Hili tukio limenifanya nisimuamini mwanaume yoyote

Hili tukio limenifanya nisimuamini mwanaume yoyote

Nilishapiga marufuku watoto kupanda bodaboda. Bora ukose hela ya Ada ila usithubutu kuwaacha watoto wako wa kike au wa kiume kupelekwa shule na bodaboda au Bajaj. Utakuja kunishukuru.
Siku hizi dunia imeharibika sana aisee, hata hawa ma house girl ma house boy kama unae au mtoto wa kiume mkubwa ukimuacha na wadogo zake kuwa makini ikiwezekana kama kipato kinaruhusu funga CCTV camera uwe unaangalia matukio yanayoendelea usipokuwepo
 
Hili tukio lilitokea miaka mingi iliyopita, kipindi nasoma nakumbuka kati ya form 1 au form 2.

Nitafupisha ili nisiwachoshe, baba angu alituambia kuwa kuna mwanamke alimpa mimba miaka hiyo wakaachana mwanamke akaolewa na mwanaume mwingine sasa yule mtoto alivyokuwa akaambiwa baba yake ni mzee wetu, akaanza kumtafuta, hatimaye akampata.

Huyu mtoto mwenyewe alikuwa tayari mtu mzima ana mke wake na watoto alikuwa kama ana miaka 30 hivi kipindi hicho, alivyotambulishwa kwetu kuwa ni kaka yetu, basi tukaanza undugu rasmi na huyu kaka yetu tukawa tunamtembelea nyumbani kwake. Haswa haswa mimi nilikuwa nikitoka shule napitia mara nyingi kwa kaka nakula napewa nauli na mkewe au hata yeye akiwepo naondoka nyumbani na hapo nyumbani kwake ilikuwa ni jirani na rafiki yangu niliyekuwa nasoma nae.

Nakumbuka siku moja baba aliniambia nikachukue hela ya mahitaji ya shule alimwambia huyu kaka yetu anipe kwahiyo nikawa nimeenda, kipindi hiki wifi yaani mke wa kaka alikuwa kaenda kujifungua kwao, sasa nikapita kwa best angu then nikaenda kwa kaka nikamkuta mwenyewe nikakaa nakumbuka alininunulia chakula.

Nikala akawa ametoka na mimi nikaenda kwa rafiki angu nikakaa kaa kidogo nikarudi nikawa nimemkuta ndani akaniambia niingie chumbani, kwake sasa mimi nikawa simuelewi maana alikuwa kabadilika macho yamekuwa mekundu alafu akawa ananiita nisogee karibu yake, hata sauti akawa anaongea sauti ya chini, katika kumsikiliza vizuri, akaniambia "nipe kidogo"

Aisee hapo akili iliruka kengele ya hatari ikagonga kichwani kwangu, nikamuuliza kaka umesemaje akarudia tena "anaomba kidogo" nilishtuka sana sikutarajia kauli na kitendo kama hicho kutoka kwa mtu niliyetambulishwa na baba kuwa ni kaka kwetu.

Niliondoka na tangu hiyo siku sijawahi kumtembelea tena mpaka kufika sasa hatuna mawasiliano, sikumwambia mtu yoyote hili tukio maana ni aibu, kaka anataka kunibaka, tukio la ajabu mno.

Mwanaume hata akiwa ndugu yangu, mume wangu au wherever siwezi kumuamini kumuachia mtoto wangu wa kike huu ndiyo msimamo wangu baada ya hili tukio, ama ninakosea wadau??
This food is too much pilipuli
 
Siku hizi dunia imeharibika sana aisee, hata hawa ma house girl ma house boy kama unae au mtoto wa kiume mkubwa ukimuacha na wadogo zake kuwa makini ikiwezekana kama kipato kinaruhusu funga CCTV camera uwe unaangalia matukio yanayoendelea usipokuwepo
Nishafunga zile za bulb
 
😁😁😁yaani kuhusu bangi sijui kama alivuta labda hisia zilizidi ndiyo zikampelekea hivyo, angekula ningemlaani kwanza nadhani hata yeye alikuwa na uoga maana angekuwa kadhamiria sana angenikamata kwa nguvu, tokea hilo tukio litokee hatujawahi kukutana mimi nilikata mguu hadi hii leo kwanza namuona kama siyo ndugu yetu maana hata hafanani na sisi wala mzee ndiyo maana sitaki shobo nae zaidi, kuhusu uzuri nipo kawaida tu, sina huo uzuri wa kutisha
Njoo nikuone kama huna uzuri wa kutosha Binti sayuni!
 
Back
Top Bottom