Hili la walimu kuchangishwa michango ya Mbio za Mwenge kwa lazima likomeshwe

Hili la walimu kuchangishwa michango ya Mbio za Mwenge kwa lazima likomeshwe

Matumizi ya amri ya michango yaaanzia mbali hebu tizama barua hiyo hapo na walioshindwa kuchanga awamu ile ya majambazi waliundiwa mizengwe ya kutosha hadi kupewa kesi za uhujumu uchumi.

Eti mtu aandae sherehe ya kutimiza miezi 6 ofisini halafu watu ndio wamchangie.

Kale kajambazi ni haki yake kuendelea kuwepo huko kalipo.
View attachment 2568265
Akae hukohuko miaka 900.
 
Michango ya Mwenge ni changamoto sana kwa watumishi. Halafu hiyo hela yote inayochangwa ni kwa ajili ya kuliwa tu na si kuendeleza miradi.

Kama Serikali itatoa tamko lihusishe nchi nzima kwa sababu ni dhahiri wengi huchangia. Wawaache watumishi wachukue kwa wadau km wapo

Sent from my SM-G977B using JamiiForums mobile app
 
Wewe tanguliza sheria kama hirizi utajua hazina maana wakati zinafika mtakuwa wewe na mmeo/mkeo mmelala njaa na kupata tabu sana
Dharahu wanazofanya hao jamaa kwa wengine na hapa ni kwa watumishi wa umma na kusema sheria zina nguvu madhara yake wakati mwingine ni makubwa sana. Nimerejea alichofanya yule jamaa wa Tunisia kujikoka moto mbele ya ofisi ya serikali,nikarejea ya Hamza wa ubalozi wa Ufaransa pale (sina picha wala video ya tukio lile) ni matokea ya dharahu za kupindukia.

Nikiwa nyumbani Musoma miaka ya 2005 km siyo 2006 mwanzoni.
Kuna jamaa walikuwaga na kawaida ya kuwinda nungunungu mashambani kwa kutumia mbwa.

Sasa siku 1 kuna mzee m1 kwa jina Kawawa akajitoa ufahamu akawapigia yowe ya wizi kisa tu walipita eneo alilokuwa amefunga mbuzi wake.

Km unavyojua mjini habari za yowe,hakuchukua muda jamaa wale wawili wakawa wameuliwa.
Sasa miongoni mwa wana yowe baadhi wakasema mbona hawa jamaa mara nyingi huwa wanawinda nungunungu humu kwenye mashamba ya mihogo,leo wamekuwa wezi?

Basi taarifa zikawa zimefika kwao hao marehemu,ni nje kidogo ya mji.
Ndugu jamaa na marafiki wakaja,wakauliza,hawa vijana leo hii wamekuwa wezi?

Huyo Kawawa kwakuwa mbuzi wake walikuwa karibu na eneo la tukio akasema walikuwa wameiba mbuzi wangu.

Basi,watu wakasema sawa,wakafanya taratibu na kuchukua ile miili na kwenda kuzika.

Miaka mi5 baadaye Dunia nzima ilishuhudia kilichotokea kwa Kawawa mwaka 2011,watu 17 ikiwa ni watu wazima na watoto,mpaka mifugo.
Anayetaka kushuhudia ni kwa nini kuheshimiana ni mhimu aingie mtandaoni ajionee mambo yalivyo kuwa.

Lkn pia nadhani wanao unga mkono dharahu tunazofanyiwa watumishi ni wale ambao wametokea Newcastle families.

Hawajawahi kupita visiwani huko ndanindani na migodini wajionee jinsi ambavyo waliowahi kufanya matukio ya hatari wanavyoishi vyema na mkono wa sheria haujawahi hata kujaribu kuwafikia,na sidhani km utaweza kuwafikia kwa7bu tu ili defender itoke kituoni tu mlalamikaji unatakiwa utoe fedha ya mafuta.

Jamani,TUHESHIMIANE TU,DHARAHU ETI KWAKUWA TU KUNA SHERIA INAFIKIA WAKATI HAZISAIDII NA NDIYO MAANA UTAMUONA KIONGOZI WA SERIKALI AKIWA SAMBAMBA NA VIONGOZI WA DINI KWA JINA WAKIITWA KAMATI YA AMANI.
 
Nondo hajui ajisemacho graduate fresh from shule anaongea ujinga kuhusu watumishi wa umma hasa walimu? Ulishawahi kuwa huko? Embu waachen8 hawa watunq ptia mengi. Nundo hujui unaongea kutolaagazetini.
Sasa wewe hapa umeongea nini?

Wengine mnajifanya mnajua kukosoa kumbe ujinga mtupu.

Nilidhani wewe unayejua vizuri kuhusu walimu na hizo halmashauri ugeweza fafanua vizuri kisha ukaeleza kasoro za hoja ya Nondo hapa ili sisi tusiojua tukuone kama unajua na kwamba sasa huyo Nondo hajui.

Kumbe loo wewe ni matusi tu unayoyajua. Kweli unaweza kuwa umesoma ukabaki na ujinga mwingi. Nondo amekwambia "argue don't shout" bado tu hauelewi halafu unataka humu jf wakuone una akili? Kama una nafasi ya uongozi wewe ni debetupu.
 
Hofu na woga tuu ,Mwalimu wangu alinifundisha yupo Igunga Paul Msabila alipinga unyonyaji wa CWT amekamatwa amewekwa ndani Kwa agizo la Mkurugenzi siku 6 ,akatolewa lakini bado msimamo wake upo palepale akipinga CWT . Hamuwezi kuleta mabadiliko kama wengine kama ww ni waoga hata kuhoji
Huyo mwalimu ndiye anayefaa kuwa mwalimu kweli wa kutuelimishia taifa la leo na la kesho, na si walimu kama huyu Kinoamiguu .
 
Kwa sababu sio mtumishi wa umma ndio maana una Shangaa !!
Ukweli hii inauma sana mwenyewe nimedaiwa hiyo elfu Tano na nikawa Sina japo Kwa Miaka mingi huwa natoa. Cha ajabu nimeitiwa mara mbili ofisi ya kata Kwa ajili ya kutoa maelezo kwanini sijatoa ela ya mwenyee binafsi sijaenda maana kwanza ni mbali na ela Sina ya nauli ya kufika hapo kwenda ni 3000 na kurudi 3000 Kwa usafiri wa pikipiki. Afisa elimu kata amenifuata shuleni siku ya Leo kaniambia unaitwa tena mara ya pili ofisi ya kata saa kumi jioni. Nikiangalia Sina ela Lakini pia muda huo kwangu muda wa kazi ushapita. Nimekasirika sana na kujikuta nikimjibu Kwa hasira kama tatizo ni pesa ya mwenge Mimi siendi popote na kama kutoa pesa ya mwenge ndio ntakuwa mtumishi wa umama basi nifukuzwe kazi ntaenda kufuga kuku na kufanya shughuli nyingine na maisha yataenda tu kuliko kutishiana na kuoneana Kwa jasho lako. Hakika kwa kuwa wote tunafanya kazi ili tupate ela basi kazi zipo nyingi za kufanya katika hili Sina ela na siwezi kwenda kukopa ela kisa mwenge huku familia yangu ikiwa inanitegemea Bora nikope elfu Tano Kwa ajili ya familia na sio mwenge. Pesa yenyewe unatoa mkononi Haina risiti ya mashine unatoa tu Haina mrejesho au taarifa ya mapato na matumizi Lakini pia ningekuwa nayo Kwa wakati waliohitaji ningewapa ila sikuwa nayo na Kwa vile ni hiari ukitaka Kwa nguvu Mimi binafsi sintaitoa kama kazi watanifukuza naamini Kila jambo hutokea Kwa mapenzi ya Mungu na Mungu analijua litakalokupa hata kabla ya kupatwa na tatizo au jambo Fulani . Hivyo nitamshukuru Mungu na kuendelea na shughuli nyingine hakika sintalaumu Wala sintatafuta chama chochote Kwa ajili ya utetezi. Ntakaa kimya na kuendelea na maisha mengine naamini sote pua zimeinama zinaangalia chini na kufa Kila mtu atakufa na malipo Kila mtu ataenda kuyapokea . Kama ni hivyo imani yangu naamini Mungu ndie Kila kitu kuishi kwangu ni Mungu kula kwangu ni Mungu hivyo ntaishi maisha ambayo naamini ndio Mungu aliyonipangia.
 
Back
Top Bottom