KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU KUELEKEA ETHIOPIA
SEHEMU YA TATU
Kwa wanaokumbuka, nilipokuwa nachambua “Operation Entebbe” iliyofanywa na jeshi la Israel kuokoa raia wao walioshikiliwa mateka nchini Uganda kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe, mwishoni mwa ile makala niliuliza swali, Kwamba oparesheni ile ilifanywa na jeshi la Israel mwaka 1976 ndani ya ardhi ya Uganda, baada ya hapo mahusianio ya Uganda na Israel yalidorora mno. Miaka miwili baadae ndipo sisi Tanzania majeshi yetu yalivamia Uganda na kumtoa Idd Ami madarakani nakukimbilia uhamishoni mpaka mwisho wa maisha yake. Nikauliza, je tunafahamu kuna uhusiano gani kati ya Operation Enntebbe ya Waisrael na Vita ya Kagera? Katika makala hii nitagusia kiduchu jawabu la swali hili. Lakini sitaishia hapo tu bali pia tutajadili ushiriki wa Paul Kagame na Fred Rwigyema kwenye vita ya Kagera.!! Yes, Vita ya KAgera…na si vita ya Kagera tu bali pia uhusika wao katika harakati za FRELIMO nchini msumbuji.! Natamani tuweze kufahamu kinagaubaga kabisa kuhusu mnyororo uliopelekea kukatikia kwenye mauaji yale ya 1994.
Lakini pia, tutajadili namna ambavyo Paul Kagame alifunzwa na kufundwa na Idara yetu ya Usalama wa Taifa (kabla ya kuanza kuitwa TISS) na hatimaye kuwa ‘Jasusi’ mbobezi wa daraja la kwanza vile ambavyo yuko sasa.!
Nimeeleza hapo juu kwamba, lengo kuu la makala hii ni kujadili mauaji ya Kimbari ya mwaka 1994 lakini nimeanzia mbali tangu historia ya Taifa la Rwanda kwa makusudi kabisa ili kuonyesha kiini cha tatizo. Kwa sababu mauaji ya 1994 ni “Matokeo” ya tatizo kubwa la muda mrefu lenye mzizi ya karne kadhaa nyuma ambayo mizizi hiyo ilikuja kumea mwaka 1994. Kwa hiyo kabla siajajadili tukio lenyewe la 1994 nataka tufahamu mnyororo wa matukio muhimu niliyoyaeleza hapo juu kwamba kiu haitakata kama sitayajadili. Lakini pia kuna msululu wa wahusika na matukio ambayo vitabu vya historia kwa makusudi au kwa kutokuwa na uelewa nayo hayasemwi (naamini hayasemwi kwa makusudi kabisa).
Katika sehemu ya nne, nitajadili, nitachambua na kuelezea wahusika, mfululizo wa matukio na yale ambayo yalitokea ‘nyuma ya pazia’ mpaka kufikia mauaji ya Kimbari ya mwaka 1994 yaliyogharimu maisha ya watu karibia milioni moja ambayo damu yake mpaka leo hii bado inalia kwenye ardh ya Rwanda na nyingine ikiendelea kutiririka kwenye mifereji ambayo wauaji wao walisema “mifereji iendayo Ethiopia.!”
Itaendelea…
The Bold