Historia ya Kiwanda cha Tanganyika packers mpaka kuja kuwa Kanisa la maombi

Ukitaka kazi yako iharibike mpe mbongo. Hata kitu kiwe bora vipi ataharibu tu.

SGR na miradi yote mikubwa tukiwapa wabongo waendeshe itakufa in no time.
 
Hii hoja ya kizuzu sana. Mtu ameleta hoja kuntu wewe unaleta uchawa. CHADEMA wanahusikaje na kiwanda wakati msimamzizi wa Sera za Maendeleo na Uwekezaji ni Serikali ya CCM.

Hii nchi imezaliza wajinga wengi sana.
Ndio think tank ya CCM huyo!
 
Akaja mungu wa chato akamleta progagabdist mwijaje atuambie cherehan ni kiwanda
 
And the whole world operates that way in running businesses!
 
Kuna sehemu Njombe panaitwa olofea, mtu mmoja akaniambia ni All Affairs ilikuwa ni kwaajili ya recreation ya wazungu baada ya kazi
nadhani ni Welfare centre zamani zilikuwepo kama recreation centres with some education programmes ...health, artistic skills
 
Pamoja na maelezo yako yooote!! Dakika za jioooooni nimegundua una chuki binafsi na mwamposa !! Uchungu wako sio kiwanda kufa ni kanisa kuwekwa pale !! Kwa taarifa fupi viwanda vilivyokufa Tanzania vinaweza kufika hata 500! Vyote ni magofu ikiwemo zzk mbeya !! Jambo la pili mwamposa pale ni mpangaji analipa Kodi ya pango isiyopungua milioni 5 Kila wiki !! Hajapewa Bure !! Habari ya mafuta na udongo havihusiani na mada yako !! Hizo ni chuki kwa kanisa la mwamposa na sio kwa serikali iliyoruhusu kiwanda kife kizembe !! Hata kama wasingemkodishia mwamposa Bado kiwanda kisingerudi mjinga mkubwa wewe !
 
(Liebig’s Extract of Meat Corporation) l
Mazungumzo yaanze waitwe, Tukae meza moja, tuone tu nafanyaje!,
°mwekezaji aje na program za kuprocess,
-ngozi
-Kwato
-pembe
-chakula cha mifugo (kuku), kwa damu za ngombe!
-vyakula vya mbwa na paka!
Too late,walifungua kiwanda nchi nyingine.Bado wana usongo wa kunyanganywa mtambo wao.
Kibaya zaidi yule mhindi aliyepewa kiwanda aendeshe alifungua mitambo yote akaiuza uhindini yakabakiza magofu.
 

Hahaa,
 
Ukitaka kazi yako iharibike mpe mbongo. Hata kitu kiwe bora vipi ataharibu tu.

SGR na miradi yote mikubwa tukiwapa wabongo waendeshe itakufa in no time.
Sio wabongo serikali sasa mtu mwanasiasa na yeye anataka awe fundi huo mchanganyo wa hapo ni tafrani
 
Wewe unadhani mafuta ya kuendesha train pamoja na posho kutoka Dar hadi Dodoma na ile convoy ya Rais eti kuzindua train ya SGR italipwaje na TRC? Kulishindikana nini mh Rais kuzindua huko Dar akaendelea na kazi yake then wenye kusafiri wakate tiketi kama abiria wa kila siku?
Utakuta mtu ni kiongozi wa serikali anaona sifa kupita njia ya mwendokasi ili awahi kazini ila wazalishaji wakubwa wao waendelee na foleni...wapo humu jamvini wanalalamika.
Mkuu wa Mkoa anajengewa nyumba private na taasisi wao wanachojali nyumba yake iishe ila taasisi washindwe kutoa huduma bora kwa jamii haiwahusu.
Katibu mkuu na waziri anapewa kiwanja bure na taasisi yeye anakenua bila kujua taasisi haitafikisha malengo yaliyokusudiwa.
Viongozi achaneni ubinafsi ili kutumikia wananchi; wakuu wa taasisi acahaneni kukipendekeza ili muendelee kuteuliwa kubaki hapo mlipo.
 
Kuna washauri wake ni washwawashwa hawawezi kutulia sehemu moja
 
Nimezikumbuka zile nyama hakika zilikuwa na viwango vya kimataifa!

CCM wameua viwanda na hata wahitimu hawapati ajira wamegeukia kamari, uchawa na ngono.
 
Ndiyo.

Kwa sababu tumeshakwama.
Kama tumeshakwama, acha tuishie hapo. Hatuwezi kutafuta mwekezaji bali mwekezaji ndiye anayekuja mwenyewe. Serikali ikimtafuta mwekezaji, basi inabidi imlipe mwekezaji huyo.
 
Mada nzuri ila sijaona umuhimu wa kumchomeka Mwamposa!!
 
Sio wabongo serikali sasa mtu mwanasiasa na yeye anataka awe fundi huo mchanganyo wa hapo ni tafrani

Wabongo wote sio serikali tu. Hao serikali wanaonekana sababu wapo kwenye spotlight ila hata kwenye private sector wabongo wanazingua sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…