la mbunge baraza la wawakilishi kuwadharau samaki aina ya Kambale na Sato wa ziwa Victoria lisipite pasipo mjadala. Linatoa picha mbaya

Hili la mbunge baraza la wawakilishi kuwadharau samaki aina ya Kambale na Sato wa ziwa Victoria lisipite pasipo mjadala. Linatoa picha mbaya

Kwa ajili ya samaki tu??
Mi sio mzanzibar ila hao sato na sangara hunilishi!
Yani niache kupochoa changu ,kolekole , koana , tasi and the likes nianze kulansmaki hawana hata ladha, !!! samaki gani hakubali nazi !
Na hizi tetesi kuwa ziwa limekuwa contaminated na zebaki za kwenye migodi ndo kabisaaaa sitaki hata kuwaona , maana kanda ya ziwa ipo juu kwa kansa , kwa sababu ya zebaki.
Siyo samaki pekee kuna mambo mengi sn wanatudharau
 
Sio kama Zanzibar hakuna kambale,wapo ila wanakuwa kama toyz ,watoto wakienda kucheza kwenye mabwawa na mito ndio huwamwagia yale majani yanayowalewesha wakafurai,ila kuwa mradi wa Taifa,kwa mabilioni ,bora muwapelekee wambeya.
 
Tuwaze vizuri kwa akili zetu alizotupa Mungu. Hivi unajua tani moja ya Sato ni shilingi ngapi? Hivi unajua mahitaji ya hao samaki kwenye soko nje nchi yakoje? Aliyekuambia ule kambare ni nani. Au mnataka wenzenu wafuge halafu mje kwenye meza ya mgao wa mapato!
Sasa si imetosha kuwafuga huko kwenye ardhi kubwa hakuna ulazima biashala hio kuileta au kuipeleka Zenji ,tena hela itoke kwenye selikali ya Zanzibar,hilo gumu halimezeki ,selikali ya muungano itoe katika lile deni wajenge huko wafuge kambale wakauze ulaya ela watulipe lile deni.
 
Siyo samaki pekee kuna mambo mengi sn wanatudharau
Ila hii ya samaki yule mwakilishi alikuwa anaongelea white elephant projects
Huwezi ukaweka mradi wa kuzalisha kambale na sato zanzibar wakati hao samaki hawaliwi kule , hiyo ni fact japo mwakilishi ametumia nyodo kuwakilisha.

Na sio dharau wala nini mtu wa pwani hali samaki wa bara , na wa bara akionja mapishi ya samaki wa pwani hatoacha kula .
 
Ila hii ya samaki yule mwakilishi alikuwa anaongelea white elephant projects
Huwezi ukaweka mradi wa kuzalisha kambale na sato zanzibar wakati hao samaki hawaliwi kule , hiyo ni fact japo mwakilishi ametumia nyodo kuwakilisha.

Na sio dharau wala nini mtu wa pwani hali samaki wa bara , na wa bara akionja mapishi ya samaki wa pwani hatoacha kula .
Sawa
 
Kuna video moja fupi inazunguka mitandaoni anaonekana mbunge wa baraza la wawakilishi akiwaongelea kwa dharau samaki wa Ziwa Victoria. Anasema wao kwa maana ya watu wa visiwani hawana utamaduni wa kula samaki wa aina hiyo, kwamba isitokee mbegu zao zikawekwa kwenye bahari iliyo karibu na visiwa vya Unguja na Pemba!.

Hii ni kebehi mbovu sana, ina maana watu wa visiwani wanaoishi kule mikoa ya Ziwa Victoria hawali samaki wanaovuliwa kutoka kwenye maji yale!!?. Huku kujiona wa maana kunakojionyesha katika maneno ya yule mheshimiwa kunaleta taswira ya dharau kwa jamii pana ya Tanzania.

Waunguja na wapemba tumeishi nao tangu utoto mwetu, tukasoma nao vyuo vikuu na kufanya nao kazi. Na ninao uhakika vyakula vingi vinavyolisha visiwa hivyo na vile vya Comoro vinatoka huku Bara. Ni mazao yanayolimwa na wakulima wa mikoa ya Bara. Kama familia moja ya Kiembesamaki au Mwanakwerekwe inaweza kula wali unaotokana na mchele wa Mbeya lipi la hatari kwa afya ya familia hiyo iwapo itakula samaki wa maji baridi?.

Mbunge huyo wa baraza la wawakilishi kwa lugha ya kweli isiyo ya kuremba ni kwamba ameropoka, tena bila ya kujua madhara ya kauli yake. Alipaswa kutumia aina ya maneno yasiyoleta ukakasi kwa wavuvi wa Ziwa Victoria na wakazi mamilioni wanaoishi maeneo ya kanda ile. Wabunge kutoka Zanzibar wanaoingia ndani ya bunge la Jamhuri wanakula kila aina ya vyakula ambavyo baadhi vinalimwa na wakulima wa kanda ya Ziwa.

Wapo wazanzibari wengi tu waliokuzwa na Sato pamoja na Sangara kule kanda ya Ziwa, wanaujua utamu wa samaki hao. Hivyo mbunge yule atahadharishwe tu na waungwana kwamba kauli yake ndani ya kikao cha baraza la wawakilishi, inaweza kuwa imekera watu.
Wewe utakua msukuma tu,hivi nyie wasukuma mbona washamba sana nyie

Halafu sio kila jambo ulitolee comment sometimes soma pita kimyakimya au wewe ni mnufaika wa hayo mabilioni?

Kwanini muwapangie watu maisha nyie wasukuma who the hell you think you are

Hivi ubora wa KIBUA utaufananisha na Sato au kambale,halafu tena muchote mabilioni ya watanzania eti muwanunulie kambale BASTARD haibiwi mtu this time yule wakala wa SHETANI hayupo sasa mkumbuke hivo


Sasa njo tena na POVU LAKO mshamba wewe we unafikiri mbuzi na ng'ombe wanafanana
 
Wewe utakua msukuma tu,hivi nyie wasukuma mbona washamba sana nyie

Halafu sio kila jambo ulitolee comment sometimes soma pita kimyakimya au wewe ni mnufaika wa hayo mabilioni?

Kwanini muwapangie watu maisha nyie wasukuma who the hell you think you are

Hivi ubora wa KIBUA utaufananisha na Sato au kambale,halafu tena muchote mabilioni ya watanzania eti muwanunulie kambale BASTARD haibiwi mtu this time yule wakala wa SHETANI hayupo sasa mkumbuke hivo


Sasa njo tena na POVU LAKO mshamba wewe we unafikiri mbuzi na ng'ombe wanafanana
Mimi sio msukuma. Yule mbunge kaongea kwa nyodo sana.
 
Msije kutuomba kodi zetu zitakazotokana na kuuza kambale Uarabuni kwa maana hamkawii kudai kuwa ni haki yenu ama la sivvyo mtavunja muungano na mkivunja muungano itabidi wengine warudi Zenj wakiwa hawana kazi bwashee😂😂😂😂
Hahahahaahahahahahahaah
 
Sasa si imetosha kuwafuga huko kwenye ardhi kubwa hakuna ulazima biashala hio kuileta au kuipeleka Zenji ,tena hela itoke kwenye selikali ya Zanzibar,hilo gumu halimezeki ,selikali ya muungano itoe katika lile deni wajenge huko wafuge kambale wakauze ulaya ela watulipe lile deni.
Kuamua kuacha kujilegeza ili uhudumiwe ni uamuzi tu.
 
Hiki ndo kinachowaharibu waunguja wengi(sio wpte)

Yani kukataa tamaduni za wengine with appreciation hawawezi,lazima kuna kauli wataziweka ambazo zinaonesha kudharau vya wenzao kana kwamba sio bora.

Yani wanaonesha kwamba wanakataa tamaduni za wenzao kwa sababu sio bora kama za kwao.

Tania hii ipo kwa wazenji wengi,ni tabia ya ajabu ambayo nimeiona sana ipo kule zanzibar.
Eti sasa Bara wanachukia hata ukionesha madharau kwa sato na sangara wao! poleni!
 
Kuna video moja fupi inazunguka mitandaoni anaonekana mbunge wa baraza la wawakilishi akiwaongelea kwa dharau samaki wa Ziwa Victoria. Anasema wao kwa maana ya watu wa visiwani hawana utamaduni wa kula samaki wa aina hiyo, kwamba isitokee mbegu zao zikawekwa kwenye bahari iliyo karibu na visiwa vya Unguja na Pemba!.

Hii ni kebehi mbovu sana, ina maana watu wa visiwani wanaoishi kule mikoa ya Ziwa Victoria hawali samaki wanaovuliwa kutoka kwenye maji yale!!?. Huku kujiona wa maana kunakojionyesha katika maneno ya yule mheshimiwa kunaleta taswira ya dharau kwa jamii pana ya Tanzania.

Waunguja na wapemba tumeishi nao tangu utoto mwetu, tukasoma nao vyuo vikuu na kufanya nao kazi. Na ninao uhakika vyakula vingi vinavyolisha visiwa hivyo na vile vya Comoro vinatoka huku Bara. Ni mazao yanayolimwa na wakulima wa mikoa ya Bara. Kama familia moja ya Kiembesamaki au Mwanakwerekwe inaweza kula wali unaotokana na mchele wa Mbeya lipi la hatari kwa afya ya familia hiyo iwapo itakula samaki wa maji baridi?.

Mbunge huyo wa baraza la wawakilishi kwa lugha ya kweli isiyo ya kuremba ni kwamba ameropoka, tena bila ya kujua madhara ya kauli yake. Alipaswa kutumia aina ya maneno yasiyoleta ukakasi kwa wavuvi wa Ziwa Victoria na wakazi mamilioni wanaoishi maeneo ya kanda ile. Wabunge kutoka Zanzibar wanaoingia ndani ya bunge la Jamhuri wanakula kila aina ya vyakula ambavyo baadhi vinalimwa na wakulima wa kanda ya Ziwa.

Wapo wazanzibari wengi tu waliokuzwa na Sato pamoja na Sangara kule kanda ya Ziwa, wanaujua utamu wa samaki hao. Hivyo mbunge yule atahadharishwe tu na waungwana kwamba kauli yake ndani ya kikao cha baraza la wawakilishi, inaweza kuwa imekera watu.
Kosa lako ni kwamba unaogopa hata kumtaja jina tu!

Huyo mbunge hajui kwamba samaki wa ziwa Victoria hawawezi kuwekwa baharini?
Bila shaka anajuwa vyema kabisa, na kama ulivyopanua mada yako, ni kwamba mbunge huyo alikuwa haongelei "Samaki", analo jambo maalum alilolenga kulifikishia ujumbe.

Ni vizuri kabisa ajulikane jina, ili kusudi siku moja tusijikute ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Umenielewa mkuu!
 
Sasa Mzanzibari unampelekea Sato na Kambale si kituko?watu wamezoea Josari,Kolekole.,Kingfish n.k.Samakj samakj tamu haina haja ya vikorombwezo
 
Kimsingi muungano uvunjwe, wazanzibar wanatudharau sn
Kwani anoutaka muungano ni nani?

ni nyie pamoja no viongozi wenu wa CCM. Wa zanzibari wengi hawautaki muungano huu ulokuwepo.

  1. Hakuna hata moja jema mnalo watakia wazanzibari.
  2. Zantel imepata taabu hata kusajiliwa.
  3. Mizigo ikitoka Zanzibar inatozwa ushuru pale bandarini Bara.
  4. Wanafunzi wa Zanzibar wanafelishwa kwenye mitihani na Zanzibar inapotaka kuweka mfumo wake pingamizi.
  5. Zanzibar ilitaka kujiunga na OIC pingamizi. uganda imo kwenye OIC
  6. Misaada ikija kutoka nje lazima ipite BOT haiwezi kuja Bank ya Zanzibar. pia Waziri wa fedha wa bara aweke signature.
  7. Zanzibar ina FM frequency ya radio inayo tumiwa na CCM hawataki kuitowa ukihoji ni msaliti.
  8. Masheik wapo ndani sababu wamehoji muungano tuu. na kubambikizwa makesi yote hayo
  9. Namengine tu ipolist kubwa
 
Hiyo unaiona kuna hoja ya kujadili kweli? Hujui tunatofautiana? Unachokula kwenu unataka nasi tule kwa sababu ya muungano? We vipi? Lete mambo ya maana hapa!
Utawalazimisha watu wale sato kumbe hawakuzoea. Nina hakika hata wakazi wa kanda ya ziwa hawapendi change au kolekole. Wakisema hivyo usiwalaumu.
 
Kula wewe hao sangara na sato, wao watakula pweza na pronzi
 
Kwani anoutaka muungano ni nani?

ni nyie pamoja no viongozi wenu wa CCM. Wa zanzibari wengi hawautaki muungano huu ulokuwepo.

  1. Hakuna hata moja jema mnalo watakia wazanzibari.
  2. Zantel imepata taabu hata kusajiliwa.
  3. Mizigo ikitoka Zanzibar inatozwa ushuru pale bandarini Bara.
  4. Wanafunzi wa Zanzibar wanafelishwa kwenye mitihani na Zanzibar inapotaka kuweka mfumo wake pingamizi.
  5. Zanzibar ilitaka kujiunga na OIC pingamizi. uganda imo kwenye OIC
  6. Misaada ikija kutoka nje lazima ipite BOT haiwezi kuja Bank ya Zanzibar. pia Waziri wa fedha wa bara aweke signature.
  7. Zanzibar ina FM frequency ya radio inayo tumiwa na CCM hawataki kuitowa ukihoji ni msaliti.
  8. Masheik wapo ndani sababu wamehoji muungano tuu. na kubambikizwa makesi yote hayo
  9. Namengine tu ipolist kubwa
Iitishwe kura ya maoni haraka tuone ni nani anautaka huu muungano
 
Back
Top Bottom