Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Kwanza nianze kwa kukusifu,unajitahidi sana kufanya majadiliano bila kutoa maneno machafu wala kuonesha hasira,hongera sana kwa hilo,sasa turudi kwenye mada,nitajibu kwa mpangilio uliouandika:

A.kuhusu utafiti wa mahakama,je unafikiri ufaransa ni nchi sahihi kufanya uchunguzi huo hasa ukizingatia kuwa nae ana mkono kwenye mauaji ya kimbari kwani alikuwa akiiunga mkono waziwazi serikali ya rwanda ya wakati huo hata akafikia hadi kupeleka jeshi lake kupigana na RPF?Je,uchunguzi huo ulikuwa huru,namaanisha ulihusisha pia kuhoji upande wa viongozi wa rpf wa wakati huo including Paul Kagame?Je,utafiti huo ulihusisha wataalamu wa ndege na makombora?Je,utafiti huo ulifanyikia Rwanda ambapo ndio sehemu ndege ilipotunguliwa au ulifanyikia ufaransa?
Lakini hata hivyo mwaka 2012 ulifanyika uchunguzi uliowahusisha wataalamu waliopewa jukumu na mfaransa huyohuyo huku ukiwajumlisha wataalamu wawili wa mabomu,wataalamu wawili wa ajali za ndege,rubani moja,masoloveya wawili na mtaalamu moja wa sauti.Matokeo ya uchunguzi wa kitaalamu yalihitimisha kuwa ndege ililipuliwa kutoka kanombe millitary base ambayo kwa kipindi hicho ilikuwa inakaliwa na wanajeshi wa serikali ya rwanda ya wakati huo na majeshi ya ufaransa na isingekuwa rahisi kwa wanajeshi wa rpf kujipenyeza kwenye base hiyo.Sasa ni kwanini imekuwa rahisi kwako kuchagua uchunguzi moja na kuutupa mwingine?

Source: 'Kagame hakudungua ndege' - Ripoti

B.Hapa umekwenda nje ya mjadala,mjadala ni mauaji ya kimbari rwanda.

1.Narudia tena,tafiti zote nilizofanya kwenye vyanzo huru,hakuna sehemu nimeona RPF walitumia mapanga,rpf walikuwa na silaha za moto,walikuwa frontline kupambana na jeshi la rwanda,nakuhakikishia mkuu,rpf wangeshika mapanga na kuanza kuhangaika na raia wasio na hatia wasingeshinda hii vita,tunaweza kuwasema rpf kwa maneno yoyote mabaya tunayotaka lakini mwisho wa siku rpf lilikuwa ni jeshi lenye displine ya hali ya juu sana,na wangefanya vitu vya namna hiyo wasingepata uungwaji mkono wa kimataifa,moja kati ya vitu vilivyofanya serikali ya rwanda ya wakati huo kushindwa vita ni kujihusisha na mauaji ya raia wasio na hatia na wakashindwa kuelekeza nguvu zao kupambana na jeshi lenye silaha.Hiyo unayoiita confession ya mwanajeshi wa rpf nimejaribu sana kuitafuta lkn hakuna sehemu yoyote nimeona kama ushahidi huo ulitolewa ICTR,nilichoambulia ni kuwa "unadaiwa kuwa ni ushahidi" lkn haukufikishwa ictr na kama ulifikishwa naomba unisaidie source kutoka kwenye vyanzo huru na pia mwisho wa siku nisaidie kama ushahidi ulikuja kuthibitishwa na mahakama kama ni kweli au ulibaki kuwa ni allegation?

2.Tukikubaliana na huo uchunguzi wa davenport na miller kutakuwa hakuna maana ya majadiliano tunayoyafanya humu,wao wamekataa kabisa uwepo wa genocide rwanda lakini tukumbuke tafiti zote za kitaalamu za mauaji ya Rwanda zikiwemo zilizofanywa na na wataalamu wa UN zili-conclude kuwa kulikuwa na genocide Rwanda.
Nahisi umenisaidia maana kwa kuandika kama umecopy kitu nilichokuwa natathmini jinsi ya kumuelimisha Kuhusu hizo riport zake!!! RPF aiongelee kwa mengine sio kwa Genocide anayosema!
 
1.Nimesoma hiyo link uliyoweka unayodai imesema watutsi walikuwa laki 7 na nimeirudia kama mara tatu lakini sijaona kitu cha namna hiyo,naku-challenge mkuu naomba uainishe hiyo sentensi inayosema namna hiyo pia uambatanishe na hiyo source.

Pia baada ya mauaji ya kimbari na serikali kuwa chini ya RPF,hakujawahi kufanyika tena sensa inayoonesha idadi ya makabila Rwanda,kipengele kinachoonesha idadi ya makabila kilitolewa kama sehemu ya jitihada za serikali kuutokomeza ukabila Rwanda,hicho ulichoweka angalau ungesema ni projection labda ungeeleweka,na kama unajiamini kwenye hili tupatie source kutoka kwa serikali ya rwanda kwasababu sensa yenyewe ya 2014 ilifanywa na serikali ya Rwanda,wikipedia sio credible source.

2.Usipuuzie sababu zilizowafanya RPF wakashika silaha na kuingia vitani,RPF walikuwa na sababu za msingi sana,ukizieweka pembeni utakuwa unaunga mkono Ideology ya "0 network" yaani ni wahutu tu ndio wenye haki ya kuwepo Rwanda.

3.Hakujawahi kuwa na double genocide Rwanda,isingekuwa rahisi kwa RPF kufanya genocide rwanda kama unavofikiri,hili iitwe genocide ni lazima kwanza iwe prepared,rpf walikuwa mstari wa mbele vitani wanapigana, wanateka maeneo wanasonga mbele,isingekuwa rahisi kwao kupata details za nani hasa ni mtusi na nani ni mhutu na anapatikana wapi,wahutu wenye msimamo mkali walianza kuiandaa genocide tangu 1990,haikuwa kazi ya siku moja au mwezi,walikuwa na details zote za aliyetakiwa kuuawa awe mtusi au mhutu mwenye msimamo wa kati,waliandaa jeshi na kulipa mafunzo kwa shughuli hiyo na kupenyeza propaganda ya kutosha kwa raia wa kawaida washiriki hivyo vitu,kulipuliwa kwa ndege ilikuwa ni kichocheo cha kuhalalisha mauaji lkn hata hiyo ingeshindikana ingetafutwa sababu nyingine,Gen. Dellaire aliitahadharisha UN kuwa kutakuwa na mauaji ya watusi miezi mitatu kabla ya ndege kulipuliwa,na Bagosora aliwahi kumwambia Dellaire matatizo ya rwanda hayawezi kuisha ni mpaka watusi watapofutika rwanda kwa hiyo haya mauaji yalipangwa na tena yalipangwa kwa muda mrefu.

Mimi nilipenda iitwe Rwandan genocide hili angalau hata wahutu ambao hawakushiriki huo unyama wasijisikie wana hatia ila kwa maneno uliyoandika ndo naanza kuona kwanini imepitishwa kuwa Tutsi Genoscide,kuna hatari kubwa sana ya historia kupotoshwa,kumbe kuna umuhimu wa kuukabili ukweli ila yote kwa yote mkuu mtu awe mtusi au muhutu anabaki kuwa kama binadamu wengine,wote wanayo haki ya kuishi,hakuna aliye bora zaidi ya mwingine,hakuna anayestahili kuishi zaidi ya mwingine,mgogoro wa watusi na wahutu rwanda na burundi ni matokeo mabaya ya ukoloni,kabla ya ukoloni watusi na wahutu waliishi bila kuchinjana kwa karibu/zaidi ya miaka 100,ila iliwachukua ubelgiji miaka michache tu kuipasua Rwanda na burundi vipande vpande.
Asante sana mkuu TWOB shule uliyosoma inahitaji pongezi! Facts zako ziko extraordinary!! Kama Kuna watanzania Wengine kama wewe nadhani muungane Kuna kitu mnaweza kusaidia katika jamii
 
Historia ya Kweli ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

031795b45fd5c0fbde56b9e68eea2404.jpg


KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA

SEHEMU YA KWANZA

“..kama unasoma ujumbe huu, muda huu… uko mpweke! Pengine ushahidi pekee uliobakia ni kijipande hiki cha maandishi. Sijui kama kuna yeyote kati yetu aliyesalimika kufika kizazi chenu mwaka huu mtakaosoma andishi langu. Sijui hata kama tumeshinda au tumeshindwa vita tunayopigana sasa hivi. Sijui, lakini naamini mwaka huu mliopo nyinyi sasa mwaweza kuwa na jibu sahihi. Vyovyote vile lakini jambo lililo dhahiri ni kwamba hakuna yeyote wa kizazi chetu mliye naye sasa hivi kwenye miaka yenu muusomapo ujumbe huu. Kwa hiyo wacha niwaeleze sisi tulikuwa akina nani, na kwa namna gani tulipambana mpaka tone la mwisho la damu mwilini mwetu ili kutetea kizazi chetu kisifutwe juu ya uso wa dunia. Wacha niwaeleze namna ambavyo japo tulikamuliwa damu mpaka kutiririka kufanya mifereji lakini lakini tulisimama kutetea kizazi chenu na ninyi watoto wetu. Wacha niwaeleze kisa kilichotikisa ulimwengu. Wacha niwaeleze kuhusu mifereji ya damu kwenda Ethiopia.!”

– Habib Anga alias The Bold

March 21, 1994 maeneo ya Uganda ambayo yanapakana na Rwanda, katika ziwa viktoria serikali ilituma vikosi vya jeshi kudhibiti eneo hilo kwa hali ya dharura. Agizo hili la serikali kutuma jeshi halikuwa kwa ajili ya kidhibiti eneo hilo kutoka kwa adui bali agizo lilikuwa ni kudhibiti eneo hilo dhidi ya maiti, maiti za binadamu. Sio maiti mbili au tatu, si mamia bali maelfu ya maiti za binadamu ambazo zilikuwa zinaingia ziwani Victoria zikiletwa na maji ya mto Kagera.

Maiti hizi zilikuwa nyingi kwa maelfu kiasi kwamba mapaka zilikuwa zinafanya maji yatoe harufu. Serikali ya Uganda ilituma jeshi eneo hili ili kudhibiti eneo hili maji yake yasitumiwe na wananchi kwa matumizi ya nyumbani au shughuli za uvuvi. Lakini jeshi lilikuwa eneo hili ili kuhakikisha kuwa taharuki iliyozuka baada ya maelfu ya miili hii kuonekana haigeuki na kuvuruga amanai katika eneo hili. Lakini pia jeshi lilikuwa hapa ili kubaini miili hii ilikuwa inatoka wapi.

Kadiri ambavyo jeshi la Uganda lilivyokuwa linafuatilia kwa kurudi nyuma kufuata mto Kagera ndivyo ambavyo walizidi kubaini kwamba maiti hizo zinaletwa na maji kutoka tawi la mto Kagera lililopita kusini mwa Rwanda. Na kadiri ambavyo walizidi kufuata chanzo cha maiti hizo zinakotoka ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia Rwanda na maji ya mto rangi yake kuwa nyekundu zaidi.

Wanajeshi wa Uganda ambao walishiriki kwenye ukaguzi huu wa mto huu wanakiri kwamba licha ya baadhi yao kupigana mstari wa mbele kwenye vita mbali mbali lakini hakuna yeyote kati yao ambaye aliwahi kushuhudia ukatili mkubwa wa kiasi hiki.

Siku hii jeshi la Uganda linakisia kwamba waliokota si chini ya miili elfu kumi ya binadamu na yote ilionekana kuletwa na maji ya mto Kagera kutoka nchini Rwanda.
Ajabu ni kwamba miili yote hii ilikiwa inamfanano fulani. Maiti zote zilikuwa za watu warefu, wembamba, wenye nyuso ndefu na pua za kuchongoka. Haikuhitaji kufikiria sana kufahamu kuwa maiti hizi zilikuwa za watu wa kabila la Tusi (Tutsi).

Miezi kadhaa baadae ndipo ambapo jeshi la Uganda na ulimwengu wote walikuja kuelewa kwa nini maiti zilikuwa zinatupwa mto Kagera. Ni ujumbe gani ambao ulikuwa unajaribu kutumwa.

Kwamba Watusi nchini Rwanda walikuwa waapenda kujisifu kuwa mababu zao wana asili ya nchi ya Ethiopia. Kitendo hiki cha watesi wao kuwatupa mtoni, walikuwa wanawaua na wakiwa wanatupa maiti zao mto wanawaambia kwamba “wanawasafirisha warudi kwao Ethiopia ambako wamekuwa wakijisifu ndio asili yao.”

Sio kwamba jeshi la Uganda hawakuwa na taarifa juu ya hali tete iliyopo Rwanda kwa muda wa karibia wiki nzima iliyopita bali hawakujua kama hali hiyo tete ilikuwa ni ya kinyama kiasi hicho.

Wanajeshi hawa wa Uganda walikuwa wameshikwa na bumbuwazi na vihoro vilivyo wapasua mioyo kwa kuona miili hii elfu kumi ya binadamu isiyo na uhai. Kitu ambacho walikuwa hawakijua na hakuna ambaye alidhahania ni kwamba ndani ya siku mia moja zijazo ulimwengu ulikuwa unaenda kushuhudia moja ya tukio la kikatili zaidi tangu kuubwa kwa ulimwengu. Karibia maiti za binadamu milioni moja zikiwa zimetapakaa mitaani nchini Rwanda iking’ong’wa na nzi na kuliwa na mbwa.


b27e3a3a6fd670dbc0a4e300cbcc558f.jpg





GENESIS

Rwanda: Kabla ya Ukoloni

Asili rasmi kabisa ya watu wa kwanza kuishi katika eneo ambalo leo tubalitambua kama nchi ya Rwanda ni watu wa kabila la ‘Twa’ (Watwa). Kabila hili la wawindaji si la kibantu bali ni sehemu ya makabila yanayotambulika na wanahistoria kama ‘pygmy’ ambao sifa yao kuu ni ufupi. Mtu mzima anayetoka makabila ya namna hii anakadirwa kuwa na wastani wa urefu chini ya sentimita 150. Watwa waliishi Rwanda enzi za kale sana miaka ya 8000 BC na 3000 BC.

Kuanzia miaka ya 700 BC mpaka 1500 AD makabila ya Kibantu kutoka maeneo ya jirani yalianza kuhamia eneo hili.

Kuna nadharia mbali mbali kuhusu ni namna gani haswa makabila haya ya kibantu yalihamia hapa na baadae kupelekea kutokea Makabila ya sasa ya Wahutu na Watusi.

Nadharia ya kwanza inadai kwamba; Wahutu ndio walikuwa wa kwanza kuhamia eneo hili na kuanzisha shughuli za kilimo. Baadae watu wenye asili ya Ukushi (Watusi wa sasa) nao wakahamia kwenye eneo hili na kulitawala.

Nadharia ya Pili inadai kwamba; kuna uwezekano kwamba Watusi si wakushi bali ni wahamiaji tu kutoka maeneo ya jirani kipindi hicho cha kale ambao walihamia na kujichanganya na jamii waliyoikuta hapo (Wahutu) lakini wao walikuwa wafugaji. Chini ya nadharia hii inadai kwamba kuibuka kwa Wahutu na Watusi hakukutokana na kuwa na utofauti wa kinasaba au asili ya mababu bali ulitokana na utofauti wa kimadaraja/matabaka ya kijamii.
Tabaka la wale walio wa daraja la juu ambao walikuwa wafugaji walijitanabaisha kama Watusi wakati ambapo tabaka la chini ambao walikuwa wakulima walijitanabasha kama Wahutu.

Makabila haya yote matatu, Watwa, Wahutu na Watusi wanazungumza lugha moja na kwa wote kwa pamoja wanajulikana kama ‘Banyarwanda’.

Idadi ya watu ilipoongezeka katika eneo hili walianza kujitambua kupitia makundi madogo madogo yaliyoitwa ‘Ubwoko’ au ‘koo’ kwa kiswahili. Ilipofika katikati ya miaka ya 1700 koo nyingi ziliungana na kuunda ‘Falme’.
Moja ya Falme ambazo zilikuwa imara zaidi ulikuwa ni ‘Kingdom of Rwanda’ ambayo watawala wake wote walitokea katika koo ya Kitusi ya Nyiginya.

Ufalme huu ulifikia kileleni kipindi cha utawala wa Mfalme Kigeli Rwabugiri chini ya falsafa yake ya kujipanua na kuteka falme nyingine na kuzifanya sehemu ya Kingdom of Rwanda.

Chini ya Mfalme Rwabugiri alianzisha mfumi wa kiuchumi wa ‘ubuhake’ na baadae ‘uburetwa’.
Katika mifumo yote hii miwili, iliwanufaisha zaidi Watusi na kuwafanya Wahutu kama vijakazi wao kuwafanyia kazi za uzalishaji na kuwa askari vitani kwa ujira wa kupata fursa ya kumiliki mifugo na kutumia ardhi.

Watusi walipaa juu zaidi na kuwa raia daraja la kwanza ma Wahutu kubakia kuwa tabaka la chini kabisa ndani ya Kingdom of Rwanda.

Rwanda: Wakati wa Ukoloni

Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884 ulilitoa eneo hili kuwa koloni la nchi ya Ujerumani. Wajerumani walitawala eneo hili kwa kushirikiana na Mfalme na hivyo kuwapa wepesi wa kutawala koloni bila kuwa na askari wengi wa kijerumani ndani ya ardhi ya Rwanda. Yuhi V Musinga ndiye walikuwa Mfalme wa Rwanda kwa kipindi hiki na anakumbukwa zaidi kwa kuwapokea Wajerumani kwa mikono miwili.
0c654baede81239ccf0ddc5664b343b5.jpg

Ikulu ya Mfalme wa Rwanda maeneo ya Nyanza

Wajerumani ndio walikuwa watu wa kwanza kuanza kuwapandikizia Watusi kasumba ya kuwa wao si Wabantu. Wakoloni wa Ujerumani ndio ambao walieneza propaganda kwa kuwafundisha Watusi kwamba kutokana na tafiti zao za kina wamegundua kwamba wao (Watusi) mababu zao wa kale walihamia eneo hilo kutokea Ethiopia. Hivyo wakawashawishi kuamini kwamba Watusi wana vinasaba vya ‘uzungu’ (Caucasian) na hivyo ni wao pekee ndani ya Rwanda walistahili kupata nafasi za ajira kusaidizana kazi na wazungu chini ya utawala huo wa Wajerumani.

Katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Ubelgiji iliziteka Rwanda na Burundi kutoka mikononi mwa Ujerumani na mwaka 1919 League Of Nations ilizifanya rasmi nchi hizo kuwa makoloni ya Ubelgiji.

Mwanzoni Wakoloni wa Ubelgiji walianza kuitawala Rwanda kwa mtindo ule ule wa kushirikiana na Ufalme lakini baadae wakajilimbikizia madaraka yote ya kutawala kama ambavyo walifanya kwenye koloni lao la Kongo.

Baadae wakaanza ‘kutaifisha’ mali za Wanyarwanda katika mfumo wa kufanana kabisa na mfumo wa asili wa uburetwa na walioathirika zaidi na kampeni hii ya utaifishaji walikuwa ni Wahutu.
Ardhi yao ilinyang’anywa… Mifugo ilitwaliwa na kuwafanya Wahutu kuwa si tu vijakazi wa Wakoloni bali pia vijakazi wa Watusi.

Mwanzoni mwa miaka ya 1930s Ubelgiji walifanya upanuazi mkubwa wa sekta ya Elimu, afya na ajira za umma. Lakini wanufaika wakuu walikuwa ni Watusi.

Mwaka 1935 Ubelgiji walifanya kitu ch a ajabu sana ambacho kilipanua zaidi mpasuko wa kijamii na kitabaka uliopo ndani ya Rwanda. Walianzisha mfumo wa raia wote kuwa na vitambulisho. Vitambulisho hivi viliwatambua raia wote katika makundi manne kulingana na makabila yao. Watwa, Wahutu, Watusi na Raia wa kuomba (Naturalised).

Kutokana na Watusi kuwa ndio raia wa daraja la kwanza na tabaka la juu huku Wahutu wakiwa ni watu hafifu wa kudharaulika nchini humo, ilifikia hatua Wahutu wenye mali au ushawishi walikuwa wanahonga fedha ili kupatiwa vitambulisho vya Kuonyesha ni Watusi na watawala hawakuwapa Utusi kamili bali waliwapa ‘utusi wa heshima’ (Honorary Tutsi).

Hadhi ya Wahutu wote iliendelea kushuka kwa kasi wakionekana ni kabila na kizazi cha “Washenzi” huku Watusi wakionekana ndicho kizazi cha “wastaarabu” na kabila lenye darja.

Lakini kuna suala ambalo lilifanyika mwanzoni likionekana kuwa na manufaa makubwa lakini kadiri siku zilivyokwenda lilianza kuwa kama mkuki mgongoni. Kanisa Katoliki.

Kanisa Katoliki lilikuwa limeenea sana nchini Rwanda na raia wake wengi wakiwa ni waumini wa kanisa hilo. Tukumbuke kwamba tangu kipindi hicho Wahutu ndio walikuwa idadi kubwa zaidi ya raia wote ndani ya Rwanda. Hii ilimaanisha pia kwamba waumini wengi wa kanisa Katoliki walikuwa ni Wahutu.

Kwa kiasi fulani ndani ya kanisa Katoliki mapadri na watawa wengine walikuwa wanajisikia hatia kuacha waumini wao kuwekwa kwenye kundi la kizazi cha “washenzi” na kudharaulika ndani ya jamii. Kwa hiyo zikaanza juhudi za makusudi za kanisa katoliki kutoa elimu kwa vijana wenye asili ya Kihutu.

Baada ya miaka kadhaa kukaanza kuwepo walau kidogo uwiano wa wasomi wa Kihutu na Kitusi.

Mwaka 1957, mwezi March kikundi cha wasomi na watu wenye ushawishi wenye asili ya Kihutu walifanya jambo la “kimapinduzi” ambalo lilipanda mbegu mpya kwenye nafsi za watu wa kabila na kizazi cha cha Kihutu. Waliandaa waraka ulioitwa _'Manifeste des Bahutu' (Bahutu Manifesto).
Huu ndio ulikuwa waraka wa kwanza rasmi kubainisha kwamba Wahutu na Watusi ni mbari (race) mbili tofauti.

Katika waraka huu, wasomi hawa na watu hawa wenye ushawishi walijenga hoja kuu kwamba… Watusi wanapaswa kutoka kwenye jukumu lao walilojivesha la kuwa watawala wa Rwanda na badala yake nafasi hiyo ya kutawala Rwanda wapewe Wahutu. Hoja yao hii waliijenga kwenye nadharia ambayo wenyewe waliita “Statistical Law”, kwamba kitakwimu Wahutu ni wengi mno kushinda Watusi. Si sawa wakiendelea kutawaliwa na kufanywa vijakazi na Watusi.

Wanasema kwamba kabla kibanda cha nyasi kuungua kwanza utaanza kukiona kinafuka moshi. Kuna vugu vugu lilianza chini kwa chini ndani ya Rwanda.

Waraka huu… Bahutu Manifesto, ulitoka tarehe 4 March mwaka 1957. Japokuwa ilikuwa ni miaka takribani 37 kabla ya mwaka 1994, lakini ndio siku ambayo mbegu ya mauaji ya kimbari ilipandwa.

Usikose sehemu inayofuata….

Itaendelea…

The Bold
To Infinity and Beyond.

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA PILI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TATU

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NNE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TANO

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SITA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SABA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NANE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TISA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA
sorry boss sehemu ya pili cjaipata
 
n
Historia ya Kweli ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

031795b45fd5c0fbde56b9e68eea2404.jpg


KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA

SEHEMU YA KWANZA

“..kama unasoma ujumbe huu, muda huu… uko mpweke! Pengine ushahidi pekee uliobakia ni kijipande hiki cha maandishi. Sijui kama kuna yeyote kati yetu aliyesalimika kufika kizazi chenu mwaka huu mtakaosoma andishi langu. Sijui hata kama tumeshinda au tumeshindwa vita tunayopigana sasa hivi. Sijui, lakini naamini mwaka huu mliopo nyinyi sasa mwaweza kuwa na jibu sahihi. Vyovyote vile lakini jambo lililo dhahiri ni kwamba hakuna yeyote wa kizazi chetu mliye naye sasa hivi kwenye miaka yenu muusomapo ujumbe huu. Kwa hiyo wacha niwaeleze sisi tulikuwa akina nani, na kwa namna gani tulipambana mpaka tone la mwisho la damu mwilini mwetu ili kutetea kizazi chetu kisifutwe juu ya uso wa dunia. Wacha niwaeleze namna ambavyo japo tulikamuliwa damu mpaka kutiririka kufanya mifereji lakini lakini tulisimama kutetea kizazi chenu na ninyi watoto wetu. Wacha niwaeleze kisa kilichotikisa ulimwengu. Wacha niwaeleze kuhusu mifereji ya damu kwenda Ethiopia.!”

– Habib Anga alias The Bold

March 21, 1994 maeneo ya Uganda ambayo yanapakana na Rwanda, katika ziwa viktoria serikali ilituma vikosi vya jeshi kudhibiti eneo hilo kwa hali ya dharura. Agizo hili la serikali kutuma jeshi halikuwa kwa ajili ya kidhibiti eneo hilo kutoka kwa adui bali agizo lilikuwa ni kudhibiti eneo hilo dhidi ya maiti, maiti za binadamu. Sio maiti mbili au tatu, si mamia bali maelfu ya maiti za binadamu ambazo zilikuwa zinaingia ziwani Victoria zikiletwa na maji ya mto Kagera.

Maiti hizi zilikuwa nyingi kwa maelfu kiasi kwamba mapaka zilikuwa zinafanya maji yatoe harufu. Serikali ya Uganda ilituma jeshi eneo hili ili kudhibiti eneo hili maji yake yasitumiwe na wananchi kwa matumizi ya nyumbani au shughuli za uvuvi. Lakini jeshi lilikuwa eneo hili ili kuhakikisha kuwa taharuki iliyozuka baada ya maelfu ya miili hii kuonekana haigeuki na kuvuruga amanai katika eneo hili. Lakini pia jeshi lilikuwa hapa ili kubaini miili hii ilikuwa inatoka wapi.

Kadiri ambavyo jeshi la Uganda lilivyokuwa linafuatilia kwa kurudi nyuma kufuata mto Kagera ndivyo ambavyo walizidi kubaini kwamba maiti hizo zinaletwa na maji kutoka tawi la mto Kagera lililopita kusini mwa Rwanda. Na kadiri ambavyo walizidi kufuata chanzo cha maiti hizo zinakotoka ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia Rwanda na maji ya mto rangi yake kuwa nyekundu zaidi.

Wanajeshi wa Uganda ambao walishiriki kwenye ukaguzi huu wa mto huu wanakiri kwamba licha ya baadhi yao kupigana mstari wa mbele kwenye vita mbali mbali lakini hakuna yeyote kati yao ambaye aliwahi kushuhudia ukatili mkubwa wa kiasi hiki.

Siku hii jeshi la Uganda linakisia kwamba waliokota si chini ya miili elfu kumi ya binadamu na yote ilionekana kuletwa na maji ya mto Kagera kutoka nchini Rwanda.
Ajabu ni kwamba miili yote hii ilikiwa inamfanano fulani. Maiti zote zilikuwa za watu warefu, wembamba, wenye nyuso ndefu na pua za kuchongoka. Haikuhitaji kufikiria sana kufahamu kuwa maiti hizi zilikuwa za watu wa kabila la Tusi (Tutsi).

Miezi kadhaa baadae ndipo ambapo jeshi la Uganda na ulimwengu wote walikuja kuelewa kwa nini maiti zilikuwa zinatupwa mto Kagera. Ni ujumbe gani ambao ulikuwa unajaribu kutumwa.

Kwamba Watusi nchini Rwanda walikuwa waapenda kujisifu kuwa mababu zao wana asili ya nchi ya Ethiopia. Kitendo hiki cha watesi wao kuwatupa mtoni, walikuwa wanawaua na wakiwa wanatupa maiti zao mto wanawaambia kwamba “wanawasafirisha warudi kwao Ethiopia ambako wamekuwa wakijisifu ndio asili yao.”

Sio kwamba jeshi la Uganda hawakuwa na taarifa juu ya hali tete iliyopo Rwanda kwa muda wa karibia wiki nzima iliyopita bali hawakujua kama hali hiyo tete ilikuwa ni ya kinyama kiasi hicho.

Wanajeshi hawa wa Uganda walikuwa wameshikwa na bumbuwazi na vihoro vilivyo wapasua mioyo kwa kuona miili hii elfu kumi ya binadamu isiyo na uhai. Kitu ambacho walikuwa hawakijua na hakuna ambaye alidhahania ni kwamba ndani ya siku mia moja zijazo ulimwengu ulikuwa unaenda kushuhudia moja ya tukio la kikatili zaidi tangu kuubwa kwa ulimwengu. Karibia maiti za binadamu milioni moja zikiwa zimetapakaa mitaani nchini Rwanda iking’ong’wa na nzi na kuliwa na mbwa.


b27e3a3a6fd670dbc0a4e300cbcc558f.jpg





GENESIS

Rwanda: Kabla ya Ukoloni

Asili rasmi kabisa ya watu wa kwanza kuishi katika eneo ambalo leo tubalitambua kama nchi ya Rwanda ni watu wa kabila la ‘Twa’ (Watwa). Kabila hili la wawindaji si la kibantu bali ni sehemu ya makabila yanayotambulika na wanahistoria kama ‘pygmy’ ambao sifa yao kuu ni ufupi. Mtu mzima anayetoka makabila ya namna hii anakadirwa kuwa na wastani wa urefu chini ya sentimita 150. Watwa waliishi Rwanda enzi za kale sana miaka ya 8000 BC na 3000 BC.

Kuanzia miaka ya 700 BC mpaka 1500 AD makabila ya Kibantu kutoka maeneo ya jirani yalianza kuhamia eneo hili.

Kuna nadharia mbali mbali kuhusu ni namna gani haswa makabila haya ya kibantu yalihamia hapa na baadae kupelekea kutokea Makabila ya sasa ya Wahutu na Watusi.

Nadharia ya kwanza inadai kwamba; Wahutu ndio walikuwa wa kwanza kuhamia eneo hili na kuanzisha shughuli za kilimo. Baadae watu wenye asili ya Ukushi (Watusi wa sasa) nao wakahamia kwenye eneo hili na kulitawala.

Nadharia ya Pili inadai kwamba; kuna uwezekano kwamba Watusi si wakushi bali ni wahamiaji tu kutoka maeneo ya jirani kipindi hicho cha kale ambao walihamia na kujichanganya na jamii waliyoikuta hapo (Wahutu) lakini wao walikuwa wafugaji. Chini ya nadharia hii inadai kwamba kuibuka kwa Wahutu na Watusi hakukutokana na kuwa na utofauti wa kinasaba au asili ya mababu bali ulitokana na utofauti wa kimadaraja/matabaka ya kijamii.
Tabaka la wale walio wa daraja la juu ambao walikuwa wafugaji walijitanabaisha kama Watusi wakati ambapo tabaka la chini ambao walikuwa wakulima walijitanabasha kama Wahutu.

Makabila haya yote matatu, Watwa, Wahutu na Watusi wanazungumza lugha moja na kwa wote kwa pamoja wanajulikana kama ‘Banyarwanda’.

Idadi ya watu ilipoongezeka katika eneo hili walianza kujitambua kupitia makundi madogo madogo yaliyoitwa ‘Ubwoko’ au ‘koo’ kwa kiswahili. Ilipofika katikati ya miaka ya 1700 koo nyingi ziliungana na kuunda ‘Falme’.
Moja ya Falme ambazo zilikuwa imara zaidi ulikuwa ni ‘Kingdom of Rwanda’ ambayo watawala wake wote walitokea katika koo ya Kitusi ya Nyiginya.

Ufalme huu ulifikia kileleni kipindi cha utawala wa Mfalme Kigeli Rwabugiri chini ya falsafa yake ya kujipanua na kuteka falme nyingine na kuzifanya sehemu ya Kingdom of Rwanda.

Chini ya Mfalme Rwabugiri alianzisha mfumi wa kiuchumi wa ‘ubuhake’ na baadae ‘uburetwa’.
Katika mifumo yote hii miwili, iliwanufaisha zaidi Watusi na kuwafanya Wahutu kama vijakazi wao kuwafanyia kazi za uzalishaji na kuwa askari vitani kwa ujira wa kupata fursa ya kumiliki mifugo na kutumia ardhi.

Watusi walipaa juu zaidi na kuwa raia daraja la kwanza ma Wahutu kubakia kuwa tabaka la chini kabisa ndani ya Kingdom of Rwanda.

Rwanda: Wakati wa Ukoloni

Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884 ulilitoa eneo hili kuwa koloni la nchi ya Ujerumani. Wajerumani walitawala eneo hili kwa kushirikiana na Mfalme na hivyo kuwapa wepesi wa kutawala koloni bila kuwa na askari wengi wa kijerumani ndani ya ardhi ya Rwanda. Yuhi V Musinga ndiye walikuwa Mfalme wa Rwanda kwa kipindi hiki na anakumbukwa zaidi kwa kuwapokea Wajerumani kwa mikono miwili.
0c654baede81239ccf0ddc5664b343b5.jpg

Ikulu ya Mfalme wa Rwanda maeneo ya Nyanza

Wajerumani ndio walikuwa watu wa kwanza kuanza kuwapandikizia Watusi kasumba ya kuwa wao si Wabantu. Wakoloni wa Ujerumani ndio ambao walieneza propaganda kwa kuwafundisha Watusi kwamba kutokana na tafiti zao za kina wamegundua kwamba wao (Watusi) mababu zao wa kale walihamia eneo hilo kutokea Ethiopia. Hivyo wakawashawishi kuamini kwamba Watusi wana vinasaba vya ‘uzungu’ (Caucasian) na hivyo ni wao pekee ndani ya Rwanda walistahili kupata nafasi za ajira kusaidizana kazi na wazungu chini ya utawala huo wa Wajerumani.

Katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Ubelgiji iliziteka Rwanda na Burundi kutoka mikononi mwa Ujerumani na mwaka 1919 League Of Nations ilizifanya rasmi nchi hizo kuwa makoloni ya Ubelgiji.

Mwanzoni Wakoloni wa Ubelgiji walianza kuitawala Rwanda kwa mtindo ule ule wa kushirikiana na Ufalme lakini baadae wakajilimbikizia madaraka yote ya kutawala kama ambavyo walifanya kwenye koloni lao la Kongo.

Baadae wakaanza ‘kutaifisha’ mali za Wanyarwanda katika mfumo wa kufanana kabisa na mfumo wa asili wa uburetwa na walioathirika zaidi na kampeni hii ya utaifishaji walikuwa ni Wahutu.
Ardhi yao ilinyang’anywa… Mifugo ilitwaliwa na kuwafanya Wahutu kuwa si tu vijakazi wa Wakoloni bali pia vijakazi wa Watusi.

Mwanzoni mwa miaka ya 1930s Ubelgiji walifanya upanuazi mkubwa wa sekta ya Elimu, afya na ajira za umma. Lakini wanufaika wakuu walikuwa ni Watusi.

Mwaka 1935 Ubelgiji walifanya kitu ch a ajabu sana ambacho kilipanua zaidi mpasuko wa kijamii na kitabaka uliopo ndani ya Rwanda. Walianzisha mfumo wa raia wote kuwa na vitambulisho. Vitambulisho hivi viliwatambua raia wote katika makundi manne kulingana na makabila yao. Watwa, Wahutu, Watusi na Raia wa kuomba (Naturalised).

Kutokana na Watusi kuwa ndio raia wa daraja la kwanza na tabaka la juu huku Wahutu wakiwa ni watu hafifu wa kudharaulika nchini humo, ilifikia hatua Wahutu wenye mali au ushawishi walikuwa wanahonga fedha ili kupatiwa vitambulisho vya Kuonyesha ni Watusi na watawala hawakuwapa Utusi kamili bali waliwapa ‘utusi wa heshima’ (Honorary Tutsi).

Hadhi ya Wahutu wote iliendelea kushuka kwa kasi wakionekana ni kabila na kizazi cha “Washenzi” huku Watusi wakionekana ndicho kizazi cha “wastaarabu” na kabila lenye darja.

Lakini kuna suala ambalo lilifanyika mwanzoni likionekana kuwa na manufaa makubwa lakini kadiri siku zilivyokwenda lilianza kuwa kama mkuki mgongoni. Kanisa Katoliki.

Kanisa Katoliki lilikuwa limeenea sana nchini Rwanda na raia wake wengi wakiwa ni waumini wa kanisa hilo. Tukumbuke kwamba tangu kipindi hicho Wahutu ndio walikuwa idadi kubwa zaidi ya raia wote ndani ya Rwanda. Hii ilimaanisha pia kwamba waumini wengi wa kanisa Katoliki walikuwa ni Wahutu.

Kwa kiasi fulani ndani ya kanisa Katoliki mapadri na watawa wengine walikuwa wanajisikia hatia kuacha waumini wao kuwekwa kwenye kundi la kizazi cha “washenzi” na kudharaulika ndani ya jamii. Kwa hiyo zikaanza juhudi za makusudi za kanisa katoliki kutoa elimu kwa vijana wenye asili ya Kihutu.

Baada ya miaka kadhaa kukaanza kuwepo walau kidogo uwiano wa wasomi wa Kihutu na Kitusi.

Mwaka 1957, mwezi March kikundi cha wasomi na watu wenye ushawishi wenye asili ya Kihutu walifanya jambo la “kimapinduzi” ambalo lilipanda mbegu mpya kwenye nafsi za watu wa kabila na kizazi cha cha Kihutu. Waliandaa waraka ulioitwa _'Manifeste des Bahutu' (Bahutu Manifesto).
Huu ndio ulikuwa waraka wa kwanza rasmi kubainisha kwamba Wahutu na Watusi ni mbari (race) mbili tofauti.

Katika waraka huu, wasomi hawa na watu hawa wenye ushawishi walijenga hoja kuu kwamba… Watusi wanapaswa kutoka kwenye jukumu lao walilojivesha la kuwa watawala wa Rwanda na badala yake nafasi hiyo ya kutawala Rwanda wapewe Wahutu. Hoja yao hii waliijenga kwenye nadharia ambayo wenyewe waliita “Statistical Law”, kwamba kitakwimu Wahutu ni wengi mno kushinda Watusi. Si sawa wakiendelea kutawaliwa na kufanywa vijakazi na Watusi.

Wanasema kwamba kabla kibanda cha nyasi kuungua kwanza utaanza kukiona kinafuka moshi. Kuna vugu vugu lilianza chini kwa chini ndani ya Rwanda.

Waraka huu… Bahutu Manifesto, ulitoka tarehe 4 March mwaka 1957. Japokuwa ilikuwa ni miaka takribani 37 kabla ya mwaka 1994, lakini ndio siku ambayo mbegu ya mauaji ya kimbari ilipandwa.

Usikose sehemu inayofuata….

Itaendelea…

The Bold
To Infinity and Beyond.

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA PILI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TATU

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NNE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TANO

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SITA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SABA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NANE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TISA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA[/QU
Historia ya Kweli ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

031795b45fd5c0fbde56b9e68eea2404.jpg


KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA

SEHEMU YA KWANZA

“..kama unasoma ujumbe huu, muda huu… uko mpweke! Pengine ushahidi pekee uliobakia ni kijipande hiki cha maandishi. Sijui kama kuna yeyote kati yetu aliyesalimika kufika kizazi chenu mwaka huu mtakaosoma andishi langu. Sijui hata kama tumeshinda au tumeshindwa vita tunayopigana sasa hivi. Sijui, lakini naamini mwaka huu mliopo nyinyi sasa mwaweza kuwa na jibu sahihi. Vyovyote vile lakini jambo lililo dhahiri ni kwamba hakuna yeyote wa kizazi chetu mliye naye sasa hivi kwenye miaka yenu muusomapo ujumbe huu. Kwa hiyo wacha niwaeleze sisi tulikuwa akina nani, na kwa namna gani tulipambana mpaka tone la mwisho la damu mwilini mwetu ili kutetea kizazi chetu kisifutwe juu ya uso wa dunia. Wacha niwaeleze namna ambavyo japo tulikamuliwa damu mpaka kutiririka kufanya mifereji lakini lakini tulisimama kutetea kizazi chenu na ninyi watoto wetu. Wacha niwaeleze kisa kilichotikisa ulimwengu. Wacha niwaeleze kuhusu mifereji ya damu kwenda Ethiopia.!”

– Habib Anga alias The Bold

March 21, 1994 maeneo ya Uganda ambayo yanapakana na Rwanda, katika ziwa viktoria serikali ilituma vikosi vya jeshi kudhibiti eneo hilo kwa hali ya dharura. Agizo hili la serikali kutuma jeshi halikuwa kwa ajili ya kidhibiti eneo hilo kutoka kwa adui bali agizo lilikuwa ni kudhibiti eneo hilo dhidi ya maiti, maiti za binadamu. Sio maiti mbili au tatu, si mamia bali maelfu ya maiti za binadamu ambazo zilikuwa zinaingia ziwani Victoria zikiletwa na maji ya mto Kagera.

Maiti hizi zilikuwa nyingi kwa maelfu kiasi kwamba mapaka zilikuwa zinafanya maji yatoe harufu. Serikali ya Uganda ilituma jeshi eneo hili ili kudhibiti eneo hili maji yake yasitumiwe na wananchi kwa matumizi ya nyumbani au shughuli za uvuvi. Lakini jeshi lilikuwa eneo hili ili kuhakikisha kuwa taharuki iliyozuka baada ya maelfu ya miili hii kuonekana haigeuki na kuvuruga amanai katika eneo hili. Lakini pia jeshi lilikuwa hapa ili kubaini miili hii ilikuwa inatoka wapi.

Kadiri ambavyo jeshi la Uganda lilivyokuwa linafuatilia kwa kurudi nyuma kufuata mto Kagera ndivyo ambavyo walizidi kubaini kwamba maiti hizo zinaletwa na maji kutoka tawi la mto Kagera lililopita kusini mwa Rwanda. Na kadiri ambavyo walizidi kufuata chanzo cha maiti hizo zinakotoka ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia Rwanda na maji ya mto rangi yake kuwa nyekundu zaidi.

Wanajeshi wa Uganda ambao walishiriki kwenye ukaguzi huu wa mto huu wanakiri kwamba licha ya baadhi yao kupigana mstari wa mbele kwenye vita mbali mbali lakini hakuna yeyote kati yao ambaye aliwahi kushuhudia ukatili mkubwa wa kiasi hiki.

Siku hii jeshi la Uganda linakisia kwamba waliokota si chini ya miili elfu kumi ya binadamu na yote ilionekana kuletwa na maji ya mto Kagera kutoka nchini Rwanda.
Ajabu ni kwamba miili yote hii ilikiwa inamfanano fulani. Maiti zote zilikuwa za watu warefu, wembamba, wenye nyuso ndefu na pua za kuchongoka. Haikuhitaji kufikiria sana kufahamu kuwa maiti hizi zilikuwa za watu wa kabila la Tusi (Tutsi).

Miezi kadhaa baadae ndipo ambapo jeshi la Uganda na ulimwengu wote walikuja kuelewa kwa nini maiti zilikuwa zinatupwa mto Kagera. Ni ujumbe gani ambao ulikuwa unajaribu kutumwa.

Kwamba Watusi nchini Rwanda walikuwa waapenda kujisifu kuwa mababu zao wana asili ya nchi ya Ethiopia. Kitendo hiki cha watesi wao kuwatupa mtoni, walikuwa wanawaua na wakiwa wanatupa maiti zao mto wanawaambia kwamba “wanawasafirisha warudi kwao Ethiopia ambako wamekuwa wakijisifu ndio asili yao.”

Sio kwamba jeshi la Uganda hawakuwa na taarifa juu ya hali tete iliyopo Rwanda kwa muda wa karibia wiki nzima iliyopita bali hawakujua kama hali hiyo tete ilikuwa ni ya kinyama kiasi hicho.

Wanajeshi hawa wa Uganda walikuwa wameshikwa na bumbuwazi na vihoro vilivyo wapasua mioyo kwa kuona miili hii elfu kumi ya binadamu isiyo na uhai. Kitu ambacho walikuwa hawakijua na hakuna ambaye alidhahania ni kwamba ndani ya siku mia moja zijazo ulimwengu ulikuwa unaenda kushuhudia moja ya tukio la kikatili zaidi tangu kuubwa kwa ulimwengu. Karibia maiti za binadamu milioni moja zikiwa zimetapakaa mitaani nchini Rwanda iking’ong’wa na nzi na kuliwa na mbwa.


b27e3a3a6fd670dbc0a4e300cbcc558f.jpg





GENESIS

Rwanda: Kabla ya Ukoloni

Asili rasmi kabisa ya watu wa kwanza kuishi katika eneo ambalo leo tubalitambua kama nchi ya Rwanda ni watu wa kabila la ‘Twa’ (Watwa). Kabila hili la wawindaji si la kibantu bali ni sehemu ya makabila yanayotambulika na wanahistoria kama ‘pygmy’ ambao sifa yao kuu ni ufupi. Mtu mzima anayetoka makabila ya namna hii anakadirwa kuwa na wastani wa urefu chini ya sentimita 150. Watwa waliishi Rwanda enzi za kale sana miaka ya 8000 BC na 3000 BC.

Kuanzia miaka ya 700 BC mpaka 1500 AD makabila ya Kibantu kutoka maeneo ya jirani yalianza kuhamia eneo hili.

Kuna nadharia mbali mbali kuhusu ni namna gani haswa makabila haya ya kibantu yalihamia hapa na baadae kupelekea kutokea Makabila ya sasa ya Wahutu na Watusi.

Nadharia ya kwanza inadai kwamba; Wahutu ndio walikuwa wa kwanza kuhamia eneo hili na kuanzisha shughuli za kilimo. Baadae watu wenye asili ya Ukushi (Watusi wa sasa) nao wakahamia kwenye eneo hili na kulitawala.

Nadharia ya Pili inadai kwamba; kuna uwezekano kwamba Watusi si wakushi bali ni wahamiaji tu kutoka maeneo ya jirani kipindi hicho cha kale ambao walihamia na kujichanganya na jamii waliyoikuta hapo (Wahutu) lakini wao walikuwa wafugaji. Chini ya nadharia hii inadai kwamba kuibuka kwa Wahutu na Watusi hakukutokana na kuwa na utofauti wa kinasaba au asili ya mababu bali ulitokana na utofauti wa kimadaraja/matabaka ya kijamii.
Tabaka la wale walio wa daraja la juu ambao walikuwa wafugaji walijitanabaisha kama Watusi wakati ambapo tabaka la chini ambao walikuwa wakulima walijitanabasha kama Wahutu.

Makabila haya yote matatu, Watwa, Wahutu na Watusi wanazungumza lugha moja na kwa wote kwa pamoja wanajulikana kama ‘Banyarwanda’.

Idadi ya watu ilipoongezeka katika eneo hili walianza kujitambua kupitia makundi madogo madogo yaliyoitwa ‘Ubwoko’ au ‘koo’ kwa kiswahili. Ilipofika katikati ya miaka ya 1700 koo nyingi ziliungana na kuunda ‘Falme’.
Moja ya Falme ambazo zilikuwa imara zaidi ulikuwa ni ‘Kingdom of Rwanda’ ambayo watawala wake wote walitokea katika koo ya Kitusi ya Nyiginya.

Ufalme huu ulifikia kileleni kipindi cha utawala wa Mfalme Kigeli Rwabugiri chini ya falsafa yake ya kujipanua na kuteka falme nyingine na kuzifanya sehemu ya Kingdom of Rwanda.

Chini ya Mfalme Rwabugiri alianzisha mfumi wa kiuchumi wa ‘ubuhake’ na baadae ‘uburetwa’.
Katika mifumo yote hii miwili, iliwanufaisha zaidi Watusi na kuwafanya Wahutu kama vijakazi wao kuwafanyia kazi za uzalishaji na kuwa askari vitani kwa ujira wa kupata fursa ya kumiliki mifugo na kutumia ardhi.

Watusi walipaa juu zaidi na kuwa raia daraja la kwanza ma Wahutu kubakia kuwa tabaka la chini kabisa ndani ya Kingdom of Rwanda.

Rwanda: Wakati wa Ukoloni

Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884 ulilitoa eneo hili kuwa koloni la nchi ya Ujerumani. Wajerumani walitawala eneo hili kwa kushirikiana na Mfalme na hivyo kuwapa wepesi wa kutawala koloni bila kuwa na askari wengi wa kijerumani ndani ya ardhi ya Rwanda. Yuhi V Musinga ndiye walikuwa Mfalme wa Rwanda kwa kipindi hiki na anakumbukwa zaidi kwa kuwapokea Wajerumani kwa mikono miwili.
0c654baede81239ccf0ddc5664b343b5.jpg

Ikulu ya Mfalme wa Rwanda maeneo ya Nyanza

Wajerumani ndio walikuwa watu wa kwanza kuanza kuwapandikizia Watusi kasumba ya kuwa wao si Wabantu. Wakoloni wa Ujerumani ndio ambao walieneza propaganda kwa kuwafundisha Watusi kwamba kutokana na tafiti zao za kina wamegundua kwamba wao (Watusi) mababu zao wa kale walihamia eneo hilo kutokea Ethiopia. Hivyo wakawashawishi kuamini kwamba Watusi wana vinasaba vya ‘uzungu’ (Caucasian) na hivyo ni wao pekee ndani ya Rwanda walistahili kupata nafasi za ajira kusaidizana kazi na wazungu chini ya utawala huo wa Wajerumani.

Katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Ubelgiji iliziteka Rwanda na Burundi kutoka mikononi mwa Ujerumani na mwaka 1919 League Of Nations ilizifanya rasmi nchi hizo kuwa makoloni ya Ubelgiji.

Mwanzoni Wakoloni wa Ubelgiji walianza kuitawala Rwanda kwa mtindo ule ule wa kushirikiana na Ufalme lakini baadae wakajilimbikizia madaraka yote ya kutawala kama ambavyo walifanya kwenye koloni lao la Kongo.

Baadae wakaanza ‘kutaifisha’ mali za Wanyarwanda katika mfumo wa kufanana kabisa na mfumo wa asili wa uburetwa na walioathirika zaidi na kampeni hii ya utaifishaji walikuwa ni Wahutu.
Ardhi yao ilinyang’anywa… Mifugo ilitwaliwa na kuwafanya Wahutu kuwa si tu vijakazi wa Wakoloni bali pia vijakazi wa Watusi.

Mwanzoni mwa miaka ya 1930s Ubelgiji walifanya upanuazi mkubwa wa sekta ya Elimu, afya na ajira za umma. Lakini wanufaika wakuu walikuwa ni Watusi.

Mwaka 1935 Ubelgiji walifanya kitu ch a ajabu sana ambacho kilipanua zaidi mpasuko wa kijamii na kitabaka uliopo ndani ya Rwanda. Walianzisha mfumo wa raia wote kuwa na vitambulisho. Vitambulisho hivi viliwatambua raia wote katika makundi manne kulingana na makabila yao. Watwa, Wahutu, Watusi na Raia wa kuomba (Naturalised).

Kutokana na Watusi kuwa ndio raia wa daraja la kwanza na tabaka la juu huku Wahutu wakiwa ni watu hafifu wa kudharaulika nchini humo, ilifikia hatua Wahutu wenye mali au ushawishi walikuwa wanahonga fedha ili kupatiwa vitambulisho vya Kuonyesha ni Watusi na watawala hawakuwapa Utusi kamili bali waliwapa ‘utusi wa heshima’ (Honorary Tutsi).

Hadhi ya Wahutu wote iliendelea kushuka kwa kasi wakionekana ni kabila na kizazi cha “Washenzi” huku Watusi wakionekana ndicho kizazi cha “wastaarabu” na kabila lenye darja.

Lakini kuna suala ambalo lilifanyika mwanzoni likionekana kuwa na manufaa makubwa lakini kadiri siku zilivyokwenda lilianza kuwa kama mkuki mgongoni. Kanisa Katoliki.

Kanisa Katoliki lilikuwa limeenea sana nchini Rwanda na raia wake wengi wakiwa ni waumini wa kanisa hilo. Tukumbuke kwamba tangu kipindi hicho Wahutu ndio walikuwa idadi kubwa zaidi ya raia wote ndani ya Rwanda. Hii ilimaanisha pia kwamba waumini wengi wa kanisa Katoliki walikuwa ni Wahutu.

Kwa kiasi fulani ndani ya kanisa Katoliki mapadri na watawa wengine walikuwa wanajisikia hatia kuacha waumini wao kuwekwa kwenye kundi la kizazi cha “washenzi” na kudharaulika ndani ya jamii. Kwa hiyo zikaanza juhudi za makusudi za kanisa katoliki kutoa elimu kwa vijana wenye asili ya Kihutu.

Baada ya miaka kadhaa kukaanza kuwepo walau kidogo uwiano wa wasomi wa Kihutu na Kitusi.

Mwaka 1957, mwezi March kikundi cha wasomi na watu wenye ushawishi wenye asili ya Kihutu walifanya jambo la “kimapinduzi” ambalo lilipanda mbegu mpya kwenye nafsi za watu wa kabila na kizazi cha cha Kihutu. Waliandaa waraka ulioitwa _'Manifeste des Bahutu' (Bahutu Manifesto).
Huu ndio ulikuwa waraka wa kwanza rasmi kubainisha kwamba Wahutu na Watusi ni mbari (race) mbili tofauti.

Katika waraka huu, wasomi hawa na watu hawa wenye ushawishi walijenga hoja kuu kwamba… Watusi wanapaswa kutoka kwenye jukumu lao walilojivesha la kuwa watawala wa Rwanda na badala yake nafasi hiyo ya kutawala Rwanda wapewe Wahutu. Hoja yao hii waliijenga kwenye nadharia ambayo wenyewe waliita “Statistical Law”, kwamba kitakwimu Wahutu ni wengi mno kushinda Watusi. Si sawa wakiendelea kutawaliwa na kufanywa vijakazi na Watusi.

Wanasema kwamba kabla kibanda cha nyasi kuungua kwanza utaanza kukiona kinafuka moshi. Kuna vugu vugu lilianza chini kwa chini ndani ya Rwanda.

Waraka huu… Bahutu Manifesto, ulitoka tarehe 4 March mwaka 1957. Japokuwa ilikuwa ni miaka takribani 37 kabla ya mwaka 1994, lakini ndio siku ambayo mbegu ya mauaji ya kimbari ilipandwa.

Usikose sehemu inayofuata….

Itaendelea…

The Bold
To Infinity and Beyond.

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA PILI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TATU

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NNE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TANO

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SITA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SABA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NANE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TISA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA
ni story ya kusikitisha sana kiukweli inauma ila nahitaji kuisoma yote mbona vipande vyengine vinakataaa?
 
Screenshot_2018-02-05-10-40-23.png
1.Nimesoma hiyo link uliyoweka unayodai imesema watutsi walikuwa laki 7 na nimeirudia kama mara tatu lakini sijaona kitu cha namna hiyo,naku-challenge mkuu naomba uainishe hiyo sentensi inayosema namna hiyo pia uambatanishe na hiyo source.

Pia baada ya mauaji ya kimbari na serikali kuwa chini ya RPF,hakujawahi kufanyika tena sensa inayoonesha idadi ya makabila Rwanda,kipengele kinachoonesha idadi ya makabila kilitolewa kama sehemu ya jitihada za serikali kuutokomeza ukabila Rwanda,hicho ulichoweka angalau ungesema ni projection labda ungeeleweka,na kama unajiamini kwenye hili tupatie source kutoka kwa serikali ya rwanda kwasababu sensa yenyewe ya 2014 ilifanywa na serikali ya Rwanda,wikipedia sio credible source.

2.Usipuuzie sababu zilizowafanya RPF wakashika silaha na kuingia vitani,RPF walikuwa na sababu za msingi sana,ukizieweka pembeni utakuwa unaunga mkono Ideology ya "0 network" yaani ni wahutu tu ndio wenye haki ya kuwepo Rwanda.

3.Hakujawahi kuwa na double genocide Rwanda,isingekuwa rahisi kwa RPF kufanya genocide rwanda kama unavofikiri,hili iitwe genocide ni lazima kwanza iwe prepared,rpf walikuwa mstari wa mbele vitani wanapigana, wanateka maeneo wanasonga mbele,isingekuwa rahisi kwao kupata details za nani hasa ni mtusi na nani ni mhutu na anapatikana wapi,wahutu wenye msimamo mkali walianza kuiandaa genocide tangu 1990,haikuwa kazi ya siku moja au mwezi,walikuwa na details zote za aliyetakiwa kuuawa awe mtusi au mhutu mwenye msimamo wa kati,waliandaa jeshi na kulipa mafunzo kwa shughuli hiyo na kupenyeza propaganda ya kutosha kwa raia wa kawaida washiriki hivyo vitu,kulipuliwa kwa ndege ilikuwa ni kichocheo cha kuhalalisha mauaji lkn hata hiyo ingeshindikana ingetafutwa sababu nyingine,Gen. Dellaire aliitahadharisha UN kuwa kutakuwa na mauaji ya watusi miezi mitatu kabla ya ndege kulipuliwa,na Bagosora aliwahi kumwambia Dellaire matatizo ya rwanda hayawezi kuisha ni mpaka watusi watapofutika rwanda kwa hiyo haya mauaji yalipangwa na tena yalipangwa kwa muda mrefu.

Mimi nilipenda iitwe Rwandan genocide hili angalau hata wahutu ambao hawakushiriki huo unyama wasijisikie wana hatia ila kwa maneno uliyoandika ndo naanza kuona kwanini imepitishwa kuwa Tutsi Genoscide,kuna hatari kubwa sana ya historia kupotoshwa,kumbe kuna umuhimu wa kuukabili ukweli ila yote kwa yote mkuu mtu awe mtusi au muhutu anabaki kuwa kama binadamu wengine,wote wanayo haki ya kuishi,hakuna aliye bora zaidi ya mwingine,hakuna anayestahili kuishi zaidi ya mwingine,mgogoro wa watusi na wahutu rwanda na burundi ni matokeo mabaya ya ukoloni,kabla ya ukoloni watusi na wahutu waliishi bila kuchinjana kwa karibu/zaidi ya miaka 100,ila iliwachukua ubelgiji miaka michache tu kuipasua Rwanda na burundi vipande vpande.
Mkuu IBUKA wameweka final survivors hivyo ni kazi yetu kutohoa je walikuwa wahutu na watutsi wangapi Rwanda sasa twende polepole

Data za world bank na UN zinasema rwanda ilikuwa na watu million 6 (nmeattach screenshot hapo chini)

Then link ya UN inasema wahutu walikuwa 84% na tutsi 15% mwaka 1994
Source: Outreach Programme on the Rwanda Genocide and the United Nations

hivyo basi 15% ya million 6 ni 900,000 si ndio.... taasisi ya watutsi IBUKA nlioweka inasema survivors ni laki 4 si ndio??
Source:https://survivors-fund.org.uk/learn/rwandan-history/statistics/

Tutsi laki 9 - Tutsi survivors laki 4 = unapata 500,000 deaths si ndio maana yake

Haya official statistics za UN na IBUIA zinasema waliokufa kwenye genocide walikuwa watu 1,078,000 source:https://survivors-fund.org.uk/learn/rwandan-history/statistics/

hivyo basi

1,078,000 - 500,000 = 578,000 je hawa ni jamii gani maana hawakuwa watutsi kwa mahesabu tuliopiga si ndio?? Hivyo tunakubaliana ni wahutu

Mpaka hapa nafkiri umeshaona kuwa statistics zangu nlizoweka za IBUKA bado ni credible

NB: Kuhusu Wikipedia.... inasema takwimu zake zimetolewa CIA world factbook ambayo ni credible sana maana serikali ya rwanda haiwezi andika namba ya wahutu na watutsi kwa sababu zilizo wazi kabisa ila wao kma serikali kwa sababu za kiusalama huwa wanakuwa na hizo data mapema kabisa hivyo sioni kma CIA world factbook as citee na wikipedia haiwezi kuaminika

2. Mkuu ni vizuri tuwe tunafanya utafiti kabla ya kulaumu.... Hao watutsi mwaka 1990 waliandikiwa barua kuruhusiwa kurudi Rwanda kma raia wa kawaida ila sio tu kwamba waligoma kuja ila hata barua haikuwahi jibiwa hivyo kma walitaka kurudi kwanni walikataa wito wa mwaka 1990??? Huoni wao walitaka kurudi kwa mabomu na risasi ili wapate madaraka pekee!! Source: https://www.google.com/amp/s/www.gl...s-behind-the-1994-rwanda-genocide/5406344/amp

3. Mkuu unaposema hapakuwa na double genocide what's your reference?? Mimi nmekuwekea ripoti ya UN kwenye post uliyoreply inayosema RPF kwa ushahidi waliopata iliua wahutu wengi sana au unafkiri hao wahutu laki 6 walikufaje mkuu???

Unasema genocide ni lazima iwe prepared.... Na lipo wazi kabisa kuendana na ushahidi wa General katumba nyamwasa aliyekimbia Rwanda kisa kutoboa siri za RPF alisema ndege ilivyotunguliwa waliambiwa wajiandae kusonga mbele ikimaanisha walipanga ile vita in advance je haiwi genocide

Pia Kumbuka kabla ya RPF kuja hakukuwa na genocide ila RPF walivyoanza kuchinja wahutu kule ruhengeri ndio ikatia hasara wahutu wa pande zingine wakaanza kuua watutsi kwenye maeneo mengineyo je unafkiri hawakupanga??

Huu hapa ushahidi kwamba genocide ilianzia ruhengeri ambapo watutsi wa RPF walichinja wahutu ndio kusababisha wahutu nao kuanza kuua tena hii ilikuwa 1991https://www.google.com/amp/s/arnaudemmanuel.wordpress.com/2008/05/23/rwanda-rpf-crimes/amp/

Pia nmeweka hapo confession ingawa unasema hauiamini ila ilitumika kwenye kesi ntakupa reference..... Jamaa alikiri walitumwa kuua wahutu wote mbele yao je hiyo sio planned genocide too??

Kuhusu dallaire nimeshasema hawezi kuaminika maana alitangaza kuwa Rwanda imewekewa vikwazo wasipewe silaha ila ndio huyo huyo kwa siri alikuwa anawapa silaha RPF kuwamaliza wahutu je unaaminije kauli za huyu msaliti?? Alidai hakuona mtutsi akiua muhutu ila ripoti ya UN inasema watutsi walichinja wahutu je huyo dallare bado anaaminika??

Kuhusu uchafu wa dallare pia soma huu utafiti https://www.google.com/amp/s/www.gl...s-behind-the-1994-rwanda-genocide/5406344/amp

Hitimisho lako nakubaliana nalo ingawa unaposema ''ANGALAU '' sidhani ni sahihi sababu nmeshakupa ripoti nyingi na article zinazoonyesha RPF wanahusika na vifo vya wahutu kibao sasa kwanini bado huoni ina deserve kuitwa RWANDAN GENOCIDE...... remember Hutus died kuliko tutsis thats still enough to call it RWANDAN genocide if not HUTU genocide

Ahsante

Ushahidi huu hapa jinsi watutsi walivyochinja wahutu zaidi ya laki 5 Rwanda mara baada ya kupindua nchi

THE SLAUGHTER OF HUTU REFUGEES IN DRC - RWANDA DEMOCRACY WATCH

The Rwandan Patriotic Front (HRW Report - Leave None to Tell the Story: Genocide in Rwanda, March 1999)

Kibeho 1995: a massacre forgotten in Rwanda’s 20-year history - Jambonews EN

Kabila Army's Mass Murder of Rwandan Hutu Refugees





Kazi kwako

Cc: 666 chata manzi james
 
Bold shusha ya 12 kaka, daaah yaani mtu unasoma kama unaangalia movie vile.

Na nyie kina Zito na Ariana kwanini toka peji ya 30 mpaka sasa ni nyie tu? Mnamlalamikia the bold kinafiki na mnaumia akimsifia kagame? Bila shaka nyie ni wahutu asilimia mia, sasa chuki sio jambo baya ila nawasihi bakieni nayo ila tuachieni uzi wetu basi tuusome tuburudike, shida iko wapi? Kweli kila peji ukisoma ni nyie wawili tu hivi hamna kazi uko labda? Na yule mtusi anaetukana mngemkalia kimya asingekua anatukana, hakuna sababu ya kulumbana kijinga, tusome tu, kama na nyie mna ya kwenu tofauti na hii basi andikeni na nyie uzi mwingine, huu ni wa the bold na sie tumeufurahia sanaa, hamko hapa hili mumsaishe the bold anajua anachokifanya.
Zito na huyo mwenzie wahutu
 
Hivi kuna Wahutu hapa Jamii forums walishawahi kuwa proud na Kagame?

Mostly Watutsi ndiyo wanakuwa front kumtetea Kagame!!
Unataka tuwatetee wahutu??? yaan waliwapiga mababu zetu wakawatimua Rwanda, unataka tuwatetee???? in make sense kwako?? mtu amewatimua jamii yenu na alikua na lengo la kuwatokomeza kabisa kwenye uso wa dunia unaanzaje mtetea?
 
View attachment 698540
Mkuu IBUKA wameweka final survivors hivyo ni kazi yetu kutohoa je walikuwa wahutu na watutsi wangapi Rwanda sasa twende polepole

Data za world bank na UN zinasema rwanda ilikuwa na watu million 6 (nmeattach screenshot hapo chini)

Then link ya UN inasema wahutu walikuwa 84% na tutsi 15% mwaka 1994
Source: Outreach Programme on the Rwanda Genocide and the United Nations

hivyo basi 15% ya million 6 ni 900,000 si ndio.... taasisi ya watutsi IBUKA nlioweka inasema survivors ni laki 4 si ndio??
Source:https://survivors-fund.org.uk/learn/rwandan-history/statistics/

Tutsi laki 9 - Tutsi survivors laki 4 = unapata 500,000 deaths si ndio maana yake

Haya official statistics za UN na IBUIA zinasema waliokufa kwenye genocide walikuwa watu 1,078,000 source:https://survivors-fund.org.uk/learn/rwandan-history/statistics/

hivyo basi

1,078,000 - 500,000 = 578,000 je hawa ni jamii gani maana hawakuwa watutsi kwa mahesabu tuliopiga si ndio?? Hivyo tunakubaliana ni wahutu

Mpaka hapa nafkiri umeshaona kuwa statistics zangu nlizoweka za IBUKA bado ni credible

NB: Kuhusu Wikipedia.... inasema takwimu zake zimetolewa CIA world factbook ambayo ni credible sana maana serikali ya rwanda haiwezi andika namba ya wahutu na watutsi kwa sababu zilizo wazi kabisa ila wao kma serikali kwa sababu za kiusalama huwa wanakuwa na hizo data mapema kabisa hivyo sioni kma CIA world factbook as citee na wikipedia haiwezi kuaminika

2. Mkuu ni vizuri tuwe tunafanya utafiti kabla ya kulaumu.... Hao watutsi mwaka 1990 waliandikiwa barua kuruhusiwa kurudi Rwanda kma raia wa kawaida ila sio tu kwamba waligoma kuja ila hata barua haikuwahi jibiwa hivyo kma walitaka kurudi kwanni walikataa wito wa mwaka 1990??? Huoni wao walitaka kurudi kwa mabomu na risasi ili wapate madaraka pekee!! Source: https://www.google.com/amp/s/www.gl...s-behind-the-1994-rwanda-genocide/5406344/amp

3. Mkuu unaposema hapakuwa na double genocide what's your reference?? Mimi nmekuwekea ripoti ya UN kwenye post uliyoreply inayosema RPF kwa ushahidi waliopata iliua wahutu wengi sana au unafkiri hao wahutu laki 6 walikufaje mkuu???

Unasema genocide ni lazima iwe prepared.... Na lipo wazi kabisa kuendana na ushahidi wa General katumba nyamwasa aliyekimbia Rwanda kisa kutoboa siri za RPF alisema ndege ilivyotunguliwa waliambiwa wajiandae kusonga mbele ikimaanisha walipanga ile vita in advance je haiwi genocide

Pia Kumbuka kabla ya RPF kuja hakukuwa na genocide ila RPF walivyoanza kuchinja wahutu kule ruhengeri ndio ikatia hasara wahutu wa pande zingine wakaanza kuua watutsi kwenye maeneo mengineyo je unafkiri hawakupanga??

Huu hapa ushahidi kwamba genocide ilianzia ruhengeri ambapo watutsi wa RPF walichinja wahutu ndio kusababisha wahutu nao kuanza kuua tena hii ilikuwa 1991https://www.google.com/amp/s/arnaudemmanuel.wordpress.com/2008/05/23/rwanda-rpf-crimes/amp/

Pia nmeweka hapo confession ingawa unasema hauiamini ila ilitumika kwenye kesi ntakupa reference..... Jamaa alikiri walitumwa kuua wahutu wote mbele yao je hiyo sio planned genocide too??

Kuhusu dallaire nimeshasema hawezi kuaminika maana alitangaza kuwa Rwanda imewekewa vikwazo wasipewe silaha ila ndio huyo huyo kwa siri alikuwa anawapa silaha RPF kuwamaliza wahutu je unaaminije kauli za huyu msaliti?? Alidai hakuona mtutsi akiua muhutu ila ripoti ya UN inasema watutsi walichinja wahutu je huyo dallare bado anaaminika??

Kuhusu uchafu wa dallare pia soma huu utafiti https://www.google.com/amp/s/www.gl...s-behind-the-1994-rwanda-genocide/5406344/amp

Hitimisho lako nakubaliana nalo ingawa unaposema ''ANGALAU '' sidhani ni sahihi sababu nmeshakupa ripoti nyingi na article zinazoonyesha RPF wanahusika na vifo vya wahutu kibao sasa kwanini bado huoni ina deserve kuitwa RWANDAN GENOCIDE...... remember Hutus died kuliko tutsis thats still enough to call it RWANDAN genocide if not HUTU genocide

Ahsante

Ushahidi huu hapa jinsi watutsi walivyochinja wahutu zaidi ya laki 5 Rwanda mara baada ya kupindua nchi

THE SLAUGHTER OF HUTU REFUGEES IN DRC - RWANDA DEMOCRACY WATCH

The Rwandan Patriotic Front (HRW Report - Leave None to Tell the Story: Genocide in Rwanda, March 1999)

Kibeho 1995: a massacre forgotten in Rwanda’s 20-year history - Jambonews EN

Kabila Army's Mass Murder of Rwandan Hutu Refugees





Kazi kwako

Cc: 666 chata manzi james



Nimekuelewa kabisaa, waliokufa wengi ni wahutu na ni clear Rwanda Genocide, ila mimi bado nasikitishwa na alieanzisha vita hivi, je ni muhutu au mtusi? Yoyote alieanzisha vita hivi ilikua halali yeye kufa,,, labda kama kuna yalio nyuma ya pazia, lakin kama sababu ni hizo tulizoziskia za wivu dhidi ya watusi kua na akili, kupenda shule na kua civilized mapema basi wahutu pengine ndio binadamu wasio faa kabisaa kuwepo africa na ningesikia raha kama wote walioanzisha izo propaganda kuawawa.
 
Historia ya Kweli ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

031795b45fd5c0fbde56b9e68eea2404.jpg


KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA

SEHEMU YA KWANZA

“..kama unasoma ujumbe huu, muda huu… uko mpweke! Pengine ushahidi pekee uliobakia ni kijipande hiki cha maandishi. Sijui kama kuna yeyote kati yetu aliyesalimika kufika kizazi chenu mwaka huu mtakaosoma andishi langu. Sijui hata kama tumeshinda au tumeshindwa vita tunayopigana sasa hivi. Sijui, lakini naamini mwaka huu mliopo nyinyi sasa mwaweza kuwa na jibu sahihi. Vyovyote vile lakini jambo lililo dhahiri ni kwamba hakuna yeyote wa kizazi chetu mliye naye sasa hivi kwenye miaka yenu muusomapo ujumbe huu. Kwa hiyo wacha niwaeleze sisi tulikuwa akina nani, na kwa namna gani tulipambana mpaka tone la mwisho la damu mwilini mwetu ili kutetea kizazi chetu kisifutwe juu ya uso wa dunia. Wacha niwaeleze namna ambavyo japo tulikamuliwa damu mpaka kutiririka kufanya mifereji lakini lakini tulisimama kutetea kizazi chenu na ninyi watoto wetu. Wacha niwaeleze kisa kilichotikisa ulimwengu. Wacha niwaeleze kuhusu mifereji ya damu kwenda Ethiopia.!”

– Habib Anga alias The Bold

March 21, 1994 maeneo ya Uganda ambayo yanapakana na Rwanda, katika ziwa viktoria serikali ilituma vikosi vya jeshi kudhibiti eneo hilo kwa hali ya dharura. Agizo hili la serikali kutuma jeshi halikuwa kwa ajili ya kidhibiti eneo hilo kutoka kwa adui bali agizo lilikuwa ni kudhibiti eneo hilo dhidi ya maiti, maiti za binadamu. Sio maiti mbili au tatu, si mamia bali maelfu ya maiti za binadamu ambazo zilikuwa zinaingia ziwani Victoria zikiletwa na maji ya mto Kagera.

Maiti hizi zilikuwa nyingi kwa maelfu kiasi kwamba mapaka zilikuwa zinafanya maji yatoe harufu. Serikali ya Uganda ilituma jeshi eneo hili ili kudhibiti eneo hili maji yake yasitumiwe na wananchi kwa matumizi ya nyumbani au shughuli za uvuvi. Lakini jeshi lilikuwa eneo hili ili kuhakikisha kuwa taharuki iliyozuka baada ya maelfu ya miili hii kuonekana haigeuki na kuvuruga amanai katika eneo hili. Lakini pia jeshi lilikuwa hapa ili kubaini miili hii ilikuwa inatoka wapi.

Kadiri ambavyo jeshi la Uganda lilivyokuwa linafuatilia kwa kurudi nyuma kufuata mto Kagera ndivyo ambavyo walizidi kubaini kwamba maiti hizo zinaletwa na maji kutoka tawi la mto Kagera lililopita kusini mwa Rwanda. Na kadiri ambavyo walizidi kufuata chanzo cha maiti hizo zinakotoka ndivyo ambavyo walikuwa wanaikaribia Rwanda na maji ya mto rangi yake kuwa nyekundu zaidi.

Wanajeshi wa Uganda ambao walishiriki kwenye ukaguzi huu wa mto huu wanakiri kwamba licha ya baadhi yao kupigana mstari wa mbele kwenye vita mbali mbali lakini hakuna yeyote kati yao ambaye aliwahi kushuhudia ukatili mkubwa wa kiasi hiki.

Siku hii jeshi la Uganda linakisia kwamba waliokota si chini ya miili elfu kumi ya binadamu na yote ilionekana kuletwa na maji ya mto Kagera kutoka nchini Rwanda.
Ajabu ni kwamba miili yote hii ilikiwa inamfanano fulani. Maiti zote zilikuwa za watu warefu, wembamba, wenye nyuso ndefu na pua za kuchongoka. Haikuhitaji kufikiria sana kufahamu kuwa maiti hizi zilikuwa za watu wa kabila la Tusi (Tutsi).

Miezi kadhaa baadae ndipo ambapo jeshi la Uganda na ulimwengu wote walikuja kuelewa kwa nini maiti zilikuwa zinatupwa mto Kagera. Ni ujumbe gani ambao ulikuwa unajaribu kutumwa.

Kwamba Watusi nchini Rwanda walikuwa waapenda kujisifu kuwa mababu zao wana asili ya nchi ya Ethiopia. Kitendo hiki cha watesi wao kuwatupa mtoni, walikuwa wanawaua na wakiwa wanatupa maiti zao mto wanawaambia kwamba “wanawasafirisha warudi kwao Ethiopia ambako wamekuwa wakijisifu ndio asili yao.”

Sio kwamba jeshi la Uganda hawakuwa na taarifa juu ya hali tete iliyopo Rwanda kwa muda wa karibia wiki nzima iliyopita bali hawakujua kama hali hiyo tete ilikuwa ni ya kinyama kiasi hicho.

Wanajeshi hawa wa Uganda walikuwa wameshikwa na bumbuwazi na vihoro vilivyo wapasua mioyo kwa kuona miili hii elfu kumi ya binadamu isiyo na uhai. Kitu ambacho walikuwa hawakijua na hakuna ambaye alidhahania ni kwamba ndani ya siku mia moja zijazo ulimwengu ulikuwa unaenda kushuhudia moja ya tukio la kikatili zaidi tangu kuubwa kwa ulimwengu. Karibia maiti za binadamu milioni moja zikiwa zimetapakaa mitaani nchini Rwanda iking’ong’wa na nzi na kuliwa na mbwa.


b27e3a3a6fd670dbc0a4e300cbcc558f.jpg





GENESIS

Rwanda: Kabla ya Ukoloni

Asili rasmi kabisa ya watu wa kwanza kuishi katika eneo ambalo leo tubalitambua kama nchi ya Rwanda ni watu wa kabila la ‘Twa’ (Watwa). Kabila hili la wawindaji si la kibantu bali ni sehemu ya makabila yanayotambulika na wanahistoria kama ‘pygmy’ ambao sifa yao kuu ni ufupi. Mtu mzima anayetoka makabila ya namna hii anakadirwa kuwa na wastani wa urefu chini ya sentimita 150. Watwa waliishi Rwanda enzi za kale sana miaka ya 8000 BC na 3000 BC.

Kuanzia miaka ya 700 BC mpaka 1500 AD makabila ya Kibantu kutoka maeneo ya jirani yalianza kuhamia eneo hili.

Kuna nadharia mbali mbali kuhusu ni namna gani haswa makabila haya ya kibantu yalihamia hapa na baadae kupelekea kutokea Makabila ya sasa ya Wahutu na Watusi.

Nadharia ya kwanza inadai kwamba; Wahutu ndio walikuwa wa kwanza kuhamia eneo hili na kuanzisha shughuli za kilimo. Baadae watu wenye asili ya Ukushi (Watusi wa sasa) nao wakahamia kwenye eneo hili na kulitawala.

Nadharia ya Pili inadai kwamba; kuna uwezekano kwamba Watusi si wakushi bali ni wahamiaji tu kutoka maeneo ya jirani kipindi hicho cha kale ambao walihamia na kujichanganya na jamii waliyoikuta hapo (Wahutu) lakini wao walikuwa wafugaji. Chini ya nadharia hii inadai kwamba kuibuka kwa Wahutu na Watusi hakukutokana na kuwa na utofauti wa kinasaba au asili ya mababu bali ulitokana na utofauti wa kimadaraja/matabaka ya kijamii.
Tabaka la wale walio wa daraja la juu ambao walikuwa wafugaji walijitanabaisha kama Watusi wakati ambapo tabaka la chini ambao walikuwa wakulima walijitanabasha kama Wahutu.

Makabila haya yote matatu, Watwa, Wahutu na Watusi wanazungumza lugha moja na kwa wote kwa pamoja wanajulikana kama ‘Banyarwanda’.

Idadi ya watu ilipoongezeka katika eneo hili walianza kujitambua kupitia makundi madogo madogo yaliyoitwa ‘Ubwoko’ au ‘koo’ kwa kiswahili. Ilipofika katikati ya miaka ya 1700 koo nyingi ziliungana na kuunda ‘Falme’.
Moja ya Falme ambazo zilikuwa imara zaidi ulikuwa ni ‘Kingdom of Rwanda’ ambayo watawala wake wote walitokea katika koo ya Kitusi ya Nyiginya.

Ufalme huu ulifikia kileleni kipindi cha utawala wa Mfalme Kigeli Rwabugiri chini ya falsafa yake ya kujipanua na kuteka falme nyingine na kuzifanya sehemu ya Kingdom of Rwanda.

Chini ya Mfalme Rwabugiri alianzisha mfumi wa kiuchumi wa ‘ubuhake’ na baadae ‘uburetwa’.
Katika mifumo yote hii miwili, iliwanufaisha zaidi Watusi na kuwafanya Wahutu kama vijakazi wao kuwafanyia kazi za uzalishaji na kuwa askari vitani kwa ujira wa kupata fursa ya kumiliki mifugo na kutumia ardhi.

Watusi walipaa juu zaidi na kuwa raia daraja la kwanza ma Wahutu kubakia kuwa tabaka la chini kabisa ndani ya Kingdom of Rwanda.

Rwanda: Wakati wa Ukoloni

Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884 ulilitoa eneo hili kuwa koloni la nchi ya Ujerumani. Wajerumani walitawala eneo hili kwa kushirikiana na Mfalme na hivyo kuwapa wepesi wa kutawala koloni bila kuwa na askari wengi wa kijerumani ndani ya ardhi ya Rwanda. Yuhi V Musinga ndiye walikuwa Mfalme wa Rwanda kwa kipindi hiki na anakumbukwa zaidi kwa kuwapokea Wajerumani kwa mikono miwili.
0c654baede81239ccf0ddc5664b343b5.jpg

Ikulu ya Mfalme wa Rwanda maeneo ya Nyanza

Wajerumani ndio walikuwa watu wa kwanza kuanza kuwapandikizia Watusi kasumba ya kuwa wao si Wabantu. Wakoloni wa Ujerumani ndio ambao walieneza propaganda kwa kuwafundisha Watusi kwamba kutokana na tafiti zao za kina wamegundua kwamba wao (Watusi) mababu zao wa kale walihamia eneo hilo kutokea Ethiopia. Hivyo wakawashawishi kuamini kwamba Watusi wana vinasaba vya ‘uzungu’ (Caucasian) na hivyo ni wao pekee ndani ya Rwanda walistahili kupata nafasi za ajira kusaidizana kazi na wazungu chini ya utawala huo wa Wajerumani.

Katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Ubelgiji iliziteka Rwanda na Burundi kutoka mikononi mwa Ujerumani na mwaka 1919 League Of Nations ilizifanya rasmi nchi hizo kuwa makoloni ya Ubelgiji.

Mwanzoni Wakoloni wa Ubelgiji walianza kuitawala Rwanda kwa mtindo ule ule wa kushirikiana na Ufalme lakini baadae wakajilimbikizia madaraka yote ya kutawala kama ambavyo walifanya kwenye koloni lao la Kongo.

Baadae wakaanza ‘kutaifisha’ mali za Wanyarwanda katika mfumo wa kufanana kabisa na mfumo wa asili wa uburetwa na walioathirika zaidi na kampeni hii ya utaifishaji walikuwa ni Wahutu.
Ardhi yao ilinyang’anywa… Mifugo ilitwaliwa na kuwafanya Wahutu kuwa si tu vijakazi wa Wakoloni bali pia vijakazi wa Watusi.

Mwanzoni mwa miaka ya 1930s Ubelgiji walifanya upanuazi mkubwa wa sekta ya Elimu, afya na ajira za umma. Lakini wanufaika wakuu walikuwa ni Watusi.

Mwaka 1935 Ubelgiji walifanya kitu ch a ajabu sana ambacho kilipanua zaidi mpasuko wa kijamii na kitabaka uliopo ndani ya Rwanda. Walianzisha mfumo wa raia wote kuwa na vitambulisho. Vitambulisho hivi viliwatambua raia wote katika makundi manne kulingana na makabila yao. Watwa, Wahutu, Watusi na Raia wa kuomba (Naturalised).

Kutokana na Watusi kuwa ndio raia wa daraja la kwanza na tabaka la juu huku Wahutu wakiwa ni watu hafifu wa kudharaulika nchini humo, ilifikia hatua Wahutu wenye mali au ushawishi walikuwa wanahonga fedha ili kupatiwa vitambulisho vya Kuonyesha ni Watusi na watawala hawakuwapa Utusi kamili bali waliwapa ‘utusi wa heshima’ (Honorary Tutsi).

Hadhi ya Wahutu wote iliendelea kushuka kwa kasi wakionekana ni kabila na kizazi cha “Washenzi” huku Watusi wakionekana ndicho kizazi cha “wastaarabu” na kabila lenye darja.

Lakini kuna suala ambalo lilifanyika mwanzoni likionekana kuwa na manufaa makubwa lakini kadiri siku zilivyokwenda lilianza kuwa kama mkuki mgongoni. Kanisa Katoliki.

Kanisa Katoliki lilikuwa limeenea sana nchini Rwanda na raia wake wengi wakiwa ni waumini wa kanisa hilo. Tukumbuke kwamba tangu kipindi hicho Wahutu ndio walikuwa idadi kubwa zaidi ya raia wote ndani ya Rwanda. Hii ilimaanisha pia kwamba waumini wengi wa kanisa Katoliki walikuwa ni Wahutu.

Kwa kiasi fulani ndani ya kanisa Katoliki mapadri na watawa wengine walikuwa wanajisikia hatia kuacha waumini wao kuwekwa kwenye kundi la kizazi cha “washenzi” na kudharaulika ndani ya jamii. Kwa hiyo zikaanza juhudi za makusudi za kanisa katoliki kutoa elimu kwa vijana wenye asili ya Kihutu.

Baada ya miaka kadhaa kukaanza kuwepo walau kidogo uwiano wa wasomi wa Kihutu na Kitusi.

Mwaka 1957, mwezi March kikundi cha wasomi na watu wenye ushawishi wenye asili ya Kihutu walifanya jambo la “kimapinduzi” ambalo lilipanda mbegu mpya kwenye nafsi za watu wa kabila na kizazi cha cha Kihutu. Waliandaa waraka ulioitwa _'Manifeste des Bahutu' (Bahutu Manifesto).
Huu ndio ulikuwa waraka wa kwanza rasmi kubainisha kwamba Wahutu na Watusi ni mbari (race) mbili tofauti.

Katika waraka huu, wasomi hawa na watu hawa wenye ushawishi walijenga hoja kuu kwamba… Watusi wanapaswa kutoka kwenye jukumu lao walilojivesha la kuwa watawala wa Rwanda na badala yake nafasi hiyo ya kutawala Rwanda wapewe Wahutu. Hoja yao hii waliijenga kwenye nadharia ambayo wenyewe waliita “Statistical Law”, kwamba kitakwimu Wahutu ni wengi mno kushinda Watusi. Si sawa wakiendelea kutawaliwa na kufanywa vijakazi na Watusi.

Wanasema kwamba kabla kibanda cha nyasi kuungua kwanza utaanza kukiona kinafuka moshi. Kuna vugu vugu lilianza chini kwa chini ndani ya Rwanda.

Waraka huu… Bahutu Manifesto, ulitoka tarehe 4 March mwaka 1957. Japokuwa ilikuwa ni miaka takribani 37 kabla ya mwaka 1994, lakini ndio siku ambayo mbegu ya mauaji ya kimbari ilipandwa.

Usikose sehemu inayofuata….

Itaendelea…

The Bold
To Infinity and Beyond.

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA PILI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TATU

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NNE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TANO

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SITA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SABA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA NANE

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TISA

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA KUMI NA MOJA
Nimesikia na kuona kwa maandishi kwamba kuna group la whats app ambako mambo haya yote yanapatikana naomba na mm uniunge katika group hili
 
Mkuu Tutsi mlikuwa 700,000 pekee before october 1993.... According to Ibuka ambayo ni organisation ya genocide survivors 300,000 Tutsis sirvived!!!

Sasa kama mlikufa laki 4 pekee na hao wahutu walikufa laki 6 kwanini mnaita tutsi genocide?? Kuna ripoti nyingi tu za human rights watch na transparency international zimetoa ripoti juu ya RPF kuhusika na mauaji ya wahutu wasio wapiganaji yaani wanawake na watoto!! Ikimaanisha genocide was both sides

Unaposema majority where do u get ur statistics from??? Mbona IBUKA says otherwise??
Mheshimiwa
Kuna pande mbili. Upande mmoja umenuia kuangamiza kabisa mbari fulani, na hapo inaangamiza pia hata wanaoonekana kutetea 'maadui'. Upande mwingine ni mbari inayoangamizwa inajitahidi kujitetea. Katika makabiliano hayo wakafa watu kutoka pande zote mbili. Lakini nia ya waliotaka kuangamiza ilibaki kwenye history, nayo ni genocide against tutsi. Hawa wengine walikuwa wanajitetea tu, hakuna genocide hapo.
Kwa hiyo ni sahihi kusema ile genocide ilikuwa dhidi ya watutsi, japo katika vurugu hizo walikufa wahutu pia.
 
Back
Top Bottom