MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,018
- 16,802
1. Timu ya Simba SC tulijiamini kupita Kiasi.
2. Timu ya Simba SC tuliwadharau sana Wapinzani.
3. Timu ya Simba SC ilijiandaa Kupata Mapato Uwanjani na siyo Matokeo mazuri Uwanjani.
4. Timu ya Simba SC imemkaribisha Kiongozi Mmoja wa Serikali ambaye anakiharibu Kikosi.
5. Kocha wa Simba SC hasa Mchezo wa leo atakuwa Kapanga Kikosi kwa Shinikizo.
6. Kocha wa Simba SC hakutakiwa kabisa Kumpanga leo Golini Kipa Aishi Manula kwani bado hakuwa na Utayari wa Kucheza na Kitendo cha kumwacha Benchi Kipa Beno Kakolanya ambaye alishakuwa vizuri na hata Mechi ya awali na hawa UD Songo alidaka Yeye alikuwa tayari katika nafasi nzuri ya Kuwasoma na alishawafahamu tofauti na Aishi Manula ambaye aliitizama UD Songo akiwa Dar es Salaa akiuguza Majeraha yake. Hapa Kosa Kubwa mno la Kiufundi limefanyika na Kocha wa Simba SC anatakiwa atuombe Radhi wana Simba SC wote.
7. Kiongozi aliyeamuru Kuachwa kwa akina Kotei, Okwi na Niyonzima ametugharimu mno kwani Kikosi hakikutakiwa Kubadilishwa vile kutokana na kwamba hata Wachezaji walikuwa tayari wameshazoena vyema. Sijaona Tija ya Simba SC Kuwasajili Wachezaji wa Kibrazili tena ambao wengi wao ni Pancha ( Majeruhi ) na hata Uwezo wao wa Kimpira siyo ule ambao unaweza Kuwashawishi akina siye tuliobahatika kidogo Kucheza mpira hata kama siyo wa Kiwango Kikubwa kama cha Wachezaji wa Ligi Kuu.
Sijaona tatizo na hadi leo najiuliza kama kweli Simba SC ina Mwekezaji Mohammed Dewji ilishindwaje Kumalizana mapema na Wachezaji muhimu kama akina Kotei, Okwi na Niyonzima kisha wakakimbilia Kutusajilia hawa Magalasa Wabrazili? Hivi tukiacha Utani na Unafiki Francis Kahata anamfikia Haruna Niyonzima Kiuwezo? Kama kuna Wachezaji ambao naweza kusema Simba SC imefanya vyema Kuwasajili ni wawili tu Sharaf Shiboub na Deogratius Kanda ila waliobaki wote ni Takataka tupu na hawana uwezo wa Kuichezea Klabu ya Simba.
Kocha Mkuu wa Simba SC nae anaanza Kutuchanganya kwani haingii akilini anamuacha Golikipa Beno Kakolanya ambaye sasa yupo relini ( katika moto / mstari ) anatupangia Aishi Manula ambaye Kiutaalam kabisa Fitness yake haijazidi hata 25% ila Kocha analazimishwa Kumpanga kwa Shinikizo la Kiongozi fulani wa Mkoa ambaye ni Swahiba wake kwa Kusaidiana na baadhi ya Viongozi wa Simba SC bila kujua kuwa huo Upumbavu wao unaigharimu Simba SC na leo umetugharimu kweli.
Najua wana Simba SC wote tumeumia ila kama aliyeumia mno naweza kusema ni Mimi kwakuwa kwa Kuchanganyikiwa na Kutolewa mapema hivi nimekoswakoswa na dhahama moja mahala fulani Jioni hii na Kiukweli hata Usiku wangu wa leo utakuwa ni mkubwa na sijui Kesho nitaficha wapi Sura yangu na hasa ukizingatia kuwa nazungukwa na wana Yanga kwa 98% ya Maisha yangu na Mizunguko yangu.
Viongozi wa Simba SC na Wachezaji wa Simba SC leo mmetuangusha na mmetuumiza mno.
2. Timu ya Simba SC tuliwadharau sana Wapinzani.
3. Timu ya Simba SC ilijiandaa Kupata Mapato Uwanjani na siyo Matokeo mazuri Uwanjani.
4. Timu ya Simba SC imemkaribisha Kiongozi Mmoja wa Serikali ambaye anakiharibu Kikosi.
5. Kocha wa Simba SC hasa Mchezo wa leo atakuwa Kapanga Kikosi kwa Shinikizo.
6. Kocha wa Simba SC hakutakiwa kabisa Kumpanga leo Golini Kipa Aishi Manula kwani bado hakuwa na Utayari wa Kucheza na Kitendo cha kumwacha Benchi Kipa Beno Kakolanya ambaye alishakuwa vizuri na hata Mechi ya awali na hawa UD Songo alidaka Yeye alikuwa tayari katika nafasi nzuri ya Kuwasoma na alishawafahamu tofauti na Aishi Manula ambaye aliitizama UD Songo akiwa Dar es Salaa akiuguza Majeraha yake. Hapa Kosa Kubwa mno la Kiufundi limefanyika na Kocha wa Simba SC anatakiwa atuombe Radhi wana Simba SC wote.
7. Kiongozi aliyeamuru Kuachwa kwa akina Kotei, Okwi na Niyonzima ametugharimu mno kwani Kikosi hakikutakiwa Kubadilishwa vile kutokana na kwamba hata Wachezaji walikuwa tayari wameshazoena vyema. Sijaona Tija ya Simba SC Kuwasajili Wachezaji wa Kibrazili tena ambao wengi wao ni Pancha ( Majeruhi ) na hata Uwezo wao wa Kimpira siyo ule ambao unaweza Kuwashawishi akina siye tuliobahatika kidogo Kucheza mpira hata kama siyo wa Kiwango Kikubwa kama cha Wachezaji wa Ligi Kuu.
Sijaona tatizo na hadi leo najiuliza kama kweli Simba SC ina Mwekezaji Mohammed Dewji ilishindwaje Kumalizana mapema na Wachezaji muhimu kama akina Kotei, Okwi na Niyonzima kisha wakakimbilia Kutusajilia hawa Magalasa Wabrazili? Hivi tukiacha Utani na Unafiki Francis Kahata anamfikia Haruna Niyonzima Kiuwezo? Kama kuna Wachezaji ambao naweza kusema Simba SC imefanya vyema Kuwasajili ni wawili tu Sharaf Shiboub na Deogratius Kanda ila waliobaki wote ni Takataka tupu na hawana uwezo wa Kuichezea Klabu ya Simba.
Kocha Mkuu wa Simba SC nae anaanza Kutuchanganya kwani haingii akilini anamuacha Golikipa Beno Kakolanya ambaye sasa yupo relini ( katika moto / mstari ) anatupangia Aishi Manula ambaye Kiutaalam kabisa Fitness yake haijazidi hata 25% ila Kocha analazimishwa Kumpanga kwa Shinikizo la Kiongozi fulani wa Mkoa ambaye ni Swahiba wake kwa Kusaidiana na baadhi ya Viongozi wa Simba SC bila kujua kuwa huo Upumbavu wao unaigharimu Simba SC na leo umetugharimu kweli.
Najua wana Simba SC wote tumeumia ila kama aliyeumia mno naweza kusema ni Mimi kwakuwa kwa Kuchanganyikiwa na Kutolewa mapema hivi nimekoswakoswa na dhahama moja mahala fulani Jioni hii na Kiukweli hata Usiku wangu wa leo utakuwa ni mkubwa na sijui Kesho nitaficha wapi Sura yangu na hasa ukizingatia kuwa nazungukwa na wana Yanga kwa 98% ya Maisha yangu na Mizunguko yangu.
Viongozi wa Simba SC na Wachezaji wa Simba SC leo mmetuangusha na mmetuumiza mno.