Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?


Wanabodi,

Wewe kama mwana JF, unapata an added advantage to be the first to know, ambapo leo katika tukio la maboresho ya jeshi la polisi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais, Dr. John Pombe Magufuli, ametoa kauli kwa kutumia fasihi, ambapo ameliamuru jeshi la polisi, kukabiliana na majambazi wenye silaha kwa "kuwanyang'anya silaha kwa kutumia mbinu za medani, (kivita) (MM) ambazo hutumiwa na majeshi wakati wa vita, ambapo kazi huwa ni moja tuu, kumteketeza adui!.

Amri hiyo kwa Jeshi la Polisi, inamaanisha, Polisi hawahitaji tena kuwakamata majambazi wanaotumia silaha, bali kukabiliana nao kwa kuwaua papo kwa papo, na polisi wataofanya mauaji hayo ya kuwauwa majambazi hayo papo kwa papo bila kuwapeleka mbele ya vyombo vya sheria, hawatafikishwa tena mahakamani, kama zamani, bali sasa watapandishwa vyeo!.

Agizo hilo limepokelewa kwa shangwe na makofi kwa kila aliyekuwe pale.

Rais huku akisema kwa msisitizo kwa kutumia fasihi ya "kuwanyanganya silaha", kwa vile majambazi wanatumia silaha, zenye risasi kufanya ujambazi, na jeshi la polisi nalo wanazo silaha zenye risasi, haoni kwa nini majambazi hayo yasinyang'anywe silaha zao!. Namna pekee ya kunyanganya silaha jambazi mwenye silaha, ni kumalizana nao, papo kwa papo!.

Sina shaka kabisa na nia ya dhati ya rais Magufuli, kutoa amri, hiyo, kufuatia nchi na wananchi kuchoshwa na vitendo vya ujambazi kuongezeka, hivyo majambazi wakijua kuwa wakikamatwa watauwawa right away, then, amri hii badala ya kupunguza ujambazi wa kutumia silaha, ndio kwanza utaongeza impunity kwa majambazi wanaotumia silaha, na wakati huo huo kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!.

Sio majambazi wote wanaotumia silaha, zile silaha zao zina risasi!, wengine huzitumia kutishia tuu, lakini hawana nia ya kufanya mauaji, na kuna wengine hubeba silaha ambazo hazina risasi, na wengine hutumia toy pisto!, lakini kufuatia amri hii, polisi ndio kwanza wamekuwa licenced to kill!.

Tanzania ni nchi ya kidemokasia inayofuata katiba yenye kuzingatia haki na utawala wa sheria!, amri kuu ya kwanza ya haki, ni "no one is condemned unheard", yaani hakuna mtu atakayehukumiwa bila kusikilizwa!. Amri hii ya rais, imewapa mamlaka polisi, sio tena kuchunguza, kukamata na kuwapeleke majambazi wanaotumia silaha, mbele ya sheria, bali sasa polisi hawana tena haja ya kukamata na kufanya uchunguzi, bali kukitokea tuu tukio la uhalifu wa kutumia silaha, polisi wamepewa mamlaka kuwa ni wachunguzi, prosecutors, mahakimu tena kwa kutoa "capital punishment", na hakuna tena haja ya kumsubiri rais kuzisaini hizo hati za capital punishment, bali, wao wenyewe kutumia MM, kuitekeleza adhabu ya kifo, na baada ya hapo kusubirria kupandishwa vyeo!. Just imagine mashindano ya kupanda vyeo miongoni mwa polisi wetu!.

Kama wanasheria wetu, hawatashitushwa na amri hii ya rais, nitaamini sasa Watanzania wameanza kumwelewa rais wetu, na ukiisha elewa, huna haja ya kuhoji!.

Angalizo: Sitetei vitendo vyovyote vya uhalifu wa aina yoyote, bali natetea utoaji wa haki!, hata jambazi anayetumia silaha, anastahili kutendewa haki!. Natolea mfano wa nchi mbili za Maekani na Uingeeza. Miaka ya nyuma nchi zote hizi zilikubwa na vitendo vingi vya mauaji. Uingeeza ikafuta adhabu ya kifo!, vitendo vya mauaji, vikapungua kwa kiasi kikubwa!. Maekani ikaendelea na adhabu ya kifo, vitendo vya mauaji bado vimeongezeka!.

Amri ya kuwaua majambazi papo kwa papo, haitapunguza ujambazi, bali itawafanya hao majambazi ndio kugeua wauwaji wakuu, kwa hoja za "ama zao, ama zetu" na kwenye tukio lolote la ujambazi wa kutumia silaha, polisi wakitokea, sasa sio tena kutuliza amani bali kufanya a blood bath!, hivyo polisi sasa pia watakuwa ni target ya majambazi!.

Kwetu sisi waandishi, ikitokea polisi wakakutana na gun mike, au boom mike, au hata kamera wakaiona ni kama sihaha!, kama ilivyotokea mwa Daudi Mwangosi!, askai mhusika, atapandishwa cheo!. Kama wale vija wa Zombe, sasa watawadiwa vyeo!.

Huko nyuma niliwahi kushauri, kama katiba ni kikwazo, rais Magufuli, aiweke pembeni katiba na badala yake atawale kwa kutumia 'presidential decrees' tuu!. Hivyo kwa amri hii ya polisi kuua majambazi papo kwa papo, kama mahakama ni kikwazo, pia anaweza kuiweka pembeni, na kuwatumia polisi kutoa hukumu za kifo cha papo kwa papo, tena hili litaokoa fedha nyingi sana, maana majaji wa mahakama zetu, wanahudumiwa kwa gharama kubwa sana!.

Wasiwasi wangu kwa amri kama hizi, sio ili kuokoa maisha ya majambazi wanaotumia silaha, au kuwaacha tuu majambazi wanaotumia silaha kuua, lakini wao kuuliwa tuinawatetea!, no!, wasiwasi wangu ni utekelezaji wa amri za aina hii, zisije kuwa kwa majambazi ni mwanzo tuu, baadae amri kama hizi za 'kinyemela' zikaelekezwa kwa makundi mengine, yanayoonekana ni kero!.

Hata Adolfu alipoanza, alianza hivi hivi kwa kushangiliwa na umati wa watu!, ni baadae sana, ndipo watu wakajuta!, chonde chonde twendeni taratibu jamani tusije kujuta!.

Jumamosi Njema.

Pasco[/QUOTE]
Pole sana #Tanzania
 
tatizo sio IGP...tatizo ni CCM
Mimi nadhani IGP hatoshi kwenye nafasi yake, maana tumekuwa na matukio ya ujambazi kila kukicha bila njia stahiki za kukabiliana na waharifu na vile vile alikuwa anacheka cheka tu wakati rais anaongelea juu ya kuwanyang'anya majambazi silaha, sasa sijui kitu gani kilikuwa kinamfurahisha wakati kuna askari kibao tu na raia wamepoteza maisha kwa sababu ya majambazi. Mbona kipindi cha Mrema aliweza japo kupunguza?? Labda tusubiri Mwigulu. Ila kwa mtizamo wangu, Paul Makonda alifaa nafasi ya uwaziri wa mambo ya ndani.
 
Hakuna anayempenda jambazi lakini kauli ya Rais ni ya hatari sana. Tunawajua hawa polisi wetu. Polisi hawa ambao waliwahi kuwaua wafanyabiashara wa madini na kusingizia ni majambazi, hawa waliomwua Mwangosi ambaye hakuwa na silaha yoyote, halafu unawapa mamlaka ya kuua.

Tunaweza kushangilia lakini kuna siku utauawa wewe au kaka yako au mdogo wako au baba yako au mtoto wako halafu silaha itaoneshwa kwenye luninga na kusema kuwa hii silaha tuliinyang'anya kutoka kwa jambazi sugu.

Walioweka utaratibu kuwa wahalifu wafikishwe kwenye mahakama hawakuwa wajinga bali mataifa hayo yalipitia mengi, na baadaye wakaona kuwa huo ndiyo utaratibu wa kulinda haki za watu. Kama askari ameua raia awe ni jambazi au la, uchunguzi ni lazima ufanyike ili kujiridhisha kama kweli huyo marehemu alikuwa ni jambazi? Na je marehemu alikuwa tishio kwa usalama wa askari? Namna nyingine tutashuhudia sana vifo vya wasio na hatia kwa kisingizio kuwa marehemu walikuwa na silaha.
 
Pasco kuna mapungufu mengi sana kwenye Tamko la Rais.
Nadhani ange reserch madhara ya hili tamko kabla.
Yani maisha ya watu sasa yatategemea busara na hali ya askari.
Askari wanaograduate siku hizi ni vijana wadogo wenye busara ya unene wa wembe.
Halafu sidhani kama katiba inampa rais nguvu ya kuamua kipi kiende mahakamani na kipi kisiende.
Rais ametoa ruhusa rasmi ya kujichukulia sheria mkononi.
Yani I can't belive this, all one has to do is show up with a dead body and a weapon.
And no questions, no nothing, you rise in rank'
we should expect a lot of roadside justice.
Ukienda nchi kama Marekani usicheze Na Askari la sivyo unaenda na Maji. Watakuua hapo hapo ndo maana watu wanatii sheria sisi tunalea upuuzi eti ni demokrasia
 
Dr Makufuri @ his best. "kuwanyang'anya" majambazi silaha ni muendelezo mwingine wa dr makufuri KUKANYAGA haki za binadamu.
 
U
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi![/QUOTE
Hivi unawajua Polis vizuri hawa wa Tanzania? Ushawahi kuwa Polisi au askari wa Jeshi la Polisi?? Kwa ufupi tu ulivyimuelewa Mh. JPM ni tofauti na walivyoelewa askari wetu..ile ni amri kauli ya Mh.ni amri na lazima itekelezwe bila kupunguza chochote. Hapa kazi tu
 
Halafu sidhani kama katiba inampa rais nguvu ya kuamua kipi kiende mahakamani na kipi kisiende.
Rais ametoa ruhusa rasmi ya kujichukulia sheria mkononi.
Yani I can't belive this, all one has to do is show up with a dead body and a weapon.
And no questions, no nothing, you rise in rank'
we should expect a lot of roadside justice
.


Unaongea kama Mzungu wa CNN au BBC, hivyo hivyo yaani hakuna tofauti yani kasoro Pua, Mdomo, Nywele na rangi ...
 
Jpm Alikuwa amemaanisha kuwa MTU akikamatwa na bunduki hainahaja ya kunfikisha mahakamani nae auwawe, aliongea kimafumbo
 
Mimi nadhani IGP hatoshi kwenye nafasi yake, maana tumekuwa na matukio ya ujambazi kila kukicha bila njia stahiki za kukabiliana na waharifu na vile vile alikuwa anacheka cheka tu wakati rais anaongelea juu ya kuwanyang'anya majambazi silaha, sasa sijui kitu gani kilikuwa kinamfurahisha wakati kuna askari kibao tu na raia wamepoteza maisha kwa sababu ya majambazi. Mbona kipindi cha Mrema aliweza japo kupunguza?? Labda tusubiri Mwigulu. Ila kwa mtizamo wangu, Paul Makonda alifaa nafasi ya uwaziri wa mambo ya ndani.

Team Lumumba,UVCCM mshabamia jamvi
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!
Acha kuzuga ww hujui kauli ya rais ina impact gani ktk utekelezaji?
 
Pasco, kuna siku polisi wakitimiza haya, Mh. kuna mwaka atapelekwa the Hague! He has authorised the suspects to be condermed unheard! Can this justify one to face ICC for haphazard killings of suspects? (I am not a lawyer). A big point to note from your posting is MAKUNDI MENGINE YANAYOONEKANA NI KERO. TRULY THIS IS SOMETHING TO WORRY ABOUT!
Well said!
Kila neno moja analoongea rais husafiri masafa marefu na kuleta maana tofauti na madhara makubwa miongon kwene jamii
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!

splendid

watanzania wana mambo acha tu!!
 
Barbarosa unataka kutuambia Magufuli amekuwa Yesu, sasa anaongea in 'parables'?
Ok, sio mbaya kama Injinia wetu ameamua kuongea kwa 'codes'
Mtupe na sisi hizo code tuwe tunaelewa.
Yani, haki ya nani, watumishi wa umma tripu hii watakoma.
Unapewa order kwa 'metaphor'!!

Magufuli sio injinia!!
 
Wezi wa simu na vibaka wengine wananchi humalizana nao papo kwa papo. Jambazi likikuvamia nyumbani kwako lina SMG na wewe una ka shotgun ukiliwahi unamalizana nalo papo kwa papo. Sasa polisi wakikusaidia kumalizana nalo si ndiyo kazi yao? Kwa nini wasite eti lìna haki ya kuishi wakati lilitaka kukuondolea wewe haki hiyo?

Jamani tofauti hizi za itikadi za kisiasa hivi kweli zinatufikisha hapa ya watu kuyatetea majambazi yenye bunduki kali yaliyokamatwa red handed? Eti polisi iyabembeleze ili wayapeleke mahakamani?

Hata huko Ulaya na Marekani polisi wakikukuta unafanya ujambazi au ugaidi wanakumaliza hapo hapo full stop.
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!
Mheshimiwa, unaelewa vizuri maana ya Metaphor au ni neno umeliona mahali ukaona ulitumie bila kujua maana yake?! Rudi darasani na epuka kutumia maneno ya kiingereza usiyoyajua vizuri maana hata mfano uliotoa hauendani kabisa na maana na matumizi ya metaphor. Kwa taarifa yako huyo unayemsema kwamba katumia hiyo wewe unayoiita metaphor, hajui kabisa fasihi na hana uwezo nayo na hajui tamathali za semi. Sasa wewe unakuwa kama kipofu anayetaka kumuongoza mwenye chongo! Hivi viingereza mnavyong'ang[ania wakati hamuvielewi vizuri mtakuja kutukana matusi bure humu jukwaani.
 
Pasco unaupeo mkubwa sana aisee sema humu ndani kunakosekana wachangiaji mahili kwasababu jamii forum imepoteza uhalisia wa slogan yake ya Where we dare to talk openly but yote kwa yote hongera sana Pasco
 
Back
Top Bottom