Historia fupi ya maisha ya Spika Ndugai aliyoitoa bungeni. Asema alikuwa na maisha ya shida na dhiki

Historia fupi ya maisha ya Spika Ndugai aliyoitoa bungeni. Asema alikuwa na maisha ya shida na dhiki

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,420
Reaction score
18,298
Spika Ndugai amesema haya,

Katika maisha yangu sikuwahi kuwaza wala kuota kama nitakuwa Mwanasiasa, Mbunge na hata Spika ni Mungu tu ambaye katika uumbaji wake hutujua na kutupangia safari kadri anavyoona ni vyema, asanteni sana wana Kongwa, chama changu na Rais

Nakumbuka miaka niliyosoma Shule ya Msingi nilikuwa natembea Km 16 kwa siku 1, nimekulia maisha ya shida na dhiki, nikiwa mdogo nililala kwenye kitanda cha kamba na nyumba ya tembe, lakini baadaye nimesoma vyuo mbalimbali ndani na hata nje ya nchi

Nilipokuwa chuo cha MWEKA Moshi, nilikuwa mmoja wa Wanafunzi maskini sana, baadhi ya likizo sikuwa na nauli za kurudi Kongwa, nakumbuka jinsi ambavyo wenzangu walivyokuwa wakipanda magari kuondoka mimi nilikuwa najificha kwa aibu ya kuulizwa huna kwenu?

Mimi nyumbani nilikuwa mtoto wa pekee wa Mama yangu, tunapomaliza Bunge hili natamani ni-revenge sasa nirudi akanipokee, lakini bahati mbaya Mungu alishamchukua, kwahiyo wakati mwingine mnisamehe huwa napata hasira ninapokutana na mtu mjinga

Leo nimekuja na rafiki yangu, Mama umenivumilia sana, hata nilipokuwa ICU India alikuwa analala pembeni yangu masaa 24 amekaa kwenye kiti, amekuwa Daktari wangu muda wote, hakika wewe ni mke mwema, kwa kukopa maneno ya Dk Mpango, Asante sana kwa kunipa raha.


Ndugai.jpg
 
Ok Tumekuelewa.....ok tumekuelewa....

Mh.Mbowe ni kijana wa mjini mstaarabu sababu hizi hela mnazogawa gawa hovyo yeye kaziona akiwa form one, na haya ma Landcruiser yenu yeye kaishi nayo toka akiwa O'level anayasukuma!! sasa unaposema kwamba eti leo kuelewa chakali...hajitambui...unatia huruma sana mbunge...!! Hata kama ni pombe hatukatai kazijua leo Dodoma?

Ok, laah ila pole sana mbunge...ni familly Background problem....wewe ni kama mimi nilikuwa nafua nguo za wenzangu ili ka sabuni kabakie nifue za kwangu enzi za Olevel . nafikiri tutunge sheria kuthibiti hii hali..I mean famill background ni matatizo mengine ya nchi hii...

Unapata kiongozi ambaye hata hajui kujichanganya na viongozi wenzake....hasara kwa taifa...tena kubwa mno
 
Ok Tumekuelewa.....ok tumekuelewa....

Mh.Mbowe ni kijana wa mjini mstaarabu sababu hizi hela mnazogawa gawa hovyo yeye kaziona akiwa form one, na haya ma Landcruiser yenu yeye kaishi nayo toka akiwa O'level anayasukuma!! sasa unaposema mwamba eti leo kuelewa chakali....unatia huruma sana mbunge...!!

Ok, laah ila pole sana mbunge...ni familly Background problem....wewe ni kama mimi nilikuwa nafua nguo za wenzangu ili ka sabuni kabakie nifue za kwangu enzi za Olevel . nafikiri tutunge sheria kuthibiti hii hali..I mean famill background ni matatizo mengine ya nchi hii...

Unapata kiongozi ambaye hata hajui kujichanganya na viongozi wenzake....hasara kwa taifa...tena kubwa mno

Mkuu acha kumshusha hivyo Mbowe. Vitu hivyo kazaliwa navyo kwao
 
Aliishafanya ukamanda sasa makamanda wengine wa nini tena?
... NCHI HII!!!?
🤮🤮🤮🤮🤮🤬
 
Mpigaji ndiye mjinga
Hapendi watu wajinga lakini yeye ni mjinga.
Kwa hiyo huyu alimchapa gongo la kichwa kidogo afe kwa sababu ni mjinga? Kwa nini sasa Magufuli akamteua u DC MTU huyu mjinga. Hapo sasa finally nani ndio mjinga?

Mpigaji, mpigwaji au mteuzi?

 
Hapendi watu wajinga lakini yeye ni mjinga. Kwa hiyo huyu alimchapa gongo la kichwa kidogo afe kwa sababu ni mjinga? Kwa nini sasa Magufuli akamteua u DC MTU huyu mjinga. Hapo sasa finally nani ndio mjinga?

Mpigaji, mpigwaji au mteuzi?

Hivi huyo ni DC wa wilaya gani mkuu nahitaji nikafanye naye interview
 
Back
Top Bottom