Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Barbarosa unataka kutuambia Magufuli amekuwa Yesu, sasa anaongea in 'parables'?
Ok, sio mbaya kama Injinia wetu ameamua kuongea kwa 'codes'
Mtupe na sisi hizo code tuwe tunaelewa.
Yani, haki ya nani, watumishi wa umma tripu hii watakoma.
Unapewa order kwa 'metaphor'!!
Hahaaaaaaaaaaa, achana nae,,unaweza ukakwazika ukimsikiliza huyu mtu.kwake Jpm Ni zaidi ya saint!!!
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!

Mkuu kwani unafikiri hawajui Rais anamaanisha nini? Wanajua sana - kuali zake zinakuwa grossily misintepreted kimakusudi/delibaretly lengo lao kuu ni kutaka kudhilishia Dunia kwamba kumbe Dk.Magufuli uongozi hauwezi - yaani wanataka kuzuga Watanzania kwamba tulifanya makosa kumpigia kura ya ndio Mh.Magufuli, kwa mawazo yao wanafikiri propaganda zao zinaweza kubadiri mawazo ya wapiga kura come 2020 mtu wao itinge Ikulu kiulaini.

Nasena hivi: kwa mtaji wao iliyo seheni disiformation kuhusu Administration ya Tingatinga na kujaribu ku demonise Dk.Magufuli personally sioni kama mbinu hizo zitawafikisha popote.

Ingawa wanaonekana wako highly organised/determined kupotosha watu - vinara wa scam hii wanajulikana, wakumbuke wenzao wanajua jinsi ya kuwa contain kisayansi.
 
Nilisoma zamani sana Physics, kanuni moja ya mwendo ikisema hivi kama sijakosea : Action and reaction are equal but opposite. Jambazi akijua kama hafikishwi Mahakamani na amezingirwa na polisi au raia halafu ana bunduki yenye risasi sijui kama atajisalimisha hivi kikondoo asilete uharibifu mkubwa.

Wapo watu wamehukumiwa kwa kuua wahalifu mbalimbali wakiwemo majambazi kwa kosa la kujichukulia sheria mkononi.

Huu ni Mtego wa panya, utanasa hata wasio kuwemo. Wapo watakao bambikwa kesi na kuuawa kama Mwangosi ukaambiwa alikuwa na siraha.

Kama Jambazi anaua na wewe raia mwema unaua nani sasa mhalifu? Je tunajenga jamii ya aina gani?
 
mbona raia tunaua wizi vibka kwani hatuvunji sheria?kama tunavunja mbona hatuchukuliwi hatua
mungu aliandika ktk torati ya mussa aliyeua nae awawe hakuna jinsi
 
Nasikitika kuona watanzania wengi hawana mtazamo,unaweza ukaongea kijiona una I.Q nzuri,kumbe walioko pembeni wanakucheka
Kwa ujumla watu wengi hamjui dunia imefikia wapi mpaka sasa,na hamjui kwanini kunamaboresho ndani ya jeshi la polisi na vilevile hamjui hali ya hewa iliopo ndani ya hii nchi,nikuache kama ulivyo nisije nikalala mimi.



Ni bora nichekwe kwa kupinga hoja zisizo na afya kwa ustawi wa Taifa letu,kuliko kufurahiwa na kupigiwa makofi kwa "kusapoti" hoja za kujenga viwanja vya kumbukumbu ya push-ups,kujenga sanamu la Diamond,Kuleta Kilimo cha umwagiliaji wa ubuyu,kung'oa matairi ya gari na kuyauza ili askali wetu wapate vijisenti na mengine mengi yanayofanana na hayo.

Endelea kusali "Ritania ya watakatifu" na kumuomba "Mtakatifu wako akuombee".
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!
Kwenye waiting list ya U DC atakuweka pale juu kabisa. Ingawaje namna yako ya kupima IQ yachekesha kidogo. Umejiweka kuwa kiwango? Lumumba iko tatizo
 

Wanabodi,

Wewe kama mwana JF, unapata an added advantage to be the first to know, ambapo leo katika tukio la maboresho ya jeshi la polisi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais, Dr. John Pombe Magufuli, ametoa kauli kwa kutumia fasihi, ambapo ameliamuru jeshi la polisi, kukabiliana na majambazi wenye silaha kwa "kuwanyang'anya silaha kwa kutumia mbinu za medani, (kivita) (MM) ambazo hutumiwa na majeshi wakati wa vita, ambapo kazi huwa ni moja tuu, kumteketeza adui!.

Amri hiyo kwa Jeshi la Polisi, inamaanisha, Polisi hawahitaji tena kuwakamata majambazi wanaotumia silaha, bali kukabiliana nao kwa kuwaua papo kwa papo, na polisi wataofanya mauaji hayo ya kuwauwa majambazi hayo papo kwa papo bila kuwapeleka mbele ya vyombo vya sheria, hawatafikishwa tena mahakamani, kama zamani, bali sasa watapandishwa vyeo!.

Agizo hilo limepokelewa kwa shangwe na makofi kwa kila aliyekuwe pale.

Rais huku akisema kwa msisitizo kwa kutumia fasihi ya "kuwanyanganya silaha", kwa vile majambazi wanatumia silaha, zenye risasi kufanya ujambazi, na jeshi la polisi nalo wanazo silaha zenye risasi, haoni kwa nini majambazi hayo yasinyang'anywe silaha zao!. Namna pekee ya kunyanganya silaha jambazi mwenye silaha, ni kumalizana nao, papo kwa papo!.

Sina shaka kabisa na nia ya dhati ya rais Magufuli, kutoa amri, hiyo, kufuatia nchi na wananchi kuchoshwa na vitendo vya ujambazi kuongezeka, hivyo majambazi wakijua kuwa wakikamatwa watauwawa right away, then, amri hii badala ya kupunguza ujambazi wa kutumia silaha, ndio kwanza utaongeza impunity kwa majambazi wanaotumia silaha, na wakati huo huo kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!.

Sio majambazi wote wanaotumia silaha, huzitumia silaha hizo kufanyia mauaji!, sio silaha zote zinazobebwa zinakuwa loaded!, wengine huzitumia kutishia tuu, lakini hawana nia ya kufanya mauaji, na kuna wengine hubeba silaha ambazo hazina risasi, na wengine hutumia toy pisto!,na majambazi wengine, hubeba silaha, na ziko loaded, lakini hawafanyi mauaji baada ya kupata walichotaka!, lakini kufuatia amri hii, hao majambazi wenye huruma na maisha ya watu, hawatakuwa na huruma tena, na kama polisi ndio kwanza wamekuwa licenced to kill kwa mtindo wa MM, then every encounter ya polisi na majambazi, tutegemee nothing, no justice but blood bath!.

Tanzania ni nchi ya kidemokasia inayofuata katiba yenye kuzingatia haki na utawala wa sheria!, amri kuu ya kwanza ya haki, ni "no one is condemned unheard", yaani hakuna mtu atakayehukumiwa bila kusikilizwa!. Amri hii ya rais, imewapa mamlaka polisi, sio tena kuchunguza, kukamata na kuwapeleke majambazi wanaotumia silaha, mbele ya sheria, bali sasa polisi hawana tena haja ya kukamata na kufanya uchunguzi, bali kukitokea tuu tukio la uhalifu wa kutumia silaha, polisi wamepewa mamlaka kuwa ni wachunguzi, prosecutors, mahakimu tena kwa kutoa "capital punishment", na hakuna tena haja ya kumsubiri rais kuzisaini hizo hati za capital punishment, bali, wao wenyewe kutumia MM, kuitekeleza adhabu ya kifo, na baada ya hapo kusubirria kupandishwa vyeo!. Just imagine mashindano ya kupanda vyeo miongoni mwa polisi wetu!.

Kama wanasheria wetu, hawatashitushwa na amri hii ya rais, nitaamini sasa Watanzania wameanza kumwelewa rais wetu, na ukiisha elewa, huna haja ya kuhoji!.

Angalizo: Sitetei vitendo vyovyote vya uhalifu wa aina yoyote, bali natetea utoaji wa haki!, hata jambazi anayetumia silaha, anastahili kutendewa haki!. Natolea mfano wa nchi mbili za Maekani na Uingeeza. Miaka ya nyuma nchi zote hizi zilikubwa na vitendo vingi vya mauaji. Uingeeza ikafuta adhabu ya kifo!, vitendo vya mauaji, vikapungua kwa kiasi kikubwa!. Maekani ikaendelea na adhabu ya kifo, vitendo vya mauaji bado vimeongezeka!.

Amri ya kuwaua majambazi papo kwa papo, haitapunguza ujambazi, bali itawafanya hao majambazi ndio kugeua wauwaji wakuu, kwa hoja za "ama zao, ama zetu" na kwenye tukio lolote la ujambazi wa kutumia silaha, polisi wakitokea, sasa sio tena kutuliza amani bali kufanya a blood bath!, hivyo polisi sasa pia watakuwa ni target ya majambazi!.

Kwetu sisi waandishi, ikitokea polisi wakakutana na gun mike, au boom mike, au hata kamera wakaiona ni kama sihaha!, kama ilivyotokea mwa Daudi Mwangosi!, askai mhusika, atapandishwa cheo!. Kama wale vija wa Zombe, sasa watawadiwa vyeo!.

Huko nyuma niliwahi kushauri, kama katiba ni kikwazo, rais Magufuli, aiweke pembeni katiba na badala yake atawale kwa kutumia 'presidential decrees' tuu!. Hivyo kwa amri hii ya polisi kuua majambazi papo kwa papo, kama mahakama ni kikwazo, pia anaweza kuiweka pembeni, na kuwatumia polisi kutoa hukumu za kifo cha papo kwa papo, tena hili litaokoa fedha nyingi sana, maana majaji wa mahakama zetu, wanahudumiwa kwa gharama kubwa sana!.

Wasiwasi wangu kwa amri kama hizi, sio ili kuokoa maisha ya majambazi wanaotumia silaha, au kuwaacha tuu majambazi wanaotumia silaha kuua, lakini wao kuuliwa tuinawatetea!, no!, wasiwasi wangu ni utekelezaji wa amri za aina hii, zisije kuwa kwa majambazi ni mwanzo tuu, baadae amri kama hizi za 'kinyemela' zikaelekezwa kwa makundi mengine, yanayoonekana ni kero!.

Mwaka 1976, kulifanyika mauaji ya wazee waliokuwa wakituhumiwa kuwa ni wachawi. Serikali kupitia waziri wa Mambo ya Ndani kipindi hicho, Ali Hassan Mwinyi Mwinyi, kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mwanza, chini ya RC Peter Kisumo, RSO, RPC, DSO, na OCD wakadhamiria kwa kauli moja kukomesha vitendo hivyo kwa hizo hizo MM alizoamrisha Magufuli zitumike!.

Katika Mahojiano, yaliyoendeshwa eneo la Kigoto, watuhumiwa wawili, Masanja Makula Mazengenuka, na Isaack Mwanamkoboko, walipoteza maisha!.

Mwalimu Nyerere alikasika sana, Waziri Mwinyi, IGP, Pundugu, Director wa TISS Mzena, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Kisumo, RSO, RPC, DSO na OCD wote wakastaafishwa kwa manufaa, na wengine kupandishwa kizimbani, ambapo wote walifungwa, isipokuwa mshtakiwa Mzee wangu, tena aliokoka kwa vile tuu alikuwa anatetewa na wakili Murtaza Lakha!.

Utendaji wa Jeshi la Polisi unaongozwa na kitu kinachoitwa Police General Ordes ambacho tumekirithi kutoka kwa Waingereza kama tulivyorithi sheria zetu mbalimbali, ambazo zina maelekezo yote ni kwenye mazingira gani polisi anaruhusiwa kutumia silaha kuwadhibiti wahalifu na kuna polisi maalum wa kazi hiyo wanaoitwa snipers au wadunguaji, ambao wana shabaha na uwezo wa kulenga maeneo rasmi ya kulenga ili kumdestabilize mhalifu kwa lengo la kumkamata lakini sio kwa lengo la kumua!. Agizo la jana la Rais Magufuli, ni kuwaelekeza polisi kuua tena kwa haraka bila kuchelewa, na sasa kwa kila mauaji ya polisi, polisi hao badala ya kupandishwa kizimbani, sasa watapandishwa vyeo!.

Japo lengo la agizo hilo la rais, amelitoa kwa dhamira njema,(in good faith), lakini utekelezaji wake, unaweza kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!, na hata Adofu alipoanza, alianza hivi hivi kwa kuwa a populist leader, anayeshangiliwa sana na umati wa watu!, ni baadae sana, ndipo watu wakaja kugundua, by that time, it was too little too late, wakaishia kujuta!, kwa upande wetu, chonde chonde twendeni taratibu jamani, tufungue macho mapema before it is too late, tusije kujuta!.

Jumamosi Njema.

Pasco
Rejea.
Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...
IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality
Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa .
Simshangai Pasco wa JF tu; hapana, nawashangaa waandishi wote wa ..

siungi mkono police kujichukilia sheria mkononi
lakin pia sidhani kama kuna jambazi anayekwenda kufanya uhalifu na silaha ya kutishia anapoacha kufanya mauaji ni pale tu anapofanikisha kazi yake.

amri hii ya raisi ikifanyiwa kazi ipasavyo
bila mizengwe itasaidia kupunguza uhalifu.

ni aibu kwa police kubeba silaha isiyoweza kumsaidia kumnyanga'nya jambazi silaha.
 
Kwa mfululizo wa kauli za rais nimeshamsoma ni mtu wa aina gani. Tulieni baada ya miaka yake mitano tutapata majibu. Anaendesha nchi kwa moyo wake badala ya kichwa.
 
Mkuu kwani unafikiri hawajui Rais anamaanisha nini? Wanajua sana - kuali zake zinakuwa grossily misintepreted kimakusudi/delibaretly lengo lao kuu ni kutaka kudhilishia Dunia kwamba kumbe Dk.Magufuli uongozi hauwezi - yaani wanataka kuzuga Watanzania kwamba tulifanya makosa kumpigia kura ya ndio Mh.Magufuli, kwa mawazo yao wanafikiri propaganda zao zinaweza kubadiri mawazo ya wapiga kura come 2020 mtu wao itinge Ikulu kiulaini.

Nasena hivi: kwa mtaji wao iliyo seheni disiformation kuhusu Administration ya Tingatinga na kujaribu ku demonise Dk.Magufuli personally sioni kama mbinu hizo zitawafikisha popote.

Ingawa wanaonekana wako highly organised/determined kupotosha watu - vinara wa scam hii wanajulikana, wakumbuke wenzao wanajua jinsi ya kuwa contain kisayansi.

Hawaelewi kwanini TTCL imechukuliwa jumla na simu zote fake zimezimwa, na nini kipo nyuma ya pazia.

Ni aibu sana kwa mtu kama Pasco kuendelea kuja JF kupotosha umma.

Raisi Magufuli, piga kazi mkulu.

Wananchi wa kawaida tupo nyuma yako asilimia 100.
 
Acheni kuingiza siasa kwenye maisha ya watu kama rais anatoa taMAILko kama lenye kulenga kulinda usalaama wa raia harafu mnaleta siasa. Kwahiyo pasco unashabikia majambazi au nawewe ni moja wao nn?? Kama hawajahi kukuvamia hawa watu hutajua uchungu ila wakikutembelea cku moja utajua umuhimu wa kauli ya raisi




Usilete utetezi mwepesi kwenye masuala mazito,hakuna anayepingana na nia njema ya Mh.Rais ya kupambana na uhalifu,tunachopinga ni Lugha na maelekezo anayoyatoa kwa vyombo vyake.

Mheshimiwa M.P.K.Pinda aliwahi"kuchomoka bungeni kwa mwendokasi uliokadiriwa kufikia division 4.30km/saa, akaagiza watakaokamatwa kwa kosa la kuua Albino nao wauwawe,pamoja na kuonesha kuguswa na mauwaji ya ndugu zetu albino,mh.Pinda alipingwa vikali na kwa uungwana wake japo hoja yake aliitoa huku akimwaga machozi mbele ya bunge,lakini aliisahihisha baada ya kuona ilikuwa na mapungufu mbele ya sheria.

Uungwana ni vitendo,kuliko kukomaza shingo kuzitetea kauli zenye ukakasi,ni bora watu wakiri kuwa walipotoka na kutoa nafasi kwa Taifa kuimaliza mijadala hii yenye kuleta utata.

Kuwalazimisha watu wote waitikie "mdundo" wa ngoma(matamko ya serikali) hata pale mdundo huo unapokuwa na tafsiri zenye utata,ni kuwaweka watu kwenye "vifungo vya fikra". Hatuwezi kukubali kutiishwa na kuwekewa mipaka ya ukomo wa fikra zetu kama walivyofanya kwa wabunge wa ccm pale walipowapiga marufuku kutofautiana na hoja za serikali bungeni.Hilo halikubariki.
 
Hapa naona kila polis wote watapandishwa vyeo maana akiona hajapanda na ana siraha piga raia hpa lamcng raia na wale weny tabia ya udokoz kaz kwao
 
Mimi nilidhani dhana ya maboresho ya jeshi la polisi ililenga ktk haya;

1. Jeshi la polisi kufanya kazi yake ya kulinda usalama wa raia na mali zao kwa mbinu za kisasa zaidi

2. Jeshi la polisi kutumia mbinu hizo za kisasa kuzuia uhalifu kabla haujatokea

Kauli ya Mr President ina kasoro na matobo tobo mengi. Nakubaliana na Pasco kuwa kinachobaki ni busara za mapolisi wenyewe kutumia akili zao kuamua huku wakikumbuka kuwa sheria zipo zinazowaongoza kutekeleza majukumu yao

Wakumbuke kuwa kwa mujibu wa katiba yetu ya JMT ya mwaka 1977 mwenye kinga ya kutoshitakiwa ni Rais pekee akiwa madarakani na aachapo madaraka yake.....nyie wengine mapolisi wenzangu sheria za nchi hii zipo na kamwe hamuwezi kuzipiga chenga!!

Huwezi kukomesha uhalifu kwa kutenda uhalifu. Nimesemema sheria zipo na Pasco kashauri vyema sana kuwa, kama Rais JPM anataka kuwalinda hawa aliowapa hii amri batili iliyo kinyume na katiba aliyoapa kuilinda, basi afanye hivyo kwa kutumia "Presidential decree" ambayo hii huwalinda wale wote wanaotekeleza maagizo ya serikali kama hili!!

Kinyume chake hakuna polisi mjinga atakayeamua kuua tu eti kwa kuwa Rais kasema kwa kauli tu za kisiasa za majukwaani na ukaenda mahakamani ukajitetea kwa kusema nilikuwa natekeleza maelekezo ya Rais!!

Nyie polisi wetu nyie, nawashauri muazime busara za kauli hii kutoka kwa Rais mtaafu wa awamu ya nne ndg Kikwete aliyowahi kuitoa wakati mmoja kuwashauri wafuasi wa vyama vya upinzani waliokuwa wakiandamana mara kwa mara kama njia ya kushinikiza mambo flani flani hata pale ambapo jeshi la polisi liliwakatalia. Kwa mtazamo wake Kikwete ni kuwa aliamini wafuasi hawa walikuwaga wanashinikizwa na viongozi wao kuandamana. Alisemaga...

"....akili za kuambiwa changanya na za kwako......" kabla ya kuchukua uamuzi flani

Polisi wetu akili hizi za kuambiwa changanyeni na za kwenu kabla ya kuchukua maamuzi yoyote ktk hili.

Na zaidi sana tekelezeni majukumu yenu ya ajira zenu kwa mujibu wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo na mliyopewa ya utekelezaji wa majukumu yenu!!

Vinginevyo kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe
 
  1. Ninamshangaa sana Mpemaanavyoshabikia majambazi nayeye nimojawao nn?? Badala ya kuleta haja maendeleo unakomaa na habari zamajambazi siku wakikutembeleautaelewa vizuri umuhimu wa kauli ya raisi.

    ReportEditDelete
    + QuoteReply
1101112131415
 
Hapa naona kila polis wote watapandishwa vyeo maana akiona hajapanda na ana siraha piga raia hpa lamcng raia na wale weny tabia ya udokoz kaz kwao

Mkuu kumbuka Mapolisi si mazuzu wana akili timamu na weledi wa kujua wafanye nini wahache nini - Polisi wa Taifa letu hawana kanuni ya ku "shoot first and ask questions later" - Polisi wa Tanzania hawana hulka ya Ma-polisi wa Kiyankee.
 
Back
Top Bottom