Mwana Mtoka Pabaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 15,118
- 16,485
Mwambieni Yanga ni timu ya soka sio siasa. Na wizara ya michezo, haihitaji hasira!Jana waziri Mwakyembe alilazimika kutoka uwanjani ( Jamhuri stadium Dodoma ) kwa hasira kisa YANGA wamepeleka uwanjani kikosi cha pili ili kucheza mechi ya kirafiki na kimbaini ya timu ya vikosi vya ulinzi,ameongea maneno mengi kwa hasira hadi watu wanashangaa na akasahau kuwa yanga inakabiliwa na mashindano makubwa ikiwemo jumapili dhidi ya mbao fc.
Kama alikuwa ana hamu kubwa ya kumuona Kamusoko na Niyonzima, au Tambwe mabao na kijana wetu Msuva, basi ajisikie huru kujongea Kirumba tutakapokuwa tunachana mbao na chain saw