Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

magufuli alichomaanisha ni kuwa wale majambazi wanaokuwa na silaha na kwenda kuvamia kituo cha polisi polisi achukue tahadhari ya kuanza kumshambulia, binafsi sijaona tatizo hapa, yaani jambazi anapora silaha polisi halafu asiuawe?
 
Words should be given their literal meaning before going into the intricacies of employing other meanings
 
Si juzi tu kasema anasimamisha vyeo kwa muda kama miezi hivi leo tena vyeo. Halafu huwezi kuwa unapandisha vyeo tu kwa watu wakitekeleza majukumu yao vinginevyo itakuwa kila mtu boss. Na ile dhana ya kubana matumizi imepotea maana cheo ni pesa pia.
 
Mnaogopa nini mjambazi wamejichagulia kazi ya kupora Mali za watu na kuwauwa wakiwa hawana hatia mbona majambazi hawatumii sheria katika kuuwa watu wala hawachaguwi wa kumuuwa badhi ya watanzania ni wa ajabu mnasimama kutetea majambazi bila aibu!!!!!!
 



Tatizo vijana wa Lumumba wengi wao wanakosa hekima kama hizi sijajua wamepatwa nanini!! Maana hoja iliyopo mezani ni sensitive sana kwa mutakabali wa Taifa letu na maisha yakila mmoja wetu lkn wao wanaleta siasa hata kwenye mambo yasiyokuwa ya kiitikadi!! Huwa nafurahia sana ninapopata comments zilizoshiba kama hizi ajabu inakuja mijinga fulani fulani ikiongozwa na tutusa mmoja aitwae lizaboni inaharibu atmosphere humu[emoji15] [emoji15]
 
Well said mkuu..
Comment Yako inafaa iwe Uzi mkuu...
Point tupu..shukrani
 
Hili ni jema maaana majambazi hawana nia nzuri wanapotaka kumuibia mtu wanakuja kwa kuua kabisa......so kama wana siraha wanyang'anywe harakaharaka na police atakayefanikisha apandishwe cheo tu!
Ngoja tuone.
 
Hakuna anaetetea majambazi hofu yetu kubwa ninamna jeshi letu litakavyoitumia hiyo opportunity kujinufaisha kwa kutenda kinyume na maagizo ya Rais maana uzoefu unaonesha kwamba polisi huwa natabia zakuwabambikia watu kesi za ajabuajabu ambapo hata muheshimiwa Rais amewahi lizungumzia hadharani, mm binafsi nalaani kwa nguvu zangu zote mauaji ya polisi wetu pamoja na raia wasio nahatia lkn kuruhu polisi kuua bila taratibu watu wengi wataguswa na hili either direct au indirect
 
😀😀 ina maana makomda ana uelewa zaidi ya mwigulu? Huu sasa utani jamani
 



Hoja zilizopo kwenye huu Uzi wa mkuu Pasco zinakuzidi "kimo cha fikra",hata ukichuchumia au kupanda juu ya stuli,bado hutoweza kuzifikia. Pasco ametumia fikra za juu sana kufikisha hoja yake hapa jukwaani.

Kwanza una umri gani? Nisije nikapoteza muda kubishana na mtoto.Lakini ngoja nikupe" benefit of doubt" kuwa wewe ni mtu mzima.Unakikumbuka vema kisa cha Mauwaji ya Mh.IMRAN KOMBE? Mh.huyu(Mungu amrehemu)aliuwawa kikatili na jeshi letu tukufu la polisi kwa kuhisiwa kuwa ni jambazi.Marehemu Kombe hakuwa mtu kapuku asiyefahamika kiasi cha polisi kutomfahamu na kupelekea kumuhisi ni jambazi.Alikuwa ni kiongozi Mwandamizi wa vyombo vyetu vya ulinzi,kama intelijensia ya jeshi letu ilishindwa kumtambua bosi wao(Marehemu Kombe) na kuishia kumuua kikatiri sana kwa kumuhisi ni jambazi,jiulize hali itakuwaje kwa makapuku kama Mimi na wewe tusiofahamika popote chini ya amri hii dharimu na uchu wa kupandishwa vyeo si tutauliwa makumi kwa maelfu?

Hatuyasemi haya kwa bahati mbaya,pamoja na nia njema ya Mh.Rais na kuonesha kukelwa na vitendo vya kihalifu,bado hakupaswa kutoa maagizo ya aina ile kwa jeshi letu la polisi lenye sifa ya "kutii bila shuruti" amri za kisiasa hata kama amri hizo zinaenda kinyume na katiba yetu.

Ni vema kile kilichoitwa "maboresho kwa jeshi letu" kingejikita katika kuwajengea uwezo wa kiintelejensia ya kisasa zaidi na kuachana na intelijensia za kuzuia shughuli za kisiasa za washindani wa serikali.Kauli za kuwahimiza polisi kumvamia mtu bila weledi,kumpola silaha au kung'oa matairi ya Gari na kuyauza hata kama tunaozipinga tunaonekana tuna I.Q ndogo,bado si kauli zilizopaswa kutoka kwenye kinywa cha kiongozi wetu.Masikio yetu yanapata shida kuamini kama yalichokisikia kimetoka kwa kiongozi au kwa mtu aliye pembeni yake?

Hii ni nchi yetu sote,hakuna anayetetea uhalifu,ila tunashauli uhalifu ukomeshwe kwa mbinu sahihi na si kutumia uhalifu kupambana na uhalifu,hilo halikubariki.Tusipoyakemea haya huko tuendako tunaweza kushuhudia viongozi wetu wapendwa ambao baadhi yetu tumeshawaingiza kwenye "orodha ya Sala za Ritania ya Watakatifu" wakikumbana na mkono wa sheria kwa kupelekwa ICC wakikabiliwa na mashitaka ya kuchochea uvunjifu wa haki za kibinadamu.Kitendo hicho cha "Mtakatifu wetu" kupelekwa ICC kinaweza kuikwaza imani yetu.Hatutaki tufike huko.
 
Well said Mkuu na quote usemi wako tena "Kinachobanwa sana sana kina nafasi ya kujiachia". Maji ya kipanwa sana uwezekano wa kupasua pipe ni mkubwa. Uhuru ukibanwa sana uwezekano wa kutafuta namna ya kuwa huru utatafutwa kwa nguvu zote hata kwa kuruka ukuta. Hongera kwa maneno ya busara.
 
mi nadhani kwa kauli hii ya rais, hakuna haja ya magereza yetu kujaa majambazi nao wafumuliwe risasi tu...Mana wakirudi mtaani na hii hali ya uchumi itakuwa shida mpya, pia kubana matumizi ya magereza yetu.
 

Nasikitika kuona watanzania wengi hawana mtazamo,unaweza ukaongea kijiona una I.Q nzuri,kumbe walioko pembeni wanakucheka
Kwa ujumla watu wengi hamjui dunia imefikia wapi mpaka sasa,na hamjui kwanini kunamaboresho ndani ya jeshi la polisi na vilevile hamjui hali ya hewa iliopo ndani ya hii nchi,nikuache kama ulivyo nisije nikalala mimi.
 
Acheni kuingiza siasa kwenye maisha ya watu kama rais anatoa taMAILko kama lenye kulenga kulinda usalaama wa raia harafu mnaleta siasa. Kwahiyo pasco unashabikia majambazi au nawewe ni moja wao nn?? Kama hawajahi kukuvamia hawa watu hutajua uchungu ila wakikutembelea cku moja utajua umuhimu wa kauli ya raisi
 
Katika hili,ni vema kila anayefahamiana na jambazi
amshauri abadilishe mbinu ya kupata pesa.
sikubaliani na yeyeyote anayesema jambazi ana huruma(Tafuta maana ya jambazi kwenye kamusi).

Huruma si kuishia kutoua,kuna vifo vingine vinavyotokana
na madhara uliyosababishiwa na jambazi kukufanyia ujambazi.
mfano ni kukopa fedha benki na jambazi akakupola pesa hizo
ila akakuacha hai.Hujafa kwa risasi ila unakufa kwa presha ya nyumba yako uliyoweka
bond kuuzwa kwani fedha uliyokopa hukufanyia biashara uliyokusudia.

Polisi naamini mmemuelewa rais,wanyanganyeni majambazi silaha HARAKA.
wakiwapa silaha haraka wa hiari yao,zichukueni.Wakiwanyima wanyanganyeni msisahau neno "HARAKA"

Mwisho nawakaribisha wale waliojihusisha na ujambazi
njooni tukalime,mbona poa tu na maisha yanaenda
msisubiri kunyanganywa silaha HARAKA,Hii inaweza kuwaletea madhara.
 
Siku zooote unaongea pumba na kutetea uozo, lakini kwa hili, wow wow wooow, umenena point sana
 
Huyu jamaa vp au na ww jambaz nn unatetea upumbavu kwan wamekosa kaz za kufanya mpaka wapole raia Mali zao safi jpm nikuwagonga tu maana hamna namna na yeyote anayetetea mawili ajui uchungu wa kuibiwa au yeye mwenyewe mwizi
 
Majambazi sahvi ni mwendo wa kupigwa shaba tu,mleta mada hii elewa tangia kipindi cha nyuma polisi wamekuwa wakiwaua wale majambazi sugu....kwa siri Ila mains sasa magu kawapa green light polisi ya kuwashugulikia majambazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…