Historia imeandikwa Rais Samia Mwenyekiti wa Kwanza mwanamke ndani ya Chama cha Mapinduzi

Historia imeandikwa Rais Samia Mwenyekiti wa Kwanza mwanamke ndani ya Chama cha Mapinduzi

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Jumatano anaweka rekodi ya kipekee katika historia ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa wajumbe wa Mkutano mkuu wa 10 kumchagua kuwa Mwenyekiti wa kwanza mwanamke wa chama hicho tawala. Tangu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiasisiwe mwaka 1977, hakijawahi kuongozwa na mwanamke, bali Rais Dk. Samia Suluhu ambaye anachaguliwa leo katika Mkutano Mkuu wa 10 wa chama hicho.

Aidha alielezea juu ya utekelezaji wa ilani wa chama hicho kwa kipindi kifupi cha uongozi Rais Samia anasema
"Wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2020 CCM iliahidi kuwa iwapo Watanzania watakichagua kazi ya serikali itakuwa ni kutekeleza ahadi zilizoainishwa ktk Ilani hiyo na kwa kweli kazi ya utekelezaji wa Ilani inaendelea kwa kasi kubwa"

Kuhusiana na uchaguzi unaofanywa na chama siku hiyo Rais Samia Suluhu anasema wajumbe wote waliochaguliwa kugombania ni washindi hata kwani waliaminiwa na chama kugombea nafasi hizo.

"Wote walioteuliwa kugombea nafasi walizoomba ni washindi, kwa sababu chama kimewaamini kuwa yoyote ambaye angechaguliwa ni mwanachama thabiti, na ambaye anaweza kuongeza nguvu yake katika kukijenga chama"

"Uchaguzi tutakaofanya hapa ni kielelezo muhimu sio tu cha ukomavu wa Demokrasia bali pia haki, usawa, amani na maendeleo, mambo ambayo ndio nguzo na itikadi za siasa zetu"- Dkt Samia Suluhu.

1670415580866.png
 
Kina shafi na shilole wamepenyA

Shilole jmn hana elimu yoyote nae anataka kuwa mjumbe duh bora hata shafi ana diploma yake ifm

Shilole shule aliendekeza mapenzi leo anatka kuwa mjumbe
 
Shilole shafii vunja bei manara vp nao wamepita ..? Bora apite shafii dauda hao wengine wote mmmh hamna kitu kwakweli bure kabsa machawa
 
Toka Tanzania ipate uhuru chama cha mapinduzi hakikuwai kuongozwa na mwanamke lakini sasa historia imeandikwa baada ya Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuchanguliwa kuwa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi 2022 mpaka 2027 kwa kura za ndio 1914 kati ya kura 1915 na kura 1 imesema hapana.
 
Wameanza kukiri wenyewe bila shuruti kuwa nchi inaongozwa na mbumbumbu
 
Back
Top Bottom