Hili neno "Umehonga" linawapa msongo wa mawazo wanaume. Tafadhali tusilitumie kwa wanaume wetu

Hili neno "Umehonga" linawapa msongo wa mawazo wanaume. Tafadhali tusilitumie kwa wanaume wetu

Asante kwa kututetea. Ni mara chache sana kukuta mwanamke anamtetea mwanaume, haswa katika mambo yanayohusiana watu wawili kati ya mke na mume.
 
Wanawake tuliowengi kwa sasa tunaendeshwa na hisia tu badala ya uhalisia

Kwa sasa tunaamini na kuhisi kwamba iwapo mmeo hakupi pesa ya matumizi ya kutosha au akakwambia hana pesa kwa muda huo basi neno litakalotamkwa na mke wake au mpenzi wake ni kuwa amehonga pesa wanawake na kumnyima mkeo au mpenzi.

Hata Kama mwanaume anafanya saving kwa ajili ya kununua kitu fulani au kujenga na mwanamke atataka ajue huwa anasave Wapi na huwa anasave kiasi gani na asipoona hiyo saving basi neno kuhonga hutamalaki katika ndoa hiyo au mahusiano hayo

kuna mwanaume alimwambia mke wake kuwa pesa aliyokuwa nayo amemtumia mama yake kiasi cha laki 4,lakini mwanamke hakuamini na kupiga sim kwa mama mkwe kuuliza Kama baba D amemtumia pesa na ni kiasi gani?

Nashauri wanawake wenzangu tusiwape wanaume wetu msongo wa mawazo kwa kuwatuhumu kuwa wanahonga ,sikatai kuwa hawahongi ila wapo wanaohonga serious ila wengine wanahonga pesa za ziada extra money

Tuepuke kuhonga,kila kitu Umehonga,akiteteleka jambo fulani amehonga,akisusua kulipa kodi ya nyumba au ada ya shule amehonga

Tusiamini katika kuhonga ili wanaume wasiwe na msongo wa mawazo
Kwakwer nikijumlisha magumu nayokutana nayo kutwa nzima pesa ngumu alafu unakuta mwanamke anakwambia pesa unahonga aloooo hua ubongo unakua pyruuuuuuu
 
Back
Top Bottom